Mhache
JF-Expert Member
- Jun 20, 2008
- 345
- 24
Serikali ya awamu ya nne imepata misukosuko mingi sana. Sina maana kwamba serikali zilizotangulia hazikuwa na misukosuko kama hiyo. Ilikuwepo kwa kiwango chake. Maamuzi yanayogusa maisha ya watu yanafanywa bila kufanyika kwa utafiti wa kina. Kwa mfano wafanyakazi wanatakiwa kupandishwa vyeo ambavyo vyeo hivyo hutakiwa kufuatwa na fedha kiasi fulani. Ni kwa nini kitengo kinachohusika kisiwe na maandalizi ya kutosha ili kukwepa matatizo yanayoweza kujitokeza likwepo suala la migoma isiyokuwa na tija.
Migomo imekua kila kukicha ikiwa ni suluhisho la wahusika kupata ufumbuzi wa matatizo yao. Kwa mfano tishio la walimu kugoma. Zoezi hili limewezesha walimu kadhaa japo sio wote kupata haki yao. Muhimbili wametishia kugoma, jana serikali imetoa tamko tarehe ya kuwalipa madai yao 23/09/2009. Je tumekuwa kama kichwa cha wenda wazimu? Serikali ni lazima iamshwe kwa matishio ya migomo ndio haki itoke.
Migomo imekua kila kukicha ikiwa ni suluhisho la wahusika kupata ufumbuzi wa matatizo yao. Kwa mfano tishio la walimu kugoma. Zoezi hili limewezesha walimu kadhaa japo sio wote kupata haki yao. Muhimbili wametishia kugoma, jana serikali imetoa tamko tarehe ya kuwalipa madai yao 23/09/2009. Je tumekuwa kama kichwa cha wenda wazimu? Serikali ni lazima iamshwe kwa matishio ya migomo ndio haki itoke.