Marehemu amemaliza fujo zake hapa duniani,maisha hayana maana kwa sababu tuna zaliwa ilitufe, mtu anapo zaliwa tu huanza kukisaka kifo. Maisha ni kifo cha polepole, MWANGA WA MILELE MPE EE BWANA.
Looh, Du!
Philosophia hii:
"...hapa duniani maisha hayana maana..."
"...tunazaliwa ili tufe..."
Yaani, maana ya 'kuzaliwa' ni 'kufa'.
Mbona hapo tayari kuna 'maana' mkuu Junior Lecturer, yaani 'kuzaliwa' maana yake ni 'kufa', au sio?
Nakubaliana nawe kwamba "Maisha ni kifo cha polepole" kwa spidi mbalimbali, wengine hata dakika haitimii, wanaondoka. Baadhi ni miaka na miaka, lakini kwa sasa haizidi miaka 120.
Tutajitahidi sana kuahirisha mauti kwa njia mbali mbali kwa ufahamu wetu wa sayansi, au hata kuhamia sayari nyingine, lakini kifo kiko palepale, au?
'Genetic engineering,' /'cloning' haviwezi kutupatia jibu tuepuke kifo kama tunavyokijua?
Turudi mwanzo wa bandiko lako: kama "maana ya kuzaliwa ni kufa", basi tuzuie 'kuzaliwa'! Tutakuwa tumekishinda kifo!
Samahani kwa mjadala wa ajabu sana huu.
Kezilahabi apumzike kwa amani... hili nalo linaweza kuzua mjadala mkubwa!