TANZIA: Mzee Kitwana Kondo afariki dunia

TANZIA: Mzee Kitwana Kondo afariki dunia

Wadau Kwema?

Kuna tetesi kua Mbunge wa zamani wa Kigamboni na Meya wa Jiji la Dar es salaam Bwana Kitwana Kondo (KK) amefariki Dunia Mchana huu; kuna mwenye taarifa zaidi ya hii kitu?

Alikuwa amelazwa hospitali ya Hindu Mandal

======
UPDATE:
======

Toka kwa Tunkamanin,

Inna lillahi wainna ilaihi rajiuun.

Mzee Kitwana Kondo, KK amefariki dunia jioni hii katika Hospitali ya Hindu Mandal. Atazikwa kesho 25/5/2017 In Shaa Allah

Wakati wa uhai wake, Kitwana Kondo aliwahi kuwa Mbunge wa jimbo la Kigamboni na Meya wa Jiji la Dar es Salaam.


Ni hivi karibuni alitembelewa na Ndg. Edward Lowassa > Mzee Edward Lowassa amtembelea Mzee Kitwana Kondo hospitali ya Hindu Mandal

Aidha, unaweza kusoma pia > Hotuba ya Al Hajj Kitwana Kondo, Mbunge wa Kigamboni mwaka 1999 Bungeni Dodoma

Ni matumaini yangu makubwa angalau katika Msiba huu Mheshimiwa Rais wa JMT Dkt. Magufuli atakuwepo / atahudhuria.
 
Inna lillahi wainna ilaihi rajiuun. Nakukumbuka mzee Kitwana Kondo uliyekuwa huna elimu kabisa ya kuwa meya wa Dar. Nakukumbuka hasa kwa ule ufisadi wako wa kuuza open spaces za jiji! Na hasa ile kali uliyotaka kuwauzia kina Dewji open space ya mnazi mmoja bila aibu!!!! Dewji alishaanza kuizungushia uzio mchana kweupe. Baada ya wananchi kuwashikia mabango halmashauri ya jiji hatimaye serikali ikaingilia kati na kufuta mkataba ule wa kifisadi.
 
Inna lillahi wainna ilaihi rajiuun. Nakukumbuka mzee Kitwana Kondo uliyekuwa huna elimu kabisa ya kuwa meya wa Dar. Nakukumbuka hasa kwa ule ufisadi wako wa kuuza open spaces za jiji! Na hasa ile kali uliyotaka kuwauzia kina Dewji open space ya mnazi mmoja bila aibu!!!! Dewji alishaanza kuizungushia uzio mchana kweupe. Baada ya wananchi kuwashikia mabango halmashauri ya jiji hatimaye serikali ikaingilia kati na kufuta mkataba ule wa kifisadi.

Stara haiuzwi Dukani!

Sifa na Kigezo cha kuwa Meyor mpaka Leo ni kujua kusoma na kuandika lakin umeamua kumuadhiri Maiti kwa Matusi ya Reja reja!

1963 Mzee KK anamaliza Shahada yake USA Babu yako ( age mate wa KK) Pengine hata kuandika Jina lake Kafa hawezi

Mola akusamehe na Ndugu wa Mzee Kondo pia wakusamehe Inshallah!
 
R I P Mzee Kondo, tunakukumbuka kwa mengi hasa hili la wanafunzi kumuita Mzee wa wakati huo "shemeji"
Mkuu umenikumbusha mbali, nilikuwepo wakati huo wasichana wa Jangwani wakimuita Mzee R shemejiiiii kila msafaa unapopita pale nilkuwa Azania. Wale mabinti walikuwa mapacha mmoja akahamishiwa Uk.
 
Inna lillahi wainna ilaihi rajiuun. Nakukumbuka mzee Kitwana Kondo uliyekuwa huna elimu kabisa ya kuwa meya wa Dar. Nakukumbuka hasa kwa ule ufisadi wako wa kuuza open spaces za jiji! Na hasa ile kali uliyotaka kuwauzia kina Dewji open space ya mnazi mmoja bila aibu!!!! Dewji alishaanza kuizungushia uzio mchana kweupe. Baada ya wananchi kuwashikia mabango halmashauri ya jiji hatimaye serikali ikaingilia kati na kufuta mkataba ule wa kifisadi.
Abudist,
Ingetosha kwa mimi kukunyamazia kimya lakini nimeona vyema nikufahamishe
lile ambalo wewe hulijui.

Mzee Kondo amekaa darasani vizuri yeye ni mhitimu wa Howard University,
Marekani.

Mzee Kondo bila shaka kwa yale mafunzo yake katika Idara ya Usalama ya
Kiingereza alikuwa bingwa wa kumpoteza yeyote asimjue.

Nakueleza haya kwa kuwa mimi Mzee Kondo alikuwa baba yangu kwa hiyo
nimekuwa karibu na yeye, nimemfahamu vizuri na nimejifunza mengi kutoka
kwake.

Kwanza alikuwa na ujuzi mkubwa sana wa lugha ya Kiingereza lakini hakupenda
watu walijue hili.

Mzee Kondo alikuwa anaijua vyema historia ''ancient,'' na ''modern.''

Nakumbuka siku moja alipotushangaza mimi na wenzangu alipotupa historia ya
Oliver Cromwell.

Siku nyingine alitushangaza tena alipotupa historia ya Saddam Hussein na Abdul
Karim Kassim
aliyekuwa Waziri Mkuu wa Iraq.

Mzee Kondo alikuwa hodari wa kuhifadhi nukuu za wasomi wakubwa neno kwa neno
kwa lugha zote, Kiingereza na Kiswahili.

Mzee Kondo akimpenda sana mshairi, Muyaka bin Haj (1776 - 1840) na alihifadhi
beti zake nyingi.

Ajabu ni kuwa Kitwana Kondo ukimchukulia kuwa, ''hamna kitu,'' hatokukatisha tamaa
alipenda, kile Waingereza wanaita, ''to play dumb,'' yaani kujifanya mbumbu, ikiwa wewe
utamchukulia hivyo.

Abdudist, wewe kama wengi wa mfano wako umelambwa kichogo na baba yangu.
Mwisho ningependa kukunasihi kuwa maiti haisemwi vibaya.

Tumwache mzee wetu apumzike kwa amani.
 
Mzee wangu umefanya vyema kuliweka vizuri hilo jambo,unajua nchi yetu wapo baadhi ya watu wana chuki iliyopitiliza dhidi ya uislam na waislam hasa wale waislam wanaojitahidi kuienzi dini yao kwa kuishi katika misingi yake basi hao ndio uwakera zaidi hivyo hujikuta wanashindwa kuvumilia na kuanza kuwatukana na kuwadhihaki
Haichachi,
Ahsante ndugu yangu lakini taratibu tutafahamishana ukweli.
 
  • Thanks
Reactions: OTG
Back
Top Bottom