Tanzania's Unusual Immigration Case

Tanzania's Unusual Immigration Case

acha uongo dunia nzima inalaani vitendo vya hili kundi kuua,kubaka,kupora mali za wa congomani,kupora madini na maliasili,kama wanasimamia haki ni kwa nini wakina ntaganda wako icc!!!na kuna wengine kibao wanatafutwa!!!!

Tatizo watu kamanyie sio watafiti ilimjue ukweli,hao wanao andika hizo article za kuwafanya M23 Kua wauaji ni hao watu wasiopenda watusi na akina ntaganda kwenda ICC nivisa vya kabila tu akishirikiana na hao wafaransa ili waonejinsi watakavyo waondoa watusi congo,jaribu kufanya utafiti wa kina.
 
mokala 1989 unanichosha mdogo wangu....kwani mtu kwenda anakotaka shida ipo wapi?hata kama ni ------ au msukuma anahaki ya kuhamia nchi yoyote atakayo...balali (R.I.P)si alikuwa(kama kweli alikufa) mmarekani unajua hilo?usiseme hivo brain drain iliyopo huko bongo pekee inatisha achana na watu wanaohama nchi....wewe siyo mahaka kutuhumu Gen James Kabarebe......watutsi ni watu....Tuache ubaguzi

kabarebe ni sehemu tu ya muuaji aliyeuvaa vizuri utusi wake wapo wengine wengi, watusi mnaubaguzi wa hali ya juu sana ! issue ya kabarebe haina uhusiano wowote na brain drain bali ni uuaji uliojawa na uchu wa madini, tamaa ya kutawala wengine, chuki na UBAGUZI DHIDI YA JAMII NYINGINE! Jiheshimu mimi siyo dogo ni mambo ya id tu ni age ya mwanagu wa pili.
 
Nguruvi3,
Sisi si watoto wadogo. Kikwete aliposema wakimbizi haramu akiwa mkoa wa Kagera kila mtu mwenye akili alijua wanaolengwa ni akina nani. Hata kama Waganda 50 wamekumbwa katika msako huo walioathirika zaidi ni Wanyarwanda, hata wale ambao wameishi Tanzania zaidi ya miaka sitini. Sijaona popote pale zoezi la kuwakamata na kuwafukuza Wachina ambao wana madanguro yao Dar-es-Salaam likiendelea, au Wahindi na wapakistan ambao wanaitana na kupeana ajira katika viwanda wanavyoongoza, au wasomali ambao nasikia wamejaa na kununua mashamba Rufiji. Sijaona. Mpaka nitakapoona hivyo, na muda unazidi kwenda, nitaendelea kuamini kuwa Kikwete alilenga Wanyarwanda kwa sababu za kisasi chake tu kwa Kagame.
Mkuu Jasusi zoezi la wahamiaji haramu lilifanyika huko nyuma mwaka 2002 kama sijakosea. Mbona hakukuwa na malalamiko haya? Pili, mbona raia wa nchi nyingine hawalalamika kama Wanyarwanda.

Worse still Wanyarwanda wanasema target ni watusi hivi hapo huoni spinning. Zitto alishawahi kulalamika kuhusu usalama na kusema ni wahamiaji haramu ambao ushahidi ulikuwepo ni kutoka Rwanda na Burundi. Tulipita maeneo hayo tukiwa na polisi na maiti kisa Wanyarwanda wanateka nyara. Hivi hawa viumbe mnawaonea huruma kwa msingi upi? Kwamba sisi tuwe wakimbizi ndani ya nchi yetu ili kumfurahisha mnyarwanda.

Tatu, wengi wana umri wa miaka 30-40 sasa hiyo ya mwaka 60 inakujaje?

Nne, wengi wameoa kwa kutegemea uraia, je ndivyo sheria zinasema?

Tano, wamefika mahali wanapiga kura na wana miliki ardhi badala ya kutafuta ukaazi halali, nani wakaulaumiwa kwa uzembe huo?

Sita, waliambiwa wakae makambini ili baadae wapewe uraia kama wale 160,000 mbona hawakutaka

Saba, mbona tulipotoa uraia kwa wakimbizi 160,000 hatukulalamika kutotendewa haki wasomali na wahindi

Nane, kuna tishio gani kubwa ukilinganisha wapakistan 100 na watu karibia 20,000. Hivi hapo hakuna umuhimu wa kuangalia kipaumbele kweli. Ni kweli sheria ni msumeno na kutofanya haivyo kuna toa picha tofauti lakini picha hiyo iangaliwe kwa ukubwa zaidi. Lini uliona mchina katika jeshi na cheo cha kanali ? Sasa unapoachia mambo yaende tu vipi siku ukisikia Mkuu wa Majeshi ni mhamiaji haramu? Kuna rationale mkuu.

Tisa, kuna sheria gani au haki gani za binadamu zimekiukwa na zoezi hili lilipaswa lifanywaje?

Kumi, je unakubali kuhusu madai kuwa zoezi limewalenga watusi.
Na mwisho MkamaP ameeleza hawa wenzetu wamepata wapi birth certificate ikiwa mzawa hana. Je, hizi kampeni si dalili nzuri kuwa hawa watu i wa kuangalia kwa macho mawili pengine kuliko mhamiaji mwingine.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,

.....Kuna tofauti kati ya kuwa na sheria na jinsi hizo sheria zinavyokuwa administered. ............
kwa wanao-administer.......Wakuuu twende mbele turudi nyuma.......sheria ni sheria tumejiwekea na zingine kuziridhia sisi wenyewe......naona hapa kuna wandugu wanaanza kuzungumza as if hatukutakiwa kuwa na mipaka na as if....kuwa na sheria ni waste of time!!.....really!!.......I'm really shocked!.....hizi ndoto sijui zinatokea wapi.......kama sheria zetu zina kasoro hilo ni jambo jingine...lakini sheria zimewekwa ili ZITULINDE kwa kila hali......thats all!

