Tamaduni Music Punchlines Special Thread

Tamaduni Music Punchlines Special Thread

Kunifikia bado/ Uridhi pia bado/
Nigeuke Namless nikuwaze nkisinzia bado/ Hata kwa hisia bado/ Me ni Baba ako ni vile mama ako hajakaambia bado

Bado- Songa
 
Nilikutana nae pande za kinondoni/

Mida ya saba mchana ilisoma saa ya mkononi/

Stendi ya daladala maarufu Kama Morocco/

Me natokea mbagala naenda pande za kinoko/

Ghafla,nikastuka aliponigusa bega/

Kwa gadhabu nilipogeuka ni yeye nikaona shega/

Ila sikuamini nilipomuona/

kama ni Bibi au msichana mdomo haukushona/

Ikanibidi,namkumbuka nilisoma nae shule ya msingi/

Ndugu hawana mpango nae toka alipokufa dingi/

Darasa la Saba na uhakika hakumaliza/

Usawa ulikaba akikumbuka ilimuumiza/

Yamemsibu rafiki ukimwona huwezi kumjua/

Kachakaa hatamaniki hana viatu anapekua/

Dhambi kumpa kisogo hana tiba anapougua/

Shida zake tangu mdogo sasa mtu mzima amekua/

Siku ikipita hajala insha'Allah MOLA anajua/

Wapi usiku atalala ni msala anaomba dua/

Anatamani kufa msalaba apate kuutua/

Kafeli kujiua MUNGU hajapenda kumchukua/

Song:Rafiki
Artist: Stereo
Stereo ni mnyama haswa adse
 
Wakuu mmekaa kimya sana hebu tupieni mistari
 
Huku unasifia kule unaponda.
Ungeelewa mantiki ya ule Uzi usingesema hvyo

Mwanzo kabisa nime decleare kwamba mimi ni big Fan wa Tamaduni , Lakini ninawashangaa kwanini wanashindwa kutengeneza hela
 
Baba ananiambia maneno hayavunji kuti/
Sawa nachana ila mbna flow zangu hazifumi suti/
Me mweusi roho yangu haifugi chuki/
Dada anasem usiposoma mdgo wangu utarudi bush/
Songa mi ndo mfungwa niliyebaki
Na naiba Mpaka jela sijui mtanifunga wapi!
 
Baba ananiambia maneno hayavunji kuti/
Sawa nachana ila mbna flow zangu hazifumi suti/
Me mweusi roho yangu haifugi chuki/
Dada anasem usiposoma mdgo wangu utarudi bush/
Songa huyo
 
Naweka kipaza chini, na surrender...//
Siku zinatoweka zinakwenda
Huamini, chek calendar...//
Nausimika mwenge wa uhuru kama Nyirenda...//
Nasukuma duru nikimuenzi GURU Dandu na Brenda...//
Kaburu kote nazuru mpaka Nakuru...//
Mungu namshukuru kwa kila fungu ukungu na Nuru...//
Kufuru Giza kushinda nguvu za Nuru...//
Tangu enzi za walawi Mathayo natoza ushuru...//

Hakuna mabadiliko, cjui sabato nasaka pato nitoe pato Kiminyato
nafuata michakato ilipo,
Leo hii waumini ndo wachungaji....//
Lwakatare juu ya Altare na injiri za ubabaishaji...//
Majambazi wasomi mahakamani ndio majaji...//
Kwa sanaa za ndotoni kila mmoja ana kipaji...//
Ctaki kuwa Mc wala ctaki kuwa Rapper...//
Nakula bati nachapa rapa ukibaki hapa...//
Kwa hili somo dogo hawapati nnachowapa ...//
Nna apa!!
Xxx xxx xxx
Nikki Mbishi
 
Macho yangu hayakuamini,
Hivi ni yeye ama camera 360,

Picha:songa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom