TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

TANZIA: Afisa wa TAKUKURU auawa

John_mwanamme na Bhoke alikuwa mwanamke hakukuwa na kitu chochote kweli hapo? Kama kweli John alipiga risasi hewani bahati mbaya bhoke aliaamka na kumpiga kichwani mmmmmmhhhh i cant buy that.....
 
Kwamba sasa afisa wa TAKUKURU Bhoke Ryoba ameuawa na "watu wasiojulikana" mbele ya kadamnasi ya watu inaendeleza kile ambacho wengine tumekisema kwa miaka sita sasa - kuna tatizo la msingi la muundo na utendaji katika Usalama wa Taifa.

Ninakumbushia tu.

Mwanakijiji ndugu yangu, let us live in the real world. Sidhani kama kuna maana yoyote kuanza kulalamika sana au kukumbushana kitu kama hiki. It is the way of life in Tanzania now, mwenye nguvu ndiye mwenye haki,

KUna wakati kelele nyingi zilipigwa kuhusu Ulimboka, hakuna lolote lililofanyika? members hapa JF walisema la ulimboka si la mwisho, litakuja lingine, mtu atauawa hakuna hatua itakayochukuliwa na maisha yataendelea.

Kwa sasa ukitaka kuwa safe Tanzania ujitahidi kuwaunga mkono mafisadi, ukijifanya unafanya kazi ya Takukuru, yaani kupambana na rushwa ujue kuwa unatafuta kifo.

Kilichopo hapa ni kwamba tuombe Mungu waanze kuuana wenyewe kwa wenyewe, la sivyo Ulimboka, Ryoba, etc etc etc wataendelea kupotea mmoja baada ya mwingine.
 
HabariLeo

John anadaiwa kumuua mfanyakazi mwenzake, Bhoke Rioba saa tisa usiku wa kuamkia jana katika ufukwe wa Kigamboni katika eneo la Southern Sun wilayani Temeke wakiwa katika sherehe ya kuaga wenzao waliopata uhamisho kwenda mikoani.

Wote ni maofisa uchunguzi. Chanzo chetu cha habari kimeeleza kuwa John alimfyatulia risasi ya kichwa Bhoke ambaye alifia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alikokimbizwa kwa matibabu.

Kwa sasa kwa mujibu wa taarifa hiyo, John anashikiliwa na Polisi Chang’ombe baada ya kufanya mauaji hayo na mwili wa Bhoke umehifadhiwa Muhimbili.

Akisimulia kisa cha mauaji hayo, mtoa habari wetu alidai kuwa wafanyakazi hao wakiwa katika ufukwe huo usiku saa tisa; baadhi wamelala na wengine wamekaa katika kusherehekea, walivamiwa na vibaka. Mtoa taarifa huyo alidai baada ya kuvamiwa na vibaka, John alitoa bastola yake kwa nia ya kupiga juu ili kuwatawanya vibaka hao ambao haikufafanuliwa walikuwa wangapi, lakini kwa bahati mbaya Bhoke aliyekuwa amelala, aliamka ghafla na risasi ikampata kichwani.

Ofisa Habari wa TAKUKURU, Doreen Kapwani alithibitisha kutokea kwa kifo hicho huku akigoma kueleza kwa undani kuhusu tukio hilo kwa madai kuwa Polisi inafanya uchunguzi, Kapwani alisema utaratibu wa mazishi ya Bhoke unafanywa na familia yake inayoishi Kigamboni.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo akizungumzia tukio hilo alisema, “Taarifa ya tukio hilo tunayo na mtuhumiwa wa mauaji alijisalimisha mwenyewe Polisi na bado tunamshikilia kwa uchunguzi.”

Kwa mujibu wa Kiondo, mauaji hayo yalitokea kati ya saa moja na saa mbili usiku ufukwe wa Kigamboni ambako mtuhumiwa na marehemu walishiriki na wenzao kwenye masuala ya kijamii, “Walikuwa kwenye kufurahi kijamii, si shughuli ya kiofisi, walikwenda kwa gari ndogo binafsi ambayo bado namba za usajili hatujazipata, katika kufurahi huko ndipo John alipiga risasi na kumpata Bhoke katika jicho la kushoto,” alisema.

