TANAPA: Simba Joel alikimbia, tunamtafuta

TANAPA: Simba Joel alikimbia, tunamtafuta

Kwan uyo simba ni nani mbona anapewa airtime zisizokua na msingi
Mpunga wanaolipia watalii wanaenda kumuona huyo Simba kwa hio usione wanampa kipaombele HUYO SIMBA ndio PESA ZA WATALII na wanaomuulizia ni hao hao watalii waliowahi kumuona na waliompa majina itakua ni mmoja wa hao hao watalii

Kuna mzungu mmoja anatoka nje anakuja Bongo yeye hua anakuja kicheza na Cheatah tu yaan Duma ndio anicheza nao na hawamdhuru kwa hio usitumbue mijicho hio
 
Mali asili mtalaumiwa kwann kama mlijua yotehaya hamkutaka kumlinda bob Jr na familia yake ? Mmemkosea
Mnyama haingiliwi kinyume mkuu ni kosa kwa mujibu wa haki za wanyama, wao pia wana taratibu zao za kuishi ndio maana swala analiwa na Simba analiwa na Chui mamba anakula ngirimaji, Nyati analiwa na Simba, Tembo mtoto analiwa na Simba, Pundamilia analiwa na Simba, Nyumbu analiwa na mamba, na Simba wanauana wao kwa wao sio Simba tu hata Sokwe pia wana hio nature anavamia anaua mkuu wa kaya anaua madume yote au anayafukuza alafu anakomba majike yote anayatomba anayazalisha anatengeneza ukoo wake that's nature, huwezi kukuta hata siku moja hio nature ikaingiliwa na binadamu na hairuhusiwi ni haki yao wanyama kuishi wanavyotaka bila bughudha
 
Kwa hiyo anatutangazia ili iwe nn au anaamini wananchi wasio waaminifu wamemuiba .ujinga tu
 
......taarifa zinadai kuwa Bob junior na Joel ni ndugu wa karibu na kwa mujibu wa tanapa ni kwamba ugomvi ulianza Kwa Bob junior kuvamiwa......Joel alipoona mapambano makali aliamua kusepa ndo Bob kutokana na uzee alizidiwa na kufariki......inashauriwa watanzania kuwa watulivu ktk kipindi hiki kigumu.....Joel anaendelea kutafuta na bob junior atakumbukwa daima.......
R.I.P, mazishi ya kitaifa lini?
 
Mali asili mtalaumiwa kwann kama mlijua yotehaya hamkutaka kumlinda bob Jr na familia yake ? Mmemkosea
Ni nature na pia hawatakiwi waamulie ugomvi wa Simba wanaotaka kumiliki eneo lao kifalme hata baba yake Bob aliuawa pia yupo Mwingine wa Masai Mara Kenyq aliitwa Scarface nae aliuawa mwaka 2021 na alipigana vita kadhaa mpaka kuumizwa jicho la kulia na kubatizwa hilo jina...
 
Kweli ni kazi yao tanapa lkn matukio ya watu kupotea yanapotokeaga vyombo husika inafanya kazi kama inavyostahili
Hilo swali kaviulize vyombo husika, wao TANAPA kama chombo husika cha kumtafuta huyo Simba wapo kufanya kazi yao.
 
Ila huyu Bob ametawala muda mrefu sana na ndugu yake Joe na battle nyingi wameshinda...
 
Back
Top Bottom