NostradamusEstrademe
JF-Expert Member
- Jul 1, 2017
- 3,862
- 5,153
Bila kumsahau Ngalimecha NgahyomaPumzika kwa Amani Prof hakika vichwa maji na wale waliojifanya wamevaa kaptula la marx umewaacha.Mawazo yako yataishi (Kivuli kinaishi) Msalimie Shaaban Robert mwambie Tawasifu yake maisha yangu baada ya miaka 50 tunaendelea ingawa bado haijatimia,ukimuona Edwini Semzaba mwambie wakuu wa Shule siku hizi nao wamegeuka Magoswe,mpe hai nyingi Ben Mtobwa mzee wa pesa zinazonuka mwambie watu wanatanua nazo huku,bila kumsahau Elvis Musiba mzee wa njama.Wàsalimie waandishi wote ikiwezekana muendeleze fani katika Ulimwengu mwingine.Wasalamu.
Sent using Jamii Forums mobile app