GE2025 Tamko la Tume ya Haki za Binadamu Kenya: Hakuna Uchaguzi Unaofanyika Tanzania Leo 29 Oktoba 2025

GE2025 Tamko la Tume ya Haki za Binadamu Kenya: Hakuna Uchaguzi Unaofanyika Tanzania Leo 29 Oktoba 2025

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Doctor Mama Amon

Platinum Member
Joined
Mar 30, 2018
Posts
2,311
Reaction score
3,490
1761714159996.png


Ndugu Raia wa Afrika Mashariki,

Tunasimama hapa tukiwa na wasifu wa utambulisho halali kama Raia wa Afrika Mashariki, tukiwa tunasukumwa na ukweli kwamba Jumuiya ni yetu sote.

Tunaendelea kushuhudia ukiukwaji wa haki za binadamu na uharibifu wa demokrasia katika eneo lote, na kama raia wa Jumuiya, tunasimama kama kitu kimoja.

Tunasimama hapa, tukiwa tumejikita katika utambulisho wetu wa Afrika Mashariki, kama wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mipaka ya Mataifa Wanachama wa Jumuiya haiwezi na haipaswi kuweka kikomo cha udugu na undugu wetu.

Matukio ya kusikitisha tunayoshuhudia nchini Tanzania yanapingana na kanuni zilizo msingi wa kuasisiwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Tunasimama hapa kusema kwamba ukatili mahali popote ni tishio kwa haki kila mahali.

Kinyume na uvumi unaosambaa, hakuna uchaguzi unaofanyika Tanzania kesho tarehe 29 Oktoba.

Kwa kuwa makampuni yote ya vyombo vya habari vya kimataifa yamezuiwa kuingia Tanzania, na leseni nyingi za ndani zimeondolewa, tunapaza sauti zetu kwa niaba ya Jumuiya, wenzetu wa Tanzania, na watu wa Afrika Mashariki.

Watanzania wamezungumza kwa kusema, "Kwa upande wetu, hatujauelezea kama uchaguzi. Kuhusu uchaguzi kuwa huru na wa haki, lazima, angalau, kuwe na uchaguzi wa ushindani. Huu si uchaguzi. Ni maigizo. " - J.K. Tanzania

Hakuna uchaguzi huru na wa haki unaofanyika Tanzania. Samia Suluhu anajiandaa kwa ajili ya kutawazwa kwake, kwani upinzani wake pekee ni kivuli chake mwenyewe.

Wagombea wake wote wakuu wa upinzani wamekamatwa au wamezuiliwa kushiriki na Tume Huru ya Kitaifa ya Uchaguzi (INEC).

Nchi ya Tanzania imekuwa ikisumbuliwa na janga la kimya kimya la kutoweka kwa sauti zinazoikosoa serikali, utekaji nyara wa mara kwa mara, watu kufungwa kiholela, mateso ya kikatili, ubakaji wa watu wanaohojiwa na vyombo vya dola, mauaji ya watu bila kuwepo amri halali ya mahakama, na utumiaji wa kimahakama kinyanyasa umma.

Ukatili na uhalifu huu dhidi ya ubinadamu ni hasa dhidi ya wapinzani wanaoonekana wa utawala wa sasa na watu wengi wanaopinga ukiukwaji wa sheria za uchaguzi.

HAJA YA KUKOMESHA UNYANYASAJI WA WAPINZANI NA UKIUKWAJI WA HAKI ZA KIBINADAMU

Ukiukaji wa haki unaoendelea umelenga hasa CHADEMA, chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania.

Na pia umeenea hadi taasisi za kidini, unawalenga viongozi, wanaharakati, watu wenye ushawishi, na raia wenye sauti wa asili zote.


Kumekuwa na matukio zaidi ya 250 yaliyoripotiwa na kurekodiwa kuhusu watu kutoweka kwa lazima, huku wengi wa waathiriwa wakitoweka kabisa, au miili yao isiyo na uhai ikipatikana miezi kadhaa baadaye.

Ripoti hii ya watu waliotekwa na kupotezwa inapatikana mtanzanoni kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza.

Zaidi ya hayo, Tanzania imeliingiza jeshi lake la polisi katika kile kinachoonekana kuwa maandalizi ya kupigana vita dhidi ya raia wake, badala ya kuwatumia kutengeneza mazingira ya uchaguzi rafiki.

Katika wiki tatu zilizopita, zaidi ya watu 55 wametoweka kwa nguvu, kuteswa, kuuawa, na kuwekwa kizuizini.

Kulingana na ripoti ya hivi karibuni ya Amnesty International, ukandamizaji nchini Tanzania umeongezeka.

Amnesty pia imetaja hali ya kisiasa nchini Tanzania chini ya Samia Suluhu Hassan na uchaguzi ujao kama hali isiyopingwa wala kudhibitiwa na yeyote, na yenye kiukiuka misingi ya haki.

