TANROADS mna mpango gani juu ya barabara ya kimkakati inayotoka Kimara Mwisho kuelekea Tabata (Bonyokwa-Segerea-Kinyerezi)?

Mkono Mmoja

JF-Expert Member
Jan 26, 2019
1,932
4,086
Habari za wakati huu!

Moja kwa moja nawaelekea TANROADS kuhusu hii barabara ya kimkakati inayoanzia darajani kimara mwisho kuelekea tabata bonyokwa mpaka tabata segerea.

Kwa muda mrefu hii barabara imekuwa ikisahaulika kuwekewa lami ilihali ina umuhimu mkubwa sana wa kupunguza foleni ya magari yanayoelekea ubungo kwa kutoa shortcut nzuri kufika tabata pasi na kupitia ubungo kwa wale wanaotokea mbezi na goba.

Barabara hii imekuwa ikileta usumbufu kipindi cha mvua kutokana na kutokufanyiwa matengenezo yoyote.

Wito wangu kwa wizara ya ujenzi na uchukuzi kupitia TANROADS na TARURA kuhakikisha hii barabara inawekwa lami kwani imekuwa ikitumiwa na magari mengi na ni shortcut nzuri sana kwa wale wanaotokea mbezi kuelekea tabata bonyokwa, segerea,kinyerezi,ukonga na gongo la mboto.
 
Naunga MKONO hoja, barabara hiyo ni muhimu sana..shida nguvu kubwa inapelekwa Mbweni..sehemu ambako hakuna wakazi ni mahekalu tu matupu..kazi kweli kweli
 
Naunga MKONO hoja, barabara hiyo ni muhimu sana..shida nguvu kubwa inapelekwa Mbweni..sehemu ambako hakuna wakazi ni mahekalu tu matupu..kazi kweli kweli
Ni barabara yenye watumiaji wengi mno wakazi wengi wa kimara na tabata hutumia barabara hii ila miaka nenda miaka rudi zimekuwa zikiletwa siasa tu. Kipindi cha Magufuli ilisuswa kwasababu ya siasa, Mbunge wa Jimbo alikuwa akitokea chadema. Mama nae kaingia ameisusa tu hakuna maendeleo yoyote kwa ukanda huu.
 
Hakika barabara hii ni muhimu mno...
Unakata kona hapo kituo cha msikitini, unapita kwa Mahita, Bonyokwa, Kwa Kichwa... chap unaiona Stop Over hii hapa....
Bonge la shortcut.....
 
Habari za wakati huu!

Moja kwa moja nawaelekea TANROADS kuhusu hii barabara ya kimkakati inayoanzia darajani kimara mwisho kuelekea tabata bonyokwa mpaka tabata segerea.

Kwa muda mrefu hii barabara imekuwa ikisahaulika kuwekewa lami ilihali ina umuhimu mkubwa sana wa kupunguza foleni ya magari yanayoelekea ubungo kwa kutoa shortcut nzuri kufika tabata pasi na kupitia ubungo kwa wale wanaotokea mbezi na goba.

Barabara hii imekuwa ikileta usumbufu kipindi cha mvua kutokana na kutokufanyiwa matengenezo yoyote.

Wito wangu kwa wizara ya ujenzi na uchukuzi kupitia TANROADS na TARURA kuhakikisha hii barabara inawekwa lami kwani imekuwa ikitumiwa na magari mengi na ni shortcut nzuri sana kwa wale wanaotokea mbezi kuelekea tabata bonyokwa, segerea,kinyerezi,ukonga na gongo la mboto.
Ninyi huko mna kila kitu kuanzia Fry over,BRT na barabara nzuri Hadi mitaani.
Sisi huku Karagwe na Kyerwa ni vumbi Mwanzo mwisho na ni barabara za kimkakati katika uzalishaji wa kahawa,utalii na madini ya bati.
Kuna jambo Tanroads makao makuu inabidi iwe wazi ili maendeleo ya Dar yasikwamishe mikoa ya pembezoni.
Chonde chonde barabara nzuri sio kwa Dar pekee.
 
Back
Top Bottom