Tathmini: M4C Fundraising Dar wapi hapakuwa sawa na nini Kifanyike

Soma Zaburi 17.

Sala ya kuomba kuokolewa kutoka kwa wadhalimu.

Mstari wa 10 hadi 14:

Adui wa nafsi yangu wanaonizunguka,wameshupaza mioyo yao,vinywa vyao vinasema kwa kiburi. Sasa wametuvizia,wametuzingira pande zote; wameyakaza macho yao ili watuangushe chini. Wanafanana na simba atamaniye kurarua,kama wana simba wanyemeleao mafichoni. Simama, ee BWANA,uwakabili,uwaangushe chini; kwa upanga wako uokoe nafsi yangu na mwovu. Waangamize kwa upanga wako; kwa mkono wako, Bwana,waangamize;waondoshe ulimwenguni katika ujana wao. Wajaze matumbo yao kutoka hazina yako,wana wao washibe pia na wawaachie akiba yao wana wao.

Zaburi hii ni lalamiko la mtu aliyeshtakiwa kwa uongo,anamwomba Mungu,hakimu wa haki,kumthibitisha yeye na kuwaadhibu washtaki wake wabaya.
 
M4C ilikuwa kichaga zaidi nazani hata wewe umeona wengi waliopewa nafasi ya kuzungumza chochote ni wakaskazini.
2.mbowe aliponda kutangaza nia za ubuge au urais lakini kuna watu wawili wametangaza nia za ubunge serengeti na kwa mh chami.
3.kauli za kibabe za lema juu ya makampuni ya simu kana kwamba anahisa.
4.kauli ya nassari kwamba Tz ni laini sana kama maini
5!mwenyekiti mbowe kamaliza kuongea lakini bado kuna jamaa wanaendelea kuongea
6.mtangazaji hajui chochote hata jina la chama

Nilipenda kauli ya Nasari kwamba, Tanzania ni laini Kama maini. Pia ule ujumbe uliokuwa ukutani aw Gandhi kuwa " be the change you want to see in this world"
 
Its a good start and they should be more organised next time, there were several shortfalls and I didn't like Lema's comments

I think we have a long way to go, not kwenye ukombozi wa nchi kama anavyosema...maana tushakombolewa ni ukombozi wa kifikra tu!

Mie nimechangia kwa MPESA miongoni mwa wale 'waoga' wasiotaka majina yatajwe!
 
Si busara sana kulalamika kwa mapungufu yaliyojitokeza katika tukio la leo na si vibaya kupongeza na kudumisha yote mazuri katika tukio hili hapo SERENA HOTEL.

Nini Tathmini yako Mpenda mbadiliko na nini kifanyike siku zijazo?

Sikufuatilia yaliyotokea Arusha katika M4C Fundraising ya kwanza. Lakini naamini tukio la jana lingeweza kujifunza chochote toka kule.

Kwa upande wa ushauri,naona mengi yamesemwa na wadau, ila nitaongeza kidogo katika hayo:
1. Umuhimu wa kuandaa shughuli kwa umakini,kuwa na ratiba inayoeleweka, ratiba ambayo itaonyesha juu ya tukio fulani,msemaji wa tukio hilo,muda wa tukio hilo na washiriki wa tukio hilo. Kuwa na mshehereshaji anayefahamu dhumuni la shughuli. Mshehereshaji apewe kabisa ToR mapema,ili aweze kufanya kazi yake ipaswavyo.
2. Umuhimu wa uongozi wa M4C kutoa taarifa za mapato na matumizi ya pesa,si katika magazeti ila katika vikao husika vya chama. Wanaweza kutoa kwenye vyombo vya habari kama wakiona ni sawa kufanya hivyo. Hii itatoa moyo kwa wachingiaji tarajiwa kuona namna ambavyo pesa zao zinaweza kutumika na kuthaminiwa.
3. Kutoa mapema ratiba za M4C Fundraising. Kama sasa uongozi wa M4C unapaswa kusema mahala pengine ambako fundraising itafanyika. Tena ingekuwa vyema,uongozi uandae ratiba ya muda mrefu wa M4C Fundraising,kama almanac vile. Ili ifahamike kabisa,nini kitafanyika,wapi kitafanyika na lini kitafanyika. Hili litasaidia pia katika kufanikisha zaidi zoezi zima la uchangishaji.

Zaidi ya yote,hongereni M4C Dar kwa kufanikisha shughuli. Hongereni wana DSM kwa kukubali kujitoa kwa ajili ya kuchangia msingi wa mabadiliko.
 
