Tangazo la ATCL linatia aibu mno!

Tangazo la ATCL linatia aibu mno!

Njoo na solution kuliko kulalamika tu.
Ndo kilichoua hili shirika, lawama kuliko solution, nakumbuka zile technical faults zilizotokea watu walikuwa wanalizonga shirika mpaka headline za magazeti wakati wapinzania wao wakipata ilikuwa kimyakimya na mwisho wa siku wananchi wakapoteza imani na shirika

By the way ameibua mjadala huenda wakaona wakaboresha
 
Tatizo unataka liandikwe kama unavyotaka wewe. Sasa kila mtu akitaka tangazo liandikwe anavyotaka si itakuwa kero.
 
Nikiangalia au kusikiliza matangazo ya ndege mfano Rwandair,KQ au Fastjet hua naihurumia ATCL. Tangazo la Atcl limekaa ovyo sana wao wanashinikiza uzalendo wakati wako kwenye biashara ya ushindani.
Badala kutaja vitu vitakavyomvutia mteja wao wanashinikiza uzalendo kwanza.
Kwa kiingereza tunaita BEGGING
 
Nimeshuhudia tangazo la ATCL clouds t.v asubuhi hii. Niseme tu kwamba, tangazo lile ni la kiwango cha chini sana katika kila hali, kuanzia namna lilivyobuniwa hadi ghraphics zilizotumika. Yaan utafikiri ni Hussein Pamba kali anatangaza yale maduka yake ya pale Kinondoni manyanya au kule Sinza, kumbe ni Air Tanzania??!!! Hivi hawana bajeti ya matangazo, hii ni kujiaibisha, be serious!
Bajeti zipo vitambini mwa watu... welcome to Tanzania ya viwanda
 
Back
Top Bottom