Ubungoubungo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2008
- 2,502
- 739
Jamani, tuboreshe reli ya kati toka Dar hadi Kigoma, pale tuunganishe reli toka Tabora au kigoma hadi Burundi na Rwanda(waziri wa Rwanda alishakuja hapa unakumbuka), pia tutengeneza barabara nzuri itakayopitia kule Bukoba au kama kuna uwezekano tuunganishe na reli hadi Uganda, huku zambia wanatutegemea kwa Tanzania Zambia Road authority, tanzania railway authority(Tazara) na bomba la mafuta tazama. kule mozambique, daraja likiisha tu mwaka huu mtu anaweza akasafiri kwa gari haraka sana hadi s.africa kwasababu wareno walijenga barabara safi toke mozambique hadi sauz, malawi ni kuwaunganisha kidogo tu pale Kyela au hata na barabara au reli toka Mtwara(mtwara corrido) hado Kyela au hata mpakani na malawi. tumezungukwa na milango mingi ya kuexport.
nimeangalia kuna jamaa mtz mmoja hivi kule mashada ya wakenya, aisee amefafanua sana hili nikapenda. itaisha lini watz wanaoenda bukoba au mwanza kupitia kenya na uganda wakati wanaenda kwenye nchi yetu humuhumu? hivi kwanini? au hili lilishaisha wajameni wanaojua tuelezeni. kwanini tusitengeneza na barabara toka Bongo hapa hadi bukoba na mwanza mtu asafiri kwa siku moja hata kwa gari ndogo ya mark two? sina uhakika kama ni solved mtanirekebisha, lakini kitu cha muhimu, nilitaka watu wajue namna tz inavyowez kufanya mambo makubwa hapa.
Burundi inatutegemea kuingiza mizigo yao, Rwanda nayo hata kama kwasasa wanawategemea kenya through uganda, lakini wanataka direct isipitie nchi nyingine. uganda itafika tu kipindi watakapoona kupitia kenya ni ukoloni, hivyo tutawanyang'anya wakenya wateja wao wa mombasa port.
kuipiku mombasa port ni muhimu sana. tufanyeje? ni kuiboresha bandari ya Dar, na pia kama tulivyoambiwa kipindi sha nyuma kuwa wawekezaji toka Saudi Arabia wanakuja kujenga Bandari kubwa Bagamoyo, hiyo ingekuwa kitu kikubwa sana. hivi hili wazo lilienda wapi? UJENZI WA BANDARI YA BAGAMOYO? na kuboresha bandari ya Tanga na Mtwara daraja la mzumbiji likiisha? vipi hapo? kama viongozi wetu ni wazalendo na wana uchungu na nchi kama sisi wengine tulivyo, hivi tutashinda kufika mbali kweli? hapana, tunaweza. Mungu ibariki Tanzania. Amin.
nimeangalia kuna jamaa mtz mmoja hivi kule mashada ya wakenya, aisee amefafanua sana hili nikapenda. itaisha lini watz wanaoenda bukoba au mwanza kupitia kenya na uganda wakati wanaenda kwenye nchi yetu humuhumu? hivi kwanini? au hili lilishaisha wajameni wanaojua tuelezeni. kwanini tusitengeneza na barabara toka Bongo hapa hadi bukoba na mwanza mtu asafiri kwa siku moja hata kwa gari ndogo ya mark two? sina uhakika kama ni solved mtanirekebisha, lakini kitu cha muhimu, nilitaka watu wajue namna tz inavyowez kufanya mambo makubwa hapa.
Burundi inatutegemea kuingiza mizigo yao, Rwanda nayo hata kama kwasasa wanawategemea kenya through uganda, lakini wanataka direct isipitie nchi nyingine. uganda itafika tu kipindi watakapoona kupitia kenya ni ukoloni, hivyo tutawanyang'anya wakenya wateja wao wa mombasa port.
kuipiku mombasa port ni muhimu sana. tufanyeje? ni kuiboresha bandari ya Dar, na pia kama tulivyoambiwa kipindi sha nyuma kuwa wawekezaji toka Saudi Arabia wanakuja kujenga Bandari kubwa Bagamoyo, hiyo ingekuwa kitu kikubwa sana. hivi hili wazo lilienda wapi? UJENZI WA BANDARI YA BAGAMOYO? na kuboresha bandari ya Tanga na Mtwara daraja la mzumbiji likiisha? vipi hapo? kama viongozi wetu ni wazalendo na wana uchungu na nchi kama sisi wengine tulivyo, hivi tutashinda kufika mbali kweli? hapana, tunaweza. Mungu ibariki Tanzania. Amin.