Tathmini ya awali ya uvurugaji wa Mchakato wa uchaguzi kwenye hatua za kuchua fomu, kurejesha na uteuzi na mwelekeo

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
TATHMINI YA AWALI YA UVURUGAJI WA MCHAKATO WA UCHAGUZI KWENYE HATUA ZA KUCHUKUA FOMU, KUREJESHA NA UTEUZI NA MWELEKEO WA ACT WAZALENDO KWENYE UCHAGUZI HUU.

A. Utangulizi

Kama tulivyoeleza awali, Chama chetu kupitia Kikao cha Kamati Kuu kilidhamiria kushiriki uchaguzi wa marudio ulioitishwa kwenye Jimbo la Buyungu na Kata 79 nchi nzima. Tuliweka bayana kwamba tutagombea kwenye maeneo kadhaa ya kimkakati kwetu na tutafanya hivyo kwa kushirikiana na wenzetu wa vyama vingine vya upinzani. Imani yetu ni kuwa uchaguzi huu si tu utakuwa jukwaa la kitaifa la kuwaeleza ukweli wananchi kuhusu mwelekeo wa nchi yao bali utakuwa ushahidi mwingine wa kufilisika kisera na kimvuto kwa Chama cha Mapinduzi na kutokubalika kwake kwa wananchi.

Dalili za haya yote zimejionesha kwenye hatua za uchukuaji fomu, urejeshaji wa fomu hizo na uteuzi wa wagombea. Ni dhahiri kwamba CCM haiku tayari kushindana na vyama vya upinzani kwenye majukwaa na sanduku la kura. Bila haya, chama hicho kupitia vyombo vya dola kimeamua kutumia mbinu za kinyang'anyi na kihuni kuhakikisha kwamba kinapita bila kupingwa kwenye kata mbalimbali.

B. Uchambuzi wa Awali wa Dosari Kwenye Hatuaza Uchukuaji wa Fomu, Urejeshwaji wa Fomu na Uteuzi wa Wagombea;
  1. Muda mwingi, Wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi walifunga ofisi zao baada ya wagombea wa CCM kupewa fomu na kuzirejesha. Lengo ni kuhakikisha wapinzani hawapati au kurejesha fomu kwa wakati.
  2. Kwenye baadhi ya maeneo, Chama cha Mapinduzi kilitumia mtandao wake au vyombo vya dola kuwatisha watia nia wa vyama vya upinzani ili wasichukue fomu.
  3. Vyombo vya dola vilitumika kuwakamata baadhi ya watia nia wa vyama vya upinzani na kuwaweka mahabusu ili wasiweze kurejesha fomu.
  4. Wagombea wa upinzani kutangazwa kuwa si raia ili kunyimwa sifa ya kugombea kama ilivyotokea hukoTunduma. Tutaelezea hapa chini.
  5. Wagombea wa upinzani kushambuliwa na kupokonywa fomu wakati wa kuzirejesha.
  6. Wagombea wa upinzani waliopitishwa kuendelea kutishwa na kufuatiliwa na vyombo vya dola ili kuwanyima amani ya kufanya kampeni.
  7. Tume ya uchaguzi kutotoa ushirikiano wa kutosha kuhusu malalamiko haya na mengine yanapowasilishwa kwake.

C: Kisa cha Tunduma: Wagombea wote wa Upinzani Wapokonywa Uraia.

Huko Tunduma, vyombo vya dola vimetumika kuwatisha, kuwakamata na kuwaweka ndani wagombea wa upinzani kwa malengo kwamba wasiweze kuchukua fomu.
Kwa wale waliofanikiwa kuchukua fomu, Idara ya Uhamiaji imewatangaza kuwa wagombea wote nane si raia wa Tanzania na hivyo hawana sifa ya kugombea. Hata wagombea wetu watatu (Kata za Kaloleni, Mpemba na Mwakakati) walipopeleka vielelezo na vitambulisho kuthibitisha uraia, msimamizi wa uchaguzi aligoma kuvipokea.