Kamanda Kiondo alisema Bhoke alipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili usiku huo kwa matibabu, lakini baadaye alifariki akiwa hospitalini hapo na mwili umehifadhiwa hapo.

Kiondo alisema Polisi inachunguza sababu za John kupiga risasi kutokana na tukio hilo kutawaliwa na utata. Takukuru na Polisi wamekanusha kuhusu kuwepo kwa uhusiano wa kimapenzi baina ya wahusika hao wawili.
Source: Afisa wa TAKUKURU apigwa risasi na kufa - wavuti.com

Hapa inaonekana kama ni kweli kulitoke vibaka, uzoefu wa utumiaji wa silaha ulikua mdogo,
My take! Watu wengi sasa wanapenda kila mmoja ajihami na awe na bastola lakini je mafuno ya matumizi ya hizi bastola wanayajua?
 
Usalama wa Taifa jukumu lao ni kuhakikisha CCM inashinda kwa kishido na kuvishughulikia vyama vya upinzani na wapinzani. Kukiwa hakuna mawazo tofauti kila mtu anasema kidumu chama cha mapinduzi hapo usalama unakuwa umetekeleza majukumu yake barabara. Kama Bhoke Ryoba alikuwa na dalili za kupinga pinga mambo fulani fulani ndiyo anashughulikiwa ipasavyo.Wakati wasiojua majukumu ya usalama wa Taifa wanalaumu, wanaoyajua majukumu yao wanawatuza. Kibe, kama napotoka nifafanulie tafadhali ukibainisha bayana wapi nimekosea kwa mifano maana mimi ni mgumu sana kuelewa. Wakati taarifa waliponusa hali ya hatari Arusha wakafa watu watatu, Morogoro akafa mtu mmoja Iringa akafa mwandishi wa habari, hata RPC Mwanza Usalama wa Taifa ulifanya kazi nzuri sana maana waliona kabla na kutahadhalisha.
sijui kama unafahamu majukumu ya usalama wa taifa.au ili mradi nawe umeweka topic leo
 
Tatizo si katika usalama wa Taifa tu, bali ni system nzima ya kuanzia Ikulu! Na hili linatokana na ukweli kuwa kila mtu anajiona ni kiongozi mwenye amri mahali alipo.

.
Itakuwa ni demokrasia imekua ama ni vurugu inayotokana na udhaifu wa kiongozi mkuu?
.
 
mtanzania newspaper

Ofisa wa TAKUKURU amuua mwenzake Dar
Jumatatu, Desemba 24, 2012 03:43 Na Christina Gauluhanga, Dar es Salaam

*Walikuwa kwenye sherehe, akamtwanga risasi jichoni
*Alipomaliza kuua, akajisalimisha kituo cha polisi
OFISA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Makao Makuu jijini Dar es Salaam, Mussa John (34), amemuua kwa risasi ofisa mwenzake, Bhoke Ryoba (32).
Tukio hilo lilitokea juzi usiku wakati wafanyakazi hao pamoja na wenzao, walipokuwa katika sherehe za kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2013.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo, alisema mauaji hayo yalitokea juzi saa 1.30 usiku, katika ufukwe wa Hoteli ya Sourthen Beach iliyopo Kigamboni, Temeke Dar es Salaam.
"Watumishi hao walikodi gari ndogo na kwenda kwenye ufukwe huo, kwa ajili ya kupata vinywaji na chakula. Wakati walipokuwa wakifurahia, ghafla inasemekana John alichukua bastola kisha akampiga Bhoke kwa risasi iliyompata jichoni.
 
mnazungumzia TAKUKURU au USALAMA WA TAIFA? au kila anaefanya kazi Takukuru ni usalama?
 
Kwamba sasa afisa wa TAKUKURU Bhoke Ryoba ameuawa na "watu wasiojulikana" mbele ya kadamnasi ya watu inaendeleza kile ambacho wengine tumekisema kwa miaka sita sasa - kuna tatizo la msingi la muundo na utendaji katika Usalama wa Taifa.

Ninakumbushia tu.

