Tanzanian Lodge Named Best Hotel in The World

Kwa kweli hii lodge ni master piece. Ila kwa mtazamo wangu hii siyo property ambayo mtanzania anaweza kujivunia nayo. Tunaweza kusema nchi inanufaika kwa mapato kutokana na park fees (kuna wakati huko nyuma kulikuwa na mpango wa kuwatoza wageni wanaokaa kwenye lodge hiyo extra park fees kama USD 500 kwa mtu kwa siku baadala ya USD 50 kwa mtu kwa siku), vinginevyo mimi nakerwa sana kuona mbuga zetu mashuhuri zimetekwa na hao wawekezaji kutoka nje. Kwa mfano, hakuna hata lodge moja ambayo iko kwenye National Park zetu inayomilikiwa na mzawa. Zote ni za hao wazungu, wahindi kupitia Agakhan Foundation na wahindi wengine kutoka Kenya. Kuna zile ambazo serikali ilishindwa kuziendesha nazo ni Lake Manyara National Park, Ngorongoro Wildlife Lodge, Seronera Wildlife Lodge na Lobo WildlifeLodge. Hizi zote ziliuzwa kwa mhindi mmoja anaeitwa Kotak wa GAPCO.! Tatizo kubwa la kiuchumi hapa kwetu ni hiki kisingizio cha Globalization (Ukoloni Mamboleo). Tanzania kuna watu serious ambao wangeweza kuzi run hizo hoteli kama wangewezeshwa kifedha, lakini umasikini wetu unatuhukumu na hizi Funding Institutions au mabenki yaliyozagaa hapa nchini hayana shughuli na watanzania hasa wazawa. Mikopo watapewa watu wenye pesa tu, sisi tutabakia kuwa washangiliaji siku zote tukiona hivi hivi urithi wa maliasili yetu ukibakwa kila kukicha na hao manyan'gau wa nje wakishirikiana na mafisadi wachache kwenye wizara mbali mbali.

Ili tuweze kufaidi rasilimali zetu inabidi tubadilike, Watanzania wengi tumeridhika sana au niseme tunaridhika kwa kupata mlo wa siku nyumba ya kuishi na gari.

Ubinafsi ni tatizo kubwa sana, mtu anaona akipaform vizuri kwenye kazi yake anamfaidisha bosi wake, bila kujua ni kwa faida yake mwenyewe na jamii inayomzunguka.

Watanzania wengi hawapendi kuumiza vichwa vyao, na wakiona mtu anaumiza kichwa ili afanikiwe au afanikishe anachofanya hawafurahii, hii inasababisha wale waliofanikiwa kutokushirikisha watanzania wenzake kwa kuogopa kuharibiwa. Mfano mzuri ni jinsi baadhi ya watanzania wanaoishi nje nchi wanavyosengenyana badala ya kufikiri jinsi ya kuleta maendeleo nnchini mwao, wengi wanaishia kurudi bila hata kuwa na kitu cha kueleweka nyumbani.

Unapofungua biashara yako na ukamuachia mtu aisimamie, huwezi kukuta faida badala yake utakuta madeni, tofauti na mzungu ukimkabidhi biashara yako anajitahidi azalishe faida, maana ni aibu kupata hasara.

Kwa ajili hiyo na ndivyo wazungu wengi wanavyotuangalia. Wanapokuja kuinvest kwetu wanakua tayari na huu mtazamo ndio maana tunaishia kuwa wafagiaji na wabeba mizigo.

Hotel industry needs committed people, its called hospitality industry. Is not a Joke! we need to change and to help our future generation to change. To let them know Job is life, we are not working because we don`t have something to eat or where to sleep, but working is life.

We have to change, we have to accept our weakness and find a way out.
 
The question is: watanzania/bantus wanaruhusiwa kuingia hapo hotelini? Manake nasikia kuna baadhi ya hotels Zanzibar na bara kama wewe ni mweusi huingii!!....what a shame wananchi wananyanyaswa ktk nchi yao!!
Fedha yako tu.
 
