DOKEZO TAKUKURU na Usalama wa Taifa, fuatilieni haya; nchi inahujumiwa. Kuna rushwa, urasimu na ufisadi mkubwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hili la nauli ni uongo wa mchana,mbona ushahidi haipo? Nimesafiri siku za karibuni mbona sijakutana na Hilo? Mbona watu wasilalamike?

Nida huko Kuna shida Toka kitambo sana Hadi Leo haijulikani shida ni ipi maana Kila Bunge Hawa wanasemwa ila hakuna kinachobadilika,labda Bunge litengeneze azimio.

Kuhusu Petrol ni kawaida kukiwa na uhaba lazima wafanyabiashara watumie fursa hiyo kutafuta faida kubwa,japo binafsi Mkoa wangu hiyo shida haipo Mikoa yote ya Nyanda za Juu Kusini mafuta yapo na bei ni Ile Ile sijui Kwa Vijijini.

Kuhusu Mwendokasi Wala hakuna shida uzuri mkataba uko clear ukijenga chini ya kiwango Kuna kipindi Cha Matazamio ikiharibika mkandarasi atarudia Kwa gharama yake.mfano wale waliopita Barabara ya Mpemba -Isongole na Mpanda-Tabora na Sumbawanga -Kasanga mtaona Kuna sections kibao wakandarasi wamefumua na wanarudia.

Bunge litoe azimio kuhusu nida Ili tujue shida Iko wapi
Yote niliyoandika ni kweli. Na ushahidi ninao mwingi tu.

Siandiki uongo hapa, ili iweje.

Hilo la nauli, sijataka kuandika linavyofanyika. Nimefanya "due diligence" kidogo. Kwa hiyo ukiwa hujafuatilia jambo, usiseme tu eti uongo.

Hiyo barabara ya mwendokasi Mbagala, ishu sio hicho kipengele cha kuja kurudiwa, hii barabara imeanza kuharibika hata matumizi bado .

Na vituo n.k ni substandard.

Barabara ya KIMARA iko imara na inatumika mwaka wa 7 sasa, hii inameguka, mashimo, unasema kipengele cha kurudiwa?! Shit
 
Nimeipitia ripoti Yako ni kweli kabisa,mfano juzi niliamua kukata tiketi online bus Shabiby lakini nikaiona ipo ya saa saba na saa nane mchana semi luxury Kwa tsh 25000/= bus za asubuhi hawakuziweka.Ila nikaenda stand Mbezi Kwa Magufuli nikazikuta Shabiby nyingi hazijajaa na ticket bei ni tsh 30000/=
Bei juu na Latra haiwajibiki.Kwa ujumla vyombo vya serikali haviwajibiki na Wala hakuna kiongozi anaechukua hatua.
Asante kwa ushahidi huu.

Cc: ChoiceVariable ,

Mie nina ushahidi wa mbinu nyingi tu wanazotumia ku overcharge nauli.

Sasa ndio maana nikashauri kama hawa wa mabus wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, basi zipandishwe, kwani ndio hizo hizo abiria wanazolipishwa juu ya LATRA.
 
Yote niliyoandika ni kweli. Na ushahidi ninao mwingi tu.

Siandiki uongo hapa, ili iweje.

Hilo la nauli, sijataka kuandika linavyofanyika. Nimefanya "due diligence" kidogo. Kwa hiyo ukiwa hujafuatilia jambo, usiseme tu eti uongo.

Hiyo barabara ya mwendokasi Mbagala, ishu sio hicho kipengele cha kuja kurudiwa, hii barabara imeanza kuharibika hata matumizi bado .

Na vituo n.k ni substandard.

Barabara ya KIMARA iko imara na inatumika mwaka wa 7 sasa, hii inameguka, mashimo, unasema kipengele cha kurudiwa?! Shit
Bila ushahidi ni porojo za chuki,weka ushahidi wa jinsi watu wanalipishwa nauli kinyume na bei ya Sumatra

Hiyo Barabara yenu iwe chini ya kiwango au vinginevyo contractor atarudia Wala Halima ubishi

Mwisho ukipenda cheap ndio madhara yake hayo unalazimisha bei ya chini ndio uwe tayari na matokeo yake mkandarasi asilaumiwe Bali yule Rais wenu aliyekuwa analazimisha bei za chini ndio alaumiwe.

