Tangulia Lukuga, Dkt. Amani Walid Kabourou - Kinara wa Mageuzi ya Vyama Vingi Nchini. - Mwami Kabuyuki, Mwamba wa Kigoma

Yeye ndiye aliyepandikiza mbegu nzuri ya Watanzania kukataa kuburuzwa na kusimamia haki zao, ambapo kupitia kwake mwanga wa ukombozi katika siasa za vyama vingi ulienea kote nchini.

Jambo hili alilifanya zaidi hapa Kigoma, kwa maana nyingine, Kigoma ndio mkoa wa kwanza kuonesha kwa vitendo utayari wa kupokea vyama vingi nchini, yote ni kwa sababu ya kazi ya ‘Uamsho’ ya Dkt. Kabourou. Ni mbegu hii ya mageuzi aliyoipanda ndiyo iliyofanya wakati flani Mkoa wote wa Kigoma ukawa na idadi kubwa ya wabunge kutoka vyama vya upinzani.

Namkumbuka sana Dkt. Kabourou, nilipenda sana jina lake. Nilipenda alivyojiamini. Poleni wana Kigoma na watanzania kwa ujumla.

Lakini tutoapo wasifu wa marehemu, basi tusiongezee na hisia zetu. Unasema kupitia yeye ukombozi wa vyama vingi ulienea chini. Na kuna sehemu unasema yeye alikuwa mbunge wa kwanza wa upinzani basi ni vema ukasema kwa Kigoma.

Ninachokumbuka vuguvugu la vyama wakati huo kabla halijaanza, kuna watu kama Mtikila waliokuwa wanaleta vuguvugu, hata mfumo wa vyama vingi kuanzishwa. Kuna akina Mabere Marando, Kasanga Tumbo, Kuna Mzee Mapalala, Mzee Mtei, na wengineo ambao hawa waliongoza kuweka vuguvugu la kudai vyama vingi bila kumsahau Oscar Kambona. So unaposema kupitia kwake mwanga wa ukombozi ulienea nchini je waliokuwepo kabla ya yeye kuja toka Marekani?

Pia kudai Kigoma ilionesha mfano si kweli kwani wakati huo kuna majimbo yaliyotoa wabunge wa upinzani, kama Kilimanjaro, Arusha, Mara amabako Balozi Ndombho alishinda kwenye jimbo la Baba wa taifa Mwl Nyerere kama mpinzani. Akina Marando walikuwa wabunge pia wote toka upinzani.

Mhe. Zitto tueleze historia ila tusipindishe histroria ili kukuza mambo.

Wakati huo wasomi wengi walirudi nchini. Nakumbuka Cheyo Chama chake kilitikisa maeneo ya Shinyanga hasa huko Bariadi. Sasa, ukisema alikuwa mbunge wa kwanza bila kuchanganua wapi inaonesha kama yeye ndiye alikuwa mwanamageuzi wa kwanza Tanzania.

Namkubali, na nilimpenda sana. Ila tuwetunaweka historia sawa. Si kueleza kwa hisia binafsi. Asante kwa mengine yote uloeleza kikubwa ni kumuenzi kwa kile alichosimamia.

Mungu amlaze mahala pema. Amen!
 
اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُ وَارْحَمْهُ، وَعَافِهِ، وَاعْفُ عَنْهُ، وَأَكْرِمْ نُزُلَهُ، وَوَسِّعْ مُدْخَلَهُ، وَاغْسِلْهُ بِالْمَاءِ وَالثَّلْجِ وَالْبَرَدْ، وَنَقِّهِ مِنَ الْخَطَايَا كَما نَقَّيْتَ الثَّوْبَ الأَبْيَضَ مِنَ الدَّنَسِ، وَأَبْدِلْهُ دَاراً خَيْراً مِنْ دَارِهِ، وَأَهْلاً خَيْراً مِنْ أَهْلِهِ، وَزَوْجاً خَيْراً مِنْ زَوْجِهِ، وَأَدْخِلْهُ الْجَنَّةَ، وَأَعِذْهُ مِنْ عَذَابِ الْقَبْرِ وَعَذَابِ النَّارِ

Jazakallahu khair Zitto, tunahitaji watu waandike zaidi kwa wanasiasa na watu maarufu ili kizazi kipya kijufunze historia yetu, mie ni mtu wa Tabaora natamani sana kama watu wangendi ka kuhusu wanasaiasi na watu mashuhuri wa mkoa wetu.

Pia shukran kwa kuandika kuhusu Samwel Sitta
 
Ni kweli alikuwa jabali la siasa la mageuzi ya vyama vingi, lakini hakumaliza safari yake vizuri ktk kuleta mageuzi.

Alifanya makosa kurudi CCM hata kama kulikuwa na mivutano ktk chama chake cha upinzani.
 
Wote walikijenga CHADEMA kwa wakati wao na uhuru wao wa mawazo na maamuzi uliwaondoa chadema. Kaburu kamaliza muda wake na katuachia historia. Inasikitisha kuwa amefariki akiwa mwanachama wa CCM.

Zitto keshasema tujitafakari, tumalize tofauti zetu za ndani bila ya kutengana kwa kuhama au kufukuzana. Labda amebaini shida ya kuondoka CHADEMA na kuachwa na washirika wake. Tumpe muda atafakari na kasema atatukuta ngeke.

Sasa ni muda wa msiba, maombolezo ya kifo cha mtu, tuungane na familia na jamii kumzika mzee wetu. Tusifanane na wapinzani wetu wanaojali vyeo na maslahi binafsi kuliko utu, na wabo tayari kwa gharama yoyote. Kuwa chadema lazima uheshimu demokrasia na maendelea kwa vitendo. Ukiweza karibu Ujiji ushiriki kwa vitendo mazishi au la unaweza hata kutwiti kama wengine waliobize.

Nawapa pole familia, kigoma, ccm,chadema na watanzania kwa msiba huu. Mungu awafariji wote.
 
Hakika Chadema wanapaswa kumuenzi mwamba huyu, kumuita msaliti ni kumkosea heshima maana kumbe hata Ofisi wanayotumia leo alinunua yeye.
Haha, Hakika Mwenyezi Mungu angekuwa mwanadamu hukumu ingekuwa ngumu. Sidhani km marehemu hakujua nafasi aliyoichukua ingempa jina gani hadi kufa. Ya siasa yameishia ktk hukumu ya siasa, Yamebaki ya Mungu.

Tuache kufanya mambo ya wasio na tumaini mbele ya Mungu na hukumu zake. Hakuna jema wala baya iwapo tuyasemayo yatakuwa kweli km ilivyo kweli bila kumdhalilisha. Ni kujilisha uchafu na kununu dhambi km tutasema yatupendezayo macho n masikioni mwetu,ila ikawa ni uongo MBELE YA MUNGU.

Kwa waliobaki, ile kweli tuichukiayo ndio inayostahili kusema ili wasiyoipenda wajirekebishe ili wastahili kuambiwa wanayoyapenda.
 
Kaburou ndiye alimfunza Mbowe siasa.
Sidhani km inaleta maana sana kusema Ronaldinho kwa vile alipewa jukumu la kumuongoza Messi ktk chumba cha wakubwa ndio alimfundisha mpira. Tufikie mahali tuache kuzidisha ujinga hadi kuharibu kila kitu.Mbowe alikuwa mwanasiasa mwenye vigezo vya kuingi ktk chama,kuwa karibu na mkongwe ili kuanza ppitia miendendo ya chama hakumaanishi asingekuwa mwanasiasa bila kaburu.Sidhani km Kaburu alikuw ana somo la siasa za zaidi yake ambazo alimfundisha Mbowe tuu na yeye hakujifunza.
 
Huyu Kabourou akiwa CHADEMA mwaka 1994 nakumbuka watu wengi walipigwa, wengine vilema wengine walikufa kwa ajili yake.

Badae akaja kuhama CHADEMA na kuhamia CCM na kusahau yote yaliyotokea. Huyu mtu hatokuja kusahaulika ktk historia ya wana Kigoma.
Teh teh. Mkuu sio muda wa kumhukumu ingawa Idd Amini,Hitler,Karl Peters na wengine tunawalaani sana ingawa akina Kinje,Mkwawa na wengine tunawaita mashujaa ghafla wakati tunaowalaani wanaushiaid mzuri sana wa dili za utumwa za hawa jamaa.Ila ningeshauri wanaotaka futa baadhi ya vitu vya kujifunza ktk njia za huyu mzee wetu, wanakosea sana.

Mzee alipitia njia nyingi,alibadili njia sana, na ktk njia aliacha watu njia panda sana.aliumiza wengi sana hadi anakuafa.Na walikuwa hai na wapo hai. Km yeye mwenyewe hakufanya jambo la suluhu ni wazi alipenda historia yake.Kwanini leo watu wafute kwa kutaka kusema mashairi wayapendayo?Nini tutajifunza kwake, nini tutajifunza kuacha na nini tutajifunza kuendelea fanya.?
 
Rip MZEE Labour, hongera Mh. Zito kwa kutujuza. Kiukweli Mimi nilimfahamu kwa jina 1994 nikiwa kidato cha NNE kupitia matangazo ga REDIO BBC nafikiri, enzi hizo Mrema alikuwa zaidi ya Lissu kwa sasa japo vyombo vya habari nilikuwa vichache.
Nimependa jinsi mlivyomuelezea.
Nimependa harakati za Mzee Mtei kuhakikisha Chama chske kinapsta vichwa vizuri HD kusafiri kumfuata MTU America kumshawishi. Waliwaza mbali sana. Hongereni.
 
Dkt Amani Kaborou pamoja na harakati zake zote za siasa amefariki akiwa mwanachama wa CCM hiyo inatoa picha kamili ubora wa CCM. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahala pema peponi.
 
"...kulimfanya aamue kubadili siasa na kuhamia CCM, akiondoka Chadema, chama ambacho alinunua Ofisi za Makao Makuu yake, pale Kinondoni, mtaa wa Ufipa, wakati akiwa Kiongozi..."

Alisimamia ununuzi kwa niaba ya Chama ama alitoa pesa zake mwenyewe?


Asante kwa kutueleza historia hii. Nilikiwa simjui vizuri huyu kiongozi.
 
Asante sana Mh. Zitto, kutukumbusha tulivyoshahau, kwani mwenyezi Mungu kaumba kusahau, asante kutuelewesha kwani si wote waliokuwa wana ufahamu uwepo wa historia hii.
Hakika kwa hayo uloyooandika ni dhahiri Marehemu anastahili kumbukumbu ya kudumu mkoani kigoma
 
HUTAAMINI CCM WAMESHINDWA KUMPATIA HESHIMA STAHIKI ...KWELI CCM INA WENYEWE ....

HUYU NI SHUJAAAA LAKINI AMESHINDWA KUONDOKA KISHUJAAAA
 
Back
Top Bottom