Ukitaka kujua chuki kutoka baadhi ya watu (nawaita wasio kuwa na ncha ya uchungu kuhusu Taifa letu......since they do not care) ni kama huyo mwandishi wa hiyo makala.....he simply does not care and in my opinion he just throws garbage because he loses nothing!......utaona mtu kama huyu anavyotumia njia mbali mbali kutoa propaganda......who knows!...... he may supported by criminals....wanaoihujumu au wanaotaka kuihujumu nchi yetu.....hivi vitu wala si vigeni.......kwa sisi ambao tumeishi maisha ya mipakani......

Kama tulivyokwishaongelea hili suala katika mada mbali mbali......hili zoezi halijawalenga watu wa nchi fulani na wala si mara ya kwanza kwa Tanzania kufanyika kwa hili zoezi......its just so happened wakati kuna kutokuelewana lugha baina ya viongozi wa nchi mbili....then wapuuzi kama huyo mwandishi wanataka kutumia upenyo huo kutimiza haja zao chafu dhidi ya nchi yetu......very sorry we will enforce our law at any time "t" and whenever we feel so doing......and in so doing kuna kasoro zitakuwepo....na..wenye shida kama huyo mzee.........wawasiliane na balozi zetu ili suala lao lishughulikiwe........

....nina ndugu zangu walipelekwa Uganda katika zoezi kama hili huko miaka ya nyuma (not this year) na through that route.....walirudi nchini.......

Wandugu ....mwenzenu hivi nazungumzia hili zoezi sio kwa kusoma magazetini na mitandaoni.....ni vitu ambavyo nilishawahi kuvi-face (kwa baadhi ya ndugu zangu) na nina first hand experience.......

Kule mipakani Maafisa Uhamiaji wa nchi husika wanawasiliana........and these people (wahamiaji haramu) are being processed......hivyo kama kuna kasoro kama hizo taarifa hurudishwa kwa Uhamiaji kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa vielelezo.....na makao makuu hushughulikia hayo masuala wakishirikiana na balozi zetu......wakati mwingine hata Task force huundwa kushughulikia hizi issues......yote hii ni pesa yako na yangu zinatumika as a result ya wahamiaji haramu......

Pamoja na kwamba ni kazi ya Waandishi kuandika lakini kazi zao wakati mwingine huingiliwa na "nyongo" zisizo na msingi na Kukimbilia kuandika kwenye magazeti na mitandao kwa nia ya kuichafua Tanzania huku wakificha chuki zao dhidi ya nchi yetu.......

Sisi Tanzania bado....lakini tunaelekea huko kwenye kuwa na vitambulisho vya Taifa......majirani zetu wengine wana vitambulisho vyao......na haya "mazagazaga" ya watu kuulizwa vitambulisho vyao barabarani kwenye hizo nchi wala sio jambo la ajabu....na kama huna.....kuna sheria zake na zitachukuliwa dhidi yako...deportation ikiwa mojawapo......

Nawapongeza Uhamiaji na vyombo vingine vya dola vinavyohusika na utekelezaji wa kuondoa wahamiaji haramu nchini kwa kutumia uzoefu pale inapobidi......kwani sio siri bila vitambulisho halali vya Taifa kazi yenu ni ngumu....na hata kama kuna kasoro........mnajitahidi sana cases ni chache.......
 
Hivi, wewe kwa akili zako timamu unaweza kulaani kabila zima au jumuiya nzima kwa vitendo vya wachache? Kwa sababu Ntaganda yuko ICC basi Watusi wote au wanyarwanda wote wenye asili ya kitutsi ni guilty? Mkimaliza kuwahukumu Wanyarwanda mtageukia akina nani tena? Kwa sababu dhambi ya ubaguzi wa kikabila ni kama kula nyama ya mtu.

angalia jibu langu vizuri mimi nimesema kundi la m23 sijasema kabila lote!!!!!
 
Tatizo watu kamanyie sio watafiti ilimjue ukweli,hao wanao andika hizo article za kuwafanya M23 Kua wauaji ni hao watu wasiopenda watusi na akina ntaganda kwenda ICC nivisa vya kabila tu akishirikiana na hao wafaransa ili waonejinsi watakavyo waondoa watusi congo,jaribu kufanya utafiti wa kina.
kama hilo kundi ni la kutetea watu ni kwa nini kila mtu anakana kuhusika nalo si rwanda,si uganda!!!ni kwanini taasisi za haki za binadamu wanalituhumu kwa mauaji ya kimbari!!!! Ni kwanini jumuiya ya kimataifa inawatafuta viongozi wake!!!!!
 
Ogah hakika mimi sielewi kwanini watu wnakubali hizi spinning za wahamiaji haramu.
Sheria zipo na kutojua sheria hakutoi msamaha kwa mtu.

Mtu ameingia na kuamua kununu au kupora kkiwanja, akazaa watoto kama 'human shield' leo sheria inapomhukumu mhalifu huyo sheria hiyo inageuka kuwa mbaya, very strange!

Kenya wana kitu inaitwa kipande, (piece of ID) kama huna hiyo wewe unalako tu. Sisi tupo katika process eti bado watu wanataka watu 20,000 wahamiaji haramu wapewe vitambulisho ili kuwafurahisha wananchi wa nchi zingine! very strange

Kuzaa watoto si sehemu ya sheria za uhamiaji na aliyekiuka ni mhalifu mkubwa tu.
Kuhamia miaka 20 si sehemu ya uhamiaji kama umezamia, mzamiaji ni mhamaiji haramu tu.

