Tanzania tumejiandaaje kwa Ebola?

Tanzania tumejiandaaje kwa Ebola?

Huwezi kutunga katiba kwa siku sitini au tisini ikakubalika na wananchi walio wengi huko ni kujidanganya!! Msione aibu ,hilo bunge la katiba liahirishwe mpaka hapo wananchi watakapopiga kura ya maoni ni aina gani ya muungano wanaoutaka!! Mtatuumiza bure kwa kuwahonga hao wabunge kwa posho mtakazowapa ilihali budget yenyewe ni tegemezi kwa ruzuku ya wafadhili kwa kazi isiyokuwa na tija kwa taifa hili maskini. Viongozi ni lazima muwe na hekima badala ya kupenda madaraka! Nakubaliana na hoja kuwa hizo hela za hilo bunge ziwekwe kama tahadhali ya ugonjwa wa Ebora.
 
Nikiitizama TANZANIA kwa sasa swala ni katiba tu yaani kwenye magazeti,tv stations hata mijadala mbalimbali,si ubaya mana ni inshu muhimu sana kwa taifa langu ila jamani kuna ugonjwa wa hatari hasa wa EBOLA,sijui viongozi wangu mnalichukuliaje hili swala mana ukiingia huu hata katiba tutaisahau,hasa waziri wa afya na mh.raisi na waziri mkuu take care EBOLA INAUA
 
Hata lile la viungo vya binadamu limeshasahaulika, dah hii ndio Bongo bwana
 
kwanza ikiingia bongo itauwa wengi sana hasa kwenye daladala na kariakoo kwenye makutano ya watu
 
We never learn. Tushasahau dengue. Ikija Ebola ndo tutaanza kwenda mbio.
 
Swali la leo: Tanzania iko tayari kwa kupata mgonjwa wa kwanza wa Ebola? Je, tunaangalia na kufuatilia wageni wanaoingia katika mipaka yetu na kuangalia kama yeyote kati yao ametokea Afrika ya Magharibi siku za hivi karibuni? Je, endapo itagundulika mtu ana dalili za ugonjwa huo ni protocol gani iliyoandaliwa kukabiriana na hili au tunaweza kujikuta tunafanya kama Nigeria kutengeneza protocol baada ya kuwa na mgonjwa?
Mapendekezo yangu:
a. Tuanze mara moja kumonitor watu wanaoingia kutokea nje hasa ambao kati pasi zao za kusafiria wanaonekana kupitia Afrika ya Magharibi hasa katika miezi hii mitatu au minne ya hivi karibuni.
b. Kuandaa vikosi vya afya (rapid response unit) karibu na viwanja vyetu na ndege vikiwa vimeandaliwa kupokea mtu mwenye dalili za maambukizi.
c. Hospitali kubwa karibu na maeneo ya mipakani ziandaliwe sehemu ya kuwatengea watu wenye dalili za ugonjwa huu (isolation units) pamoja na magari ya kuwasafirishia.
d. Tutenge fedha ya kutosha kukabiriana na hili.
Kama tulivyoona kwenye ugonjwa wa dengue kujiandaa kwa majanga ndio kujiepusha na maafa kama ambavyo nimewahi kusema mara nyingi. Isije kuwa tuna watu "wanaombea" kuwa Ebola isije kwetu. Kwamba uwezekano wa kutokea unaongezeka siku kwa kwa siku kwa kadiri ya kwamba watu bado wanaweza kusafiri kutokea nchi zenye maambukizi.
Vinginevyo, tusije kushangaa tutakapoambiwa kuwa kuna mtu ana Ebola itakuwa tayari mtu huyo alishatembelea Kariakoo, kwenye vilabu, n.k na tukajikuta tunashindwa hata pa kuanzia.
 
Swali la leo: Tanzania iko tayari kwa kupata mgonjwa wa kwanza wa Ebola? Je, tunaangalia na kufuatilia wageni wanaoingia katika mipaka yetu na kuangalia kama yeyote kati yao ametokea Afrika ya Magharibi siku za hivi karibuni? Je, endapo itagundulika mtu ana dalili za ugonjwa huo ni protocol gani iliyoandaliwa kukabiriana na hili au tunaweza kujikuta tunafanya kama Nigeria kutengeneza protocol baada ya kuwa na mgonjwa?
Mapendekezo yangu:
a. Tuanze mara moja kumonitor watu wanaoingia kutokea nje hasa ambao kati pasi zao za kusafiria wanaonekana kupitia Afrika ya Magharibi hasa katika miezi hii mitatu au minne ya hivi karibuni.
b. Kuandaa vikosi vya afya (rapid response unit) karibu na viwanja vyetu na ndege vikiwa vimeandaliwa kupokea mtu mwenye dalili za maambukizi.
c. Hospitali kubwa karibu na maeneo ya mipakani ziandaliwe sehemu ya kuwatengea watu wenye dalili za ugonjwa huu (isolation units) pamoja na magari ya kuwasafirishia.
d. Tutenge fedha ya kutosha kukabiriana na hili.
Kama tulivyoona kwenye ugonjwa wa dengue kujiandaa kwa majanga ndio kujiepusha na maafa kama ambavyo nimewahi kusema mara nyingi. Isije kuwa tuna watu "wanaombea" kuwa Ebola isije kwetu. Kwamba uwezekano wa kutokea unaongezeka siku kwa kwa siku kwa kadiri ya kwamba watu bado wanaweza kusafiri kutokea nchi zenye maambukizi.
Vinginevyo, tusije kushangaa tutakapoambiwa kuwa kuna mtu ana Ebola itakuwa tayari mtu huyo alishatembelea Kariakoo, kwenye vilabu, n.k na tukajikuta tunashindwa hata pa kuanzia.