Hata hiyo njia 8 Serikali imelazimika kufumua Baadhi ya sections na kuongeza activities plus pesa vinginevyo nayo ingekuwa kituko
 
Ni usiku mnene. Naamua kuandika DOKEZO hili.

Kwa uchungu wa yanayoendelea katika nchi yangu.

Katika mada hii, nitaomba wachangiaji kujadili kwa uwazi kabisa, na kuongezea mifano mingine baada ya hii nitakayokuwa nimeiweka hapa.

Lengo ni Nia njema kabisa kurekebisha pale tulipokosea na kusaidia WaTz ambao wanakosa kufaidi matunda ya nchi yao.

Hapa chini ni jinsi ambavyo mambo ya ovyo yanafanywa wazi na TISS wala TAKUKURU hawafanyi kazi yao iliyotukuka.

1. NIDA na Utoaji wa NAMBA/Vitambulisho vya Taifa.

Hili jambo ni kubwa sana. Mimi nimelithibitisha. Na wote wanaofika kuhudumiwa katika ofisi zote za NIDA nchi nzima wanasema wazi.

Iko hivi, huwezi kufanikisha kupata namba ya NIDA ikiwa huna kiasi fulani cha fedha. Na huwezi kupata ile ID ikiwa huna kiasi kikubwa zaidi cha fedha.

Yani utaenda utafuata taratibu zote na kuwa na viambatanisho vyote, lakini huwezi kupata kimojawapo kati ya hivyo bila fedha. Kiufupi hadi mlinzi wa getini anajua hilo.

Baadhi ya Ofisi za NIDA DSM kupata namba ya NIDA inaanzia sh. 150,000/-. Kupata ID ni kuanzia sh. 500,000/-
Lakini kadri utakavyoongeza dau maana yake utawahishiwa zaidi mchakato wako.

Kwanza hakuna huduma pale, zaidi ukifika upangwe foleni na walinzi, ukiingia unakuta mtu anachat tu, hadi jioni uambiwe njoo tena kesho.

Haya yana muda mrefu yanafanywa wazi kabisa. Hatari hii ni kwamba sasa hata mgeni je, akiwa na milion zake mbili si anapewa zake ID kama MTz??

Mh. Rais wetu ni msikivu, je, ulishasikia amepewa ripoti hii akashindwa kuifanyia kazi?!

Nani wa kumpelekea ripoti kama sio TISS?


2. Mradi wa mwendokasi Mbagala

Huu mradi nendeni mchunguze, ni mbovu na umejengwa chini ya viwango vibaya mno.

Uchunguzi unaonesha baadhi ya miundombinu kuanza kuharibika hata kabla ya matumizi rasmi kuanza.
Wasichokijua ni kwamba hii miradi ya miundombinu ya barabara huwa na zaidi ya miaka 20 ya uhai kabla ya marekebisho.

Sasa ukifika pale ukakuta baadhi ya beacon zimeanguka, kumeguka, n.k, Unajiuliza shida ni nini? Bajeti ndogo ya ujenzi? Lakini hilo linakataa kwa sababu hizi fedha ni mkopo tumepata kutoka Benki ya Dunia (WB), hawawezi kutenga fedha chini ya inayotakiwa.!

Sasa vile vituo vya abiria ndio utacheka kabisa. Mabati ni chini ya viwango, hizo frame walizichomelea ni chini ya viwango, uchomeleaji wenyewe ni wa dizaini za fundi maiko.

Hata wakibisha, nawahakikishieni, barabara ya mwendokasi ya Posta KIMARA itadumu, na hii ya Mbagala itakuja kuharibika mapema kabla yake. Tuko hapa mtakuja kuthibitisha panapo uhai.

Sasa kwa hali hii, utasema Rais wetu alivyo msikivu, ana hii ripoti mezani kweli? Na hatujasikia akichukua hatua zozote?


3. UHABA wa Petroli sasa hivi nchini.

Hapa siandiki sana.

Fahamuni kwamba mafuta yapo. Si mlisikia hata Waziri anasema hakuna upungufu wa petrol. Si amesema mara nyingi tu!