MC's walikuwa na wasi wasi sana, hawakuwa vocal wala kuchangamka. Huku mwingine akisisitiza kwamba ndo mara ya kwanza kukaa na wanasiasa
 
jamaa wanajitahidi sana.. ila hizo fedha zitumike kwa malengo husika.. niwaone mpka kwenye kata yangu
 
Lema amezoea kuongea na machalii, pia ana hasira ya hukumu dhidi ya ubunge wake. Ni vizuri kukaonekana kwamba walioandaa shuhuli walijipanga ikiwa ni pamoja na kupanga nani aongee na aongee nini. Ilikuwa wazi kwamba mtu pekee aliyejiandaa atasema nini na kwa malengo gani ni Mbowe

Nitafurahi kama next event itaonekana kuna order fulani ambayo waandaaji walijipanga na kukubaliana. Ikiwezekana Lema akae mezani tu aache walioandaliwa kuongea na kuendesha shuhuli.

Endeleeni kuchangia, kwa SMS tuma neno Chadema kwenda 15710. Kwa benki CRDB akaunti namba 01j1080100600
 
Mi tatizo kubwa nililoona ni mpangilio wa shaghuli yenyewe ambacho watu wanakosea kusema ni maandalizi. Kwangu maandalizi sina tatizo nayo coz kama maandalizi yasingekuwa mazuri wasingeweza kupata pesa nyingi hivyo katika mda mchache.

Kwangu mpangilio na taarifa za kutosha kwa viewers ndo vya kuangaliwa kwa sana.
 
Zitto kakosa mvuto, so he has to slow down as chadema frontliner until he resolve his corruption allegation.

stop running around the bush,be specific,mbowe hana mvuto toka enzi,padre wamagumashi ameshapoteza mvuto wake wa bandia aliokuwa nao(mask personality)mkumbusheni alipe deni alilokopa pale saccos kinondoni manyanya.zitto muwajibikaji,mzalendo na kijana muadilifu ndie kiongoz bora chadema ,mfano wa kuigwa!
 
Sikufanikiwa kuiona hiyo, lakini Lema G, asingepaswa kuwa MC, kama ni kweli alikosea sana....kwa mtazamo tu, yeye alitakiwa kuwa mhamasishaji asiye rasmi.

Kushusu suala la Chadema leo Dar, Kesho Moro, Keshokutwa Iringa, hilo sio tatizo....kwani hiyo ni sawa na "Twanga kotekote Campaign".

Niungane na mtambuzi kuwa huu ndio wakati muafaka kwa CDM kujipanga kiakili na kuweka mikakati ya kuchukua nchi kiulaini kabisa.

Na baada ya kuchukua nchi, jambo la kwanza ni kutekeleza ahadi kuu ilizoahidi...
 
Kwenye kauli zake na kampeni zake mashuhuri duniani, mweshimu miwa barack obama alikuwa akitumia slogan ya yes we can. Nashangaa kama jamaa anafikiri bado watanzania hawana TV, nitanukuu kauli yake ya jana mara baada ya nassari kuongea alisema "YES WE CAN" mbona sioni kauli hata moja ya wanachadema. hivi siyo kwamba Mbowe bado anamwigiza OBAMA?embu wadau tuwaelimishe hawa wasanii
 
Yaani hilo neno la yes we can ndo limekuthangaisha hivyo? Kwani kuna ubaya gani? Amekosea nini? Mtu anapozungumza anaweza kusema lolote, including imitating, or quoting somebody.pole kama amekukukwaza.
 
Hiyo si kauli tu mkubwa?! Ina maana haturuhusiwi kutumia slogan zilizowahi kutumiwa na watu fulani? Na title ya huu uzi haijakaa kimantiki, hiyo siri iliyofichuka iko wapi???
 
Kwenye kauli zake na kampeni zake mashuhuri duniani, mweshimu miwa barack obama alikuwa akitumia slogan ya yes we can. Nashangaa kama jamaa anafikiri bado watanzania hawana TV, nitanukuu kauli yake ya jana mara baada ya nassari kuongea alisema "YES WE CAN" mbona sioni kauli hata moja ya wanachadema. hivi siyo kwamba Mbowe bado anamwigiza OBAMA?embu wadau tuwaelimishe hawa wasanii

Harufu ya huozo sijuwi ni kijambo mhh mhh
 
Back
Top Bottom