Tanzania Now Faces Sanctions & Diplomatic Crisis Over Iran

Tanzania Now Faces Sanctions & Diplomatic Crisis Over Iran

Status
Not open for further replies.
Please smone assure me if the The Tanzanian President knows exactly what he is doing ... !
 
nngu007,
Mzee Bush ni major shareholder katika kampuni ya Barrick. Na kupitia kwake ndivyo Sinclair alivyofanikiwa kuwakutanisha Bush mdogo na Kikwete katika ziara ya pili ya Kikwete hapa Marekani. He owns shares in the company.

You R Right... Completely Right ... From Senior Bush to Junior Bush...

George Herbert Walker Bush, whose father was a part*
ner in the powerful London-controlled private banking firm
Brown Brothers Harriman. Relevant to the Barrick story,
Bush was U.S. vice president and chief of covert operations
in the Reagan-Bush (1981-89) administration, and U.S. Presi*
dent (1989-93). As a former President and power broker, Bush
is Barrick Gold Corp.' s chief lobbyist, a stockholder in Bar*
rick, and honorary senior adviser to Barrick's international
advisory board.
 
George Bush Sr has a stake in Barrick Gold. It goes way back to Nevada mines with Adnan Kashoggi (Barrick Gold Founder). Mambo ya dunia hii ni zaidi ya ujuavyo..mpaka uunganishe Dots ndio utapata picha kamili. Bush family wana utajiri mkubwa sana ..baadhi ya utajiri wao unatoka kwenye migodi yetu. Kwa hiyo usishangae kwa nini mkulu anapenda sana kwenda Marekani.

Thanks... Completely Right...
 
Ni kuvunja muungano tu ndo soln. Kumbe sio kikwete ni serikali ya mapinduzi. Ndio juzijuzi nilisikia kuna baraza la usalama, mie nilifikiri ni kwa sababu ya Dr Uli, kumbe ni hili sakata.


Ndiyo zao hizo Magamba DHAIFU wanapokuwa hawana hoja basi wanatumia ubabe kufukuza watu bungeni, lakini kiama chao hakiko mbali. Miaka michache ijayo watasambaratishwa kama alivyowahi kutabiri Mwalimu.
 


Bravo USA-JK asituletee matatizo TZ imesaini mkataba wa kupambana na magaidi kwa nini magaidi watumie bendera yetu nasi tutaonekana tuna-support ugaidi,I support US.


Nipe Definition ya ugaidi au gaidi..?!
 
this shows how much insane you are. huyo jamaa ni member wa bunge dogo la marekani na hata siyo senator halafu anamwandikia barua raisi wa nchi anamchimba mkwala na bado unaona ni vyema tu hivi hapa Tanzania mbunge wa Tz anaweza hata kuonana na obama achana tu na kumwandikia barua.

kubali ukatae Raisi wenu anadharaulika sana pamoja ni kujikomba sana kwa hao wazungu(mzungu worshiper) lakini bado anadharaulika sana
Na wewe umekurupuka bila hata kujitawaza. Point yangu ilikuwa Huyo Berman sio Ofisa wa Wizara Kama alivyoandika jamaa niliyemquote.
b) hata Kama ni member wa Bunge dogo au kubwa wewe unajua kazi ya House of the Reps???
Mbunge wa Tanzania unawezaje kulinganisha na Congressman Berman!!?? Are you out of your little mind!!

c) Kama unafikiri Berman ni mtu mdogo ngoja uone reaction ya hiyo barua ndio utajua wenzetu wanafuata sheria na sio Cheo au madaraka.

Read between the lines kabla hujakurupuka. Wassira mkubwa wee
 
Duh... ama serikali hii kweli sasa imechanganyikiwa ile mbaya... madudu kila sehemu, nje, ndani, kushoto, kulia, juu, chini. Kwa nini lakini?
Hayo ndiyo malupulupu ya kutegemea nguvu za majini kutawala nchi!! Hana ulinzi tena! Yale majini yake Sheikh Yayha alishuka nayo kuzimu!!
 