D. Kiini cha Tatizo:
  1. Kiini cha tatizo ni kithiri kwa makada wa CCM walioteuliwa kwenye nafasi za Ukuu wa Wilaya na Ukurugenzi. Wateule hawa wanapigana kufa na kupona kuhakikisha kwamba CCM kinajitwalia ushindi uchaguzi kwenye kata zote kwa namna yoyote ile hata kwa hila kama tunavyoshuhudia.
  2. Kuporomoka kwa kukubalika kwa CCM na serikali ya awamu ya tano kunakipa wasiwasi chama hicho kuweza kuwakabili wapinzani kwenye uchaguzi na kuwashinda. CCM kimekuwa chama chakavu kwa fikra na uwezo ambacho hakiwezi tena kushinda hata kata bila mbeleko ya dola.

E. Wito na Hatua za Kuchukua:
  1. Chama chetu kitasimama kidete kwa njia za kisheria kuhakikisha kwamba wagombea wetu waliopokwa uraia wao na CCM kwa uchu wa madaraka wanapata haki yao.
  2. Chama chetu kitashirikiana na vyama vingine vya upinzani kuhakikisha kwamba wapinzani tunatuma ujumbe madhubuti kabisa kwa CCM kuwa tumechoka na ubakaji wao wa demokrasia.
  3. Tunatoa wito kwa waangalizi wa ndani kufuatilia kwa karibu vitendo vya ukiukwaji mkubwa wa misingi ya kidemokrasia ulioshamiri kwenye uchaguzi huu wa marudio hata kabla ya kampeni kuanza.

F. Mwelekeo wa Chama kwenye Uchaguzi:

Hadi pazia la kurejesha fomu linafungwa, Chama chetu kilikuwa kimeamua kusimamisha wagombea kata 20. Wagombea wanne kati ya hao (Tunduma na Tarime) wamefanyiwa njama na kutoteuliwa.. Tunaendelea kufanya mazungumzo na wenzetu wa vyama vingine baada ya kila chama kufahamu kwa hakika kata walizofanikiwa wagombea wake kuteuliwa ili kuachiana maeneo ya kimkakati na kuwa na mkakati wa pamoja kukabiliana na vitendo vya uvurugaji wa uchaguzi.


Ado Shaibu,
Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi
ACT Wazalendo
17 Julai 2018.
 
Nilishauri kufungua kesi na kuiomba Mahakama iizue Tume ya Uchaguzi kuendesha uchaguzi wote mpaka kesi ya msingi(wafungue kesi ) kupinga sheria ya uchaguzi inayowatambua Wakurugenzi wa Halmashauri kama maafisa wa Tume (wasimamizi wa uchaguzi) na kesi ya kupinga Tume kutokuwa huru.

Sheria hii ya uchaguzi haifaa hasa kutokana na watu wanaosimamia uchaguzi kwa maana ya wasimamizi wa uchaguzi na wasaidizi wao.

Pia, ni lazima sheria itamke ni marufuku kwa vyombo vya dola kuingia maswala ya uchaguzi kwa namna yoyote.

Faida pekee ya vyama vya upinzani kushiriki hizi chaguzi ni kuwawezesha wananchi kujione kwa macho yao uovu wa hawa watu na huenda huu ndio mkakati wa upinzani (dunia ijue).
 
Yaani ni ajabu na kweli.....

Wagombea wote 8 wa udiwani katika kata za Tunduma, eti wamebainika siyo raia wa Tanzania!

Yaani mtu umezaliwa Tanzania, ukakua hadi ukaoa mtanzania, bado watu wa uhamiaji "hawajakustikia" tu, inafika wakati wa uchaguzi, kuchukua tu fomu na kugombea ndiyo nongwa zinaanza!

Hakika CCM hivi sasa ni Chama dola, siku ambayo Jeshi la Polisi litafanya kazi kwa weledi, bila kupendelea upande wowote, ndiyo itakuwa The last moments of the Giant CCM
 
Yaani ni ajabu na kweli.....

Wagombea wote 8 wa udiwani katika kata za Tunduma, eti wamebainika siyo raia wa Tanzania!

Yaani mtu umezaliwa Tanzania, ukakua hadi ukaoa mtanzania, bado watu wa uhamiaji "hawajakustikia" tu, inafika wakati wa uchaguzi, kuchukua tu fomu na kugombea ndiyo nongwa zinaanza!