Kwakweli sisi ni watu wa ajabu sana, hizo hoteli zingekuwa Kenya humu ndani watu wangeanza kusema unaona wa-Kenya walivyoendelea blah blah, blah..etc. etc.

Asilimia kubwa ya wawekezaji ni wale wale na tabia yao ni ile ile (profit maximization at any cost) iwe hapa kwetu au nchi jirani. Kinachotakiwa ni kuhakikisha kuwa TRA inawabana ili walipe kodi ya kutosha.

Kwa upande mwingine faida ya ushindi wa hoteli hii ni kuitangaza Tanzania kupitia Serengeti maana kuna jirani zetu ambao huwa wakipata kanafasi kidogo huwa wanasema hii mbuga au ule mlima viko kwao....
 
Kwakweli sisi ni watu wa ajabu sana, hizo hoteli zingekuwa Kenya humu ndani watu wangeanza kusema unaona wa-Kenya walivyoendelea blah blah, blah..etc. etc.Asilimia kubwa ya wawekezaji ni wale wale na tabia yao ni ile ile (profit maximization at any cost) iwe hapa kwetu au nchi jirani. Kinachotakiwa ni kuhakikisha kuwa TRA inawabana ili walipe kodi ya kutosha. Kwa upande mwingine faida ya ushindi wa hoteli hii ni kuitangaza Tanzania kupitia Serengeti maana kuna jirani zetu ambao huwa wakipata kanafasi kidogo huwa wanasema hii mbuga au ule mlima viko kwao....
TRA itawabanaje rafiki yangu wakati hawa ni mainvestors na wanaexemption ya miaka mitano,na baada ya miaka mitano wanabadilisha jina hawalipi kodi tena,nakuambia sisitutaendelea kuambulia sifa za kijinga
 
Ndo maana kuna Mtanzania wa Kawaida siku hizi. haturuhusiwi kujua wala kutembelea huko! ukiuliza utaambiwa ardhi ni ya kwake hapo sasa BONGOOOO zaidi ya uijuavyo!
 
Hivi hii ni mojawapo za zile zinamilikiwa na bilionea wa kimarekan paul tudor jonson(ptj)?
 
wakuu mimi nyumbani kabisa ni serengeti na hili la hii hoteli nalifahamu kwa kiwango changu.
1. ni kweli kabisa hii hotel ni funuka, ile kilimanjaro hotel kule dar ni cha mtoto.
huyu mzungu kwa ninavyo fahamu ni moja kati ya matajiri walioko katika hii sayari ya dunia, na amewekeza sehemu nyingi sana hapa africa kama vile zimbabwe, south africa, namibia na kwingineko.

- kwa nini si swala la kujivunia kwa hoteli yake kuwa bora duniani?

1. kule serengeti amepewa kipande cha iliyo kuwa game reserve ya pembeni mwa hifadh ya serengeti- ikorongo game reserve, na ni eneo kubwa mno wakuu, yaani ana hifadhi yake mwenyewe

2. Amepewa mkataba wa miaka 99 pale na tangia aanze hata miaka kumi hajamaliza fikilia hiyo 99

3. Ile hoteli, wabongo wako katika hizi section ndogondogo kama kutandika vitanda, usafi. Ulinzi na kazarika, but idara kubwa na zenye pesa zimeshikwa na makaburu, watu kutoka zimbabwe, namibia na kenya na hata ulaya

4. Jamii inayozunguka hiyo hifadhi yake na hoteli yake ni masikini wakutupwa, wao wanaishia kuhesabu magari yanayoingia hotelini na kutoka

5. Waga ana miradi yake ya kusaidia jamii kama kuchimba visima vya maji, afya na elimu but hiyo misaada hailingani na mali anazo pora pale

6. Wakuu chaa ajabu ni kwamba yule mwekezaji ana jeshi lake pale, simanishi kampuni ya ulinzi kama kkguard, no, yaani ana jeshi lake kamili na wanamagari na siraha.