VILAZA SOMENI HAPATAARIFA JUU YA USAJILI WA MELI ZANJE ULIOFANYWA NA SMZ
TAARIFA KWABARAZA LA WAWAKILISHI JUU YA
USAJILI WA MELI ZA NJE ULIOFANYWA NA SMZ
KUPITIA MAMLAKA YA USAFIRI BAHARINI
ZANZIBAR MARITIME AUTHORITY – ZMA
Friday, June 29, 2012

Mhe. Spika,
Tarehe 27/06/2012 Vyombo vya Habari hapa Tanzania (The Citizen) na nchi za nje(International news Agency – Bloomberg) viliandika makala kuhusu usajili wameli 10 za mafuta (Tankers). Ilidaiwa katika makala hayo kuwa Meli hizozilisajiliwa Zanzibar na zinapeperusha Bendera ya Tanzania na kwamba zinafanyabiashara na Kampuni ya Serikali ya IRAN. Gazeti la “The Citizen la tarehe 27Juni, 2012 lilikuwa na kichwa cha habari “Iran Tankers adopt TZ Flag to avoidembargo” (meli za mafuta za Iran zinatumia bendera ya Tz kukwepa vikwazo.

TAARIFA YA ZMA
Mamlaka yaUsafiri Baharini Zanzibar Maritime Authority – ZMA ni Mamlaka iliyoundwa kwasheria No. 3 ya mwaka 2009 ambayo pamoja na kazi nyengine inasimamiautekelezaji wa Sheria ya usafiri wa Bahari Zanzibar ya mwaka 2006 (Zanzibar MaritimeTransport Act 2006).
Sheria yaZanzibar Maritime Transport Act 2006, kifungu no. 8 cha sheria hii, kinasomekakama ifuatavyo:
Section 8 (1).There shall be established the registers of Tanzania Zanzibar ships to be Knownas:-
o (a). TanzaniaZanzibar International Register of Shipping for ocean going ships; and
o (b) TanzaniaZanzibar Register of Shipping for coastal Ships.
• (2). A shipshall be a Tanzania Zanzibar ship for the purpose of this Act if that ship isregistered under this part.
Katika kutekelezajukumu la usajili wa meli kama ilivyoelekezwa katika kifungu 8(1)(a) hapo juu,Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetiliana mkataba na kampuni ya PHILTEX yaDubai kufanya usajili wa meli za kimataifa. (Open Registry). Usajili huuumekuwa ukifanyika tangu mwaka 2009 na mpaka sasa ZMA kupitia Wakala wakeimesajili meli 399 ikiwa ni pamoja na meli za mafuta, makontena, General cargona meli za Abiria.
Kamanilivyoeleza hapo awali, vyombo vya habari vimechapisha makala ya usajili wameli 10 ambazo zinadaiwa ni meli za IRAN kulingana na makala zao hizo.
SMZ inatoataarifa rasmi juu ya meli za mafuta ilizosajiliwa wiki mbili zilizopita pamojana majina ya meli, ukubwa wake, majina ya makampuni inayomiliki meli hizo nanchi zilizotoka kabla ya kupata usajili kwa ZMA, kama ifuatavyo:
Jina la meliGRT (Ukubwa) Company name Ilikotoka
1. Daisy 81479Daisy Shipping Co. Ltd Malta
2. Justice164241 Justice Shipping Co. Ltd Cyprus
3. Magnolia81479 Magnolia Shipping Co. Ltd Malta
4. Lantana81479 Lantana Shipping Co. Ltd Malta
5. Leadership164241 Leadership Shipping Co. Ltd Cyprus
6. Companion164241 Companion Shipping Co. Ltd Malta
7. Camellia81479 Camellia Shipping Co. Ltd Malta
8. Clove 81479Clove shipping Co. Ltd Malta
9. Courage163660 Courage Shipping Co. ltd Cyprus
10. Freedom163660 Freedom shipping Co. Ltd Cyprus
11. valor160930 valor Shipping Co. Ltd. Cyprus
Jumla ya GRT ni1,388,368 tons
Meli hizi ni 11kama zinavyoonekana katika orodha hapo juu ni miongoni mwa meli nyingizinazobadilisha usajili wao (De registration). Meli zilizosajiliwa na ZMAzinatoka nchini Cyprus na Malta. Sambamaba na meli hizi 11 zilizosajiliwa naZMA, meli za mafuta nyengine 20 ambazo zinasemekana zilikuwa kwenye usajili wanchi za Ulaya zimebadilisha usajili wao na kwenda usajili wa “TUVALU Islands”.
