Tanzia: Mwanajamvi afariki Dunia.

Tanzia: Mwanajamvi afariki Dunia.

Rest in Peace our Wasaimon. Michango yako hapa jamvini itaendelea kuwanufaisha wengi wanaopitia hapa kama wageni na members kwa ajili ya jamii yetu kwa ujumla. Amani iatawale familia yake hasa mke na watoto wake.
 
Nimepigiwa simu jioni hii, dakika kadha zilizopita kuwa Mwanajamvi mwenzetu anayekwenda kwa ID ya wasaimon amefariki dunia muda kama dakika 45 zilizopita, katika hospitali ya Selian hapa Arusha, na sasa hivi ndiyo anaingizwa chumba cha ubaridi.
:A S cry::A S cry:

Taarifa hizo zinasema kuwa amenguka akiwa katika harakati za kuonana na Daktari, akiwa amesindikizwa na baba yake mzazi.

Wasaimon alijiunga na jamvi 6.10.2010.

Binafsi nilikuwa nafahamiana sana na wasaimon, alikuwa ni mtu wa kutoa ushauri wa hekima sana kuhusiana na maisha ya miaka hii, na alikuwa mpiganaji asiyechoka, akitumikia kampuni mojawapo ya Tours mjini Arusha. Naelekea msibani, nitawajuza kinachojiri.
wasaimon alivinjari hapa majukwaani hadi juzi 14.01.2012, na naambiwa kuwa hadi jana alikuwa mzima wa afya.
Ameacha Mke na watoto 3.

Mungu Ilaze Roho ya Marehemu wasaimon Mahala Pema Peponi.

Kamanda, nimejaribu kupitia mabandiko machache tu ya wasaimon, kwakweli alikua upande ule wenye nuru, probably only 5-10% ya wanaJF

he was positive, God fearing, blessed na wa kupeana moyo

Its a loss, hasa kwa wakati huu ambao JF imejawa zaidi na watu type yangu
 
Nimepigiwa simu jioni hii, dakika kadha zilizopita kuwa Mwanajamvi mwenzetu anayekwenda kwa ID ya wasaimon amefariki dunia muda kama dakika 45 zilizopita, katika hospitali ya Selian hapa Arusha, na sasa hivi ndiyo anaingizwa chumba cha ubaridi.
:A S cry::A S cry:

Taarifa hizo zinasema kuwa amenguka akiwa katika harakati za kuonana na Daktari, akiwa amesindikizwa na baba yake mzazi.

Wasaimon alijiunga na jamvi 6.10.2010.

Binafsi nilikuwa nafahamiana sana na wasaimon, alikuwa ni mtu wa kutoa ushauri wa hekima sana kuhusiana na maisha ya miaka hii, na alikuwa mpiganaji asiyechoka, akitumikia kampuni mojawapo ya Tours mjini Arusha. Naelekea msibani, nitawajuza kinachojiri.
wasaimon alivinjari hapa majukwaani hadi juzi 14.01.2012, na naambiwa kuwa hadi jana alikuwa mzima wa afya.
Ameacha Mke na watoto 3.

Mungu Ilaze Roho ya Marehemu wasaimon Mahala Pema Peponi.


Ama kweli sisi tu wasafiri tu! Hebu fika eneo la tukio utujuze yanayoendelea kwa ujumla! Ila kupitia mtandao inaonekana ni tarehe 14/01/2013
 
Poleni sana ndugu jamaa na marafiki mungu awape nguvu kwenye kipindi hiki kigumu cha majonzi.
 
So sad ameacha mke na watoto 3, aise imeniuma sana kwani walikuwa bado wanhitaji sana kuwa na Baba yao Mungu awape ujasiri wa kukabiliana na hali hii.
 
Ciku zote tunatamani maisha mazuri ya baadae ambayo tumeahidiwa na Muumba wetu.. Japo miili yetu haiko radhi lakini roho ciku zote i radhi.. Mwenzetu ametangulia kwenye maisha mazuri tulioahidiwa.. Hatuna budi kumshukuru Muumba wetu kwa kutupa nafaci ya kuishi pamoja na mwenzetu.. Tunasema mapenzi yake Muumba yametimizwa..

Muumba na awape mioyo ya ustahamilivu na awape nguvu familia ya marehemu..
poleni sana wafiwa.. Poleni sana wana Jamii Forums..

Bwana alitoa.. Na Bwana ametwaa.. Jina la Bwana na lihimidiwe..
 
Back
Top Bottom