Tangu lini Wizara ya Afya imekuwa ya Muungano?

rodrick alexander

JF-Expert Member
Feb 12, 2012
15,297
20,371
Katika ripoti ya ukaguzi wa CAG imeeleza kuwa Aprili 2022 kwa mujibu wa ripoti hiyo, Wizara ya Afya iliingia mkataba na kampuni ya Zenj Motors wa ununuzi wa magari 12 ya wagonjwa yenye thamani ya Sh1.97 bilioni kwa ajili ya hospitali za Zanzibar ambao haukutekelezwa ipasavyo.

Chini ya mkataba huo, magari hayo yalitakiwa yawe yamefikishwa wizarani ndani ya siku 90 lakini hadi Novemba 2022 (zaidi ya mwaka mmoja), magari hayo yalikuwa hayajapokewa na hakuna ushahidi wa kuongezewa muda.

Lini wizara ya afya imekuwa wizara ya muungano kwani Zanzibar pia wanayo wizara yao ya Afya au ndio zile kero tulizoambiwa na Jafo kuwa mama amezitekeleza? Pia tunaambiwa CAG anafanya ukaguzi hata kwa mambo yasio ya muungano.

Kwa upande wake Wizara ya Afya ya Zanzibar iliingia mikataba saba na wazabuni ya kuwasambazia vifaa kwa ajili ya hospitali nane, yenye thamani ya Sh10.41 bilioni, lakini hadi Novemba 22, 2022 hakuna kifaa hata kimoja kilichokuwa kimepokewa.

Pia, ripoti imebaini Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi iliipa Comfix Engineering zabuni ya vifaa vya uvuvi vyenye thamani ya Sh139.5 milioni na vilipaswa kukabidhiwa Julai 23, 2022 lakini hadi Novemba 23 mwaka jana havikuwa vimepokewa.

CAG anasema katika ripoti hiyo Shirika la Umeme Zanzibar (Zesco) liliingia mkataba na Vuka Timbers Februari 3, 2022 wa kulipatia nguzo 10,000, lakini hadi Novemba mwaka jana walikuwa wamekabidhi nguzo 1,089 huku zilizosalia (asilimia 89) hazikuwa zimepokewa.

Wizara ya Nishati na Shirika hilo la Umeme walilazimika kukubaliana kuongeza muda wa makabidhiano kwa miezi mitatu hadi Desemba 2022, lakini nguzo hizo bado hazikukabidhiwa hata baada ya muda wa nyongeza kuisha.

Zanzibar wana mkaguzi wao kwanini watumie rasilimali za Bara kwa mambo yasio ya kimuuungano?
 
Huoni mpka kuna wakuu wa wilaya toka Zanzibar, lini TAMISEMI ni muungano? tafuta mbara kwao anayefanya kazi hata ya VEO
Mkuu wa wilaya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania,siyo wilaya ya Tanganyika,muwe mnaelewa mbuzi nyie,unadhani watafanya Jambo lisilo la muungano kuwa mambo ya muungano!?
 
Nadhani hizo ni fedha JMT iliyokopeshwa kwa ajili ya UVIKO 19 na zina simamiwa nayo.
 
Mkuu wa wilaya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania,siyo wilaya ya Tanganyika,muwe mnaelewa mbuzi nyie,unadhani watafanya Jambo lisilo la muungano kuwa mambo ya muungano!?
Punguza upumbavu angalau ubakize ujinga. Kuna Mkuu wa wilaya Zanzibar anayewajibika Kwa TAMISEMI? Huyo mzanzibar aliyeletwa Bara anawajibika wapi zaidi ya kuziba nafasi za watanganyika?
 
Punguza upumbavu angalau ubakize ujinga. Kuna Mkuu wa wilaya Zanzibar anayewajibika Kwa TAMISEMI? Huyo mzanzibar aliyeletwa Bara anawajibika wapi zaidi ya kuziba nafasi za watanganyika?
Hakuna Tanganyika mbuzi wewe, Tanganyika ilishauawa na watanganyika wenyewe
 
Mkuu unahoji hayo tu, mbona yako mengi? Awamu hii rais wa Tanzania anatokea Zanzibar. Kwahiyo kama ilivyokuwa Chato awamu ya 5 ndiyo Zanzibar awamu hii.
 