MWANAKIJIJI KWA KUWA UMEJITIA UPOFU NGOJA TUKUPOFUE UPUNGUZE UONGO NA CHUKI ZAKO

Ofisa wa TAKUKURU amuua mwenzake Dar
mtanzania, Jumatatu, Desemba 24, 2012 03:43 Na Christina Gauluhanga, Dar es Salaam
*Walikuwa kwenye sherehe, akamtwanga risasi jichoni
*Alipomaliza kuua, akajisalimisha kituo cha polisi
OFISA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Makao Makuu jijini Dar es Salaam, Mussa John (34), amemuua kwa risasi ofisa mwenzake, Bhoke Ryoba (32).
Tukio hilo lilitokea juzi usiku wakati wafanyakazi hao pamoja na wenzao, walipokuwa katika sherehe za kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2013.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo, alisema mauaji hayo yalitokea juzi saa 1.30 usiku, katika ufukwe wa Hoteli ya Sourthen Beach iliyopo Kigamboni, Temeke Dar es Salaam.
"Watumishi hao walikodi gari ndogo na kwenda kwenye ufukwe huo, kwa ajili ya kupata vinywaji na chakula. Wakati walipokuwa wakifurahia, ghafla inasemekana John alichukua bastola kisha akampiga Bhoke kwa risasi iliyompata jichoni.
"Tukio hilo lilisababisha Bhoke atokwe damu nyingi na wenzake walipoona hivyo, wakaanza kutimua mbio huku na kule.
"Baadaye walimchukua majeruhi na kumkimbiza Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akiwa katika hali mbaya na alifariki dunia usiku wa kumkia jana, wakati akiendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo.
 
Mnaona matatizo ya Chama chenu yamepamba moto mnaanza kuleta mada za ku divert attention nendeni mkaendelee na vikao vyenu vya kufukuzana huko msitake tusahau kwamba bifu ni Zitto na Slaa.
 
Na huyo "afisa" aliyemuua Bhoke "hana akili timamu". Mark this...
 
Kwamba sasa afisa wa TAKUKURU Bhoke Ryoba ameuawa na "watu wasiojulikana" mbele ya kadamnasi ya watu inaendeleza kile ambacho wengine tumekisema kwa miaka sita sasa - kuna tatizo la msingi la muundo na utendaji katika Usalama wa Taifa.

Ninakumbushia tu.

Ofisa wa TAKUKURU amuua mwenzake Dar
mtanzania, Jumatatu, Desemba 24, 2012 03:43 Na Christina Gauluhanga, Dar es Salaam

*Walikuwa kwenye sherehe, akamtwanga risasi jichoni
*Alipomaliza kuua, akajisalimisha kituo cha polisi
OFISA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Makao Makuu jijini Dar es Salaam, Mussa John (34), amemuua kwa risasi ofisa mwenzake, Bhoke Ryoba (32).

Tukio hilo lilitokea juzi usiku wakati wafanyakazi hao pamoja na wenzao, walipokuwa katika sherehe za kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2013.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Temeke, Engelbert Kiondo, alisema mauaji hayo yalitokea juzi saa 1.30 usiku, katika ufukwe wa Hoteli ya Sourthen Beach iliyopo Kigamboni, Temeke Dar es Salaam.

“Watumishi hao walikodi gari ndogo na kwenda kwenye ufukwe huo, kwa ajili ya kupata vinywaji na chakula. Wakati walipokuwa wakifurahia, ghafla inasemekana John alichukua bastola kisha akampiga Bhoke kwa risasi iliyompata jichoni.

“Tukio hilo lilisababisha Bhoke atokwe damu nyingi na wenzake walipoona hivyo, wakaanza kutimua mbio huku na kule.

“Baadaye walimchukua majeruhi na kumkimbiza Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akiwa katika hali mbaya na alifariki dunia usiku wa kumkia jana, wakati akiendelea kupatiwa matibabu hospitalini hapo.

“Kutokana na tukio hilo, mtuhumiwa John alijisalimisha mwenyewe katika Kituo cha Polisi Chang’ombe Temeke, ambako bado anashikiliwa huku uchunguzi zaidi wa tukio hilo ukiendelea. Mwili wa marehemu umehifadhiwa hapo hapo Muhimbili.

“Bado tunaendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hili, ili tuweze kujiridhisha na mazingira halisi ya tukio zima kwani wakati linatokea, hapakuwa na ugomvi wowote.

