Talaka Haijakatazwa

Talaka Haijakatazwa

Mathayo 19: 3-9
3. Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?
4. Akajibu, akawaambia, hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo , aliwaumba mtu mume na mtu mke,
5.akasema, kwasababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?
6. Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe.
7. Wakamwambia, jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
8.Akawaambia, Musa kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu lakini tangu mwanzo haikuwa hivi.
9. Nami nawaambia ninyi, kila mtu atakaye mwacha mkewe, isipokuwa ni kwasababu ya uasherati, akaoa mwingine , azini naye naye amwoaye yule aliyeachwa azini.

Sent using Jamii Forums mobile app


Kwanza hongera kwa kuchangia. Nikirudi kwenye hoja zako. Je hiyo nukuu ni kutoka kitabu cha torati au injil?. Hujui tufouti ya Torati na injili Mkuu?

3. Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu?
Mkuu nimekoleza neno kwa kila sababu iliujue msingi wa swali la mafarisayo. Mkuu si kila sababu inayomfanya mtu kutoa talaka, talaka haitolewi eti kisa mtu kaamua bali ikiwa kuna uvunjifu mkubwa wa sheria za maadili. ndio maana nikasema hapo mwanzo, bikra ilikuwa moja ya vigezo vinavyoweza mfanya mtu atoe talaka. kwani mwanamke asiye na bikra moja kwa moja huhusishwa na uasherati yaani alishazini. Sio mwanamke kakosea kupika ndio umfukuze, hapana hili ni kosa. ndio maana swali la mafarisayo lilijikita kuuliza kila sababu.
 
Soma vizuri hilo andiko na ulielewe. 8. Musa kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa. Hili lilitokana na watu kutaka wapewe ruhusa kuwaacha wake zao kwa sababu tu ya tamaa zao.
Tangu mwanzo Mungu hakutaka tuwakiane tamaa. Alitaka tutimiziane haja zetu kistaarabu. Mtu unamkandia mkeo, mke wako mwenyewe unamkandia bao 6!! Za nini?? Kwani yu aenda safari??
Akilalamika kuwa punguza kiu hadi kesho, tiyari; Unaninyima. Huwa nawahurumia saana wanaume wenzangu wanao wakandia mabao 6 na zaidi wake zao. Kisa asichepuke. Kule nje cha mchepuko kimoja tena haraka haraka nako anaona raha zaidi kuliko huo mchezo wako wa kumuumiza.


Mkuu ishu inayozungumziwa pale ni kuona neno Ovu yaani ikiwa utagundua mke wako amecheat unaweza kutoa talaka.
 
Tunatetea talaka kwakuwa tumejiandaa kutenda maovu.


Hatutetei Talaka kwa kutenda Maovu Mkuu. Talaka ni kitu rasmi kabisa. Kama ni suala la kuoa wake wawili au watatu mbona liko wazi kabisa.
 
Hapa talaka imeruhusiwa ila kwa kosa la uzinzi. The problem is, je ni uzinzi wa wote au wa mke tu?

Mwanaume yeye anaruhusa kuoa wake wawili na zaidi hivyo akizini ni uzembe wake. Kwani sheria zipo na zinamruhusu kufanya hivyo
 
Naona talaka uiongeleayo ipo upande mmoja wa wanaume! Kwa maelezo yako na mwanamke anaruhusiwa talaka iwapo mumewe yupo kinyume nae!


Kwa msingi wa Biblia Mwanamke hana Mamlaka ya kutoa talaka. Unajua maana ya Talaka lakini Mkuu?

Talaka inavigezo vyake ambavyo ni:
1. Kutoa mahari
2. Kuoa

Huwezi toa Talaka ikiwa hujatoa Mahari wala hujaoa. Sasa jiulize kati ya mwanaume na mwanamke nani anatoa Mahari na nani anaoa?
 
