kindikwili
JF-Expert Member
- Oct 5, 2016
- 1,862
- 2,871
Wakuu amani iwe kwenu!
Leo sina mengi ila nataka niwaombe wajomba zangu wa TAKUKURU kwamba kuna wateja wao Kawe tena wateja wakubwa sana. Leo usiku wateja hao walikuwa wanapita nyumba kwa nyumba na kila mwenye kitambulisho cha kura alikuwa anakula pesa halali za kitanzania kati ya 30000/= na 40000/= Familia ya mjomba wangu wanaoishi nyumba moja watu 6 wenye vitambulisho walikula sh 180000/=
Mimi nimewapa taarifa kazi ya kujua hiyo rushwa inatolewa na nani ni kazi yenu, fanyeni ziara Kawe usiku kuanzia saa tatu kuendelea. Nawashukuru kwa imani kwamba mtalifuatilia hili nina imani kwamba huu ni muda wa TAKUKURU kufanya kazi usiku na mchana ili tupate viongozi wanaotokana na kura na si rushwa. kwa pamoja tutokomeze rushwa ya uchaguzi.
Kindi.
Leo sina mengi ila nataka niwaombe wajomba zangu wa TAKUKURU kwamba kuna wateja wao Kawe tena wateja wakubwa sana. Leo usiku wateja hao walikuwa wanapita nyumba kwa nyumba na kila mwenye kitambulisho cha kura alikuwa anakula pesa halali za kitanzania kati ya 30000/= na 40000/= Familia ya mjomba wangu wanaoishi nyumba moja watu 6 wenye vitambulisho walikula sh 180000/=
Mimi nimewapa taarifa kazi ya kujua hiyo rushwa inatolewa na nani ni kazi yenu, fanyeni ziara Kawe usiku kuanzia saa tatu kuendelea. Nawashukuru kwa imani kwamba mtalifuatilia hili nina imani kwamba huu ni muda wa TAKUKURU kufanya kazi usiku na mchana ili tupate viongozi wanaotokana na kura na si rushwa. kwa pamoja tutokomeze rushwa ya uchaguzi.
Kindi.