“Kwa hiyo, tukio linahitaji uchunguzi wa kina tujue namna bastola hiyo ilivyotumika kumpiga marehemu na sherehe hizo zilikuwa zinahusu nini kwani waliohusika ni baadhi tu ya watumishi wa TAKUKURU,” alisema Kamanda Kiondo.

Wakati Kamanda Kiondo akitoa taarifa hiyo, Ofisa Habari wa TAKUKURU, Doreen Kapwani, alitoa taarifa kwa vyombo vya habari jana akithibitisha kutokea kwa mauaji hayo.

Katika taarifa hiyo, Dorren hakueleza kwa undani juu ya tukio hilo, licha ya kusema kuwa uchunguzi zaidi unafanywa na Jeshi la Polisi.

“Tumekuwa tukipokea simu nyingi kutoka kwa watu mbalimbali, wakihitaji kufahamu ukweli kuhusu tukio la kupigwa risasi kwa mtumishi wa TAKUKURU, Bhoke Ryoba.

“Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Dk. Edward Hoseah, anapenda kutoa ufafanuzi kuhusu tukio hili, kwamba ni kweli mtumishi Bhoke Ryoba, amefariki dunia Jumamosi usiku baada ya kupigwa risasi. Uchunguzi wa polisi kuhusu chanzo cha tukio hilo bado unaendelea,” alisema Doreen kwa kifupi katika taarifa yake hiyo.
 
010812.jpg
 
Kwamba sasa afisa wa TAKUKURU Bhoke Ryoba ameuawa na "watu wasiojulikana" mbele ya kadamnasi ya watu inaendeleza kile ambacho wengine tumekisema kwa miaka sita sasa - kuna tatizo la msingi la muundo na utendaji katika Usalama wa Taifa.

Ninakumbushia tu.

Usalama wa Taifa unahusika vipi hapo? Unajuaje labda ugomvi wa mapenzi?

Aliyekwita mwanakijiji hakukosea.
 
Mnaona matatizo ya Chama chenu yamepamba moto mnaanza kuleta mada za ku divert attention nendeni mkaendelee na vikao vyenu vya kufukuzana huko msitake tusahau kwamba bifu ni Zitto na Slaa.

Kumbe ndiyo hivyo sikujua basi mimi ni kichwa cha panzi maana ZZK ni pandikzi la kikwete binafsi na CCM kwa nyuma, na Dr Slaa ni mwiba na ruba inayoiliza CCM hata hivyo mpira dakika 90 yaani Oct 2015.
 
Na mlinzi wa Ultimate security juzi juzi alimvizia mwenzake amelala usiku akamtia kirungu mwenzake akafa na hii nayo lazima USALAMA WA TAIFA wanahusika :becky::becky::becky:

Yaani kuna vioja sana hapa JF hili jukwaa lilishapoteza mwelekeo long time kutokana na watu kama kina mwanakijiji
 
Hapa inaonekana kama ni kweli kulitoke vibaka, uzoefu wa utumiaji wa silaha ulikua mdogo,
My take! Watu wengi sasa wanapenda kila mmoja ajihami na awe na bastola lakini je mafuno ya matumizi ya hizi bastola wanayajua?


Kwanza vibaka walikwenda katika hoteli watu wakiwa macho. Ni vibaka au ni majambazi?

Katika hiyo hoteli hakuna ulinzi wowote?

Walikaa mpaka saa tisa usiku

John (ofisa wa Takukuru) alikuwa na bastola. Kama ofisa wa Takukuru? Raia wa kawaida? kama ni vibaka walikuja kwa shari na walikuwa na silaha hadi ikabidi watishiwe na bastola, au kelele za mwizo zilikuwa zinatosha.

Kwa mnaojua bastola, na matumizi yake...ufanyaji kazi wake..mnaweza kutwambia kama mtu akitaka kupoiga risasi hewani anaweza kukosea na kumpiga mtu kichwani.
 
JK anawaza safari tu,wapi aende,wapi akatambe,hana muda wa kuwajibika wala kuwajibisha mtu...ni mtu wa "mtajiju" flani ivi,so akili kumkinga!
Pole kwa wafiwa wote,Mungu amlaze mahali pema peponi,Amina!!!!!!!
 
Wafanyakazi wa TAKUKURU wanalindwa na Usalama wa Taifa?
 
Back
Top Bottom