Niko msibani hapa Mbezi Goigi ambako mwili wa marehemu Ustadh Ilunga Hassan Kapungu umelala. Kitu kizuri ni kuwa hakuna alietetereka kwa msiba huu kwani kila mmoja wetu anajua kila nafsi itaonja mauti na huu ni muda wa Ustadh Ilunga. Kizuri kingine ni kuwa amefariki kwa ugonjwa ambao ulimuanza zaidi ya miaka kumi na tani iliyopita, kabla hata ya umaarufu wake, kabla hata ya propaganda zidi yake kuenezwa. Watu wamehamasika kwa kazi yake aliyoifanya hapa dunia na wako tayari kuiendeleza. Ustadh Ilunga amefariki na atazikwa leo saa kumi jioni lakini kazi yake katika uislamu itadumu milele.