Hakika CCM hivi sasa ni Chama dola, siku ambayo Jeshi la Polisi litafanya kazi kwa weledi, bila kupendelea upande wowote, ndiyo itakuwa The last moments of the Giant CCM
Hivi msimamizi wa uchaguzi wa Tunduma ni kabila gani ? ni msukuma ?
 
kwa tume hii ya kuteuliwa magogoni sina muda wa kwenda kupanga foleni kamwe. kwa sasa hakuna uchaguzi bali uchafuzi.
 
Yaani ni ajabu na kweli.....

Wagombea wote 8 wa udiwani katika kata za Tunduma, eti wamebainika siyo raia wa Tanzania!

Yaani mtu umezaliwa Tanzania, ukakua hadi ukaoa mtanzania, bado watu wa uhamiaji "hawajakustikia" tu, inafika wakati wa uchaguzi, kuchukua tu fomu na kugombea ndiyo nongwa zinaanza!

Hakika CCM hivi sasa ni Chama dola, siku ambayo Jeshi la Polisi litafanya kazi kwa weledi, bila kupendelea upande wowote, ndiyo itakuwa The last moments of the Giant CCM
CCM hawana aibu kabisa. wanasema wanashinda kumbe ni wezi, wavurugaji na wanaotishia wananchi, kuwapiga na kuwateka ili wasipige au wasichaguliwe kupitia sanduku la kura. CCM HAWAJAWAHI KUSHINDA NA HAWANA AIBU WANASHANGILIA USHINDI AMBAO HAWAKUSHINDA BALI KWA KUIBA KURA. AIBU AIBU...AIBU TUPU.
 
hata mimi sitakaa nipoteze muda wangu kwenda kupiga kura,,,bora muda huo niutumie kwenda tu shamba nikalime mbaazi
 
Umeshasomeshwa Number sio..

Naona unaleta mafumbo ya Ajabuajabu
NA BADOOOO MNAONA TUNAHAMIA CCM MNAHISI WAJINGA

HAPAKAZI MWENDO WA MANNOTA WANA KMR MSIKOSEW
 

Attachments

  • FB_IMG_1531848416667.jpg
    FB_IMG_1531848416667.jpg
    39.3 KB · Views: 29
Nanukuu toka kwa watu wenye hekima; "The only thing necessary for the triumph of evil is for good men to do nothing" !
 
TATHMINI YA AWALI YA UVURUGAJI WA MCHAKATO WA UCHAGUZI KWENYE HATUA ZA KUCHUKUA FOMU, KUREJESHA NA UTEUZI NA MWELEKEO WA ACT WAZALENDO KWENYE UCHAGUZI HUU.

A. Utangulizi

Kama tulivyoeleza awali, Chama chetu kupitia Kikao cha Kamati Kuu kilidhamiria kushiriki uchaguzi wa marudio ulioitishwa kwenye Jimbo la Buyungu na Kata 79 nchi nzima. Tuliweka bayana kwamba tutagombea kwenye maeneo kadhaa ya kimkakati kwetu na tutafanya hivyo kwa kushirikiana na wenzetu wa vyama vingine vya upinzani. Imani yetu ni kuwa uchaguzi huu si tu utakuwa jukwaa la kitaifa la kuwaeleza ukweli wananchi kuhusu mwelekeo wa nchi yao bali utakuwa ushahidi mwingine wa kufilisika kisera na kimvuto kwa Chama cha Mapinduzi na kutokubalika kwake kwa wananchi.

Dalili za haya yote zimejionesha kwenye hatua za uchukuaji fomu, urejeshaji wa fomu hizo na uteuzi wa wagombea. Ni dhahiri kwamba CCM haiku tayari kushindana na vyama vya upinzani kwenye majukwaa na sanduku la kura. Bila haya, chama hicho kupitia vyombo vya dola kimeamua kutumia mbinu za kinyang'anyi na kihuni kuhakikisha kwamba kinapita bila kupingwa kwenye kata mbalimbali.

