Tanzania tuachane mfumo wa kupandishia watu mishahara bila kuwa na vigezo vya utendaji (performance)

FaizaFoxy

Platinum Member
Apr 13, 2011
92,883
109,211
Tanzania tuachane kabisa na mfumo wa kuwapandishia watu mishahara au vyeo bila kuwa na vigezo na vipimo vya "performance" zao.

Nashauri kwanza viwekwe vigezo na vipimo vya "performance" kazini ndivyo vitumike kuwapandisha watu vyeo na mishahara.

Ni wepesi sana kupanga vigezo vya ubora wa utendaji kwa kila kazi katika kila sehemu ya kazi. Tena siku hizi kila kitu kinakuwa kwenye data base kidigitali ni wepesi sana. Wale watendaji bora (best performers) watapanda mishahara na vyeo haraka na wale wazembe (kama ilivyo kwa Watanzania wengi) watasota hapo hapo na mshahara wa "entry level" mpaka wabadilike au wajiachishe wenyewe kazi.

Mfumo huu wa "performance based" upo na unatumika sana ulimwenguni, hususan kwenye kazi zisizo za Serikali, pia serikali nyingi zimeanza kutumia mfumo huo, bila kuoneana aibu wala huruma za kijinga.

Uzoefu wangu wa kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda mrefu sana katika nchi zilizoendelea umenifundisha hayo.
 
Na hayo ndiyo yanachangiza pia africa maendeleo kuchelewa,sehemu kubwa ya bajeti zetu zinatumika kwa matumizi ya hovyo na mambo ambayo hayana msingi wowote
Kweli kabisa, mfumo mzima wa kuendesha nchi unatakiwa upinduliwe kabisa.

Serikali inatakiwa iwe nyembamba sana na iwe ni "policy makers, facilitators and inspectors" tu.
 
Mambo ya kubebanabebana hatuwezi pata watu competent ni vilaza tia maji watu wenye skills, well educated wanasugua benchi
Kweli kabisa. Ni mfumo ambao hata tuhangaike vipi na takwimu hautotupandishia uchumi kwa haraka. Ukichukulia kuwa Serikali ndio moja ya waajiri wakubwa sana Tanzania na nnauhakika over 90% ya waajiriwa serikalini ni underperformers.

Wengi wanaokimbilia kazi za serikalini ni wazembe na wabadhirifu.
 
Tanzania tuachane kabisa na mfumo wa kuwapandishia watu mishahara au vyeo bila kuwa na vigezo na vipimo vya "performance" zao.
Nashauri kwanza viwekwe vigezo na vipimo vya "performance" kazini ndivyo vitumike kuwapandisha watu vyeo na mishahara.

Ni wepesi sana kupanga vigezo vya ubora wa utendaji kwa kila kazi katika kila sehemu ya kazi. Tena siku hizi kila kitu kinakuwa kwenye data base kidigitali ni wepesi sana. Wale watendaji bora (best performers) watapanda mishahara na vyeo haraka na wale wazembe (kama ilivyo kwa Watanzania wengi) watasota hapo hapo na mshahara wa "entry level" mpaka wabadilike au wajiachishe wenyewe kazi.

Mfumo huu wa "performance based" upo na unatumika sana ulimwenguni, hususan kwenye kazi zisizo za Serikali, pia serikali nyingi zimeanza kutumia mfumo huo, bila kuoneana aibu wala huruma za kijinga.

Uzoefu wangu wa kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda mrefu sana katika nchi zilizoendelea umenifundisha hayo.
Hata hizo fomu za perfomnce appraisal zilizo serikalini watu hawajazi uhalisia ni upuzi tu mtu anapika data then anajaza anasubmit, shirika moja ndiyo utaratibu unatubana ni lazima uambatanishe na documents ulizofanyia kazi na unajazia kwenye system hiyo perfomnce appraisal inakua at least inakubana huwezi kuongopea
 
Nashauri kwanza viwekwe vigezo na vipimo vya "performance" kazini ndivyo vitumike kuwapandisha watu vyeo na mishahara.
Unamshauri nani?

Na ni kazi gani hizo ambazo uta monitor utendaji wa kila mtu?

Nikupe mfano Wizara ya mambo ya ndani inapandisha vyeo kwa mtindo hii miwili moja Elimu pili muda wako kazini haina mingine.

Mtu wa kidato cha nne asiye na fani yoyote anapata cheo kwa muda wa miaka mitatu hadi kumi anapata cheo. Kwa mwenye elimu ya zaidi ya form 4 au fani ni faida zaidi hii wizara performance ni nyumbani kwenu kwa maarabu huko
 
Tanzania tuachane kabisa na mfumo wa kuwapandishia watu mishahara au vyeo bila kuwa na vigezo na vipimo vya "performance" zao.
Nashauri kwanza viwekwe vigezo na vipimo vya "performance" kazini ndivyo vitumike kuwapandisha watu vyeo na mishahara.

Ni wepesi sana kupanga vigezo vya ubora wa utendaji kwa kila kazi katika kila sehemu ya kazi. Tena siku hizi kila kitu kinakuwa kwenye data base kidigitali ni wepesi sana. Wale watendaji bora (best performers) watapanda mishahara na vyeo haraka na wale wazembe (kama ilivyo kwa Watanzania wengi) watasota hapo hapo na mshahara wa "entry level" mpaka wabadilike au wajiachishe wenyewe kazi.