Sasa Mimi na wewe tuulizane, Waziri anasema yapo, vituoni ukifika hakuna, yapo wapi? Eeh...

Jamaa wana mafuta, ila hawatoi kuyauza. Wanasubiri bei mpya za August, zipande usiku wa leo tarehe 31/07/2023 ndio wataanza kutoa mafuta.

Sasa "syndicate" ya namna hii, hapo unasema TISS wapo na wananchi, au wametuma ripoti Rais hajachukua hatua?!

Achaneni na mambo ya ooh Dola $ kuadimika, hiyo inaathiri uagizaji wa mzigo mpya. Sio stock iliyopo ambayo huagizwa miezi mitatu au zaidi nyuma.

4. Nauli za mabasi za LATRA.

Hivi mnajua mabasi yote ya mikoani katika stendi zote za mikoani wanachaji nauli zaidi ya zile zilizoidhinishwa na LATRA?!

USHAHIDI upo.

Hapa namaanisha hata LATRA na mapolisi wanalijua hilo. Je, ni fungu wanapewa au kuamua kuacha tu unyang'anyi huu uendelee?!

Nasisitiza iko hivyo, stendi zote, mikoa yote.

Nenda Dsm, Mwanza, Morogoro, Iringa, Dodoma, Tabora, Kagera, Mbeya, Arusha, Tanga, Mtwara, Kigoma, n.k, kote huko wana 'overcharge'.

Sasa kama watu wa mabasi wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, si bora LATRA ipitishe hizo hizo wanazolipishwa wananchi ili ifahamike moja.

Je, unataka kusema ripoti za haya zipo mezani kwa mh. Rais ila jinsi alivyo anajali watu wake kweli asichukue hatua.?!

Narudia ripoti hii ni kwa nia njema ya kujenga Taifa letu.

Ukweli huduma za umma zimezorota kiasi kikubwa, tusifiche tatizo na wananchi wengi wanaumia sana na hili.

Naomba kuhitimisha hapo kwa leo.

Karibuni wachangiaji kwa mengi zaidi.
TISS nayo wapewe waarabu tu yaishe. Maana sababu zilizotajwa kuwa hasa zimefanya bandari wapewe waarabu, hata TISS wanazo
 
Asante kwa ushahidi huu.

Cc: ChoiceVariable ,

Mie nina ushahidi wa mbinu nyingi tu wanazotumia ku overcharge nauli.

Sasa ndio maana nikashauri kama hawa wa mabus wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, basi zipandishwe, kwani ndio hizo hizo abiria wanazolipishwa juu ya LATRA.
Sasa kwani gari ni Shabiby tuu? Harafu kama bei za Sumatra mnazijua Kwa nini ulipe zaidi?

Huu ni ujinga mwingine wa kutegemea Serikali Kwa Kila kitu wakati mtu wa kwanza kulinda haki Yako ni wewe raia.
 
Sasa kwani gari ni Shabiby tuu? Harafu kama bei za Sumatra mnazijua Kwa nini ulipe zaidi?

Huu ni ujinga mwingine wa kutegemea Serikali Kwa Kila kitu wakati mtu wa kwanza kulinda haki Yako ni wewe raia.
Shida hujadili mada, unarukia rukia watu tu .

USHAHIDI wangu siwezi kuuweka hapa. Nina sababu za kufanya hivyo, na it's proven mathematically.
Natumia akili na elimu yangu.
 
Shida hujadili mada, unarukia rukia watu tu .

USHAHIDI wangu siwezi kuuweka hapa. Nina sababu za kufanya hivyo, na it's proven mathematically.
Natumia akili na elimu yangu.
Acha porojo wewe,ingekuwa hivyo watu wangeshalalamika.ila.kama ulipigwa na kampuni Moja ni wewe imekula kwako usitake ku generalise
 
Hapo kwenye NIDA ni hatari kweli. Kazi ipo. Na sasa hivi nchini hapa wamejazana waNigeria kibao, usikute tayari wana vitambulisho vya taifa kabisaa.
 
Ni usiku mnene. Naamua kuandika DOKEZO hili.

Kwa uchungu wa yanayoendelea katika nchi yangu.

