Tanzania ina Simu za Mkononi za Kawaida na Smart Phone zaidi ya Milioni 70.6 zinazotumika kila siku

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
1698257683083.png

Kati ya Juni hadi Septemba 2023, kulikuwa na Vifaa 70,613,504 vya Mawasiliano ya Simu za Kawaida (Feature Phone) na Simu Janja (Smart Phone) zilizounganishwa na Mitandao ya Simu sawa na 83% ambapo Simu Janja zilikuwa Milioni 18.9 na Simu za Kawaida za Mkononi (Feature Phone) zilikuwa Milioni 51.6.

Ripoti ya Huduma za Mawasiliano iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeonesha hadi kufikia mwishoni mwaka Septemba, kulikuwa na Vifaa vya Mkononi vilivyounganishwa na Huduma za Mawasiliano 1,698,654, Modem 562,325 na vinginevyo 838,817.

Simu za Kawaida (Feature Phone) zimechukua zaidi ya 70% ya Vifaa vilivyounganishwa na Mawasiliano huku Simu Janja (Smart Phone) zikichukua nafasi ya pili kwa 25.72%
 
Kwa mfano Mimi Iko na two, na mleta mada Iko having two = 4
Si ndio maana simu zimekuwa nyingi kuliko makadirio ya watu wanaoishi Tanzania.
Mfano mimi nina simu mbili na zipo active hivyo, zote zimejumuishwa
 
Saa hii kila mtu ana smart nyie, hivyo vitochi ni ajili ya kulinda chaji tu, nafikiri kinyume ndio sahihi,
Sipingi tafiti ila nimedokeza tu
 
Back
Top Bottom