Mfumo huu wa "performance based" upo na unatumika sana ulimwenguni, hususan kwenye kazi zisizo za Serikali, pia serikali nyingi zimeanza kutumia mfumo huo, bila kuoneana aibu wala huruma za kijinga.

Uzoefu wangu wa kufanya kazi za kuajiriwa kwa muda mrefu sana katika nchi zilizoendelea umenifundisha hayo.
Msiwe mnakurupuka kuandika na kujifurahisha hovyo. Kupanda mishahara kwa watumishi ni takwa la kikatiba. Ndio maana hoja ya msingi huwa ni uwiano wa ughali wa maisha na kima cha chini cha mshahara.
 
Kweli kabisa. Ni mfumo ambao hata tuhangaike vipi na takwimu hautotupandishia uchumi kwa haraka. Ukichukulia kuwa Serikali ndio moja ya waajiri wakubwa sana Tanzania na nnauhakaika over 90% ya waajiriwa serikalini ni underperformers.

Wengi wanaokimbilia kazi za serikalini ni wazembe na wabadhirifu.
Hicho kiparagraph cha chini umemaliza vizuri sana ni kwasababu mtu anasema serikalini mpaka ufukuzwe sio leo, yani kuna job security ukiwa serikalini sasa hiyo dhana inapelekea watumishi kuwa malazy pindukia maana hajali hata akiharibu kazi haogopi maana anajua hatafukuzwa hiyo ina zalisha wavivu wezi wabadhirifu na kutofikia malengo
 
Msiwe mnakurupuka kuandika na kujifurahisha hovyo. Kupanda mishahara kwa watumishi ni takwa la kikatiba. Ndio maana hoja ya msingi huwa ni uwiano wa ughali wa maisha na kima cha chini cha mshahara.
Ewaaaa! Ni walimu wangapi hawatapanda madaraja kama kigezo kitakuwa performance?
 
Ewaaaa! Ni walimu wangapi hawatapanda madaraja kama kigezo kitakuwa performance?
Madaraja na kima cha chini cha mshahara ni ishu nyingine. Ndio maana mtu anatakiwa apande daraja baada ya miaka mitano. Na hii huwa inasadakiwa kila baada ya miaka mitano atakuwa amepata experience nyingine. Sasa kama wewe kila baaada ya miaka mitano hujapata kitu kipya basi una shida.
 
Hata hizo fomu za perfomnce appraisal zilizo serikalini watu hawajazi uhalisia ni upuzi tu mtu anapika data then anajaza anasubmit, shirika moja ndiyo utaratibu unatubana ni lazima uambatanishe na documents ulizofanyia kazi na unajazia kwenye system hiyo perfomnce appraisal inakua at least inakubana huwezi kuongopea
Sijuwi mfumo wa Tanzania upoje. Hizo "performance appraisal" kwa Tanzania anazijaza nani?

Mfano nchi niliyokuwepo kuna "performance appraisal" lakini inajazwa na "Private inspecting consultants". (Factor) kigezo cha kwanza kabisa ni katika kila kazi kuna kitu kinaitwa "fundamentals "za hiyo kazi. Inspector ndicho kitu cha kwanza anatazama. Asiyefata "fundamentals" za hiyo kazi anarudishwa akaisomee tena hiyo kazi (akiwa kazini), Akirudishwa huko ni automatically "entry level pay" yake inashuka kwa nusu nzima, inakuwa ni ya mwanafunzi wa kazi.
 
Msiwe mnakurupuka kuandika na kujifurahisha hovyo. Kupanda mishahara kwa watumishi ni takwa la kikatiba. Ndio maana hoja ya msingi huwa ni uwiano wa ughali wa maisha na kima cha chini cha mshahara.
Katiba wapi imekataza kuwekwa vigezo vya kupandishwa mshahara?
 
Mimi sio mtumishi wa umma ila hili wazo lingeanza na katiba mpya itakayokiondoa chama chochote madarakani kitakachoharibu. Tusianze na watumishi wa umma tuanze na katiba mpya itakayo waondoa wasimamizi wa sera na watunga sheria.
 
Nimeupenda sana huu uzi.

Natamani Rais lingemfikia na kulifanyia kazi japo hata yeye mwenyewe kwa thathmini yangu ni MZEMBE No. 1.

"Mfumo huu wa "performance based" upo na unatumika sana ulimwenguni, hususan kwenye kazi zisizo za Serikali, pia serikali nyingi zimeanza kutumia mfumo huo, bila kuoneana aibu wala huruma za kijinga."

Alhamdulillah nimebahatika kufanya Kazi Serikalini na Sekta Binafsi. Serikalini kwa kua hakuna Mfumo basi ni 'Choo Cha Umma' au sawa na kusema ni 'Shamba la Bibi' kwa jinsi na namna Watumishi wanavyojifaidia.

Sekta binafsi hasa kwenye Makampuni makubwa na yanayojielewa aisee... One Mistake, One Goal.

Wafanyakazi wote hawawezi kuwa sawa katika utendaji na haswa katika suala la kutekeleza majukumu yao kwa wakati na usahihi ndiyo maana Sekta Binafsi zinaishinda Serikalini parefu sana.

Hongera sana kwako Mtoa Mada kwa kuliona hilo FaizaFoxy

Unajua ni ukweli kwamba: Tutafika Tukiwa Tumechoka Sana au Hatutafika Kabisa.

Kwasababu:

"Ng'ombe walioko mbele ndiyo wanao chelewesha Msafara hivyo wanasababisha na kupelekea Kuchapwa kwa Ng'ombe zilizopo nyuma karibu na Mchungaji"
 
Back
Top Bottom