Ripoti hiyo, yenye kichwa "Wimbi la Hofu Linaenea Tanzania," inapatikana mtanzaoni.

Kumekuwa na kukamatwa kwa nguvu kwa kiongozi wa chama cha CHADEMA, Tundu Lissu, na mshindani mkuu wa Suluhu, na kushtakiwa kwa mashtaka ya uhaini yasiyo na msingi kwa sababu tu ya kudai mageuzi ya kimfumo kabla ya uchaguzi.

Kukamatwa kwake na mashtaka ya uongo, na utawala usiosikia kiu ya haki, viliashiria kuongezeka zaidi kwa ukiukwaji wa uhuru wa raia.

Baadaye kidogo, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi iliipiga marufuku CHADEMA kushiriki katika uchaguzi kwa sababu CHADEMA walidai mabadiliko katika kanuni za uchaguzi.

Aidha, kwa kutumia amri ya mahakama, CHADEMA ilipigwa marufuku zaidi kufanya shughuli zozote za kisiasa.

Maafisa wa CHADEMA na raia baki wamekamatwa kiholela, kuwekwa mahabusu kienyeji, kushambuliwa, kufanyiwa unyanyasaji wa ujumla, na hata kuzuiwa kuhudhuria kesi ya uwongo dhidi ya Lissu, ambayo kwa mujibu wa sheria ya Tanzania ni kesi inayopaswa kusikilizwa katika mahakama ya wazi.

Shaban Moyo, Felisuts Festo, Dkt. Fred Chacha Hatari, miongoni mwa wengine, wanataja uzoefu wao wa moja kwa moja, pamoja na kutoa ushahidi wa picha kuhusu mateso waliyopitia mikononi mwa mamlaka ya Tanzania, hapa mtandaoni.

Sote tunakumbuka kwamba timu ya waangalizi sita kutoka Kenya ilizuiwa kuingia Tanzania walipokuwa kwenye misheni ya kufuatilia uendeshaji wa Kesi ya uwongo ya Lissu.

Walizuiliwa kwa muda na kurudishwa Nairobi bila sababu yoyote halali, kinyume na masharti ya mkataba wa Afrika Mashariki.

Wawili kati ya waangalizi hao, Boniface Mwangi wa Kenya na Agather Atuhaire wa Uganda, walitekwa nyara kwa ukali, walizuiliwa kiholela, waliteswa, walibakwa wakati wa mahojiano, na kutendewa aina nyingine za ukatili, unyama, na udhalilishaji wakiwa mikononi mwa vyombo vya ulinzi vya Tanzania.

Aidha, hivi karibuni, John Heche, Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, alikataliwa kuingia Kenya ili kuhudhuria mazishi ya Raila Odinga, huku pasipoti yake ikichukuliwa na mamlaka ya uhamiaji wakati akiwa bado upande wa Tanzania, katika mpaka wa Kenya-Tanzania, kitendo kilichofanywa bila kufuata sheria zilizotungwa na bunge kuhusu masuala ya uhamiaji.

Siku chache baadaye, John Heche alitekwa nyara akiwa nje ya Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar Es Salaam, kinyume na sheria za nchi zinazosimamia ukamataji wa watuhumiwa.

Vitendo hivi vinaonyesha ukosefu wa utawala wa sheria na mateso ya kisiasa yanayofanywa na mawakala wa serikali bila hofu ya kuadhibiwa na mtu yeyote.

Taarifa zaidi zinaonyesha kuwa, vizuizi holela vya usafiri visivyo rasmi na vilivyo kinyume cha sheria vimewekwa kwa karibu kila kiongozi wa CHADEMA na mkosoaji yeyote wa serikali.

HUJUMA ZINAZOLENGA TAASISI ZA DINI NA NA VIONGOZI WAO WAKUU

Ukandamizaji pia umeenea hadi kwenye taasisi za kidini na viongozi wao wanaopinga ukiukwaji wa haki za binadamu.

Mnamo Juni 2 mwaka huu, utawala wa Samia Suluhu Hassan ulifuta usajili wa Kanisa la Ufufuo na Uzima nchini Tanzania, linaloongozwa na Askofu Dkt. Josephat Gwajima.

Askofu Gwajima anajulikana sana kwa ukosoaji wake wa waziwazi wa utawala mbaya na ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Tanzania, na hasa kwa sababu ya wito wake wa kuitaka serkali kuwajibika kwa sababu ya matukio ya utekaji wa raia yanayoendelea nchini Tanzania.

Utawala Samia Suluhu Hassan uliishutumu Kanisa la Askofu Gwajima kwa kusema uwongo, kwa nia ovu dhidi ya serikali, ukidai kwamba Kanisa la Askofu Gwajima limekiuka Sheria ya Vyama.

Kanisa hilo lilifutwa usajili siku chache baada ya Askofu Gwajima kutoa wito wa kukomeshwa kwa utekaji nyara unaofuatiwa na kutoweka kwa watu waliotekwa nchini Tanzania.

Kufutwa kwa usajili huo kumezuia uhuru wa kuabudu wa maelfu ya waumini wa Ufufuo na Uzima.

Askofu Dkt. Benson Bagonza wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe, pia amesema hadharani kwamba anahofia maisha yake baada ya kupokea vitisho vya kuaminika kutoka kwa watu wanaofahamika kama "watu wasiojulikana," neno linalomaanisha watekaji nyara na watekelezaji wa amri za kisiasa kuhusiana na utekaji huo.

Mnamo 16 Machi 2025, mwinjilisti mmoja wa televisheni, Stephen Gumbo, alitekwa nyara kwa nguvu kutoka nyumbani kwake huko Muriet, Arusha, na watu wawili wenye bunduki waliojitambulisha kama maafisa wa polisi.

Baadaye aliokotwa katika msitu wa Kilimanjaro Magharibi, umbali wa kilomita 200 hivi, baada ya kujeruhiwa vibaya, kuteswa, na kufanyiwa ukatili na watu wenye bunduki waliomtuhumu kwa "kuwakashifu" viongozi wa kitaifa katika mahubiri yake.

Vivyo hivyo, Askofu Machumu Kadatu, maarufu kama Mwanamapinduzi, pia wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, alilazimika kukimbia nchi baada ya kulengwa na watekaji na watesaji.

Askofu Dickson Kabigumila ndiye wa hivi karibuni kukimbia nchi, akihofia maisha yake, baada ya kupokea vitisho vingi kutoka kwa watekaji na watesaji.

Hapo awali, mnamo 6 Septemba 2024, Ali Mohammed Kibao, afisa mwandamizi wa chama cha CHADEMA mwenye umri wa miaka 69, alitekwa nyara kutoka kwenye basi jijini Dar es Salaam.

Aliripotiwa kupotea kwa saa kadhaa kabla ya mwili wake kupatikana karibu na ufukwe wa Bahari ya Hindi, uitwao Ununio, asubuhi iliyofuata.


Kibao alikuwa ameuawa kikatili, huku uso wake ukiwa umeharibika kwa kumwagiwa tindikali, ikionyesha dhahiri mateso aliyopitia.

Hakuna dalili zozote zenye kuonyesha kufanyika kwa jitihada yoyote ya uchunguzi wa kifo cha Kibao hadi sasa.

Kufuatia mauaji ya kutisha ya Ali Kibao, kumekuwa na utekaji nyara, kukamatwa, na mateso mengi, ikiwa ni pamoja na ubakaji na aina nyingine za unyanyasaji wa kijinsia, kwa maafisa wa CHADEMA, wafuasi wao, na Watanzania wengine wanaotoa maoni tofauti au kupinga utawala wa kikatili wa Samia Suluhu Hassan.

Mnamo Mei 2025, Mdude Nyangali, mwandishi wa habari na mtunzi wa vitabu, alitekwa nyara na watu wenye silaha wanaoaminika kuwa maafisa wa usalama.

Inasemekana kutekwa kwake kulikuwa kwa ukatili, kwani eneo la utekwaji wake lilijaa damu, na haswa kwenye njia aliyoburuzwa na watekaji.


Tangu kutekwa kwake, na licha ya wito, maandamano, na juhudi za kisheria, Nyangali bado hajulikani alipo.

Vile vile, balozi wa zamani wa Tanzania na mkosoaji mkuu wa utawala wa Samia Suluhu Hassan, Humphrey Polepole, alitekwa nyara nyumbani kwake, eneo la utekwaji wake likiwa limejaa damu iliyomwagika kutokana na mapambano wakati wa harakati za kumteka.

Bado haijulikani kama bado Humphrey Polepoleyuko wapi na endapo yuko hai au amekufa.

Mashambulizi haya ni sehemu ya mwenendo mpana wa vurugu na vitisho dhidi ya wakosoaji wakuu wa utawala wa Tanzania, wakiwemo viongozi wa kanisa.

Yanaashiria ukiukwaji wa uhuru wa dini (unaolindwa katika Kifungu cha 18 cha ICCPR) na uhuru wa kujieleza wa viongozi wa kidini (unaolindwa katika Kifungu cha 19 cha ICCPR).

KUMINYWA KWA VYOMBO VYA HABARI NA KUDHIBITIWA KWA UHURU WA MTANDAONI

Mlolongo wa sheria na mifumo isiyo ya kisheria imetumika kuharamisha upinzani, kudhibiti vyombo vya habari, na kudhibiti matumizi ya kidijitali.