ZMA ilimtakaWakala wake Philtex Corporation kuwaita wenye meli hizi na kuwataka kujielezakuhusu uhusuiano wao na Serikali ya au makampuni ya mafuta ya IRAN. Philtexilikutana na Wamiliki hao siku ya Alkhamis tarehe 28/06/2012 katika afisi zaPhiltex Corporation na Wamiliki hao wameeleza kwamba hawana uhusianao naSerikali au mamlaka yoyote nchini Iran na wameamua kuja kusajili meli ZMA kwaridhaa yao na kwa kufata matangazo ya usajili wetu wa nje (Open Registry).
Pamoja namaelezo hayo, wamiliki hao wametangaza kwamba ikiwa ZMA haiko tayari kuendeleana usajili wa meli zao, wanaweza kufuta usajili wao na tayari wanafikiriakufanya mazungumzo na open Registry nyengine (PANAMA) lakini hawana nia yakurudi walikotoka, yaani Cyprus na Malta.
Kinyume namaelezo yaliyotolewa na vyombo vya habari juu ya uraia wa wamiliki wa melihizi, Wamiliki wa meli hizi kama walivyojieleza katika usajili wa meli zao wanauraia wa British Vergin Islands na Sychelles.
Kulingana na“United Nations Convention Law of the Sea”, Article 91, na za “Genevaconvection of Registration” articles 6, 7 na 8, na kulingana na ZanzibarMaritime Transport Act of 2006, section 8, Zanzibar ikiwa ni nchi moja kati yanchi mbili zinazounda Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayo haki ya kusajilimeli yeyote kulingana na taratibu na Sheria za Zanzibar, na sheria za Kimataifazinazoongoza usajili huo.
Maelezo hayayanatolewa ili kutoa usahihi wa uvumi kuwa Zanzibar imesajili meli za IRANambazo zimewekewa vikwazo na Marekani na nchi za Umoja wa Ulaya (EuropeanUnion) juu ya usafirishaji na uuzaji wa mafuta kutoka Iran.
Mhe. Spika,taarifa hizi za vyombo vya habari hazina madhumuni yeyote zaidi ya kuwavunjamoyo wenye Makampuni ya meli wanaotaka kusajili meli zao kwetu.
Hivyo basiSerikali inatamka wazi kwamba Usajili uliofanywa kwa meli hizi umefuatataratibu zote zilizowekwa kisheria na kwamba Serikali imekuwa ikifanya naitaendelea kufanya mazungumzo na wenye meli mbalimbali ili kuongeza idadi naukubwa wa meli inazosajili nje ya nchi. Biashara hii ya ukubwa wa GRT 1,388,368Tons katika kipindi cha wiki mbili na maombi mapya matano kwa meli zitakazokuwana ukubwa wa zaidi ya GRT 500,000 imeshtua Makamuni mengine na hata nchinyengine zisizoitakia mema Zanzibar katika juhudi zake za kukuza mapato nauchumi wake.
Hata hivyomamlaka itafata sheria zote zilizowekwa kitaifa na kimataifa katika biashara yausafiri baharini na itahakikisha meli zinasajiliwa chini ya mamlaka hiizinafata taratibu ilizoweka.
Mhe. Spika,kabla ya taarifa hizi za vyombo vya habari (The Citizen), Waziri wa Uchukuzi waSMT Mhe. Harisson Mwakyembe) alipokuwa akijibu suala Bungeni hivi juzihakuonyesha kurishika kwake katika usajili wa meli (Open Registry) inayofanywana Zanzibar na kuahidi kufanya ziara ya kuja Zanzibar kuonana na Wazirianaehusika kuzungumzia suala hili. Taarifa za “The Citizen” zaweza kuwa nimuendelezo wa Mhe. Mwakyembe kutoridhika kwake katika usajili unaofanywa naSerikali kupitia uwakala wake huko Dubai.
Mhe. Spika,Zanzibar haifungiki kusajili meli za nchi yeyote.
Hili ni sualala kibiashara na kwamba kwa Serikali yetu ni njia moja ya kuongeza mapatoyanayoendesha Serikali, alimradi tu usajili huo hauvunji sheria za Kimataifa.
Mhe. Spika,
Zanzibar ina uhusianomkubwa na wa muda mrefu na nchi nyingi ikiwemo IRAN na hivi karibuni Zanzibarilipata ugeni (Makamo wa Rais wa Iran) na viongozi wetu walifanya mazungumzo yanamna gani IRAN itaendelea kusaidia Zanzibar katika miradi ya Maendeleo.Zanzibar haingependa kuingizwa kwa visingizio vyovyote na kwa njama zozotekatika migogoro isiyowahusu.
Hivyo, kwataarifa hii, Serikali inakanusha rasmi uvumi wa vyombo vya habari kuhusiana nasuala hili kama taarifa hii ilivyofafanua hapo juu.
Mhe. Spika,naomba kuwasilisha.
Hamad MasoudHamad
WAZIRI WAMIUNDOMBINU NA MAWASILIANO