Hatuwezi kuwa wakimbizi ndani ya nchi yetu. Wananchi wa Kagera wameteseka sana. Nimeshuhudia haya.
Ogah watu walionya kuwa kusafiri na mzigo wa maiti kuna Wanyarandwa.

Watu wana maiti wanafikiria kuizika porini kwasababu hali inakuwa mbaya kwasababu tu wahalifu wa Kinyarwanda na nchi za jirani wameamua kuvuna mali kwa mateso ya watanzania, bado tunadhani hawa ni wanadamu wema kabisa.
Inasemwa wazi, kuna wahalifu wa Rwanda wapo na wanatesa watu, leo tunaona kama raia wema. Jamaani!

Kama tutatoa fursa kwasababu wamezaa basi tuachie majambazi yaliyoko magereza kwasababu nayo yana watoto na sheria inatoa msamaha kama kwa wahalifu hawa.

Lazima ifike mahali tuwe na uchungu na taifa letu na watu wetu. Kuwatelekeza wananchi wa Kagera ili kuwafurahisha raia wa kigeni ni moral decay ya hali ya juu. Kwanini mtu wa Kagera aishi kwa mashaka na hofu kwa katiba ya JMT, wakati huo huo sheria zinazotokana na katiba hiyo zimtetee mhalifu. Please!

Kwanza walitakiwa wafikishwe mahakamani kama wasomali na waethipoia, baada ya hapo kwao.
Eti mhalifu anadai hakupewa nafasi ya kuaga nyumbani, wakati anakuja kwa njia za panya alipiga hodi.

Kibaya zaidi wao wamegeuza hii issue na kuwa Wanyarwanda, hali warundi, wakongo n.k. wameondolewa pia.
Sasa wanaipaka matope Tanzania kwa neno target Watusi, hivi hawa wana jema na nchi yetu kweli.
Tuache tu wawe makanali na wakuu wa majeshi kwasababu sisi ni watu wema sana kwa majirani zetu! please please.

Sheria ifanye kazi, kama kuna aliyesalimika naye ichukue mkondo wake lakini hakuna sheria inayotoa msamaha kwasababu mbona fulani hajahukumiwa! hakuna sheria inayotoa msamaha kwa kutoijua.
 
What are we becoming as a people? Mtu anafukuzwa tu kwa kutizama urefu wa pua yake na wembamba? Kikwete is a national disgrace.

....tunasema hiviii.......hilo ni kosa.....kwani HAKUNA sheria ya nchi yetu inayobainisha kuangalia maumbile ya mtu ili kujua Utaifa wake........however......Maafisa Uhamiaji pamoja na makosa madogo madogo....wao SIO wapumbavu...na kwenye zoezi hili wanashirikiana na watu wazoefu sana.......kwani wakati mwingine unaweza kuwa deceived na makaratasi feki.......ambayo ni mengi.......kuna technic nyingi zinatumika kufanya kazi ya utambuzi.....wewe mzee mwenzangu utakuwa unafahamu hilo......lakini technic hizo wakati mwingine hukosea na kuumiza.........na vilevile wakati mwingine still inakula kwetu i.e. watu huponyoka.......well tunajifunza.....na makosa pole pole hurekebishwa!

....on another note...... wewe ni Mkuu "Jasusi".....bila hiyana yeyote.....hivi una habari ni kwa jinsi gani passport zetu....zinatumika na watu siyo!!......well unaweza kusema "hilo ni tatizo letu na system yetu mbovu...na hivyo tusionee watu"......well kwenye hili zoezi kuna watu special trained wa kutambua watu wa aina hiyo...na matatizo kama hayo........hivi hujawahi kukerwa pale Mlangoni Airport DIA unapotoka unakutana na vijana wakaomba kukagua passport yako?.......
 
Hawa wamekuja baada ya mwaka 1996. Mwaka 1996 wanyarwanda warirudishwa rwanda na burundi. Nakumbuka enzi hizo walikua wana amuru kuimba hata ubeti mmoja wa wimbo wa taifa ama wa tanzania tanzania. Hawa waliopo sahizi ni wajuzi juzi tu, na nifikiri si kweli wanatumia hiyo creteria ya urefu kwani hakuna watanzania warefu? wanaorudishwa ni wahamiaji kweli kweli, sema kuna mapungufu kwa wale walio olewa na kuolewa, lakini majority ni wahamiaji haramu.

Na je umesikia katika walalamishi kwamba yeye ni msukuma, ama mhaya ama mkwele? Tanzania hatuna kabila la wahutu ama watusi. Hivyo yoyote ambaye hajaolewa ama kuoa mtanzania na hana karatasi ni mhamiaji haramu.

Birth certificate, zilikua hazitolewi mahospitalini mtu alipokua anazaliwa kwa sehemu kubwa sana ya Tanzania na tena huko ngara,karangwe na b,mulo zilikuwa hazitolewi kabisa na ilikua haiwezekani kuipata labda kama unataka kujiunga na jeshi,polisi ama chuo. Sasa hao wenye nazo wamezipata lini waweke copy kwenye mtandao. Eti kisingizio zimechukuliwa, wote wamenyang'anywa hata wale waliopitia porini na ng'ombe zao?

MkamaP......heshima mbele sana.....

....Mkuu kuna birth certificates feki nyingi sana......kule vyuoni na sehemu nyingine serikalini watu kibao walikutwa na vyeti bandia vya kuzaliwa.....now you can imagine how many passport ziko kwenye mikono ya wasio......Passport ni mali ya serikali ya Tanzania.....Afisa mwenye mamlaka wa Uhamiaji anaweza kui-demand wakati wowote kwa ajili ya investigation ili kujua/ku-establish uhalali wake.......nimeshuhudia watu wakinyang'anywa passport na wakati mwingine kuharibiwa.........

I really feel other people concern about wahamiaji haramu waliopo mijini na kwamba hatushuhudii au atleast wao hawashuhudii wahamiaji haramu hao wakichukuliwa hatua kama wengine kule mipakani......zoezi hili liko kote nchini....however......all I can say here...not only mijini hata kule mipakani RUSHWA kwa maafisa wetu ni rampant......kiasi kwamba......pamoja na mazoezi haya kuendelea....bado kuna wahamiaji haramu wana "sepa".......na wakati mwingine baadhi ya wananchi hushiriki katika vitendo viovu vya kuwaficha.......iko siku sheria itwaangukia hawa culprits........

KInachoombwa na serikali kutoka kwetu ni ushirikiano......sisi wananchi tutoe ushirikiano tuwaumbue wale wahamiaji haramu na pia tuwaumbue wale wananchi wasio waadilifu kwa sheria za nchi yetu..........
 
Habari hii hapa http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/16173-kiama-cha-jeuri-ya-wahamiaji-haramu

Mkoa unatarajia idadi ya watu 52,000. Kwa maana hiyo kulikuwa na sensa iliyokuwa inaendelea chini chini kuwabaini.

Kagera, kigoma na Geita : wahamiaji 1851 wamenaswa wakiwa na magobori 6 na Short gun moja
Kigoma : 885, magobori 2 na Shortgun 1
Geita : wahamiaji 246, gobori 3 na sare za JWTZ na kibuyu cha maji.
Kagera : wahamiaji 750, gobori 52, shortgun 10

Wahamiaji na majambazi wametakiwa kusalaimisha silaha zao.
Nchimbi amesema wahamiaji waondoke na ngo'ombe wao bila kunyang'anywa
Kanali masawe anasema waliotenganishwa na familia warejee ili kupewa kibali cha muda wakisubiri uraia.

My take
Hawa watu wanaosemwa ni masikini wamkeja kusalimisha maisha, hivi wanabeba magobori na short gun za nini?
Mkoa wa Kagera tu zimekamatwa short gun 10 ambazo ni ka platoon ka jeshi la msituni.

Kwa hesabu ya haraka hadi sasa zimekamatwa silaha kwa idadi hii
Short gun =11
magobori = 64

Unaweza kwenda nwilaya nzima ya Muheza usipate idadi hiyo ya silaha. hawa wenzetu ambao si rai wamekuja na silaha nyingi za nini? Hivi hapa kuna huruma ya nini jamani. Fikiria silaha hizo zimetoa roho Watanzania wangapi na kwanini tuone ni halali Wenye nchi kunyofolewa roho zao na wahamaji haramu.

Idadi ya 52,000 inahitaji kituo cha afya kwa mujibu wa takwimu za kitabibu Tanzania. Wtahitaji waganga na manesi, watahitaji shule zaidi ya 20, watahitaji huduma za afya. Kumbuka hawa hawajulikani kama wapo katika idadi ya wananchi. Hii maana yake ni kutumia resource zetu kuwaumiza raia wetu wanaolipa kodi kwa mujibu wa katiba ya JMT kwa hisani ya wahalifu wasiofuata sheria. Hivi hili linahitaji mjadala zaidi.

Wakati wakitumia resource zetu wao wanajitapa kwao wana maendeleo. Kwamba Tanzania ni shamba la bibi la kulea watu wa mataifa mengine. Jamani hili hatulioni?

Hivi huyu anayesema ametenganishwa na mkewe na watoto, short gun aliitumia wapi na kwa kibali gani. Ni raia gani wa Tanzania anayemiliki short gun. Hili hatulioni kama tatizo tunataka kuwafurahisha wahalifu wakubwa.

Mtu gani anayetafuta hifadhi akiwa na short gun, huyu alikuja mwaka gani? maaana mwaka 1959 hazikuwepo Tanzania na kama zilikuwepo zilikuwa 'strong room'. Tunaambiwa walikuja mwaka 1959 nasi tunaitikia bila chembe ya fikra. Silaha za nini wanabeba hawa kama si kujiandaa na vita?

Watu hawajui kuwa Goma ilianza hivi hivi wkafikia malaki sasa wanataka kujitenga. DRC inalipa gharama kwa ujinga tunaotaka kuutetea au kuulea. Hawa ni wahalifu wakubwa halafu tunawapa huruma, please give me a break!
 
Nipo eneo la Oparesheni mkoa wa Kagera...hao wanaodai kuwa wanaporwa mifugo, ardhi na kuteswa ni waongo sana. Kabla opareshen haijaanza, mkuu wa Opareshen mkoa wa Kagera alitoa angalizo kwa wote watakaokuwa frontline.

Katika kutekeleza hilo, askari hao walitakiwa kuzingatia haki za binadamu, kutowasumbua raia wa Tanzania wenye asili ya Rwanda, kutotenganisha ndoa baina ya Mtz na mgeni, kuhakikisha mali za mhamiaji zinalindwa na mambo mengine yenye kuzingatia haki na utu wa mtu. Alitishia kwamba atakaye kwenda kinyume atafukuzwa kambini na kazi pia.

Nipo hapa nikiwa mmoja wa wanaofuatilia kuwa haki inatendeka, na hadi sasa hakuna tukio la ukiukwaji wa haki za binadamu.

Hao wanaolalamika ni namna ya kutafuta huruma za vyombo vya habari. Kwa taarifa yenu ni kwamba, raia wa Rwanda ndio wanaoongoza kwa kuwa wahamiaji haramu kwani wakisha ingia nchini wanamalizana na viongozi wa vijiji basi kwao ndio wameahakuwa raia wa Tanzania. Sheria ya Uraia Tanzania haisemi kwamba ukiiishi nchini kinyume cha sheria kwa miaka 40 utakuwa umeshakuwa raia. Hii ndio inaowatafuna baadhi ya wanyarwanda. Kagera bila wahamiaji haramu inawezekana
 
BINADAMU WOTE NI NDUGU ZANGU NA AFRIKA NI MOJA! hiyo ni dhana ya TANU, na imejengwa katika msingi wa UMAJUMUI, PAN AFRICANISM. tokea ilipotokea JENERALI ULIMWENGU, pamoja na jamaa wengine kadhaa, kutangazwa kuwa si raia, na wakaondoloewa hadhi zote walizokuwa nazo wakati ule, niliona kwamba Tanzania imechukua mwelekeo wa hatari. kwamba kuna idadi kubwa tu ya watu ambao URAIA wao una mashaka, lakini hawasumbuliwi kwa sababu? - NI WENZETU! Hoja kubwa iliyotumika hapo ni msimamo wa Jenerali Ulimwengu, au tuseme uhusiano wake na SYSTEM. Alipoanza kuandika mambo yanayokosoa SYSTEM, tayari akawa KANYEA KAMBI. lakini tunaweza kujiuliza, hiyo criticism yake ilikuwa na maslahi kwa taifa? ni kweli alikuwa anawanyima raha watu binafsi - lakini si taifa. Suala la uraia tokea hapo limekuwa likitumiwa kama fimbo ya kuwapiga watu fulani wanaoonekana "kuleta shida". na haishangazi katika mazingira tuliyonayo, ya kutamalaki kwa ufisadi, wizi, rushwa, ulafi (greed), unyanyasaji na uonevu, basi kuendesha zoezi kama hili la "kusaka wahamiaji haramu" lazima watu watatia ajenda zao za ulaji na wizi. Suala hili ni nyeti, linahitaji umakini, kuzingatia sheria inasemaje, haki za binadamu, lakini juu ya yote ukweli kwamba sisi ni waafrika, tumegawanywa tu kwa sababu za mahitaji ya wakoloni. hatulazimiki kujigawa kufuata ukoloni ulivyotugawa. tuanzishe taratibu zetu. kama ni ujambazi, ushugulikiwe kama ujambazi kwa taratibu za kudumu, siyo operesheni kama hizi zinazoendana na uporaji, wizi, unyanyasaji, na kuonesha jinsi tulivyofilisika kifikra na kifalsafa
 
Tusitafute mchawi hapa. Hawa wahamiaji haramu,regardless wameloea hapa nchini kwa muda gani,they must go back to their country of origin. Tusiwalee wahamiaji haramu kwa kisingizio rahisi kama hiki. Tanzania isigeuzwe kuwa shamba la bibi. Watanzania halisi wanakosa ardhi ya kuishi huku ardhi yetu imekaliwa na wavamizi.
 
habari hii hapa http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/16173-kiama-cha-jeuri-ya-wahamiaji-haramu

mkoa unatarajia idadi ya watu 52,000. Kwa maana hiyo kulikuwa na sensa iliyokuwa inaendelea chini chini kuwabaini.

Kagera, kigoma na geita : Wahamiaji 1851 wamenaswa wakiwa na magobori 6 na short gun moja
kigoma : 885, magobori 2 na shortgun 1
geita : Wahamiaji 246, gobori 3 na sare za jwtz na kibuyu cha maji.
Kagera : Wahamiaji 750, gobori 52, shortgun 10

wahamiaji na majambazi wametakiwa kusalaimisha silaha zao.
Nchimbi amesema wahamiaji waondoke na ngo'ombe wao bila kunyang'anywa
kanali masawe anasema waliotenganishwa na familia warejee ili kupewa kibali cha muda wakisubiri uraia.

My take
hawa watu wanaosemwa ni masikini wamkeja kusalimisha maisha, hivi wanabeba magobori na short gun za nini?
Mkoa wa kagera tu zimekamatwa short gun 10 ambazo ni ka platoon ka jeshi la msituni.

Kwa hesabu ya haraka hadi sasa zimekamatwa silaha kwa idadi hii
short gun =11
magobori = 64

unaweza kwenda nwilaya nzima ya muheza usipate idadi hiyo ya silaha. Hawa wenzetu ambao si rai wamekuja na silaha nyingi za nini? Hivi hapa kuna huruma ya nini jamani. Fikiria silaha hizo zimetoa roho watanzania wangapi na kwanini tuone ni halali wenye nchi kunyofolewa roho zao na wahamaji haramu.

Idadi ya 52,000 inahitaji kituo cha afya kwa mujibu wa takwimu za kitabibu tanzania. Wtahitaji waganga na manesi, watahitaji shule zaidi ya 20, watahitaji huduma za afya. Kumbuka hawa hawajulikani kama wapo katika idadi ya wananchi. Hii maana yake ni kutumia resource zetu kuwaumiza raia wetu wanaolipa kodi kwa mujibu wa katiba ya jmt kwa hisani ya wahalifu wasiofuata sheria. Hivi hili linahitaji mjadala zaidi.

Wakati wakitumia resource zetu wao wanajitapa kwao wana maendeleo. Kwamba tanzania ni shamba la bibi la kulea watu wa mataifa mengine. Jamani hili hatulioni?

Hivi huyu anayesema ametenganishwa na mkewe na watoto, short gun aliitumia wapi na kwa kibali gani. Ni raia gani wa tanzania anayemiliki short gun. Hili hatulioni kama tatizo tunataka kuwafurahisha wahalifu wakubwa.

Mtu gani anayetafuta hifadhi akiwa na short gun, huyu alikuja mwaka gani? Maaana mwaka 1959 hazikuwepo tanzania na kama zilikuwepo zilikuwa 'strong room'. Tunaambiwa walikuja mwaka 1959 nasi tunaitikia bila chembe ya fikra. Silaha za nini wanabeba hawa kama si kujiandaa na vita?

Watu hawajui kuwa goma ilianza hivi hivi wkafikia malaki sasa wanataka kujitenga. Drc inalipa gharama kwa ujinga tunaotaka kuutetea au kuulea. Hawa ni wahalifu wakubwa halafu tunawapa huruma, please give me a break!

watanzania tujiulize :viongozi wa magamba walikuwa wapi mpaka hali ikafikia kiwango hiki????
nadhani walikuwa wanawatumia kuwapigia kura!!!!magamba jamani we acha tu.!!!!
 
binadamu wote ni ndugu zangu na afrika ni moja! Hiyo ni dhana ya tanu, na imejengwa katika msingi wa umajumui, pan africanism. Tokea ilipotokea jenerali ulimwengu, pamoja na jamaa wengine kadhaa, kutangazwa kuwa si raia, na wakaondoloewa hadhi zote walizokuwa nazo wakati ule, niliona kwamba tanzania imechukua mwelekeo wa hatari. Kwamba kuna idadi kubwa tu ya watu ambao uraia wao una mashaka, lakini hawasumbuliwi kwa sababu? - ni wenzetu! Hoja kubwa iliyotumika hapo ni msimamo wa jenerali ulimwengu, au tuseme uhusiano wake na system. Alipoanza kuandika mambo yanayokosoa system, tayari akawa kanyea kambi. Lakini tunaweza kujiuliza, hiyo criticism yake ilikuwa na maslahi kwa taifa? Ni kweli alikuwa anawanyima raha watu binafsi - lakini si taifa. Suala la uraia tokea hapo limekuwa likitumiwa kama fimbo ya kuwapiga watu fulani wanaoonekana "kuleta shida". Na haishangazi katika mazingira tuliyonayo, ya kutamalaki kwa ufisadi, wizi, rushwa, ulafi (greed), unyanyasaji na uonevu, basi kuendesha zoezi kama hili la "kusaka wahamiaji haramu" lazima watu watatia ajenda zao za ulaji na wizi. Suala hili ni nyeti, linahitaji umakini, kuzingatia sheria inasemaje, haki za binadamu, lakini juu ya yote ukweli kwamba sisi ni waafrika, tumegawanywa tu kwa sababu za mahitaji ya wakoloni. Hatulazimiki kujigawa kufuata ukoloni ulivyotugawa. Tuanzishe taratibu zetu. Kama ni ujambazi, ushugulikiwe kama ujambazi kwa taratibu za kudumu, siyo operesheni kama hizi zinazoendana na uporaji, wizi, unyanyasaji, na kuonesha jinsi tulivyofilisika kifikra na kifalsafa

warudi kwao banaaa.hajamaliza kunya.???????????????
 
Gazeti la The East Africa limepoteza credibility kwasababu ya kutofanya uandishi wa kisomi bali kushabikia tu. Jk hakusema Wanyarwanda, alisema wahamiaji haramu. Ilikuwa ni juu ya mhariri kujitridhisha na madai ya msemaji au kuyaweka sawa na si kushabikia.

Tumeona makala nyingi zinatoka Kigali na zile za Nairobi ni kuongeza chumvi.
Nalipenda gazeti hili lakini limepoteza credibility sana.
Wamepoteza credibility kwa kuwa wamekuwa infiltrated. serikali ya Rwanda ina fungu maalum (special fund) kwa ajili ya PR na propaganda. Fungu hili linatumika kulipa international PR agencies ku-engineer habari, interviews na mengineyo ili kuipotray Rwanda in the positive light.
Ndio maana hata kwenye website ya the East african kuna link maalum pale juu kwa ajili ya Rwanda tu, hakuna nchi nyingine. kuna watu kama Andrew Mwenda ambao wanalipwa moja kwa moja na serikali ya Rwanda kupitia akaunti za siri uingereza. ushahidi ulishaonyeshwa hapa, kuna waandishi wetu Bongo wanalipiwa mpaka tripu kwenda Rwanda, congo, na mmoja alifanya interview na M23 na kuwatetea. Unakumbuka uchaguzi uliopita wa Rwanda tulivyopigiwa propaganda kwenye TV moja hapa nchini? hiyo ndio kazi ya hilo fungu. kama waandishi wetu wangekuwa makini wangeandika juu ya viongozi wa upinzani waliochinjwa, waliopigwa risasi, waliofungwa n.k badala yake tukaonyeshwa eti kagame anaendesha gari mwenyewe!
 
Acheni roho mbaya hiyo,mnachotaka nikupora mali zao tu,fikiri hawa munaofukuza nikixazi cha wakimbizi walio ingia tz 1959 nawengi wa wazazi wao wameisha kufa wamezaliwa tz hawajui rwanda na wala hawana ardhi ya kuishi rwanda kwani baada ya kufukuzwa rwanda ardhi zao zilichukuliwa na wahutu,wewe kumfukuza nikama kukufukuza wewe mwenyewe uende nchi ambayo huijui,fikiria hali hiyo,wanasema kabla hujatendea mtu kitu kibaya anza kwanza ujiweke mahala pake.

Wayahudi waliohamia Misri miaka mingi kabla Yesu hajazaliwa (BC) wanarudishwa kwao Israel leo hii, sembuse hawa Wanyarwanda waliohamia Tanzania majuzi tu (18th Century)? Lazima warejee makwao. Tanzania sio shamba la Bibi wala Babu!
 
