Tanzia: Sheikh Ali Comorian afariki dunia

Tanzia: Sheikh Ali Comorian afariki dunia

dos santos

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2010
Posts
256
Reaction score
128
Taarifa zilizotufikia muda si mrefu zimearifu kutangazwa kwa kifo cha Sheikh maarufu nchini Ali Mzee Comorian kilichotokea leo muda wa kuingia nyakati za adhuhuri.

Taarifa zinasema kifo cha Sheikh Comorian kinafuatia kuugua kwa muda mrefu kulikopelea kutokea kwa kifo chake.

Sheikh Comorian atakumbukwa na wengi kwa mapenzi yake yasio kifani katika kumpenda Mtume Muhammad ﷺ.
Aidha mbali na kutoa Da'awa katika shughuli nyingi za kiislamu pia Sheikh Comorian alikuwa ni mtunzi wa Qaswida na kiongozi wa kikundi cha Qaswida cha Ahbaabur Rasuul.

Moja ya Qaswida aliyotunga na kupata umaarufu mkubwa Afrika Mashariki ni 'Tumpendeni'.

Kifo cha Sheikh Comorian kimeacha simanzi kubwa kwa watu wenye mapenzi na Mtume Muhammad ﷺ.

Inna lillahi wa inna ilayhi raji’un (انا لله وانا اليه راجعو&#1606😉 Sura Al-Baqara, aya 156.

Source: Ahbaabur Rasuul
sheikh comorian.JPG
 
Alhamdulillah innalillahi wa inna ilaihi rrajiun kullu nafsin dhaaikatullmaut
 
Taarifa zilizotufikia muda si mrefu zimearifu kutangazwa kwa kifo cha Sheikh maarufu nchini Ali Mzee Comorian kilichotokea leo muda wa kuingia nyakati za adhuhuri.

Taarifa zinasema kifo cha Sheikh Comorian kinafuatia kuugua kwa muda mrefu kulikopelea kutokea kwa kifo chake.

Sheikh Comorian atakumbukwa na wengi kwa mapenzi yake yasio kifani katika kumpenda Mtume Muhammad ﷺ.
Aidha mbali na kutoa Da'awa katika shughuli nyingi za kiislamu pia Sheikh Comorian alikuwa ni mtunzi wa Qaswida na kiongozi wa kikundi cha Qaswida cha Ahbaabur Rasuul.

Moja ya Qaswida aliyotunga na kupata umaarufu mkubwa Afrika Mashariki ni 'Tumpendeni'.

Kifo cha Sheikh Comorian kimeacha pengo kubwa kwa watu wenye mapenzi na Mtume Muhammad ﷺ.

Inna lillahi wa inna ilayhi raji’un (انا لله وانا اليه راجعو&#1606😉 Sura Al-Baqara, aya 156.

Source: Ahbaabur Rasuul

Ndio babaake na Saidi Comorian or? Innalilah wa innailaihi rajiun.
 
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Mwenyezi Mungu afanyike faraja kwa watu wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja ama nyingine.
 
Innaa lilah wainnaa ilaih raajiun. Allah amsamehe madhambi yake anamueke mahala pema kwa mapenzi yake.

Lakini si sahihi kusema eti kuondoka kwake kutaacha pengo kwa wapenzi wa rasulullah.

Kumpenda Mtume Muhammad salam na amani zimfikie ni kwakufuata mafundisho yake na sio kwakuimba na kucheza.

Hakuna shaka kwamba Maswahaba Allah awawie radh walikuwa wakimpenda sana na kumfuata Rasulullah lakini kamwe hawakuwahi kuyaonyesha mapenzi yao kwakuimba au kupiga ngoma.
 
shukrani, maoni mazuri yatafanyiwa kazi
Innaa lilah wainnaa ilaih raajiun. Allah amsamehe madhambi yake anamueke mahala pema kwa mapenzi yake.

Lakini si sahihi kusema eti kuondoka kwake kutaacha pengo kwa wapenzi wa rasulullah.

Kumpenda Mtume Muhammad salam na amani zimfikie ni kwakufuata mafundisho yake na sio kwakuimba na kucheza.

Hakuna shaka kwamba Maswahaba Allah awawie radh walikuwa wakimpenda sana na kumfuata Rasulullah lakini kamwe hawakuwahi kuyaonyesha mapenzi yao kwakuimba au kupiga ngoma.
 
Sisi wote ni wa Allah na marejeo ni ngamani (kwake)
Btw nina utashi wa kujua maisha yake (maskani) alikua akiishi wapi , na inatarajiwa atazikwa wapi?
 
To Sheikh Ali Comorian's family, please accept my deepest sympathies during your unbelievable time of loss.
 
kifo kinafuatia kuugua kwa muda mrefu kulikopelea kutokea kwa kifo chake.

kwa mapenzi yake yasio kifani katika kumpenda Mtume Muhammad

Taarifa zilizotufikia muda si mrefu zimearifu
Unawapa waumini taswira mbaya.
 
allahuma ghufirllahu wa arhamahu wamaskanaa fii jannat.. (sheikh comorian)
 
M/mungu ailaze roho ya marehem pepa pepon., polen wafiwa
 
...ndo nani ? aliokoka ? isije ikala kwake, alale mahali anapostahili na Mungu wangu awatie nguvu wafiwa na marafiki walioguswa na msiba huu...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom