PakaJimmy, Asante kwa taarifa ya msiba wa mwana JF mwenzetu. Nina swali moja dogo, pamoja na kwamba mwenzetu ametangulia mbele ya haki bado tuna sababu ya kuficha jina lake halisi? Kwa nini usimtaje tu kwa jina lake? Nakumbuka kuna mwana jamvi mmoja alifariki mwaka juzi tulifahamishwa kifo chake na jina lake halisi lilitajwa. Lakini kama una sababu za msingi za kutotaja jina lake halisi, basi ibaki kama ilivyo. Kuna watu wawili watatu hapa JF wanajua jina langu halisi. Siku nikatagulia mbele ya haki, nilishawaruhusu kutangaza kifo changu na kutaja jina langu halisi. RIP Kamanda Waisamon!!! Tiba