7. Amewahonga madiwani wote wa magamba pamoja na viongozi wa serikali pale wilayaani kiasi kwamba, wamepiga marufuku uwindaji wa kisheria ulio kuwa unafanywa na wananchi wa serengeti ili kujipatia riziki.

8. Kama mtakumbuka ni katika hii hoteli kamati ya bunge ya mahesabu ya serkari inayo ongozwa na cheyo walizuiwa kuingia ndani ya hiyo hoteli wakafungiwa nje ya hotel, ilikuwa mwaka juzi nazani kwenye bunge lililo pita


9. Chamwisho wakuu, huyu mwekezaji hadili na hoteli na watalii peke yake, ile eneo alilomegewa lina madini ya dhahabu na anacho fanya ni kuchimba kisirisiri na kuweka kwenye makontena na kupeleka south africa.


10. Hiyo hoteli kwa wabongo hata kama unapesa yako utaishia mlangini meansa kwenye gaden ya hoteli, utahudumiwa soda huko huko, ndani wanaingia wazungu tu na viongozi wakubwa wa serikali yetu.

11. Halipi kodi kama kawaida amepewa msamaha wa kodi na serikali yetu.

12. Lile jeshi lake kwa jamii ya kule wanawaogopa ile mbya make huwa wanafanya msako wa nyumba kwa nyumba kuangalia ni nani kapika nyama ya wanyama poli, wanaingia jikoni na kukagua vyungu ya kupikia
 
kuna mzawa yoyote alishakwenda hapo wakakataa kumuhudumia?
huyo mtanzania wa kawaida kwenda hapo labda awe fisadi,au mwizi.bado sijaona mfanyabiashara hapa tanzania ambaye amepata utajiri kwa kutoka jasho kihalali na kama yupo mleteni hapa,na matajiri wa bongo kwa namna moja ingine wote wamewahi kuwa na kesi mahakamani za utapeli,kudaiwa na mabenki,tra n.k
 
wangu hayo maelezo yako siungi mkono wala kuyapinga

lakini ujue tu kuwa singiti ni brand kuubwa kuliko zote kwenye luxury resort

siku zote wako namba moja sio tu hii ya serengeti.bali hata ile ya southafrica

halafu hii sio hotel,ni luxury resort,ina wahudumia matajiri wakubwa wa dunia..

chumba mpaka dola 9000 kwa siku.
hadithi ya cheyo ina utata,je alitaka kulala bure kwa sababu ni kamati ya bunge?????/


bado siko convinced na kuchimba dhahabu kisiri siri
 
wakuu mimi nyumbani kabisa ni serengeti na hili la hii hoteli nalifahamu kwa kiwango changu.
1. ni kweli kabisa hii hotel ni funuka, ile kilimanjaro hotel kule dar ni cha mtoto.
huyu mzungu kwa ninavyo fahamu ni moja kati ya matajiri walioko katika hii sayari ya dunia, na amewekeza sehemu nyingi sana hapa africa kama vile zimbabwe, south africa, namibia na kwingineko.

- kwa nini si swala la kujivunia kwa hoteli yake kuwa bora duniani?

1. kule serengeti amepewa kipande cha iliyo kuwa game reserve ya pembeni mwa hifadh ya serengeti- ikorongo game reserve, na ni eneo kubwa mno wakuu, yaani ana hifadhi yake mwenyewe

2. Amepewa mkataba wa miaka 99 pale na tangia aanze hata miaka kumi hajamaliza fikilia hiyo 99

3. Ile hoteli, wabongo wako katika hizi section ndogondogo kama kutandika vitanda, usafi. Ulinzi na kazarika, but idara kubwa na zenye pesa zimeshikwa na makaburu, watu kutoka zimbabwe, namibia na kenya na hata ulaya

4. Jamii inayozunguka hiyo hifadhi yake na hoteli yake ni masikini wakutupwa, wao wanaishia kuhesabu magari yanayoingia hotelini na kutoka

5. Waga ana miradi yake ya kusaidia jamii kama kuchimba visima vya maji, afya na elimu but hiyo misaada hailingani na mali anazo pora pale

6. Wakuu chaa ajabu ni kwamba yule mwekezaji ana jeshi lake pale, simanishi kampuni ya ulinzi kama kkguard, no, yaani ana jeshi lake kamili na wanamagari na siraha.