Yaani leo kwa sababu inawahusu wanyarwanda ndio tunaona vyombo vyetu vya dola kuwa paragons of fairness! Hao ambao kila kukicha tunawasakama kwa kuwaonea wananchi, kwa kutumia nguvu kupita kiasi n.k. tukiambiwa kuwa vitendo hivyo hivyo vinafanywa dhidi ya wanyarwanda tunadai ni spinning. Tuna tofauti gani na wajerumani na makaburu ambao mara tu ya tawala zao dhalimu kuanguka wakapata collective amnesia.
Hivi kweli, mpenda haki, unaweza kusimama na kusema kumuweka mtu katika makambi ya wakambizi kwa zaidi ya miaka 10 ni haki! Ati kwa sababu sheria inasema hivyo. Mbona humu humu hatusiti kuzipinga hizo sheria pale tunapoona kuwa ni za kionevu.

Unadai, Mkuu, kuwa hawa jamaa wameoa au kuolewa na watanzania kwa sababu moja tu ya kujipatia uraia. Sasa kama hiyo ni sababu kwa nini hao unaowaita wahalifu wakubwa hawakupeleka vyeti vyao vya ndoa kuomba uraia? Mnasema kuwa haiwezekani wakaweko wahamiaji waliokuja hata kabla ya uhuru kwa sababu ati waliisharudshwa wote na wengine walipewa uraia. Kama hivyo ni kweli mbona wakina Jenerali Ulimwengu walilazimishwa kuomba uraia? Hamuwezi kusema kuwa kwa sababu wakimbizi warundi 160,000 waliowasili miaka ya 70 walipewa uraia basi hakuna ambao waliachwa. Tunasahau kuwa waliopewa uraia ni wakimbizi lakini kuna wengi tu ambao hawakujihesabu kama wakimbizi bali watanzania wenye asili ya Rwanda.

Wengine wenu mnadai kuwa hawa wanyarwanda ndio wanaosababisha ujambazi katika mikoa ya mipakani, conveniently mkisahau kuwa hawawezi kufanya uhalifu huo bila ya kushirikiana na ndugu zenu. Na ukweli ni kuwa hata wakiondoka wote, majambazi na wahalifu kila siku watatafuta njia ya kurudi na kufanya uhalifu. Kibaya zaidi, mtizamo wenu ni kama wale wamarekani wanaosema kuwa ukifunga asilimia 50 ya wamarekani weusi na walatino wote, tatizo la uhalifu litapungua sana. Nanyi mnasema, tukifukuza wanyarwanda wote basi tatizo la ujambazi Kagera litakoma.

Wengine wenu mnalalamika kuwa kwa nini wanyarwanda peke yao wanaolalamika wakati wengine wamekaa kimya. Mnasahau kuwa hili zoezi limefanyika wakati mahusiano kati ya nchi zetu mbili kuwa tete na hivyo kuwafanya waone kuwa wanaadhibiwa kutokana na hali hii. Wengi wenu mlilalama kwa kitendo cha Rwanda kupandisha kodi ya kuingia rwanda kwa magari ya kitanzania na kudai kuwa ilikuwa ni kulipiza kisasi hata pale mlipoambiwa kuwa RRA ilishawasiliana na TRA muda mrefu wakiomba TRA ipunguze kodi inayotoza magari yanayotoka Rwanda ifanane na ile ambao Rwanda inatoza magari ya kitanzania. TRA wakapuuza, Rwanda wakapandisha kodi ifanane na ya TRA, mashabiki mkapiga kelele foul!

Wengine wenu mmewahukumu wanyarwanda kwa kujivuna. Tangu lini kujivuna kumekuwa kosa tosha kumtendea ukatili mwenzio?

Tunachosema wengine hapa ni kuwa hili zoezi timing yake ilikuwa mbaya. Pamoja na timing kuwa mbaya, tunajua kuwa watu waovu wapo watakaotumia zoezi hili kuwaonea wenzao, kuwapora mali n.k. Sasa badala ya kudai spinning, mpenda haki yeyote alitakiwa aumie kuona binadamu wenzake wanateseka hivi na kufanya kila jitihada kuhakikisha kuwa wasio na hatia hawaonewi. Kama nia ni kupunguza ujambazi, tusake majambazi bila kujali yametoka wapi. Kama nia ni kupambana na wahamiaji haramu basi zoezi hilo liwe endelevu na liwahusu wote, wazungu, wahindi, wachina, wanyasa, wajaluo, wamasai n.k. Wakati tukifanya hivyo tuwape nafasi wale ambao wameonyesha nia ya dhati ya kuwa raia wema wa nchi yetu kuanza katika safari hiyo.

Kushangilia wakati watu wanaburuzwa kwa sababu tu ya uasili wao ni xenophobia na si uzalendo kama ambavyo mngetaka wengine tuamini. Tukumbuke kuwa hao tunaowaita wahamiaji haramu ni binadamu kama sisi na ni wachache tu ambao ni wahalifu kama ilivyo kwa wamarekani weusi au ndugu zetu wachaga na wengine wanaokuwa vilified.

Amandla.......
 
Habari hii hapa http://www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/16173-kiama-cha-jeuri-ya-wahamiaji-haramu

Mkoa unatarajia idadi ya watu 52,000. Kwa maana hiyo kulikuwa na sensa iliyokuwa inaendelea chini chini kuwabaini.

Kagera, kigoma na Geita : wahamiaji 1851 wamenaswa wakiwa na magobori 6 na Short gun moja
Kigoma : 885, magobori 2 na Shortgun 1
Geita : wahamiaji 246, gobori 3 na sare za JWTZ na kibuyu cha maji.
Kagera : wahamiaji 750, gobori 52, shortgun 10

Wahamiaji na majambazi wametakiwa kusalaimisha silaha zao.
Nchimbi amesema wahamiaji waondoke na ngo'ombe wao bila kunyang'anywa
Kanali masawe anasema waliotenganishwa na familia warejee ili kupewa kibali cha muda wakisubiri uraia.