 
Kweli tanzania hatuna viongozi mpaka tunaamua kushirikiana na iran isiyo na msaada wowote kwetu na viongozi wetu wanajua kabisa usa tunao wategemea kwa misaada pamoja na utalii wa rais wetu ni maadui wakubwa wa iran.
 
SIJAONA onyo lolote kwenye barua husika....sana sana nilichoona ni diplomatic request(I respectfully request that Tanzania cancel the re-flagging of the NITC vessels) iliyotolewa na kinara wa vikwazo dhidi ya Iran(Rep. Berman has been a champion of Iran sanctions in Congress, building), Rep Berman. Hili nalo, ni jambo la kawaida kabisa ambalo hata kama lingefanywa na nchi yoyote bado similar REQUEST ingetolewa tu! By the way, how much does it cost for a tanker to have a flag of country X?! Mbona hata meli za maharamia huwa na bendera za nchi mbalimbali duniani hata kama hawakuzipata kihalali!!
 
Kumbe uamsho walikuwa na kiburi cha fedha za Iran! Wamekatiwa mirija sasa wakunje mikia!
 
Inadaiwa hizi meli zilisajiliwa Zanzibar maana Znz inaruhusu reflaging ya meli za nje. Hii implication zake kama SMZ ikikataa kuzitoa hizo meli kwenye usajili ni kubwa. Maana ukiangalia sisi serikali yetu ni tegemezi sana na hata kama tusingekuwa tegemezi hii dunia ecosystem yake inategemea sana USA na Ulaya, mfano angalia hao Iran wanavyohaha sasa kutafuta mtu wa kuweka bendera kwenye meli zao.

Nafikiri muda huu tunaoongea simu ziko busy kati ya JK, Karume na mawaziri wao wa transport pamoja na wakala husika, hili si jambo dogo, kasheshe hapo...

Chezea marekani wewe zitapigwa na drones!.
 


I am writing to express my
deep dismay that Tanzania..... has permitted the National Iranian Tanker Company (NITC), to reflag at least 6 and as many as 10 of its vessels under the Tanzanian ship registry,

This action by your government has the
effect of assisting the Iranian regime in evading U.S. and EU sanctions and generating additional revenues for its nuclear enrichment and weapons research programs and its support for international terrorism.

It is
profoundly disappointing to me to learn that your government has acted in contravention of the broad international coalition that is working together to use peaceful means, including economic sanctions, to change the threatening behavior of the Iranian regime.

It would be preferable that Tanzania take this action of its own accord.

...In my view, reflagging Iranian oil tankers falls within the scope of sanctionable activity under that Executive Order.

Nimejaribu kusoma tena hiyo barua, hebu angalieni kwenye red. Inaelekea huyu Seneta alikuwa na high hopes kwa rais wetu lakini mambo yamekuwa ndivyo sivyo.

Lakini sehemu iliyonistua ni hapo kwenye blue, anametumia maneno own accord. Hii ni aibu kweli kweli kwetu sisi Tanzania. Basically, anatuambia either we do it or else. Membe aling'aka sana na kauli ya Cameroon, sijui kama atakuwa na msuli wa kujibu hii order kwa mtindo ule ule? Tukiondoa flag ni aibu maana tunapata order toka nje (uhuru?), tusipoondoa ni mtihani (njaa?). ah, tumepatikana!
 
SITAKI...NATAKA!!
Sitaki vikwazo vya kiuchumi kwa nchi yetu kwani tupo tayari taabani kwa matatizo mengi nchini!
Nataka vikwazo,hivi vinaweza kutukumbusha kuwa tuna madini,gesi,ardhi,misitu na rasilimali kemkem!!
Hivi vingeweza kutumika kwa maslahi ya nchi yetu na kuepuka dharau hizi zinazo oneshwa na mabeberu!
 
so far hakuna aliyeleta hiyo sheria ya kimataifa ambayo Tanzania imekiuka

sasa tunajadili upepo?
 
Marekani usitupangie marafiki naona humu kuna watumwa wa kiakili wanadhani Marekani wapo kwa ajili ya kutetea wanyonge hawajua kama Marekani yeye pesa ndio kitu cha kwanza...mbona mmekaa kimya Marekani kachukuwa migodi yenu yote kwa mkataba wa miaka 99 kuchimba dhahabu.

Pamoja sana Mkuu!!! Tanzania haifungamani na Nchi yoyote (NAC). Hawa USA wanajipambanua kuwa Hawana Maadui wa Kudumu wala MARAFIKI wa Kudumu - MASLAH YA TAIFA LAO SIKU ZOTE HUTANGULIZWA MBELE!!! Mbona Wanachimba URANIUM SELOUS Kinyume na Mikataba ya kimataifa? 100% ya GOLD zetu zinachukuliwa na USA...Tunafaidika kwa madini yetu kukwapuliwa???!!! WEZI HAO ...

JK anatakiwa awe kama KIBAKI yeye alisema wazi kuwa anageuka kutoka WESTERN Block anahamia EASTERN Block, since then WAKENYA wametuacha mbali sana kiuchumi ...

Kamwe USA haijawahi kuzisaidia nchi masikini duniani ...
 
Ndiyo zao hizo Magamba DHAIFU wanapokuwa hawana hoja basi wanatumia ubabe kufukuza watu bungeni, lakini kiama chao hakiko mbali. Miaka michache ijayo watasambaratishwa kama alivyowahi kutabiri Mwalimu.

Nasikia smz wamegoma kufuta hizo meli, wazanzibari washikilie msimamo huo huo, wapeperushe meli za washiraz kwa bendera ya Tz. Ili kikwete atambue kwanini tunamwambia avunje muungano.
 
Nasikia smz wamegoma kufuta hizo meli, wazanzibari washikilie msimamo huo huo, wapeperushe meli za washiraz kwa bendera ya Tz. Ili kikwete atambue kwanini tunamwambia avunje muungano.

Hawa Wazenj si inadaiwa tayari wana bendera ya Taifa lao la Zenj? au hakuna kitu kama hicho? Kama wana bendera yao basi waruhusu bendera yao itumike badala ya ile ya Tanganyika.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom