Game Theory
Platinum Member
- Sep 5, 2006
- 8,545
- 835
Mnahitaji kuipata sheria ya mabadiliko ya 14 ya Katiba.
Mnahitaji kuipata sheria ya mabadiliko ya 14 ya Katiba.
Mnahitaji kuipata sheria ya mabadiliko ya 14 ya Katiba.
NA KWA KUWA misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika
jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na
Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha
wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu
wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo
kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na
kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu:
KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE
MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii
kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania
inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia
na ujamaa.
Vyombo vyenye mamlaka ya utendaji vitakuwa ni
Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, vyombo vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki
vitakuwa ni Idara ya Mahakama ya Serikali ya Jamhuri ya
Muungano na Idara ya Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, na vyombo vyenye mamlaka ya kutunga sheria na
kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma vitakuwa ni
Bunge na Baraza la Wawakilishi.
Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka
yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo
ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake
39.-(1) Mtu hatastahili kuchaguliwa kushika kiti cha Rais wa
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama-
(b) ametimiza umri wa miaka arobaini;
(c) ni mwanachama, na mgombea aliyependekezwa na
chama cha siasa;
34.-(1) Kutakuwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano
ambayo itakuwa na mamlaka juu ya mambo yote ya Muungano
katika Jamhuri ya Muungano, na pia juu ya mambo mengine yote
yahusuyo Tanzania Bara.