Kitu kilichonifurahisha ni jinsi ulivyo jijengea hoja yako ya namna ya kumfukuza mwanamke uliyempiga sound kuwa unampenda kumbe unamtamani tu.
Nadhani kama mambo yenyewe yamekuwa hivi, basi tusioe kabisa bali tuwalale huko huko kwao au gesti tujirudie nyumbani wepesi.
Mke sio papuchi tu ila mke ni msaidizi. Tena mmoja tu. Hujiulizi, Adam alikuwa na mbavu ngapi ila Mungu akautoa mmoja tu na kuufanya mwanamke?? Hujiulizi, kwa nini Mungu hakumwongezea Adam mke mwingine??
Usioe, kama unataka kumlala halafu umwache. Huyo sio wako ni wa mtu hivyo wazini. Na wazinzi mwisho wenu ni lile shimo la moto milele. Mbona mnamwona huyo mwanamke ka takataka flan hivi mnayoweza kuitupa nje tu ikawe mbolea na wanaume sisi ndio bora zaidi?? Kwani huyo mwanamke hawezi kututimizia wanaume 2, 4, 6 kwa siku nasi tukatosheka? Tumpe basi na yeye ruksa kuolewa siku akitaka na kutoa talaka siku akitaka.
Mungu hajawahi kukosea na hatakaa akosee. Aliujua ugumu wa moyo wako ndo maana akakuacha ufanye utakalo ila alishakuambia; Mume mmoja kwa Mke mmoja tu. Zaidi ni uzinzi na uasherati na mwisho ni ukimwi


Nipe andiko Mkuu linalosema Mume mmoja na mke mmoja kwa watu wa kawaida isipokuwa Askofu, wachungaji na Makuhani. Ukinipa hilo andiko nafuta mada nzima. Wapo watu wanaweza kuoa mke mmoja, wapo wengine wawili, watatu mpaka ishirini. Ila wapo watu ambao hata mke mmoja tuu anamsumbua.

Maandiko yanasema Mwanamke aliumbwa kwaajili ya mwanaume.
 
Kitu kilichonifurahisha ni jinsi ulivyo jijengea hoja yako ya namna ya kumfukuza mwanamke uliyempiga sound kuwa unampenda kumbe unamtamani tu.
Nadhani kama mambo yenyewe yamekuwa hivi, basi tusioe kabisa bali tuwalale huko huko kwao au gesti tujirudie nyumbani wepesi.
Mke sio papuchi tu ila mke ni msaidizi. Tena mmoja tu. Hujiulizi, Adam alikuwa na mbavu ngapi ila Mungu akautoa mmoja tu na kuufanya mwanamke?? Hujiulizi, kwa nini Mungu hakumwongezea Adam mke mwingine??
Usioe, kama unataka kumlala halafu umwache. Huyo sio wako ni wa mtu hivyo wazini. Na wazinzi mwisho wenu ni lile shimo la moto milele. Mbona mnamwona huyo mwanamke ka takataka flan hivi mnayoweza kuitupa nje tu ikawe mbolea na wanaume sisi ndio bora zaidi?? Kwani huyo mwanamke hawezi kututimizia wanaume 2, 4, 6 kwa siku nasi tukatosheka? Tumpe basi na yeye ruksa kuolewa siku akitaka na kutoa talaka siku akitaka.
Mungu hajawahi kukosea na hatakaa akosee. Aliujua ugumu wa moyo wako ndo maana akakuacha ufanye utakalo ila alishakuambia; Mume mmoja kwa Mke mmoja tu. Zaidi ni uzinzi na uasherati na mwisho ni ukimwi


Manabii wakubwa karibu wote walikuwa na Wake wawili sasa wewe unayesema hivyo sijui umeyatoa wapi hayo maneno.
Ibrahimu Wake watatu Sarah, Hajiri, Ketura
Yakobo/Israel Wake wawili, Rahel na Lea Dada yake. Na vijakazi wao wawili
Suleiman wake Mia saba, masuria 300
Daudi wake wengi ila hamfikii mwanae Suleiman
Lameck wake wawili
 
Habari zenu Wakuu!

Mimi ni Mkristo, nimezaliwa huku na nimekulia huku. Nimelelewa na kufundishwa Biblia na maandiko mengi ya kidini. Hivyo ni kusema kwa habari ya dini ya kikristo ambayo inamadhehebu mengi kuliko hata dini nyingine huwezi nidanganya kitu chochote.

Wakristo wengi hufuata mapokeo kuliko neno la Mungu. Husikiliza sauti za wachungaji kuliko hata kile ambacho neno la Mungu linasema. Madhebu bora zaidi katika ukristo ni yale yanayofuata kila kisemwacho na maandiko yaliyomo katika biblia.

Mapokeo hayo yamewafanya waumini kuishi kama misukule, wakiishi bila raha na kuona maisha hayana maana yoyote ile.
Leo nitazungumzia habari za Talaka katika ndoa.

