Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Katavi imewafikisha mahakamani watumishi saba wa serikali kwa tuhuma za kujihusisha na ubadhilifu wa fedha za serikali zaidi ya shilingi bilioni 1.23
Akizungumzia ubadhilifu huo Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi, Faustine Maijo amesema kufuatia uchunguzi waliofanya kwa muda wa zaidi ya wiki mbili uliowahusisha watumishi hao, walibaini kufujwa kwa fedha na watumishi hao kutoka Halmashauri ya Mpimbwe, Manispaa ya Mpanda na ofisi ya Mkuu wa Mkoa Katavi.
Maijo amesema fedha hizo ambazo zilikuwa kwenye akaunti ya halmashauri ya Mpimbwe zimefujwa na watumishi kwakudanganya kuwa walikua wakiwalipa wakandarasi waliofanya shughuli mbalimbali katika halmashauri hiyo.
Amesema uchunguzi umethibitisha kuwa fedha hizo ambazo ni zaidi ya bilioni moja zililipwa kwa watu binafsi ambao hawakua na kazi zozote walizofanya katika halmashauri hiyo na walikuwa ni watu ambao wanafahamiana nao.
Kesi hiyo namba 5 ya mwaka 2023 imetajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Katavi Gway Sumaye na mwendesha mashtaka Gregory Mhangwa amesema watuhumiwa wanashitakiwa kwa makosa matatu kujihusisha na genge la uharifu, uhujumu uchumi na wizi.
Akizungumzia ubadhilifu huo Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi, Faustine Maijo amesema kufuatia uchunguzi waliofanya kwa muda wa zaidi ya wiki mbili uliowahusisha watumishi hao, walibaini kufujwa kwa fedha na watumishi hao kutoka Halmashauri ya Mpimbwe, Manispaa ya Mpanda na ofisi ya Mkuu wa Mkoa Katavi.
Maijo amesema fedha hizo ambazo zilikuwa kwenye akaunti ya halmashauri ya Mpimbwe zimefujwa na watumishi kwakudanganya kuwa walikua wakiwalipa wakandarasi waliofanya shughuli mbalimbali katika halmashauri hiyo.
Amesema uchunguzi umethibitisha kuwa fedha hizo ambazo ni zaidi ya bilioni moja zililipwa kwa watu binafsi ambao hawakua na kazi zozote walizofanya katika halmashauri hiyo na walikuwa ni watu ambao wanafahamiana nao.
Kesi hiyo namba 5 ya mwaka 2023 imetajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Katavi Gway Sumaye na mwendesha mashtaka Gregory Mhangwa amesema watuhumiwa wanashitakiwa kwa makosa matatu kujihusisha na genge la uharifu, uhujumu uchumi na wizi.