TAKUKURU: Chenge hahusiki na tuhuma za RADA

Kwanini hii taarifa itoke sasa wakati huyu fisadi anagombea kuwa spika? Mafisadi wanaendelea kulindana lakini upo mwisho wao.

Tiba
 
Politics za Tanzania ni kama michezo ya kuigiza ya comedy. Juzi juzi Kikwete aliwanadi washutumiwa wa kesi za ufisadi kuwa ni viongozi safi. Leo baada ya 'ushindi' na kuwa raisi, wanamtaka Chenge awe Speaker ili azuie mijadala ya ufisadi bungeni. Ghafla taasisi ya kuzuia rushwa inatokea sawia na kusema kuwa Chenge hahusiki na kashfa ya radar. What a coincidence.

Poleni sana Watanzania wenzangu kwa kuonyeshwa huu mchezo ambao kusema kweli hauchekeshi bali ni mchezo wa mauti kwa Watanzania wengi. Poleni sana wale ambao hawakumchagua Kikwete, maana athari zake ndio zinaanza kujitokeza, hata juma halijapita tangu matokeo ya uchaguzi yatangazwe. Poleni sana, tena sana wale mliotaka kuondoa utawala wa kifisadi, lakini wakashinda kwa kutumia ufedhuli na nguvu za dola.

Hii michezo ya kuigiza ndio inaanza. Huu wa kwanza ni curtain raiser tu. Kuna mingine mingi inakuja, na sipendi kufikiri kuwa baada ya miaka mitano hali ya Watanzania itakuwaje. :A S angry:
 
Nafikiri kirefu hiki kimetulia zaidi, ingawa hakionyeshi kama kupamba rushwa ndiyo kusafisha wala rushwa!! je wana JF twaweza kukubaliana na kirefu rasmi cha taasisi hii?
Hii mijamaa ya ovyo kweli kweli, haina hata utu wala mishipa ya huruma kwa Watanganyika wanyonge wanaoibibiwa rasilimali za nchi yao kila siku! Hivi huyu hosea alizaliwa na mwanamke kweli? mbona mi namuona mtu feki sana? Hiyo Doctorate imepatikana je? au ametunukiwa na Mamet kile chuo cha Rostam na Salva Rweyemamu

...how about;

TAASISI YA KULINDA NA KUTETEA RUSHWA
 
Kwanini hii taarifa itoke sasa wakati huyu fisadi anagombea kuwa spika? Mafisadi wanaendelea kulindana lakini upo mwisho wao.

Tiba
Kwa sababu anagombea uspika ili akawalinde mafisadi bungeni.
 
siioni mantiki ya kuendelea kuiongelea PCCB ni wahafu kama walivyo hao wengine na hana hata mmoja mwenye uwezo wa kumkemea mwingine every thing that emerge from corruption it is corruption itself tujiulize PCCB imetoka wapi na inawajibika kwa nani majibu tunayo inawajibika kwa baba wa ufisadi!
 
Politics za Tanzania ni kama michezo ya kuigiza ya comedy. Juzi juzi Kikwete aliwanadi washutumiwa wa kesi za ufisadi kuwa ni viongozi safi. Leo baada ya 'ushindi' na kuwa raisi, wanamtaka Chenge awe Speaker ili azuie mijadala ya ufisadi bungeni. Ghafla taasisi ya kuzuia rushwa inatokea sawia na kusema kuwa Chenge hahusiki na kashfa ya radar. What a coincidence.

Poleni sana Watanzania wenzangu kwa kuonyeshwa huu mchezo ambao kusema kweli hauchekeshi bali ni mchezo wa mauti kwa Watanzania wengi. Poleni sana wale ambao hawakumchagua Kikwete, maana athari zake ndio zinaanza kujitokeza, hata juma halijapita tangu matokeo ya uchaguzi yatangazwe. Poleni sana, tena sana wale mliotaka kuondoa utawala wa kifisadi, lakini wakashinda kwa kutumia ufedhuli na nguvu za dola.

Hii michezo ya kuigiza ndio inaanza. Huu wa kwanza ni curtain raiser tu. Kuna mingine mingi inakuja, na sipendi kufikiri kuwa baada ya miaka mitano hali ya Watanzania itakuwaje. :A S angry:

...Halafu kuna Mazumbukuku humu ndani hata hayaelewi kwa nini tulikuwa tunataka kuung'oa huu Utawala na yanautetea kwa nguvu na akili zao zote.

 
...Halafu kuna Mazumbukuku humu ndani hata hayaelewi kwa nini tulikuwa tunataka kuung'oa huu Utawala na yanautetea kwa nguvu na akili zao zote.

..............waliokuwa wanautetea utawala ni kuwa wanafaidika nao!
 
Same old kukukuruka by Takukuru.
Smells Richmond-like, doesn't it?
 
edward-hosea-mkuu-wa-takukuru-229x300.jpg

Bosi wa TAKUKURU Dk. Edward Hosea


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: UCHUNGUZI KUHUSU TUHUMA ZA RADA

Tunapenda kuujulisha umma kuwa uchunguzi na ushahidi uliokusanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Shirika la Upelelezi - SFO la Uingereza kuhusu tuhuma za Rushwa katika ununuzi wa Rada, umeshindwa kumhusisha Bw. Andrew Chenge katika tuhuma hizo.

TAKUKURU inawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa chombo hiki kwa kutoa taarifa za kuwafichua wale wote wanaojihusisha na Rushwa kwani jukumu hili ni la kila mmoja wetu.

Imetolewa na
Doreen J. Kapwani,
Afisa Uhusiano-TAKUKURU
Novemba 08 , 2010
S. L.P. 4865,
Dares Salaam.