Mungu alimpomuumba Adam alimpa zawadi muhimu ambazo ni:
1. Kumiliki na kuvitawala Viumbe wengine
2. Chakula
3. Bustani
4. Mwanamke

Baada ya kutoa zawadi hizo Mungu alitoa vigezo na masharti kwa kila zawadi alizompa.
Zawadi ya mwisho inazaa kitu kinaitwa ndoa. Yaani Muunganiko wa kimahusiano ya kimwili, kiroho, hisia, kimwili, kiuchumi, kijamii n.k baina ya mwanaume na mwanamke.

lengo la zawadi ni kumfurahisha mtu, hivyo Mungu alijua kuwa moja ya zawadi itakayompendeza mwanaume ni kumpatia msaidizi ambaye ni mwanamke. Hakika ilikuwa hivyo. Kitu cha pekee ambacho Mungu alikitaka kutoka kwa Adamu ni kumuona akifurahi. Ndio maana upweke wa Adamu ulimfanya Mungu afikiri kitu kingine kitakacho ondoa ukiwa wake.

Kumbuka Dunia iliumbwa kwaajili ya Mwanaume, Vingine vyote ni zawazi na rasilimali ambazo zitamuwezesha Mwanaume aishi maisha ya raha Mustarehe. Hivyo Mwanaume usijichukulie Poa. Hii dunia ipo kwaajili yako. Tumia chochote ukipendacho kwa mapenzi ya Mungu.

Baada ya watu kuwa wengi, wanawake walikuwa wengi kuliko wanaume. haikutokea kwa bahati mbaya hii. Bali yote ni kuhakikisha kuwa Mwanaume anakuwa na option nyingi ili apate uhuru wa kuchagua akipendacho. Mungu alijua kama angefanya idadi ya wanaume na wanawake kuwa sawa ingeleta tabu sana. Kwani kwa jinsi alivyomuumba mwanaume alijua wapo wanaotaka kuoa wanawake zaidi ya mmoja. Hivyo wengine wangekosa na hii ingezua balaa chini ya jua. Hakuna mwanamke anayependa kiasili kumilikiwa na wanaume wawili. Hata Maandiko yanasema huwezi tumikia Mabwana wawili Lakini haijasema huwezi kutumikia mabibi?wake wawili.

Talaka katika Biblia inaelezewa katika Torati ya Musa ambapo ndio msingi wa sheria ya Mungu. Hayo mengine ni historia na mafundisho ya kuwafunza watu na kuelezea hiyo Torati. Hivyo ni kusema, vitabu kama zaburi, injili na vitabu vya unabii ni mafundisho kuhusu Mungu lakini Totati ndio msingi na kitu pekee kitakachotumika kukutia hatiani. Hata siku ya hukumu kitabu pekee kitakachotumika ni torati yaani sheria ya Mungu.

Kumbukumbu la torati 24
1 Mtu akiisha kutwaa mke kwa kumwoa, asipopata kibali machoni mwake, kwa kuwa ameona neno ovu kwake, na amwandikie hati ya kumwacha, akamtilie mkononi mwake, na kumtoa katika nyumba yake.
2 Naye akiisha kuondoka katika nyumba yake, ana ruhusa kwenda akawa mke wa mtu mwingine.
3 Na huyo mumewe wa sasa akimchukia, na kumwandikia hati ya kumwacha, na kumpa mkononi mwake, na kumtoa katika nyumba yake; au akifa yeye mumewe wa sasa, aliyemtwaa kuwa mkewe;
4 yule wa kwanza aliyemwacha asimtwae kuwa mkewe tena, akiisha kutiwa unajisi; kwa kuwa haya ni machukizo mbele za Bwana; kwa hiyo usiitie dhambini nchi, akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi.
5 Mtu atwaapo mke mpya, asiende vitani pamoja na jeshi, wala asipewe shughuli juu yake yo yote; akae faragha mwaka mmoja nyumbani mwake, apate mfurahisha mkewe aliyemtwaa.

Aya ya kwanza inaelezea kuwa mtu akiisha kutwaa Mke kwa kumwoa, lazima apate kibali machoni mwake. Hapa ni kulingana na muono wa mhusika. Endapo ataona neno Ovu juu yake, neno ovu kulingana na aya zingine linaweza kuwa endapo hajakuta ubikra anaweza pia kuvunja ndoa hiyo na kutoa talaka. lakini ni kulingana na muono wa muoaji. Ikiwa bikra si tatizo lakini anatatizo la kitabia basi pia anaweza kumpa talaka. Lengo si kuishi kwa taabu katika ndoa bali kufurahia maisha.