Mkuu wa wilaya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania,siyo wilaya ya Tanganyika,muwe mnaelewa mbuzi nyie,unadhani watafanya Jambo lisilo la muungano kuwa mambo ya muungano!?
Kuna wakuu wa wilaya za Jamhuri ya Muungano kule Zanzibar?
Kama wapo, alishawahi kuteuliwa mtu kutoka bara kushika wadhifa huo?
Majibu ya maswali haya yatatupatia uelekeo.
 
Juzi nimeona Tundu Lissu kapokelewa JNIA akapakizwa kwenye prado ina vibao vyeupe... nilinyong'onyea vibaya mno

Watanganyika hatuna sense of self worth
 
Katika ripoti ya ukaguzi wa CAG imeeleza kuwa Aprili 2022 kwa mujibu wa ripoti hiyo, Wizara ya Afya iliingia mkataba na kampuni ya Zenj Motors wa ununuzi wa magari 12 ya wagonjwa yenye thamani ya Sh1.97 bilioni kwa ajili ya hospitali za Zanzibar ambao haukutekelezwa ipasavyo.

Chini ya mkataba huo, magari hayo yalitakiwa yawe yamefikishwa wizarani ndani ya siku 90 lakini hadi Novemba 2022 (zaidi ya mwaka mmoja), magari hayo yalikuwa hayajapokewa na hakuna ushahidi wa kuongezewa muda.

Lini wizara ya afya imekuwa wizara ya muungano kwani Zanzibar pia wanayo wizara yao ya Afya au ndio zile kero tulizoambiwa na Jafo kuwa mama amezitekeleza? Pia tunaambiwa CAG anafanya ukaguzi hata kwa mambo yasio ya muungano.

Kwa upande wake Wizara ya Afya ya Zanzibar iliingia mikataba saba na wazabuni ya kuwasambazia vifaa kwa ajili ya hospitali nane, yenye thamani ya Sh10.41 bilioni, lakini hadi Novemba 22, 2022 hakuna kifaa hata kimoja kilichokuwa kimepokewa.

Pia, ripoti imebaini Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi iliipa Comfix Engineering zabuni ya vifaa vya uvuvi vyenye thamani ya Sh139.5 milioni na vilipaswa kukabidhiwa Julai 23, 2022 lakini hadi Novemba 23 mwaka jana havikuwa vimepokewa.

CAG anasema katika ripoti hiyo Shirika la Umeme Zanzibar (Zesco) liliingia mkataba na Vuka Timbers Februari 3, 2022 wa kulipatia nguzo 10,000, lakini hadi Novemba mwaka jana walikuwa wamekabidhi nguzo 1,089 huku zilizosalia (asilimia 89) hazikuwa zimepokewa.

Wizara ya Nishati na Shirika hilo la Umeme walilazimika kukubaliana kuongeza muda wa makabidhiano kwa miezi mitatu hadi Desemba 2022, lakini nguzo hizo bado hazikukabidhiwa hata baada ya muda wa nyongeza kuisha.

Zanzibar wana mkaguzi wao kwanini watumie rasilimali za Bara kwa mambo yasio ya kimuuungano?
Wacheni ujinga kwa kukurupuka kuandika. Hiyo ni miradi pesa za uviko zile 1.5bil kutoka world bank( kama sijakosea). Pesa zimeyolea na Jamuhuri ya muungano. Kwa hivyo auditing yake inafanywa na GAG wa Tanzania.
 
Kuna wakuu wa wilaya za Jamhuri ya Muungano kule Zanzibar?
Kama wapo, alishawahi kuteuliwa mtu kutoka bara kushika wadhifa huo?
Majibu ya maswali haya yatatupatia uelekeo.
Ofisi ya mkuu wa wilaya Zanzibar ipo chini ya serikali ya mapinduzi Zanzibar, semi-autonomous(not sure spellings) wakati Tanganyika haipo
 
Wacheni ujinga kwa kukurupuka kuandika. Hiyo ni miradi pesa za uviko zile 1.5bil kutoka world bank( kama sijakosea). Pesa zimeyolea na Jamuhuri ya muungano. Kwa hivyo auditing yake inafanywa na GAG wa Tanzania.
Mbona povu limekutoka wewe mwenye akili elezea mgawanyo ulivyotajwa au kisu kimegusa kwenye mfupa.
bara na zanzibar kila moja ilipewa mgawo wake we endelea kusifia tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom