Tathmini: M4C Fundraising Dar wapi hapakuwa sawa na nini Kifanyike

Tathmini: M4C Fundraising Dar wapi hapakuwa sawa na nini Kifanyike

Nahisi wewe ndio ubongo wako umechaka inabidi uwekewe ata wa mbuzi

Hii inaonesha Chadema imeanza kuchokwa tokana na kutokuwa na mipango mizuri. Mara leo Morogoro, mara dar, mara Ulaya.
 
Inabidi swala la mshehereshaji lishughulikiwe walipooza sana.

Lakini na shukuru watu wameonesha muamko mzuri.

Kweli watanzania tunataka mabadiliko na wameonesha wanataka mabadiliko!
 
Si busara sana kulalamika kwa mapungufu yaliyojitokeza katika tukio la leo na si vibaya kupongeza na kudumisha yote mazuri katika tukio hili hapo SERENA HOTEL.

Nini Tathmini yako Mpenda mbadiliko na nini kifanyike siku zijazo?

M4C ilikuwa kichaga zaidi nazani hata wewe umeona wengi waliopewa nafasi ya kuzungumza chochote ni wakaskazini.
2.mbowe aliponda kutangaza nia za ubuge au urais lakini kuna watu wawili wametangaza nia za ubunge serengeti na kwa mh chami.
3.kauli za kibabe za lema juu ya makampuni ya simu kana kwamba anahisa.
4.kauli ya nassari kwamba Tz ni laini sana kama maini
5!mwenyekiti mbowe kamaliza kuongea lakini bado kuna jamaa wanaendelea kuongea
6.mtangazaji hajui chochote hata jina la chama
 
Inabidi swala la mshehereshaji lishughulikiwe walipooza sana.

Lakini na shukuru watu wameonesha muamko mzuri.

Kweli watanzania tunataka mabadiliko na wameonesha wanataka mabadiliko!

Mabadiliko ya nini?, unaposema watanzania una maana gani?. Sema wewe unataka maendeleo.
 
Hii inaonesha Chadema imeanza kuchokwa tokana na kutokuwa na mipango mizuri. Mara leo Morogoro, mara dar, mara Ulaya.

It is Ok Kidatu, when you fight you need to apply different strategies. Pia katika fight hiyo mbinu wanayotumia ni nzuri, ukiwa na mashambulizi toka huku na kule, adui anachanganyikiwa !
 
It is Ok Kidatu, when you fight you need to apply different strategies. Pia katika fight hiyo mbinu wanayotumia ni nzuri, ukiwa na mashambulizi toka huku na kule, adui anachanganyikiwa !

Kuna ukweli kwenye kauli yako hii. Maana naona kila sehemu Chadema wakienda tu basi wabunge husika wa maeneo hayo wanakwenda huko mara moja kuweka mambo sawa. Niliona Membe alivyokimbilia jimboni kwake wakati M4C walivyokuwa jimboni kwake. Hii yote inaonesha ni kuchanganyikiwa kwa CCM.
 
kiukweli alichemsha mbaya. Hana courtesy, kifupi ni mropokaji hafikiri kabla ya kusema. Big up kamanda Mbowe kwa busara.

Ni kuvumiliana tu. You know what, in any fight kila mmoja ana style ya kupiga pending on jinsi alivyoumizwa na adui yake. Mwingine atapiga kwa busara, mwingine atapiga bila huruma, mwisho wa siku adui ameshindwa, BASI. It is all about change, and change for ever !
 
Kuna ukweli kwenye kauli yako hii. Maana naona kila sehemu Chadema wakienda tu basi wabunge husika wa maeneo hayo wanakwenda huko mara moja kuweka mambo sawa. Niliona Membe alivyokimbilia jimboni kwake wakati M4C walivyokuwa jimboni kwake. Hii yote inaonesha ni kuchanganyikiwa kwa CCM.

Asante, mimi naamini something is coming up ! Labda hakitakuwa kikubwa kivile, but ukiangalia hayo mashambulizi, zile juhudi za akina Ndugai pale Bungeni, utaona ni wazi kabisa kuwa kuna Kimbunga kinakuja. Ile kazi ya Ndugai na Makinda, ni kazi ya makusudi ya kuokoa chama tawala, They know what they do and why they do it, ndiyo maana wanafanya bila aibu. Haiwezekani hata siku moja spika akatetea tusi la mchangia hoja kama alivyofanya Ndugai wakati Werema akimtukana Lisu kuwa anatumia kichwa kwa kufugia nywele tu !
 
Samahani sikujua kama unaumwa kiasi hiki! Niwie radhi.

Ruta, angalia sana usije ikawa wewe ndiye unaumwa. Kutofautiana kimtazamo na kimawazo isiwe shida kabisa bali jaribu kukubaliana kutokubaliana. Kama sisi sote tunafikiria basi kuwa na mawazo tofauti lazima itatokea labda kama mmoja kati yetu hafikirii.

Ninachopigia kelele na kukipa kipaumbele ni kubadili KATIBA kwanza then mengine yafuate. Kumbuka tulipiginia uhuru kumtoa mkoloni mweupe kama tunavyofanya leo. Lakini kwa sababu ya katiba tuliyonayo tumefika hapa tulipo leo hii. Na katiba hii kwa asilimia kubwa tuli-copy katiba ya mkoloni ingawa tuliongeza mambo yetu kidogo sana. Elewa kwamba hata Chadema wakichukua madaraka leo hii bado watatawala kwa kufuata katiba iliyopo ambayo ina mapungufu mengi na ya kutisha. Hivyo na wao cahdema watafanya madudu yaleyale yanayofanywa na CCM leo hii.

Mimi kwa upande wangu nataka mabadiliko ya katiba kwanza, samahani kwa kutofautiana kimawazo na kimtazamo. Na kama huo ni ugonjwa basi kila mtu mwenye akili timamu ni mgonjwa.
 
Mc hakua kiviiile ila 2nahtaj break dwn ya kilichptkana......pipooooooozzzzzzzz poweeeeer
 
Muendelezo wa kuchangia m4c ni mzuri isipo kuwa maandalizi ya shughuri hayatakiwi kufanywa kwa kushtukiza kama hii. Huu ulitakiwa kuwa hata mpango wa majuma matatu au hata mwezi, kuiandaa shughuri kuwa katika viwango vya uhakika kuanzia uandaaji, ma mc wabobezi na kuhamasisha sana kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Lakini lingine kubwa next m4c contributions gathering iwe inatoa mrejesho wa kilicho changwa na jinsi kilivyotumika. Mfano leo wangeweza ku breaka down mapato ya m4c Arusha na matumizi yake then impact yake kwa ujumla kwenye chama.

Muhimu.
Waziri kivuli wa fedha ambae pia ana cheo cha unaibu katibu mkuu kutokujihusisha na mambo ya chama kwenye fund rising ambayo naamini ni moja ya mambo muhimu na miongoni mwa majukumu ya pamoja ni dosari kubwa kwake. Hawezi kuwa raisi kwa kuota kwenye vyombo vya habari! Apambane ili chama kiopate fedha kifike kule anakota azipate kura za uraisi.

slaa alikuwa moro akipambana,mbowe alikuwepo dar.zitto lazima abaki bungeni hawawezi kuliacha bunge bila kiongozi
 
Back
Top Bottom