Laptop01
JF-Expert Member
- Nov 29, 2009
- 1,365
- 796
Well, una hoja nzuri sana Mkuu. Ingawa kwa maendeleo ya sayansi na teknolojia yaliyopo sasa kama vile Matumizi ya Walimu wa chache waliopo ikimuishwa na Matumizi ya IoT and Artificial Inteligence tunaweza kufundisha masomo hayo vizuri kabisa Mkuu. Shida itakuwa ni haya maumeme yetu yanayo katika kila dakika na hayajafika kila Kijiji.Nimeona taasusi mpya zilizotolewa na wizara ya elimu Tanzania. Naomba tusaidieni mawazo kama zinatekelezeka na zina tija kwa watoto wetu
1. Tuambieni waalimu wa lugha ya kiarabu, Kifaransa na Kichina tunao? Chuo gani cha ualimu kinafundisha haya masomo kwa ngazi ya degree? Nauliza degree kwa sababu mwalimu wa kidato cha tano lazima awe na degree.
2. Ni nani kati yetu amewahi kushirikishwa kutoa maoni kuhusu mabadiliko haya?
3. Je, wanaosoma dini watakwenda kusoma nini chuoni? Wataenda vyuo gani hapa nchni?
4. Dunia inakimbilia kwenye TEHAMA, kwanini mfumo huu umejikita zaidi nje ya TEHAMA?
5. Ni nchi gani Duniani ina Tahsusi za aina hii tulipokwenda kujifunza au tunarudia aliyoifanyia hii nchi Mungai wakati anapanga kuua elimu yetu huku elimu ya Kenya ikiwa inapanda?
6. Waalimu wa kufundisha dini tuliwaandaa katika vyuo gani?
Kwamba hizi tahasusi zimeridhiwa au zimeletwa kwa ajili ya maoni? Nchi ya viwanda, biashara na kilimo kweli itatoboa kwa mfumo wa elimu ambao hauungani kati ya primary, secondary na chuo?