TANZANIA vs ALGERIA LIVE ON....

TANZANIA vs ALGERIA LIVE ON....

Nina hasira! ningekuwa uwanjani kocha angelambwa bakora!
 
Poulsen: hana jipya kwa Starz, tangu akabiziwe timu kiwango kinazidi kushuka, kuna haja ya kuachia ngazi si mpaka aundiwe tume.
Binafsi pia sijaona lolote la muhimu lililoletwa na Poulsen....

Ni kwa nini kamuweka bench Victor Costa?,

Ni kwa nini hakumuanzisha Mrisho Ngassa?.....

Ni kwa nini amemtoa Shaban Nditti ambaye alionesha kuelewana vizuri sana na Henry Joseph kiasi cha kuleta uhai pale kati?...

Mechi ya leo ilikuwa ni rahisi sana kwa Stars,tungeweza kushinda hata kwa magoli matatu kama sio manne....Victor Costa ni beki ambaye yupo kwenye kiwango bora kabisa lakini kocha kamuweka benchi na kuwaanzisha Nyosso na Aggrey na sote tumeona uzembe wa Nyosso na Nsajigwa ndio umepelekea Algeria wasawazishe goli,Nyosso kachelewa kuruka hivyo kumpa nafasi mchezaji wa Algeria kufunga goli....Ifikie kipindi Shadrack Nsajigwa apumzike sasa,awaachie vijana wacheze mpira....kawa mzito sana...

Pale katikati kulikuwa na maelewano amzuri sana kati ya Henry Joseph na Shaban Nditi na walikuwa wanapeleka mipira sana mbele kiasi cha kufanya Mbwana Samatta ang'are pale mbele lakini cha kushangaza kocha anamtoa Nditti na kumuingiza Machupa ambaye hajafanya lolote...Kutolewa kwa Nditti kumepelekea Abdi Kassim arudi kwenye kiungo cha kushambulia na Henry Joseph kucheza kiungo cha kukaba hivyo kupooza mchezo/kupunguza kasi ya mchezo.....Baada ya kutoka Nditti mipira mingi haijaenda mbele hivyo kumfanya Samtta asing'are tena kama ilivyokuwa kipindi cha kwanza.....

Kule mbele Abdi Kassim na Danny Mrwanda walikuwa ni mzigo......Walitakiwa kutolewa mapema sana....Sijui ni kwa nini kocha alimuweka mchezaji kama Ngassa benchi....Sote tunamjua Ngassa kwamba ni mchezaji ambaye daima hutengeneza ushindi kwa timu ama kwa kufunga ama kutengeneza magoli..........Inaumiza sana.....

Namkumbuka sana Marcio Maximo.....Sijaona jipya lolote lililoletwa na Jan Poulsena wala Kim Poulsen tangu waje nchini......

Je kuna haja ya kurudi nyuma na kufikiri kwamba sasa ni wakati wa kuwapa timu aifa ya Taifa makocha wazalendo(akina Jamhuri Kihwelo,Dkt.Mshindo Msolla,Juma Mwambusi na wengine) badala ya kupoteza fedha za walipa kodi kwa makocha wageni ambao hakuna jipya lolote wanalolileta kwa Taifa letu????

Tafakari.....................Chukua hatua
 
Sasa wadau, nchi ye2 tutaitofautishaje na Jehanamu! Kwani kila kona Maumivu. Tanzania bwana du.
 
Tushazoea.Halafu ooo watu hawana uzalendo wanashabikia sana ligi za nje.Kwa mtindo huu tutashabikia sana ligi za nje!!!
 
Mtalaumu makocha bure. System nzima ya mpira Tanzania ni mbovu. Msitegemee maajabu yoyote bila ya kusafisha system yote kwanza.
Binafsi namlaumu sana Poulsen........Kwa leo naweza kusema ametunyima ushindi......

Ni system ipi hasa unayoizungumzia?.....Maana mfumo wetu na wakenya na Uganda hauna tofauti.....Kenya wameshinda leo na uganda wanahitaji sare tu kuqulify kwa ajili ya AFCON 2012
 
Nilishazoea, jana nimeangalia riadha Daegu mita 5000,dada mmoja kutoka Tz alivyokuwa anakimbia utadhani anatania.
 
