Tanzania Now Faces Sanctions & Diplomatic Crisis Over Iran

Tanzania Now Faces Sanctions & Diplomatic Crisis Over Iran

Status
Not open for further replies.
Tanzania tunapaswa kuwa na uhuru wa kuamua ni nchi gani tunashirikiana nayo kidiplomasia, kiuchumi n.k. Lakini kimsingi uhuru huo hatuna kwa sasa kwani nchi tajiri na wahisani wanatuamria nani tushirikieane naye na nani tufarakane naye kwa kigezo cha utegemezi wetu kwao. Tunahitaji mabadiliko katika dira ya uongozi ili tuwe nchi yenye uhuru kamili.

Mkuu, nakubaliana na wewe hususan hapo kwenye wekundu.
Lakini kilichofanyika hapo kuhusu hizo meli kubwaa za mafuta siyo uhuru tena ni uhuni.

Haiwezekani kama nchi, mkakubali kubadilisha majina ya meli zisizowahusu na kuzipa bendera ya nchi yenu kupeperushwa ilhali dunia yote inajua nchi ya Iran ina ugomvi na karibu dunia nzima kuhusu matumizi ya vinu vya nishati ya nyuklia.

Mimi ninaamini kabisa kwamba serikali haijui lolote kuhusu huo uhuni, kwani inajua madhara yake. Bali kuna wahuni wachache ambao wameutumia mwanya fulani uliokuwepo kutekeleza uhuni huo.
 
Iran ndio wafadhili wa uamsho sasa wamepatikana kwa muda mrefu wamejiingiza Zanzibar kwa mwamvuli wa dini na kugawa pesa ambazo zilikuwa zinachangia vurugu ikiwemo kuchoma makanisa,kuchoma baa na kupinga muungano lakini nyuma yake walikuwa wanalinda maslahi yao sasa siri imefichuka sijui watajificha wapi
 
Ni vyema watu wakafahamu kwamba kwenye maritime law kuna uhuru wa meli/tanker kujisajili na kupepea bendera ya nchi yeyote.Liberia,Philippines na Panama ni katika nchi zinazoongoza kusajili meli nyingi sana na wanapata mamia ya mamilioni ya dola kutokana na ada za kila mwaka zinazolipwa na meli wanachama.Vilevile inatoa fursa ya ajira kwa mabaharia na maofisa mbalimbali wa meli kutoka nchi inayosajili meli husika.Vile vile ni fursa kwa wakaguzi wa nchi sajili kupata kazi za ukaguzi kwani kila baada ya muda inabidi zikaguliwe na ili kurenew leseni zao.Haya matanker yamesajiliwa na kupewa bendera ya Tanzania katika sheria halali za kimataifa na wala watu wasifikiri labda kuna dili ambalo mheshimiwa raisi wetu amecheza.Hakuna dili lolote ni normal practice ambayo inafanyika dunia nzima.Kikubwa watu wajue kuipa meli flag(flag state) ni process ambayo ofisi ya raisi haiuhusiki hata kidogo.Wanaotoa hizo flag state ni SUMATRA na Zanzibar Maritime Authority.Tujitahidini kufanya utafiti badala ya kukurupuka na kuchafuana bila sababu ya msingi.Ni vema vile vile kujiuliza kama taifa hivi tutaburuzwa mpaka lini na hawa mabeberu.They are only thinking of their business interest in the middle east lakini what about our interest as developing country.Okay tutazifuta meli za Iran basi wao USA wawe tayari kutupa meli zao tuzisajili na kuzipa Flag yetu ili tusipoteze mapato ya kila mwaka na fursa lukuki za ajira,sifikirii kama wataskubali.
 
SMZ imekiri kuwa imesajili meli hizo kwa sababu zanzibar ina mamlaka kamili ya kusajili meli hizo na sio jambo la muungano.Hii ndiyo sababu ya safari za viongozi wa iran kuja nchini.Nadhani zanzibar itumie bendera yake kupeperusha katika meli hizo na sio ya jamhuri ya muungano.Lakini zanzibar hawana ubavu wa kupambana na Marekani meli hizi zitafutiwa usajili wake muda sio mrefu na Kikwete atawashauri SMZ waachane na meli hizo za wairan ili kuepusha vikwazo.
 
.....Kikubwa watu wajue kuipa meli flag(flag state) ni process ambayo ofisi ya raisi haiuhusiki hata kidogo.Wanaotoa hizo .....
Umeandika mengi lakini hapo kwenye red ni wimbo uleule wa siku zote - raisi kapotoshwa, anaangushwa na wasaidizi wake, n.k. Hakuna aliyesema ofisi ya Rais inahusika na usajili wa meli lakini kwa jambo kubwa kama hili la kidiplomasia Ofisi ya Rais kutokujua kinachoendelea ni zaidi ya uendawazimu!

Kama waliopaswa kumshauri au kumpaa taarifa iwe za moja kwa moja kiofisi au hata za kiupelelezi/intelijensia hawakufanya hivyo au walimshauri "vibaya" hadi Wamarekani wameiandikia barua ofisi yake, wahusika wanachukuliwa hatua gani? Na kama Rais alifahamu haya mambo kabla na hakuchukua hatua then tumweleweje?

Kwa hili usitake kuitetea Ofisi ya Rais, inahusika moja kwa moja ama kwa uzembe, kujua, au kutokujua - mambo ambayo hayakupaswa kufungamana na Ofisi yenye hadhi hiyo. PERIOD.
 