B. Uchambuzi wa Awali wa Dosari Kwenye Hatuaza Uchukuaji wa Fomu, Urejeshwaji wa Fomu na Uteuzi wa Wagombea;
  1. Muda mwingi, Wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi walifunga ofisi zao baada ya wagombea wa CCM kupewa fomu na kuzirejesha. Lengo ni kuhakikisha wapinzani hawapati au kurejesha fomu kwa wakati.
  2. Kwenye baadhi ya maeneo, Chama cha Mapinduzi kilitumia mtandao wake au vyombo vya dola kuwatisha watia nia wa vyama vya upinzani ili wasichukue fomu.
  3. Vyombo vya dola vilitumika kuwakamata baadhi ya watia nia wa vyama vya upinzani na kuwaweka mahabusu ili wasiweze kurejesha fomu.
  4. Wagombea wa upinzani kutangazwa kuwa si raia ili kunyimwa sifa ya kugombea kama ilivyotokea hukoTunduma. Tutaelezea hapa chini.
  5. Wagombea wa upinzani kushambuliwa na kupokonywa fomu wakati wa kuzirejesha.
  6. Wagombea wa upinzani waliopitishwa kuendelea kutishwa na kufuatiliwa na vyombo vya dola ili kuwanyima amani ya kufanya kampeni.
  7. Tume ya uchaguzi kutotoa ushirikiano wa kutosha kuhusu malalamiko haya na mengine yanapowasilishwa kwake.

C: Kisa cha Tunduma: Wagombea wote wa Upinzani Wapokonywa Uraia.

Huko Tunduma, vyombo vya dola vimetumika kuwatisha, kuwakamata na kuwaweka ndani wagombea wa upinzani kwa malengo kwamba wasiweze kuchukua fomu.
Kwa wale waliofanikiwa kuchukua fomu, Idara ya Uhamiaji imewatangaza kuwa wagombea wote nane si raia wa Tanzania na hivyo hawana sifa ya kugombea. Hata wagombea wetu watatu (Kata za Kaloleni, Mpemba na Mwakakati) walipopeleka vielelezo na vitambulisho kuthibitisha uraia, msimamizi wa uchaguzi aligoma kuvipokea.

D. Kiini cha Tatizo:
  1. Kiini cha tatizo ni kithiri kwa makada wa CCM walioteuliwa kwenye nafasi za Ukuu wa Wilaya na Ukurugenzi. Wateule hawa wanapigana kufa na kupona kuhakikisha kwamba CCM kinajitwalia ushindi uchaguzi kwenye kata zote kwa namna yoyote ile hata kwa hila kama tunavyoshuhudia.
  2. Kuporomoka kwa kukubalika kwa CCM na serikali ya awamu ya tano kunakipa wasiwasi chama hicho kuweza kuwakabili wapinzani kwenye uchaguzi na kuwashinda. CCM kimekuwa chama chakavu kwa fikra na uwezo ambacho hakiwezi tena kushinda hata kata bila mbeleko ya dola.

E. Wito na Hatua za Kuchukua:
  1. Chama chetu kitasimama kidete kwa njia za kisheria kuhakikisha kwamba wagombea wetu waliopokwa uraia wao na CCM kwa uchu wa madaraka wanapata haki yao.
  2. Chama chetu kitashirikiana na vyama vingine vya upinzani kuhakikisha kwamba wapinzani tunatuma ujumbe madhubuti kabisa kwa CCM kuwa tumechoka na ubakaji wao wa demokrasia.
  3. Tunatoa wito kwa waangalizi wa ndani kufuatilia kwa karibu vitendo vya ukiukwaji mkubwa wa misingi ya kidemokrasia ulioshamiri kwenye uchaguzi huu wa marudio hata kabla ya kampeni kuanza.

F. Mwelekeo wa Chama kwenye Uchaguzi:

Hadi pazia la kurejesha fomu linafungwa, Chama chetu kilikuwa kimeamua kusimamisha wagombea kata 20. Wagombea wanne kati ya hao (Tunduma na Tarime) wamefanyiwa njama na kutoteuliwa.. Tunaendelea kufanya mazungumzo na wenzetu wa vyama vingine baada ya kila chama kufahamu kwa hakika kata walizofanikiwa wagombea wake kuteuliwa ili kuachiana maeneo ya kimkakati na kuwa na mkakati wa pamoja kukabiliana na vitendo vya uvurugaji wa uchaguzi.


Ado Shaibu,
Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi
ACT Wazalendo
17 Julai 2018.
Naunga mkono na ndio ushauri nilioutoa hata mimi kwa viongozi wa vyama vya upinzani
 
Back
Top Bottom