Binafsi pia sijaona lolote la muhimu lililoletwa na Poulsen....<br />
<br />
Ni kwa nini kamuweka bench Victor Costa?,<br />
<br />
Ni kwa nini hakumuanzisha Mrisho Ngassa?.....<br />
<br />
Ni kwa nini amemtoa Shaban Nditti ambaye alionesha kuelewana vizuri sana na Henry Joseph kiasi cha kuleta uhai pale kati?...<br />
<br />
Mechi ya leo ilikuwa ni rahisi sana kwa Stars,tungeweza kushinda hata kwa magoli matatu kama sio manne....Victor Costa ni beki ambaye yupo kwenye kiwango bora kabisa lakini kocha kamuweka benchi na kuwaanzisha Nyosso na Aggrey na sote tumeona uzembe wa Nyosso na Nsajigwa ndio umepelekea Algeria wasawazishe goli,Nyosso kachelewa kuruka hivyo kumpa nafasi mchezaji wa Algeria kufunga goli....Ifikie kipindi Shadrack Nsajigwa apumzike sasa,awaachie vijana wacheze mpira....kawa mzito sana...<br />
<br />
Pale katikati kulikuwa na maelewano amzuri sana kati ya Henry Joseph na Shaban Nditi na walikuwa wanapeleka mipira sana mbele kiasi cha kufanya Mbwana Samatta ang'are pale mbele lakini cha kushangaza kocha anamtoa Nditti na kumuingiza Machupa ambaye hajafanya lolote...Kutolewa kwa Nditti kumepelekea Abdi Kassim arudi kwenye kiungo cha kushambulia na Henry Joseph kucheza kiungo cha kukaba hivyo kupooza mchezo/kupunguza kasi ya mchezo.....Baada ya kutoka Nditti mipira mingi haijaenda mbele hivyo kumfanya Samtta asing'are tena kama ilivyokuwa kipindi cha kwanza.....<br />
<br />
Kule mbele Abdi Kassim na Danny Mrwanda walikuwa ni mzigo......Walitakiwa kutolewa mapema sana....Sijui ni kwa nini kocha alimuweka mchezaji kama Ngassa benchi....Sote tunamjua Ngassa kwamba ni mchezaji ambaye daima hutengeneza ushindi kwa timu ama kwa kufunga ama kutengeneza magoli..........Inaumiza sana.....<br />
<br />
Namkumbuka sana Marcio Maximo.....Sijaona jipya lolote lililoletwa na Jan Poulsena wala Kim Poulsen tangu waje nchini......<br />
<br />
Je kuna haja ya kurudi nyuma na kufikiri kwamba sasa ni wakati wa kuwapa timu aifa ya Taifa makocha wazalendo(akina Jamhuri Kihwelo,Dkt.Mshindo Msolla,Juma Mwambusi na wengine) badala ya kupoteza fedha za walipa kodi kwa makocha wageni ambao hakuna jipya lolote wanalolileta kwa Taifa letu????<br />
<br />
Tafakari.....................Chukua hatua
Naunga mkono hoja, tutumie makocha wazalendo huenda wakawa na jipya!
 
Mkuu Bala umetoa tathmini nzuri sana, wengi wetu tunakerwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona uwezo na mapungufu ya mchezaji mmoja mmoja na kujipanga namna ya kutengeneza "combinations" za kutupatia ushindi, hii haikuwa mechi ya kutoka sare.


Poulsen na kurugenzi ya ufundi TFF hovyo kabisa, wamesababisha tukose ushindi leo!
 
Mkuu Bala umetoa tathmini nzuri sana, wengi wetu tunakerwa na uzembe wa Mwalimu kushindwa kuona uwezo na mapungufu ya mchezaji mmoja mmoja na kujipanga namna ya kutengeneza &quot;combinations&quot; za kutupatia ushindi, hii haikuwa mechi ya kutoka sare.<br />
<br />
<br />
Poulsen na kurugenzi ya ufundi TFF hovyo kabisa, wamesababisha tukose ushindi leo!
<br />
<br />
mkuu kwa sare hii tutakuwa tunaendelea mbele au ndio kibarua kimeota nyasi maana bado sijajua hatima ya stars...
 
Jamani endeleeni kutuvujishia nyepesinyepesi huku simbioni wameng'oa nguzo
 
Binafsi namlaumu sana Poulsen........Kwa leo naweza kusema ametunyima ushindi......

Ni system ipi hasa unayoizungumzia?.....Maana mfumo wetu na wakenya na Uganda hauna tofauti.....Kenya wameshinda leo na uganda wanahitaji sare tu kuqulify kwa ajili ya AFCON 2012

Jiulize ni makocha wangapi walikuwepo kabla ya Poulsen? What have they achieved? Mtabadilisha makocha lakini matokeo yatakuwa yaleyale. Kama target yetu ni kuwa kama Kenya au Uganda, then sina la kusema.
 
HongeraTaifa Stars! Tuache kulalama .. Algeria ni timu kubwa tu.. Ki mahesabu Poulsen = Capello (au tunaweza kusema Tanzania = England kimchezo); wote tumetoa draw na Algeria
 
Pamoja na mfumo wetu mbovu lakini tungetumia vipaji vyetu vizuri tungeshinda,timu haikupangwa vizuri ndio maana nilipoona kikosi tu nikajua kwisha! Tunaitaji wapangwe watu wanaweza kupigana kwa kasi dk 90
 
Costa,Ngasa hawakupaswa kuwa benchi.pia hata timu alivyoipanga utadhani hajui character za wachezaji! Tubaki na makocha wazalendo tu!
 
Back
Top Bottom