Mungu amempa mwanadamu uwezo wa kuchagua kile atakacho, hakuona sababu ya kukutafutia na kukulazimisha umuoe fulani wakati wewe humtaki. Ndio maana akasema utatafuta wakufanana na wewe. Si kazi yake kukutafutia mke. Baada ya kupata mke kazi yake ni kukupa watoto kwa jinsi utakavyo wewe. Suala la kuwalea lipo juu yako. Sasa Watu wanachanganya madesa kuwa kila kitu ni mipango ya Mungu jambo ambalo si kweli, na kama ni kweli basi Hakuna Hukumu.

Mungu anampa mamlaka Mwanaume kumtoa mwanamke/mke asiyepata kibali kulingana na muono wake. Mwanamke anahaki ya kupewa talaka kama hati itakayomruhusu aolewe na mwingine. kumaanisha bila talaka mwanamke hajapewa kibali cha kuolewa tena.

Sasa Watu wanachanganya maandiko, hawajui kila kitabu kinadhima yake. Vipo vitabu vya sheria, hivi vinajitegemea na vinaeleza mwanadamu aishi vipi duniani. Yani hivi ni kama Katiba. Dhima yake kubwa ni kuelezea sheria za Mungu. Vitabu vingine vinaunga mkono sheria hizo na kutoa mafundisho mengine na unabii.

Sasa Mtu sheria inasema Kwa mfano: Mtu asile chakula fulani. Mtu anatoa kifungu kutoka katika aya za injili au Zaburi, au vitabu vya unabii. huu ni upuuzi ambao Wakristo wengi wameingizwa mkenge. Huwezi vunja Torati kwa kutumia vitabu vya injili au zaburi.

Talaka ni muhimu ikiwa ndoa imekuwa chungu. Mwanamke kama hamuheshimu mume wake, endapo mumewe ataamua kutoa talaka asilaumu kwani anahaki na ni wajibu wake kufanya hivyo.

Hizo zingine ni porojo za kidunia. Eti alichokiunganisha Mungu Mwanadamu asikitenganishe. Hii nukuu imechukuliwa tofauti sana. Mungu akiunganisha kitu hata mwanadamu afanyeje hawezi kukitenganisha na Mungu akikitenganisha kitu Mwanadamu hata afanyeje hawezi kukiunga. Ndoa haipo kwenye listi ya vitu vilivyoungwa na Mungu. Bali ni makubaliano baina ya mke na mume. Endapo ndoa ingeunganishwa na Mungu isingewepo sheria ya talaka kwenye Biblia au Quran. Na pia ndoa zisingefunjika kamwe.

Nawasilisha
NAKARIBISHA POVU
Unakaribishaje povu wakati wewe ndo unatoa povu kwa niaba ya ule...!!
 
Hapa talaka imeruhusiwa ila kwa kosa la uzinzi. The problem is, je ni uzinzi wa wote au wa mke tu?
philosopher do not philosophize everything...you will be too busy in this world!
 
Naona kila kukucha ukweli unazidi kujiweka wazi na uongo kutoweka kidogo kidogo. Ahsante kwa bandiko lako mkuu, tatizo ni je! Watakubali?
 
Naona kila kukucha ukweli unazidi kujiweka wazi na uongo kutoweka kidogo kidogo. Ahsante kwa bandiki lako mkuu, tatizo ni je! Watakubali?

Nani asikubali.

Ikiwa Mungu mwenyewe hajafunga pingu za maisha na wewe sembuse mtu. Mtu akivunja miiko basi awajibike tuu
 
Nani asikubali.

Ikiwa Mungu mwenyewe hajafunga pingu za maisha na wewe sembuse mtu. Mtu akivunja miiko basi awajibike tuu
Tatzo watu washakalilishwa, kwamba mwenye uwezo wa kuvunja ndoa pale inapolazimika labda ni papa tu. Sasa hayo maandiko yako kwa mtu mwenye imani ya mapokeo inakua ngumu kukuelewa mkuu.
 
Tatzo watu washakalilishwa, kwamba mwenye uwezo wa kuvunja ndoa pale inapolazimika labda ni papa tu. Sasa hayo maandiko yako kwa mtu mwenye imani ya mapokeo inakua ngumu kukuelewa mkuu.


Imani pasipo akili ni upumbavu
 
uko sahihi kabisa.......huwezi ishi na mtu ukiwa huna furaha hata kdg.....unampa kibali cha kuolewa tena asonge mbele.
 
uko sahihi kabisa.......huwezi ishi na mtu ukiwa huna furaha hata kdg.....unampa kibali cha kuolewa tena asonge mbele.


Wengi wanaelewa hii kimya kimya, sema mdomoni wanapinga
 
Back
Top Bottom