Hizi ni baadhi ya sifa za marehemu NEMELA MANGULA, binti wa makamu mwenyekiti wa CCM, bw. Phillip Mangula, aliyefariki jana tarehe 18/08/2013:-
1. Mpole
2. Mtaratibu
3. Mchapa kazi
4. Ana akili
5. Ana adabu/heshima
6. Anapenda ushirikiano
7. Kiongozi
8. Msikivu
9. Mshauri mzuri
10. Hana makuu
11. Hajikwezi
12. Ana upendo
14. Mpiganaji
15. Hatumii kilevi
16. Msomi
17. Mtetezi wa 'wanyonge'
18. Mwanadiplomasia
19. Mwanajamii
20. Mpenda amani
21. Mpatanishi
22. Rafiki wa wote
23. Mwafrika halisi kwa umbo, ngozi, sura na tabia
24. Mfuasi wa utamaduni wa kiafrika
Kuna la kujifunza hapo? RIP Nemela. Pole Mangula. Namba 26-30 mpo? Ingawa nikiri nakichukia chama cha 'ccm', huyu binti kama angekuja kugombea kwenye nafasi ya kisiasa ningefikiria kumsapoti.
LICHA YA SIFA ZOTE HIZO NZURI NIZIJUAZO KUHUSU YEYE, KAFA. Wakati kila mtu akisikitia kufa akiwa binti mdogo hata kabla ya 'thirties'. Kama jamii sasa tujitazame. Madhara ya uovu kama ufisadi, wizi, rushwa, uzembe na jamii isiyotii kanuni za msingi na sheria yanatugusa wote chadema na ccm, wakristo kwa waislamu, maskini kwa matajiri. Tuviangalie vifo vya wananchi wetu hasa vijana. Je, vilipaswa kutokea? Je, mifumo yetu inatulinda au inasadia kueendeleza na kutetea uovu? Nemela hakupaswa kugongwa. TUREKEBISHE MIFUMO YETU YOTE YA MAISHA. RIP, once again, NEMELA