Katika mada hii, nitaomba wachangiaji kujadili kwa uwazi kabisa, na kuongezea mifano mingine baada ya hii nitakayokuwa nimeiweka hapa.

Lengo ni Nia njema kabisa kurekebisha pale tulipokosea na kusaidia WaTz ambao wanakosa kufaidi matunda ya nchi yao.

Hapa chini ni jinsi ambavyo mambo ya ovyo yanafanywa wazi na TISS wala TAKUKURU hawafanyi kazi yao iliyotukuka.

1. NIDA na Utoaji wa NAMBA/Vitambulisho vya Taifa.

Hili jambo ni kubwa sana. Mimi nimelithibitisha. Na wote wanaofika kuhudumiwa katika ofisi zote za NIDA nchi nzima wanasema wazi.

Iko hivi, huwezi kufanikisha kupata namba ya NIDA ikiwa huna kiasi fulani cha fedha. Na huwezi kupata ile ID ikiwa huna kiasi kikubwa zaidi cha fedha.

Yani utaenda utafuata taratibu zote na kuwa na viambatanisho vyote, lakini huwezi kupata kimojawapo kati ya hivyo bila fedha. Kiufupi hadi mlinzi wa getini anajua hilo.

Baadhi ya Ofisi za NIDA DSM kupata namba ya NIDA inaanzia sh. 150,000/-. Kupata ID ni kuanzia sh. 500,000/-
Lakini kadri utakavyoongeza dau maana yake utawahishiwa zaidi mchakato wako.

Kwanza hakuna huduma pale, zaidi ukifika upangwe foleni na walinzi, ukiingia unakuta mtu anachat tu, hadi jioni uambiwe njoo tena kesho.

Haya yana muda mrefu yanafanywa wazi kabisa. Hatari hii ni kwamba sasa hata mgeni je, akiwa na milion zake mbili si anapewa zake ID kama MTz??

Mh. Rais wetu ni msikivu, je, ulishasikia amepewa ripoti hii akashindwa kuifanyia kazi?!

Nani wa kumpelekea ripoti kama sio TISS?


2. Mradi wa mwendokasi Mbagala

Huu mradi nendeni mchunguze, ni mbovu na umejengwa chini ya viwango vibaya mno.

Uchunguzi unaonesha baadhi ya miundombinu kuanza kuharibika hata kabla ya matumizi rasmi kuanza.
Wasichokijua ni kwamba hii miradi ya miundombinu ya barabara huwa na zaidi ya miaka 20 ya uhai kabla ya marekebisho.

Sasa ukifika pale ukakuta baadhi ya beacon zimeanguka, kumeguka, n.k, Unajiuliza shida ni nini? Bajeti ndogo ya ujenzi? Lakini hilo linakataa kwa sababu hizi fedha ni mkopo tumepata kutoka Benki ya Dunia (WB), hawawezi kutenga fedha chini ya inayotakiwa.!

Sasa vile vituo vya abiria ndio utacheka kabisa. Mabati ni chini ya viwango, hizo frame walizichomelea ni chini ya viwango, uchomeleaji wenyewe ni wa dizaini za fundi maiko.

Hata wakibisha, nawahakikishieni, barabara ya mwendokasi ya Posta KIMARA itadumu, na hii ya Mbagala itakuja kuharibika mapema kabla yake. Tuko hapa mtakuja kuthibitisha panapo uhai.

Sasa kwa hali hii, utasema Rais wetu alivyo msikivu, ana hii ripoti mezani kweli? Na hatujasikia akichukua hatua zozote?


3. UHABA wa Petroli sasa hivi nchini.

Hapa siandiki sana.

Fahamuni kwamba mafuta yapo. Si mlisikia hata Waziri anasema hakuna upungufu wa petrol. Si amesema mara nyingi tu!

Sasa Mimi na wewe tuulizane, Waziri anasema yapo, vituoni ukifika hakuna, yapo wapi? Eeh...

Jamaa wana mafuta, ila hawatoi kuyauza. Wanasubiri bei mpya za August, zipande usiku wa leo tarehe 31/07/2023 ndio wataanza kutoa mafuta.

Sasa "syndicate" ya namna hii, hapo unasema TISS wapo na wananchi, au wametuma ripoti Rais hajachukua hatua?!

Achaneni na mambo ya ooh Dola $ kuadimika, hiyo inaathiri uagizaji wa mzigo mpya. Sio stock iliyopo ambayo huagizwa miezi mitatu au zaidi nyuma.

4. Nauli za mabasi za LATRA.

Hivi mnajua mabasi yote ya mikoani katika stendi zote za mikoani wanachaji nauli zaidi ya zile zilizoidhinishwa na LATRA?!

USHAHIDI upo.

Hapa namaanisha hata LATRA na mapolisi wanalijua hilo. Je, ni fungu wanapewa au kuamua kuacha tu unyang'anyi huu uendelee?!

Nasisitiza iko hivyo, stendi zote, mikoa yote.

Nenda Dsm, Mwanza, Morogoro, Iringa, Dodoma, Tabora, Kagera, Mbeya, Arusha, Tanga, Mtwara, Kigoma, n.k, kote huko wana 'overcharge'.

Sasa kama watu wa mabasi wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, si bora LATRA ipitishe hizo hizo wanazolipishwa wananchi ili ifahamike moja.

Je, unataka kusema ripoti za haya zipo mezani kwa mh. Rais ila jinsi alivyo anajali watu wake kweli asichukue hatua.?!

Narudia ripoti hii ni kwa nia njema ya kujenga Taifa letu.

Ukweli huduma za umma zimezorota kiasi kikubwa, tusifiche tatizo na wananchi wengi wanaumia sana na hili.

Naomba kuhitimisha hapo kwa leo.

Karibuni wachangiaji kwa mengi zaidi.
Hayo yote kamwe Nchi hii hayawez shughulikiwa effectively!!! Zipo report kibao za kifisadi miaka sasa lkn zinafunikwa na maisha yanaendelea!! Nchi hii mpaka upatikane utawala thabiti na katiba inayong'ata nje ndan!!!
 
Hapo kwenye NIDA ni hatari kweli. Kazi ipo. Na sasa hivi nchini hapa wamejazana waNigeria kibao, usikute tayari wana vitambulisho vya taifa kabisaa.
Wa Rw, wenye hela wanaovihitaji washapewa.
 
Hayo yote kamwe Nchi hii hayawez shughulikiwa effectively!!! Zipo report kibao za kifisadi miaka sasa lkn zinafunikwa na maisha yanaendelea!! Nchi hii mpaka upatikane utawala thabiti na katiba inayong'ata nje ndan!!!
Sasa tunafanyaje, tunatokaje hapa..
 
Asante kwa ushahidi huu.

Cc: ChoiceVariable ,

Mie nina ushahidi wa mbinu nyingi tu wanazotumia ku overcharge nauli.

Sasa ndio maana nikashauri kama hawa wa mabus wanaona nauli zilizopangwa ni ndogo, haziwapi faida, basi zipandishwe, kwani ndio hizo hizo abiria wanazolipishwa juu ya LATRA.
Nauli hazipandishwi hovyohovyo... kuna policies maalum za kiuchumi ambazo huwa applied na hupelekea vitu mbalimbali nchini kupanda bei au kushuka.
 
Hapo kwenye NIDA ni hatari kweli. Kazi ipo. Na sasa hivi nchini hapa wamejazana waNigeria kibao, usikute tayari wana vitambulisho vya taifa kabisaa.
Wanavyo... nina ushahidi wa bwana mmoja anaitwa "KEVIN ANTRUM"..., ni rafiki yangu. Mmarekani mwenye asili ya Puerto rico. Kahamia hapa na familia yake, ni daktari Aga khan, alipapenda Tanzania kwa sababu aliletwa kwa ajili ya field zile za madaktari mnabadilishana. Wa hapa wanaenda kule, wa kule wanakuja hapa kwa muda. Jamaa akanogewa akahamia hapa na mkewe na watoto wao wawili. Kanunua Hekalu Bahari beach na namba yake ya Vodacom imesajiliwa kwa jina lake. Nilichoka! Na kuna wabongo asilia wanasota mwaka wa 10 huu hawana vitambulisho... waafrika bana 😅😅😅🙌🏾
 
Back
Top Bottom