My take
Hawa watu wanaosemwa ni masikini wamkeja kusalimisha maisha, hivi wanabeba magobori na short gun za nini?
Mkoa wa Kagera tu zimekamatwa short gun 10 ambazo ni ka platoon ka jeshi la msituni.

Kwa hesabu ya haraka hadi sasa zimekamatwa silaha kwa idadi hii
Short gun =11
magobori = 64

Unaweza kwenda nwilaya nzima ya Muheza usipate idadi hiyo ya silaha. hawa wenzetu ambao si rai wamekuja na silaha nyingi za nini? Hivi hapa kuna huruma ya nini jamani. Fikiria silaha hizo zimetoa roho Watanzania wangapi na kwanini tuone ni halali Wenye nchi kunyofolewa roho zao na wahamaji haramu.

Idadi ya 52,000 inahitaji kituo cha afya kwa mujibu wa takwimu za kitabibu Tanzania. Wtahitaji waganga na manesi, watahitaji shule zaidi ya 20, watahitaji huduma za afya. Kumbuka hawa hawajulikani kama wapo katika idadi ya wananchi. Hii maana yake ni kutumia resource zetu kuwaumiza raia wetu wanaolipa kodi kwa mujibu wa katiba ya JMT kwa hisani ya wahalifu wasiofuata sheria. Hivi hili linahitaji mjadala zaidi.

Wakati wakitumia resource zetu wao wanajitapa kwao wana maendeleo. Kwamba Tanzania ni shamba la bibi la kulea watu wa mataifa mengine. Jamani hili hatulioni?

Hivi huyu anayesema ametenganishwa na mkewe na watoto, short gun aliitumia wapi na kwa kibali gani. Ni raia gani wa Tanzania anayemiliki short gun. Hili hatulioni kama tatizo tunataka kuwafurahisha wahalifu wakubwa.

Mtu gani anayetafuta hifadhi akiwa na short gun, huyu alikuja mwaka gani? maaana mwaka 1959 hazikuwepo Tanzania na kama zilikuwepo zilikuwa 'strong room'. Tunaambiwa walikuja mwaka 1959 nasi tunaitikia bila chembe ya fikra. Silaha za nini wanabeba hawa kama si kujiandaa na vita?

Watu hawajui kuwa Goma ilianza hivi hivi wkafikia malaki sasa wanataka kujitenga. DRC inalipa gharama kwa ujinga tunaotaka kuutetea au kuulea. Hawa ni wahalifu wakubwa halafu tunawapa huruma, please give me a break!

Xenophobia ni hatari kweli! Mzee mzima unapoteza rationale.

Hao majambazi sugu, wanaoteka magari yetu na kuua wananchi wetu wamekutwa na magobole 64 na shotgun 11 katika population ya watu zaidi takriban 2000! Hizo SMG ambazo ndizo silaha of choice za majambazi sugu zikowapi? Hivi wakitusachi sisi tunaoishi maeneo kama hayo hawatatukuta na silaha? Hawa wanakaa katika makambi, katika sehemu ambazo zina wanyama hatari, hivi kweli ni ajabu kuwakuta na magobole na shotgun ambazo ni silaha za uwindaji!

Unapiga hesabu za services ambazo tunatakiwa kuwapa. Uko nchi gani mwenzetu? Mara ngapi hizo huduma zimetolewa huko vijijini kwa kodi yako? Kawaida ni wananchi wanaoishi katika maeneo husika ndio wanaojitolea kujenga madarasa, kliniki n.k. Na kama hawa unaowaita wahalifu wanaishi katika maeneo hayo basi bila shaka watachangia katika ujenzi wa shule na zahanati hizo.

Kwani ni uongo kuwa Rwanda imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo kuliko sisi? Kwani ni uongo kuwa Rwanda wamepiga vita uchafu na ubadhirifu wa mali ya umma kwa mafanikio kuliko sisi. Sasa kwa nini wasisifie walikotoka waliowatangulia? Hiyo nayo kweli ni sababu ya kumfuza jirani yako? Basi baada ya hawa tuwageukie wachaga na wahaya ambao hawasiti kutukumbusha kuwa wameendelea kuliko sisi wengine.

Shotgun si SMG. Kabla ya uhuru zilikuwepo pamoja na magobole ambayo yalitumika sana kuwinda nguruwe mwitu na wanyama wengine waharibifu.

Waliokimbilia Goma ni wahutu ambao walikuwa wakiwakimbia wakina Kagame. Na hawa walianza kuwashambulia wakina Kagame kutoka makambi hayo na sio wananchi wa Kongo. Wakina Kagame wakikumbuka waliyofanyiwa walijibu mapigo kwa kushambulia makambi hayo na kujaribu kuwarejesha Rwanda wale ambao waliwaona kama wanahusika na mauaji ya mwaka 1994. Sasa wewe unataka kutuambia kuwa wakina Kagame watakuja kushambulia Tanzania kwa sababu kuna watutsi wanaishi huku? Hiyo ina mantik kweli?

Mimi nakumbuka kabla hatujaanza hizi siasa za chuki, warundi walikuwa wanadharauliwa sana katika hayo maeneo. Wao walikuwa wa tabaka la chini wakilimishwa n.k. Dhulma yote hiyo tuliona sawa. Leo, wamekusanya kidogo walichovuna na kununua mashamba na mifugo tunataka kuwafukuza ati wanaringa! Ala, kumbe haja yetu ilikuwa ni kuwachuna siku zote na kuwafanya watwana wetu.

Kama nilivyosema hapo awali, hii chuki mnayoiendekeza haiendani na nchi ambayo wengi wetu tunajivunia. Hata muirembeshe vipi, ni xenophobia inayowasumbua.

Amandla......
 
Back
Top Bottom