Mathanzua
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 15,878
- 20,732
Kwa kuandika bandiko hili mtu asije akadhani kwamba mimi ni mtumishi,sio mimi ni mdau wa maendeleo ninayekerwa na hali halisi ilivyo katika Wilaya yangu ya Mvomero.Taarifa nyingi zinakera,ndio, zinakera sana,ni kama Wilaya haina mwenyewe.
Kila mahali ushirikina umekuwa gumzo, wafanyikazi wanashindwa kutoa sauti zao kufunua maovu kwa kuwa wanaogopa kulogwa. Ndio,hofu ya uchawi imeikumba Wilaya ya Mvomero.
Rasilimali za serikali sasa ni mali za watu binafsi na hakuna anayekemea tatizo hilo kwa kuogopa kulogwa.Wizi wa mali za uma nao ni kitu cha kawaida,huku wahusika wa matukio hayo wakiamini kwamba hata kama watajulikana, hakuna hatua zitakazochukuliwa kwa kuwa wataloga!
Siajabu Mvomero mtu akapelekwa masomoni na asipewe hela ya kujikimu akiwa masomoni,na anaishia kulalamika tu,na hasemi kwa kuwa anaogopa kulogwa! Haya yametokea,na akihoji anaambiwa yeye kafuata masomo.
Siajabu yakaandikwa madokezo ya malipo majina ya wafanyikazi yakaandikwa,zikatiwa sahihi zisizo zao,na fedha ikachukuliwa na mtu mwingine kabisa.
Hivi karibuni Sh.300 million zilitolewa kwa ujenzi wa madarasa Shule ya Msingi Mbigiri na TAMISEMI,lakini ni Sh.80 million tu zilizokwenda kwenye Shule hiyo. Zingine inadaiwa zinakwenda kujenga Shule ya Msingi Kwamhuzi,lakini hilo halikuwa lengo la TAMISEMI! Na nani kwanza mwenye uhakika kwamba hizo fedha zitafika huko hazitaishia hewani.
Kama muendelezo wa uozo wa Wilaya,ni muda wa zaidi ya miezi miwili sasa wananchi hawana maji.Sababu MORUWASA wanasema eti pump imeagizwa nje ya nchi!
Hili haliingii akilini, pump ya maji ya kisima cha maji inaagizwa nje ya nchi?Siamini kwamba Tanzania tupo so low.
I strongly believe pump zipo kuna matatizo somewhere yasiyo ya lazima na wananchi wanalipa gharama ya uzembe MORUWASA.Na kwa kuwa Wilaya kwa ujumla mambo yapo hovyoo,nani amfunge paka kengele?
Wito wangu kwa TAMISEMI, Wilaya ya Mvomero inahitaji kufumuliwa kabisa,hakuna linaloendelea,sio kufanya cosmetic changes.Please, please, waokoeni wananchi wa Mvomero katika janga hili,hali ni mbaya sana.
Kila mahali ushirikina umekuwa gumzo, wafanyikazi wanashindwa kutoa sauti zao kufunua maovu kwa kuwa wanaogopa kulogwa. Ndio,hofu ya uchawi imeikumba Wilaya ya Mvomero.
Rasilimali za serikali sasa ni mali za watu binafsi na hakuna anayekemea tatizo hilo kwa kuogopa kulogwa.Wizi wa mali za uma nao ni kitu cha kawaida,huku wahusika wa matukio hayo wakiamini kwamba hata kama watajulikana, hakuna hatua zitakazochukuliwa kwa kuwa wataloga!
Siajabu Mvomero mtu akapelekwa masomoni na asipewe hela ya kujikimu akiwa masomoni,na anaishia kulalamika tu,na hasemi kwa kuwa anaogopa kulogwa! Haya yametokea,na akihoji anaambiwa yeye kafuata masomo.
Siajabu yakaandikwa madokezo ya malipo majina ya wafanyikazi yakaandikwa,zikatiwa sahihi zisizo zao,na fedha ikachukuliwa na mtu mwingine kabisa.
Hivi karibuni Sh.300 million zilitolewa kwa ujenzi wa madarasa Shule ya Msingi Mbigiri na TAMISEMI,lakini ni Sh.80 million tu zilizokwenda kwenye Shule hiyo. Zingine inadaiwa zinakwenda kujenga Shule ya Msingi Kwamhuzi,lakini hilo halikuwa lengo la TAMISEMI! Na nani kwanza mwenye uhakika kwamba hizo fedha zitafika huko hazitaishia hewani.
Kama muendelezo wa uozo wa Wilaya,ni muda wa zaidi ya miezi miwili sasa wananchi hawana maji.Sababu MORUWASA wanasema eti pump imeagizwa nje ya nchi!
Hili haliingii akilini, pump ya maji ya kisima cha maji inaagizwa nje ya nchi?Siamini kwamba Tanzania tupo so low.
I strongly believe pump zipo kuna matatizo somewhere yasiyo ya lazima na wananchi wanalipa gharama ya uzembe MORUWASA.Na kwa kuwa Wilaya kwa ujumla mambo yapo hovyoo,nani amfunge paka kengele?
Wito wangu kwa TAMISEMI, Wilaya ya Mvomero inahitaji kufumuliwa kabisa,hakuna linaloendelea,sio kufanya cosmetic changes.Please, please, waokoeni wananchi wa Mvomero katika janga hili,hali ni mbaya sana.