7. Amewahonga madiwani wote wa magamba pamoja na viongozi wa serikali pale wilayaani kiasi kwamba, wamepiga marufuku uwindaji wa kisheria ulio kuwa unafanywa na wananchi wa serengeti ili kujipatia riziki.

8. Kama mtakumbuka ni katika hii hoteli kamati ya bunge ya mahesabu ya serkari inayo ongozwa na cheyo walizuiwa kuingia ndani ya hiyo hoteli wakafungiwa nje ya hotel, ilikuwa mwaka juzi nazani kwenye bunge lililo pita


9. Chamwisho wakuu, huyu mwekezaji hadili na hoteli na watalii peke yake, ile eneo alilomegewa lina madini ya dhahabu na anacho fanya ni kuchimba kisirisiri na kuweka kwenye makontena na kupeleka south africa.


10. Hiyo hoteli kwa wabongo hata kama unapesa yako utaishia mlangini meansa kwenye gaden ya hoteli, utahudumiwa soda huko huko, ndani wanaingia wazungu tu na viongozi wakubwa wa serikali yetu.

11. Halipi kodi kama kawaida amepewa msamaha wa kodi na serikali yetu.

12. Lile jeshi lake kwa jamii ya kule wanawaogopa ile mbya make huwa wanafanya msako wa nyumba kwa nyumba kuangalia ni nani kapika nyama ya wanyama poli, wanaingia jikoni na kukagua vyungu ya kupikia
Afadhali wewe umesema. Ni katika eneo hilo hilo alikokamatwa kijana wa darasa la saba aliyekuwa anachunga ng'ombe na kupewa adhabu ya kifungo. Baada ya makelele ya wanaharakati akaachiwa. Mtanzania pekee ninayejua amekaribishwa huko mara kwa mara ni Jakaya Kikwete.
Huyu Tudor alitaka aruhusiwe kujenga hoteli kama hiyo hiyo katika mbuga ama za Yellow Stone hapa Marekani lakini akakataliwa kwa sababu za kimazingira. Ndio maana alikimbilia Tanzania ambako hayuko chini ya regulations zozote.
 
wangu hayo maelezo yako siungi mkono wala kuyapinga

lakini ujue tu kuwa singiti ni brand kuubwa kuliko zote kwenye luxury resort

siku zote wako namba moja sio tu hii ya serengeti.bali hata ile ya southafrica

halafu hii sio hotel,ni luxury resort,ina wahudumia matajiri wakubwa wa dunia..

chumba mpaka dola 9000 kwa siku.
hadithi ya cheyo ina utata,je alitaka kulala bure kwa sababu ni kamati ya bunge?????/


bado siko convinced na kuchimba dhahabu kisiri siri

The Boss...hata EPA ilianzia humu humu
 
wangu hayo maelezo yako siungi mkono wala kuyapinga

lakini ujue tu kuwa singiti ni brand kuubwa kuliko zote kwenye luxury resort

siku zote wako namba moja sio tu hii ya serengeti.bali hata ile ya southafrica

halafu hii sio hotel,ni luxury resort,ina wahudumia matajiri wakubwa wa dunia..