Simu: 2150043-6/2150360
Nukushi: (022) 2150047
Baruapepe:dgeneral@pccb.go.tz
Mtandao Prevention and Combating of Corruption Bureau


Waandishi wa habari walio makini wanawezawasiliana na SFO kupata toka kwao wanasemaje. Nafikiri watapata full story ilivyokuwa. Uzuri wazungu hawana siri. Wanaweza wakasema wameachana na uchunguzi sababu hawajapata ushirikiano toka Tz.

Kama Chenge kaachiwa, Idrisa Rashid vipi?

Na je Hebu angalia mambo yalivyokuwa kwenye hii link
http://www.facebook.com/l.php?u=http%3A%2F%2Fwww.scribd.com%2Fdoc%2F11490017%2FSFO-Report-on-the-Radar-Saga&h=73ba5
 
Niswala la muda ila Chenge hakubaliki na ukitaka kuona moto subiri hyo ijumaa wapeleke jina la Chenge. Mbona wabunge watachapana ngumi! Tunamuitaji Sita. God we need Sita to ths nation.
 
Kweli SIRIKALI yetu hii kiboko (Source Global Publisher)


YAH: UCHUNGUZI KUHUSU TUHUMA ZA RADA

Tunapenda kuujulisha umma kuwa uchunguzi na ushahidi uliokusanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Shirika la Upelelezi - SFO la Uingereza kuhusu tuhuma za Rushwa katika ununuzi wa Rada, umeshindwa kumhusisha Bw. Andrew Chenge katika tuhuma hizo.

TAKUKURU inawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa chombo hiki kwa kutoa taarifa za kuwafichua wale wote wanaojihusisha na Rushwa kwani jukumu hili ni la kila mmoja wetu.

Imetolewa na
Doreen J. Kapwani,
Afisa Uhusiano-TAKUKURU
Novemba 08 , 2010
S. L.P. 4865,
Dares Salaam.
 
Hii ni dhahiri kuna njama nzito za kumpa uspika chenge, na ukweli takukuru haina msaada na uwezo wa kufanya kazi ya kukamata wala rushwa ila ni dhahiri wapo kusumbua kina mwakalebela na makarani wala efu mbili kutafuta faili, kwa upande wa wakubwa takukuru hata pua hawasogezi, nafikiri dr hossea nae huwa anapewa 'cut' haiwezekani yeye si fisadi.
tukukuru wanakula pesa ya walipa kodi bure tuuu.
 
Waandishi wa habari walio makini wanawezawasiliana na SFO kupata toka kwao wanasemaje. Nafikiri watapata full story ilivyokuwa. Uzuri wazungu hawana siri. Wanaweza wakasema wameachana na uchunguzi sababu hawajapata ushirikiano toka Tz.

Kama Chenge kaachiwa, Idrisa Rashid vipi?

Na je Hebu angalia mambo yalivyokuwa kwenye hii link
http://www.facebook.com/l.php?u=http%3A%2F%2Fwww.scribd.com%2Fdoc%2F11490017%2FSFO-Report-on-the-Radar-Saga&h=73ba5

Dr Idrisa Rashid hata kunyooshewa kidole hamna alitajwa mara mbili hivi halafu kimya, hata wandishi kuwa wakiandika mara kwa mara Dr Idrisa jina lake huwa wanaliacha
 
Kweli SIRIKALI yetu hii kiboko (Source Global Publisher)


YAH: UCHUNGUZI KUHUSU TUHUMA ZA RADA

Tunapenda kuujulisha umma kuwa uchunguzi na ushahidi uliokusanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Shirika la Upelelezi - SFO la Uingereza kuhusu tuhuma za Rushwa katika ununuzi wa Rada, umeshindwa kumhusisha Bw. Andrew Chenge katika tuhuma hizo.

TAKUKURU inawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa chombo hiki kwa kutoa taarifa za kuwafichua wale wote wanaojihusisha na Rushwa kwani jukumu hili ni la kila mmoja wetu.

Imetolewa na
Doreen J. Kapwani,
Afisa Uhusiano-TAKUKURU
Novemba 08 , 2010
S. L.P. 4865,
Dares Salaam.


Takukuru Ofisi ya ajabu, ofisi ya kusafisha bila ya sabuni.

Takukuru walimsafisha Lowasa bila maji, baadaye akatiwa hatiani na bunge.

Takukuru ofisi ya kulea na kustawisha RUSHWA, ni kesi ngapi za rushwa ya uchanguzi ziko mahakamani, wakati rushwa ilikuwa inatolewa bila ya kificho nchi nzima?

Takukuru kuna sababu gani ya idara yenu kuendelea kuwepo nchini Tanzania.

Takukuru ni mzigo mkubwa usiobebeka kwa walipa kodi wa Tanzania.

 
Waandishi wa habari walio makini wanawezawasiliana na SFO kupata toka kwao wanasemaje. Nafikiri watapata full story ilivyokuwa. Uzuri wazungu hawana siri. Wanaweza wakasema wameachana na uchunguzi sababu hawajapata ushirikiano toka Tz.

Kama Chenge kaachiwa, Idrisa Rashid vipi?

Na je Hebu angalia mambo yalivyokuwa kwenye hii link
http://www.facebook.com/l.php?u=http%3A%2F%2Fwww.scribd.com%2Fdoc%2F11490017%2FSFO-Report-on-the-Radar-Saga&h=73ba5

duh hizo data za ndani kabisa mnatoa wapi wajameni du
sasa hapo anasafishwaje jamani wakati TAKUKURU wenyewe walishasema kwenye hiyo doc kuwa Chenge mali zake anashindwa kuelezea vizuri
 
Back
Top Bottom