Tatizo la kukatika katika umeme kuikosesha kura CCM

Tatizo la kukatika katika umeme kuikosesha kura CCM

Mbeya si mnajua sana kuzomea wagombea na kupopoa mawe safari za Viongozi wa Kitaifa? Endeleeni labda hilo litawawashia umeme.
 
Ni mwendawazimu tu anaweza kuipigia kura CCM ikiwa kazungukwa na matatizo lukuki. Maji hakuna, umeme hakuna, barabara mbovu, ajira hakuna. Angalia magazeti ya nipashe na mwananchi leo , jinsi wananchi wanavyokunywa maji ya ziwa pamoja na mifugo yao.

You miss ma point soma tena urudi
 
kura zipungue mara ngapi mwaka huu ccm tunaiweka pembeni tunawapa nchi ukawa
 
Kwa kweli hii hali ya tatizo la Umeme linakera sana na hakika litapunguza sana kura za CCM. Hebu fikiria sehemu kama Mbeya umeme unakuja saa 8 usiku, unakata saa 11.

Hapo kumbuka muuza vitumbua ameshindwa kusaga unga kwa sababu ya Umeme, Fundi seremala ameshindwa kukalaza mbao zake, muuza icecream hawezi tena kufanya biashara, Mwanafunzi hawezi tena kujisomea, fundi TV Radio na vitu vingine vinavyohitaji Umeme hafanyi tena kazi zake.

Kwa kweli Umeme ni kila kitu katika shughuli za kiuchumi, hivyo hasira za watu kukosa Umeme watazimalizia kwenye sanduku la kura tarehe 25/10/2015. Kuna sehemu nyingi matokeo ya mwaka huu yatashangaza wengi.

CCM hakikisheni hili tatizo linaisha kabla ya tarehe 25, la sivyo mtapoteza kura nyingi sana za Hasira.

Umeme wala usikushangaze hiyo ni richmond iko kazini inafanya kampeni maana wanajua akiingia magufuli anawatimua wote sasa wanamuharibia makusudi ila Munguyupo.pamoja na magufuli adanganyiki mtu kijinga hv hakuna tatizo la umeme hii nchi ni ukinga wa richmond na kampeni za kitoto hizi
 
Ninawafahamu makada 5 wa Chadema kwenye nafasi za juu za uongozi wa TANESCO
 
Mbeya si mnajua sana kuzomea wagombea na kupopoa mawe safari za Viongozi wa Kitaifa? Endeleeni labda hilo litawawashia umeme.

Kwaani mikoa ambayo viongozi wanashangilia je umeme na maji ya uhakika vipo
 
Jaman mda si mrefu Nimeongea na Mtaalam mmoja wa Tanesco anasema hata kama mitambo yote ya maji ikizimwa, mitambo ya gesi na mafuta iliyopo inatosholeza mahitaji ya nchi. Big up tanesco chapeni kazi achaneni na siasa. So swala la huu umeme kukatika katika mi swala la kiufundi na sio siasa watz wenzangu. Kuna wati wanapenda kuongea viti kuwatia wenzao hasira bila ya kuwa na full details tuachen hizo jmn si nzur
 
Aonywaye Mara nyingi akishupaza shingo itavunjika ghafla na wala hatapata dawa
 
Umeme ndio kila kitu katika maisha ya kisasa.
Inashangaza eti mpaka kwenye uchaguzi huu ccm bado inasema itafanya chili, itafanya lile kuuhusu umeme!!!
Hii ni aibu kubwa!
Mtakumbuka kuwa Jk aliingia madarakani kukiwa na utatuzi wa dharura lakini ndani ya miaka 10 bado tatizo ni. lilelile
 
Kwa kweli hii hali ya tatizo la Umeme linakera sana na hakika litapunguza sana kura za CCM. Hebu fikiria sehemu kama Mbeya umeme unakuja saa 8 usiku, unakata saa 11.

Hapo kumbuka muuza vitumbua ameshindwa kusaga unga kwa sababu ya Umeme, Fundi seremala ameshindwa kukalaza mbao zake, muuza icecream hawezi tena kufanya biashara, Mwanafunzi hawezi tena kujisomea, fundi TV Radio na vitu vingine vinavyohitaji Umeme hafanyi tena kazi zake.

Kwa kweli Umeme ni kila kitu katika shughuli za kiuchumi, hivyo hasira za watu kukosa Umeme watazimalizia kwenye sanduku la kura tarehe 25/10/2015. Kuna sehemu nyingi matokeo ya mwaka huu yatashangaza wengi.

CCM hakikisheni hili tatizo linaisha kabla ya tarehe 25, la sivyo mtapoteza kura nyingi sana za Hasira.

Binafsi nina sababu nyingi sana za kutoipa kura CCM. Hata umeme ungekuwepo wa kutosha ambao unawaka tu hata ukizima switch bado sababu nyingine lukuki zitanifanya kutoipa kura CCM.
 
Back
Top Bottom