Udhibiti wa vyombo vya habari na mifumo ya kidijitali umeendelea kuenea katika kipindi hiki huku waandishi wa habari na waundaji wa maudhui mtandaoni wakiendelea kukabiliwa na kukamatwa, kupigwa marufuku, na kufuatiliwa.

Vyombo vyote vya habari vya kimataifa vimekataliwa kuingia Tanzania. Kuna mifano mingi zaidi ya kanuni za ukandamizaji zinazopitishwa nchini Tanzania zinazopatikana kupitia ripoti iliyo mtandaoni.

MARUFUKU DHIDI YA WAANGALIZI WA UCHAGUZI WANAOAMINIKA

Hakuna ujumbe wa wangalizi wa uchaguzi unaoaminika nchini Tanzania kwa sasa. Ubelgiji, Uswidi, Ujerumani, na Ireland zote zimejiondoa kwenye uchaguzi.

Marekani inafuatilia hali hiyo, ingawa haitoi waangalizi wowote rasmi. Ujumbe wa EU hauna uchunguzi sahihi na unadumisha tu utamaduni wa kidiplomasia wa 'DiploWatch'. Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) haushiriki kwa wakati huu.

Tume ya Umoja wa Afrika imetangaza rasmi kuwasili kwa Ujumbe wa Uangalizi wa Uchaguzi wa Umoja wa Afrika (AUEOM) kwa ajili ya uchaguzi huu bandia, licha ya malalamiko yanayoendelea kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu na wasiwasi kuhusu harakati za kuchakachua haki ya uchaguzi.

Mnamo Oktoba 24, Dkt. Speciosa Kazibwe alisema, "Kama jumuiya iliyoanzishwa kwa misingi ya utawala bora, utawala wa sheria, na heshima kwa haki za binadamu, EAC inaona uchaguzi unaoaminika kama msingi wa demokrasia na ujumuishaji wa kikanda."

Ni wazi kwamba wale wanaochagua kutambua uchaguzi wa Tanzania wanafumbia macho ukweli wa ukiukwaji wa haki za binadamu, ambao unawazuia wapinzani kushiriki.

Watanzania wameitisha maandamano, wakitumia haki zao za kikatiba, kutokana na uchaguzi usio wa haki ambao Samia Suluhu Hassan anapanga kuendelea nao hadi asimikwe kwenye kiti cha urais.

HAKUNA MAGEUZI, KWA HIYO, HAKUNA UCHAGUZI WA HAKI

Kile kinachoitwa "uchaguzi" nchini Tanzania ni udanganyifu. Matokeo yake yaliwekwa wakati Samia Suluhu Hassan alipowanyonga wapinzani wote, kunyamazisha vyombo vya habari, na kufunga nafasi ya kisiasa.

Waangalizi wengi wa kimataifa wanaoaminika wamejiondoa kwa sababu, hasa, hakuna kitu chochote halali kinachopaswa kushihudiwa wakati wa kutawazwa kinyemela kwa Samia Suluhu Hassan.

Waafrika wana haki ya kukasirika kwamba Umoja wa Afrika, taasisi iliyokusudiwa kutetea haki za binadamu, demokrasia, na utawala wa sheria, umechagua ukimya unaounga mkono ukatili badala ya kusimamia kanuni.

Umoja wa Afrika unazidi kufanana na klabu ya marais wanaolindana badala ya kuwalinda watu wanaodai kuwatumikia. Usaliti huo huo unaonekana wazi katika SADC na EAC.

Tunakuja kuwatetea Watanzania na kwa hivyo tunatoa taarifa kwa Tanzania na tawala zote za kimabavu katika maeneo mengine ya Afrika Mashariki na Afrika.

Madikteta wanapojikusanya upya kuwakandamiza raia, sisi, kama raia, tunajikusanya vivyo hivyo ili kurejesha nchi zetu na uhuru wetu wa asili.
Aluta continua!

Tamko limesainiwa na:

1. Jumuiya ni Yetu
2. Pan-African Progressive Leaders Network
3. Vocal Africa
4. Kenya Human Rights Commission (KHRC)
5. PAWA 254

Chanzo: Tanzania doesn't have an election but a crackdown disguised as democracy (28 October 2025)
 
Taarifa imesheheni ukwrli mtupu kuhusu utawala wa Samia.

Kwa sasa, Tanzania ndiyo inayoeleza kwa uwazi maana ya utawala wa kidikteta. Pamoja na mapungufu mbalimbali kwenye tawala zilizotangulia, lakini hakuna utawala uliowahi kufikia udhulumaji haki kwa kiwango hiki. Bila shaka Samia ataingia kwenye historia ya pekee Tanzania na Afrika nzima.
 
Back
Top Bottom