Chumba mpaka dola 9000 kwa siku.
Hadithi ya cheyo ina utata,je alitaka kulala bure kwa sababu ni kamati ya bunge?????/


bado siko convinced na kuchimba dhahabu kisiri siri

hayo ya kuchimba zahabu wewe uko town utayajuaje? Kawaulize wananchi wakule ndo watakupa mkanda kamili.
Hiyo ya huduma sipingani na wewe, but si dhani hiyo mikataba ya soth africa ni kama hii ya tz. Ile hifadhi yake miaka 99 ni sawa?
Kamati ya bunge walitaka kuonana na wakuu wa ile hoteli ili kufahamu uendeshaji wa hoteli ile na maswala ya mapato, hakuwa cheyo peke yake ilikuwa kamati nzima na c kwamba walitaka kulala, no,

 
hayo ya kuchimba zahabu wewe uko town utayajuaje? Kawaulize wananchi wakule ndo watakupa mkanda kamili.
Hiyo ya huduma sipingani na wewe, but si dhani hiyo mikataba ya soth africa ni kama hii ya tz. Ile hifadhi yake miaka 99 ni sawa?
Kamati ya bunge walitaka kuonana na wakuu wa ile hoteli ili kufahamu uendeshaji wa hoteli ile na maswala ya mapato, hakuwa cheyo peke yake ilikuwa kamati nzima na c kwamba walitaka kulala, no,



sasa kamati ya bunge wangeweza kwanza kuweka appointments
na sio kuvamia vamia

mkuu dhahabu ichimbwe kwa siri ya faida gani?
hivi unajua ni mtaji gani wameweka kwa resort hiyo??/
na advertisement expenses???????

bado siko convinced

sipingi but siko convinced yet
 
afadhali wewe umesema. Ni katika eneo hilo hilo alikokamatwa kijana wa darasa la saba aliyekuwa anachunga ng'ombe na kupewa adhabu ya kifungo. Baada ya makelele ya wanaharakati akaachiwa. Mtanzania pekee ninayejua amekaribishwa huko mara kwa mara ni jakaya kikwete.
Huyu tudor alitaka aruhusiwe kujenga hoteli kama hiyo hiyo katika mbuga ama za yellow stone hapa marekani lakini akakataliwa kwa sababu za kimazingira. Ndio maana alikimbilia tanzania ambako hayuko chini ya regulations zozote.

ni kweli mikuu pale kikwete ni kama kwake ukisikia yuko mapumzikoni kwenye hifadhi ya serengeti basi ujue ni hapo.

Na kingine nilicho sahau ni kwamba ile hifadhi yake ina mitambo maalumu pamoja na helkopta, hailuhusiwi mtu kukatiza kwenye hiyo hifadhi na ukikamatwa kesi inaendeshwa kwa dakika kadhaa na unahukumiwa fasta
 
Kumbukeni 1967 Kambarage alitaifisha mashamba ya katani, Je nani ataweza kutaifisha waliopora mali za Watanzania? Au Wananchi wenyewe wanaweza! Misri wameweza, Tunisia etc.
 
Kwa kweli kama hili jambo linaukweli basi nashawishika kusema kuna laana inatutafuna watanzania,
 
wangu hayo maelezo yako siungi mkono wala kuyapinga

lakini ujue tu kuwa singiti ni brand kuubwa kuliko zote kwenye luxury resort

siku zote wako namba moja sio tu hii ya serengeti.bali hata ile ya southafrica

halafu hii sio hotel,ni luxury resort,ina wahudumia matajiri wakubwa wa dunia..

chumba mpaka dola 9000 kwa siku.
hadithi ya cheyo ina utata,je alitaka kulala bure kwa sababu ni kamati ya bunge?????/


bado siko convinced na kuchimba dhahabu kisiri siri

You know what you are talking about Boss!!!
 
sasa kamati ya bunge wangeweza kwanza kuweka appointments
na sio kuvamia vamia

mkuu dhahabu ichimbwe kwa siri ya faida gani?
hivi unajua ni mtaji gani wameweka kwa resort hiyo??/
na advertisement expenses???????

bado siko convinced

sipingi but siko convinced yet

sijaweka hii thread ili mtu awe convised hapa but ukweli ndo huo, nisha kwambia nenda serengeti tafuta ile jamii ya kule waulize watakupa full story a to z ya huyu mwekezaji. ni kweli mimi binafisi nimefika pale na nilibahatika kuingia ndani kipindi bado haijakamilika, ni ya kufa mtu na imejengwa kwa ghalama kubwa sana.
ILA HATA UMAFIA ANAO IFANYIA TANAPA NI WAKUTISHA, NA KUHUSU WAKINA CHEYO WALIWEKA APOINTMENY WASINGEWEZA KUVAMIA TU. TATIZO PALE NI KWAMBA WATANZANIA WANADHARAULIWA FOR MAXMUM
 
wakuu mimi nyumbani kabisa ni serengeti na hili la hii hoteli nalifahamu kwa kiwango changu.
1. ni kweli kabisa hii hotel ni funuka, ile kilimanjaro hotel kule dar ni cha mtoto.
huyu mzungu kwa ninavyo fahamu ni moja kati ya matajiri walioko katika hii sayari ya dunia, na amewekeza sehemu nyingi sana hapa africa kama vile zimbabwe, south africa, namibia na kwingineko.

- kwa nini si swala la kujivunia kwa hoteli yake kuwa bora duniani?

1. kule serengeti amepewa kipande cha iliyo kuwa game reserve ya pembeni mwa hifadh ya serengeti- ikorongo game reserve, na ni eneo kubwa mno wakuu, yaani ana hifadhi yake mwenyewe

2. Amepewa mkataba wa miaka 99 pale na tangia aanze hata miaka kumi hajamaliza fikilia hiyo 99

3. Ile hoteli, wabongo wako katika hizi section ndogondogo kama kutandika vitanda, usafi. Ulinzi na kazarika, but idara kubwa na zenye pesa zimeshikwa na makaburu, watu kutoka zimbabwe, namibia na kenya na hata ulaya

4. Jamii inayozunguka hiyo hifadhi yake na hoteli yake ni masikini wakutupwa, wao wanaishia kuhesabu magari yanayoingia hotelini na kutoka

5. Waga ana miradi yake ya kusaidia jamii kama kuchimba visima vya maji, afya na elimu but hiyo misaada hailingani na mali anazo pora pale

6. Wakuu chaa ajabu ni kwamba yule mwekezaji ana jeshi lake pale, simanishi kampuni ya ulinzi kama kkguard, no, yaani ana jeshi lake kamili na wanamagari na siraha.

7. Amewahonga madiwani wote wa magamba pamoja na viongozi wa serikali pale wilayaani kiasi kwamba, wamepiga marufuku uwindaji wa kisheria ulio kuwa unafanywa na wananchi wa serengeti ili kujipatia riziki.

8. Kama mtakumbuka ni katika hii hoteli kamati ya bunge ya mahesabu ya serkari inayo ongozwa na cheyo walizuiwa kuingia ndani ya hiyo hoteli wakafungiwa nje ya hotel, ilikuwa mwaka juzi nazani kwenye bunge lililo pita


9. Chamwisho wakuu, huyu mwekezaji hadili na hoteli na watalii peke yake, ile eneo alilomegewa lina madini ya dhahabu na anacho fanya ni kuchimba kisirisiri na kuweka kwenye makontena na kupeleka south africa.


10. Hiyo hoteli kwa wabongo hata kama unapesa yako utaishia mlangini meansa kwenye gaden ya hoteli, utahudumiwa soda huko huko, ndani wanaingia wazungu tu na viongozi wakubwa wa serikali yetu.

11. Halipi kodi kama kawaida amepewa msamaha wa kodi na serikali yetu.

12. Lile jeshi lake kwa jamii ya kule wanawaogopa ile mbya make huwa wanafanya msako wa nyumba kwa nyumba kuangalia ni nani kapika nyama ya wanyama poli, wanaingia jikoni na kukagua vyungu ya kupikia

yote haya nimeyatafakari....na bado sijaamini kama kuna mambo yanayoendelea kama hayo
 
Back
Top Bottom