MM hujamsikia JK anasema hili Tatizo la West Africa?huyu bwana sijui vipi.

Saudi Arabia wamereport cases za Ebola, na wako outside Africa, huyu anadhani TZ ni mwezini.If this disaster makes its way to TZ, people will die in hundreds, because of irresponsible leaders.here is to hope nature rescues our poor souls again.
 
Katika nchi ambayo a less severe form of Hemorrhagic disease ilikuwa ni Circus wakati watu walikufa, sidhani kama hiyo Ebola itaepukika(God forbid).

Hospitali ambapo utafiti/vipimo vya damu ni tabu(hadi hospitali kubwa), lack of isolation centre/units, dawa , 'drip' na Benki ya damu ni vya kusua sua), utayari wa viongozi ni wa 'kisiasa' zaidi, sidhani kama tumeweza/tutaweza kujiandaa.
Tumuombe MUNGU aepushie mbali.
 
Hivi kwani hii nchi imejiandaa kwa Crisis ya aina gani ? au ghafla umekuwa mgeni wa hili taifa letu...
 
If I may digress a bit....hivi unajua kuwa pale JNIA kuna Wi-Fi tena ya bure na inafanya kazi (at least mara mwisho majuzi kupita hapo ilikuwa inafanya kazi).

It was a shocker!

hata mimi ndo unaniambia now...sikutegemea iwepo
 
Jibu kwa swali ni kuwa hatupo tayari kuwa na mgonjwa wa Ebola. Nani anayetaka kukumbwa na majanga?

Hata kama ingekuwa ni marekani ambao wana uwezo mkubwa wa kukabili majanga watakujibu hawapo tayari kuwa na hilo janga.
 
Angalizo Zuri sana Mkuu LAKINI pamoja na kukubaliana na Ushauri huu mwanana, Bado Wataalam na Viongozi wa Kiafrica wameshindwa kuweka Ukweli USIOPINGIKA kuwa Ugonjwa Huu umetengenezwa LAB kwa lengo la Kupunguza Blacks Populations !!! WHO na Billy n Melinda Foundation inasemekana kuwa ndio walio eneza ugonjwa huo huko Afrika Magharibi... If that is the case, IFAKARA Institute wakitumiwa kusambaza Ugonjwa huo tutaweza kuuzuia kama Taifa? Wachina Wamepigwa na Mafua ya Ndege mara kwa mara na mara zote wameweza kui-contained ... Sisi kama nchi bado sana!!! Inasikitisha sana kuona Wakitumia Trillions kwenye Net za Mbu wakati Australia yenye hali ya hewa kama ya kwetu wana nyunyiza DDT na wamefanikiwa 100%... Africa tunatakiwa tuamke tuuone ukweli, tujipange tukabiliane na changamoto zinazotukabili badala ya kuendelea kulilia misaada ya udhalilishaji...
Swali la leo: Tanzania iko tayari kwa kupata mgonjwa wa kwanza wa Ebola? Je, tunaangalia na kufuatilia wageni wanaoingia katika mipaka yetu na kuangalia kama yeyote kati yao ametokea Afrika ya Magharibi siku za hivi karibuni? Je, endapo itagundulika mtu ana dalili za ugonjwa huo ni protocol gani iliyoandaliwa kukabiriana na hili au tunaweza kujikuta tunafanya kama Nigeria kutengeneza protocol baada ya kuwa na mgonjwa?
Mapendekezo yangu:
a. Tuanze mara moja kumonitor watu wanaoingia kutokea nje hasa ambao kati pasi zao za kusafiria wanaonekana kupitia Afrika ya Magharibi hasa katika miezi hii mitatu au minne ya hivi karibuni.
b. Kuandaa vikosi vya afya (rapid response unit) karibu na viwanja vyetu na ndege vikiwa vimeandaliwa kupokea mtu mwenye dalili za maambukizi.
c. Hospitali kubwa karibu na maeneo ya mipakani ziandaliwe sehemu ya kuwatengea watu wenye dalili za ugonjwa huu (isolation units) pamoja na magari ya kuwasafirishia.
d. Tutenge fedha ya kutosha kukabiriana na hili.
Kama tulivyoona kwenye ugonjwa wa dengue kujiandaa kwa majanga ndio kujiepusha na maafa kama ambavyo nimewahi kusema mara nyingi. Isije kuwa tuna watu "wanaombea" kuwa Ebola isije kwetu. Kwamba uwezekano wa kutokea unaongezeka siku kwa kwa siku kwa kadiri ya kwamba watu bado wanaweza kusafiri kutokea nchi zenye maambukizi.
Vinginevyo, tusije kushangaa tutakapoambiwa kuwa kuna mtu ana Ebola itakuwa tayari mtu huyo alishatembelea Kariakoo, kwenye vilabu, n.k na tukajikuta tunashindwa hata pa kuanzia.
 
If I may digress a bit....hivi unajua kuwa pale JNIA kuna Wi-Fi tena ya bure na inafanya kazi (at least mara mwisho majuzi kupita hapo ilikuwa inafanya kazi).

It was a shocker!

Kwa kweli hili hata mimi hili lilinishangaza. JNIA na JRO zote Wi-Fi inafanya kazi vizuri tu. Maajabu haya...
 
Back
Top Bottom