This country is n ICU .... !! Is n one know the xctly remedy for a rescue .. Pls volunteer otherwise ... we r soon loosing th patient!!!!!
 
Tanzania kama nchi ina haki ya kujichagulia marafiki na maadui. America na Ulaya hawana haki hata chembe ya kutuchagulia marafiki na maadui. Misaada wanayotupatia kamwe isiwe kigezo cha kututawala kwani tukiamua tunaweza kuishi bila kutegemea misaada yao. Tanzania ni taifa huru na hatufungamani na upande wowote. Mungu ibariki Tanzania.

Mawazo mgando kama haya ndiyo yanayorudisha nchi nyuma? Hivi unafikiri miaka hamsini yote tumeshindwa kujitegemea, tunawapa madini bure hao wanatupa misaada midogo midogo. Hii yote ni mazaliq ya serikali dhaifu kushindwa kujitegemea for almost 50yrs.
 
nimeangali press tv mda mchache uliopita nimeona taarifa kuwa iran imetoa madaktari 1000 kuja tanzani kutibu bure kabisa hadi hapo mgogoro na madaktari utakapoisha.
 
nimechoka! leo nimepata fursa ya kuongea na senior intelligence officers wa serikali ya uingereza wanasema wanafuatilia hili sakata kwa ukaribu zaidi na wakijiridisha bila shaka Tanzania itawekewa vikwazo vya kiuchumi pamoja na kufuta misaada yote. Pia jamaa wamenitonya hapa Washington DC kuwa wanafuatilia kwa ukaribu suala la Dr . Ulimboka na kusema endapo akifa tu na chanzo kuwa ni mateso aliyoyapata kuna kitu kikubwa chaja (kwa sasa ibaki siri).Nilipojitambulisha natoka tanzania mmoja wao amenijibu . nanukuu

"WE HATE CHAMA CHA MAPINDUZI"


mwisho wa kunukuu

kwa kweli waendelee kuwaza na wafanye kila wanaloweza maana hata sisi chama cha mapinduzi kimetuchosha,
 
Tanzania kama nchi ina haki ya kujichagulia marafiki na maadui. America na Ulaya hawana haki hata chembe ya kutuchagulia marafiki na maadui. Misaada wanayotupatia kamwe isiwe kigezo cha kututawala kwani tukiamua tunaweza kuishi bila kutegemea misaada yao. Tanzania ni taifa huru na hatufungamani na upande wowote. Mungu ibariki Tanzania.

Lini mtaamua kuushi bila misaada coz hali ishakuwa tete bado tuu hamjaamua kuishi kwa kipato na misingi ya utafa tuu kweli balaah sasa ndi hivi amua.......
 
Tanzania tuna matatizo mengi sana, elimu, afya, barabara, maji etc.Ndio, sisi ni taifa huru, lakini kwanini tutumie uhuru wetu kujiingiza kwenye migogoro isiyotuhusu? Na inakuwaje tunajiingiza kwenye huu mgogoro wakati huo huo Marekani wako kila kona, kila sehemu nyeti nchini kwetu? Uhuru wetu tunautumiaje?

Pili, kuna mambo yananza kuleta mashaka. Kwenye sherehe za miaka 50 hakuna rais yoyote kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki alikuja! Uhusiano wetu ukoje? Wazamiaji haramu wanaingia kila kona na tafsiri yake ni kwamba mipaka ya nchi haiko salama, watu wanafika Dodoma bila kuzuiwa, wangekuwa na silaha? Makampuni ya ulinzi ya nje tena yenye silaha kubwa yapo nchini!

Sasa kama haitoshi tunajiingiza kwenye mgogoro kati ya nchi za magharibi na Iran.
 
Kuna watu wanadanganyana sana ndani ya system zetu za maamuzi. Hiyo ya kuflag meli za Iran sijui wamefikilia nini. Na madaktari nao si tunawapata kutoka Iran?
 
Yametimia sasa Mapungufu katika muungano haya hapa. Zanzibar wanasajiri meli halafu inatumia bendera ya Tanzania. Kwa nini wasitumie ya Zanzibar. Halafu tunaingia migogoro ya kimataifa, kimataifa wanaijua Tanzania. Kikwete anapigwa barua wakati jambo limefanyika Zanzibar (mapungufu ya muungano). Je hawa jamaa wakiamua kutupiga nani atakuwa responsible?

Hapa tumeingia mkenge tuyamalize yetu kwanza. Hawa wamarekani naona wametukamata sasa hili hatutoki.
 
Chochote semacho mtu huwa ni kile kinaoujaza moyo wake.Baada ya uchaguzi uliopita walisema waliyokuwa nayo kwa kusema kuwa uchaguzi uo ulitawaliwa na udini! Kujiingiza kuisaidia Iran ni swala hilohilo la udini. Watu wengine wasingethubutu kufanya hivyo.
 
Nadhani wangeanza tuu na izo sanctions naona hawa vibaraka wa CCM wajue inchi wanakipeleka siko!
Its time CCM iende angalau tupate chama kingine.
Naona apo patamu angalau safari za USA zitapungua ili kusave for our bajeti!
 
Tumekwisha jamani, tuchukueni hatau wenyewe kata serikali haitaokoa nchi yetu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom