Taifa teule na mataifa

Mkuu Mshana Jr kwa maoni yangu kwa reference ya bible/apocrypha na vitabu vya kiyahudi... Ni kwamba baada ya gharika tunaona dunia nzima yaani familia ya Nuhu ilikuwa inamuabudu Mungu mmoja ila baadae alipokuja wasumeria wakaanza ibada za masanamu huko shinar chini ya mfalme Nimrod ambaye aliweza kushawishi koo za Ham na Japhet kumfuata ila ukoo wa shem pekee ndio baadhi walibaku kumuabudu Mungu

Sasa Mungu akajinasibisha kupitia shem baada ya mnara wa babeli maana dunia nzima ilishaanza kuabudu masanamu..... Kupitia shem ndipo Abraham anazaliwa na anaishi kwenye pango kwa shem na kufundishwa habari za MUNGU wa kweli na alipotoka hapo aliweza kusimama katika imani na hilo likapelekea Mungu kuendelea kujitambulisha dunia kupitia ukoo wa SHEM na hilo likaendelea hadi Abraham then Yakobo mpaka Israel iliyofuata

HOWEVER baada ya wayahudi kumkana Mungu na kuanza kufanya waliyokatazwa Mungu akawalaani na kuwapa hukumu ikiwemo kuwatawanya duniani.... Kwenda utumwani na kushambuliwa na magonjwa kibao hivyo baada ya Israel kufanya uasi Mungu akaendeleza agano na abraham ila kulingana na maandiko wote wenye imani kwa Mungu wanakuwa uzao wa abraham by default na Yesu alipigilia msumari wa mwisho maana alileta wokovu kwa mataifa yote hivyo wanadamu wote tumekuwa taifa teule sio israel tena maana leo hii Mungu anaabudiwa dunia nzima tofauti na enzi hizo kila nchi ilikuwa na ibada zake na miungu yake

So kwa maoni yangu wanadamu wote tumekuwa taifa teule ila Israel ni mambo ya agano la kale tu na unabii wa siku za mwisho ila wote tupo sawa sasa na waisrael wanaofanya maasi na kutesa watu huko palestina wataonja moto wa jehanum kama kawaida unless na wenyewe wamrudie MUNGU wa kweli

Ni hayo tu

Labda niite wataalam wa historia na maandiko waje wanirekebishe ili tujifunze zaidi

Cc Malcom Lumumba tikakami wa lopelope chabuso blackstarline popbwinyo hearly
Mkuu asante sana "" Umepita vyema kabisa..."" Sina mashaka na ma bandiko yako "".... acha niendelee kujifunza zaidi ""..
 
Hapa kuna mkanganyiko mkubwa isije kuwa tunadhulumiwa ukweli bila kujua
sio isije kuwa " tuna dhulumiwa kweli mkuu" "tafiti nyingi za kihistoria zinaonyesha kuwa "" watu weusi ndio watu wakale zaidi na ndio watu ambao walipaswa kuwa na dini kubwa zenye ushawishi kwenye huu ulimwengu""... historia inasema nimrod alikuwa mtu mweusi " lakini mbona haushangai ulimwengu wa sasa jinsi unavyo mzungumzia kuwa alikuwa ni mtu mweupe ""....
 
Na kama kuna watu wanamkataa yesu kwa nguvu zote Duniani basi ni waisrael wale Jewish. Sijui kwanini bado wanaqualify kuwa taifa teule then watu wa pale Mbeya waliokoka mkoa mzima wanakuwa watu wa mataifa? Inanivuruga kichwa hii!

Its injustice!
Ha hahaa hahaa
 
Sijakuelewa kabisa..afu ni vyema ukafafanua kuliko kuniqotia mlolongo wa maandishi haya mkuu.

Fafanua sasa nikuelewe!
hahahaa ..analeta mahubiri " mpaka kwenye mambo yanayotaka kufikirisha bongo kwaajili ya kufanya uchambuzi uwe na mantiki
 
inawezekana waisrael wangemkubali Kristo dunia au watu wa mataifa wasingemjua kwa nafasi aliyo nayo.
dini kwa ujumla wake kwa kadri ya mapokeo ina mambo mengi kwa kadri ya anayetupokelesha kwa kuwa huwa pia inaweza kubeba maslahi binafsi kwa wapokeaji.
lakini ninachojifunza kwa watu hawa ni mambo makubwa mawili.
  1. utuzaji wao wa taarifa- inawezekana hakuna taifa litunzalo taarifa kwa umakini kama hawa jamaa kwa kadri ya vizazi vyao toka ibrahimu mpaka sasa na wamefanikiwa kuyaweka kwenye maandishi yakisomwa dunia nzima. pamoja maandishi yalizinduliwa misri ambako hawa jamaa walikuwa watumwa, lakini walitumia fursa vizuri kuzidi wa misri wenyewe.
  2. kiingine shida na kutumikishwa kwa muda mrefu na wamisri (kama tunavyoona baadhi ya kazi zao za ujenzi) zimewafanya kuwa na uwezo mkubwa wa kupambana na mazingira wakitumia resource chache kuleta mafanikio makubwa. iko mifano mingi lakini wengi tunajua taifa hili lilivyo na mvua chache lakini linaongoza kwa kilimo cha matunda na mbogamboga wakitumia zaidi kwa uangalifu mvua chache zinazonyesha ka kukinga maji na sehemu zingine za milima zinatumika kama matenki ya kuhifadhia maji na kushuka bondeni(kwa kadri ya simulizi).
naogopa sana kuwachambua kwa kuwa wanahusika na imani nilionayo na muda si mrefu nimetoka kwenye jumuiya na somo la leo limetoka 2timotheo 4:1-8 nikitutaka tuwaubirie watu wa mataifa injili.
hivyo kwangu mimi cha kujifunza ni kwamba:-
  1. katika shida zetu na masumbufu yetu tujitahidi kutafuta njia ya kuyatatua kwa urahisi na kwa akili zote. ( mfano mzuri VICOBA ilianzia niger baada ya shida za kinamama kutelekezwa na waume zao kwa ulevi na pengine na umalaya kulisababisha wao kuanzisha vikundi hivi, lakini leo wazungu walishavichukua vikawa vyao na jina la kibantu la vikundi hivi likapotezwa na sasa ni wao na hawakumbuki hata kuwalipa haki miliki kwa waanzishaji.)
  2. tujifunze kutunza kumbukumbu zetu vizuri ili siku zijazo tuweze kuzielezea vizuri haiingii akilini eti ziwa victoria pamoja na mlima wake wa bismarock eti ulivumbuliwa na mzungu waswahili walikuwa hawauoni?
  3. tutumie muda na maarifa kutambulisha kile tulichonacho na tulichofanya badala ya muda mwingi kuzungumzia udhaifu mfano hakuna ubishi mpaka sasa binadamu wa kwanza aliishi tanzania hvyo tungeweza kusema taifa la tanania ni taifa teule na wale wengine ni watu wa mataifa.
yapo mengi na inawezekana nimetoka nje ya mada lakini nimeona mchango huu waweza faa kwa kadri nilivyoona leo yafaa kuchangia.
 
Israel ndio inajulikana kama taifa teule la Mungu na kuna ushahidi mwingi mitandaoni kuwa dunia ilianzia mashariki ya kati....

Mengi yanayoandikwa kuhusu hizi dini mbili zinazomtambua Mungu mmoja... Yana asili na mashariki ya kati... Mitume manabii masinagogi, historia na kumbukumbu nyingi za ulimwengu wa imani na kwa sehemu historia chimbuko lake ni mashariki ya kati....

Rejea mada ya Je dunia ilianzia mashariki ya kati? ... Kuanzia maisha ya Eden mpaka gharika ya Nuhu na kuangamizwa kwa sodoma na gomora... Haya yote hayatoki nje ya hapo

Unapoendelea kusoma historia ya dunia kiimani na vitabu vya dini.. Kuna kaliba inapewa nafasi ya 'wa mataifa'.... Yaani kwa tafsiri rahisi wale wa nje ya mashariki ya kati...! Nje ya Israel!

Tuna hizi dini tulizoletewa Afrika na wazungu na waarabu.. Uislam bado una asili na mashariki ya kati... Ukristo ulifikaje ulaya kwa wageni wa dunia (wazungu)? Kisha pengine wakauchakachua kishapo ndio wakatuletea sisi? Hili hojaji linahitaji mjadala wake tofauti?

Lakini kwa sasa kuna maswali yanahitaji majibu ili kujiridhisha na hizi imani zetu

. Je wale wote walio nje ya mashariki ya kati ndio wa mataifa?

. Je kwanini kwenye Biblia takatifu China inatajwa kipekee? Katika kitabu cha mithali kwenye kutafuta maarifa watu wanaaswa wafike hata China?

. Je mpango mkakati wa Injili kwa watu wote (wa mataifa) ya kuwahubiria neno la Mungu watubu na kuokoka... Tafsiri yake ni ipi? Je hawa hawakuwa sehemu ya uumbaji wake?

. Je wapagani wanaohitaji kuhubiriwa injili.. Si wakazi wa dunia hii?
Historia ya Israel...

Nguvu waliyo nayo utabiri wa kurejea nyumbani... Namna yao ya kuabudu nakuamini tofauti na imani nyingine ni kama vile inatoa picha kuwa hata wazungu ni watu wa mataifa na si sehemu ya taifa teule! ?
weka hicho kifungu cha methali ilipotajwa china
 
Mkuu labda umechanganya na ile hadithi ya Mtume Muhammad [SAW] aliposema

"Itafuteni elimu ijapokuwa iko katika miji ya China, kwani kutafuta elimu ni wajibu (lazima) juu ya kila Mwislamu"

Akihimiza waumini waitafute elimu hata kama ipo mbali kiasi gani.
weka hicho kifungu cha methali ilipotajwa china
Jifunze kufuatilia mjadala wote hatua kwa hatua kabla hujaamua kuchangia... Ungekuwa umefanya hivyo usingekuja na swali lako hili
 
Mimi na zungumzia imani yangu unless tukubaliane kuwa iko Taurati, injili, Zaburi, Methali nk ambazo ni za Kikristo tu na nyingine za Kiislam tu. Lakini kama Abraham, Musa, Daudi, Bwana Yesu akiwa hapa duniani, kuwa hizi ni nafsi mojamoja, basi wale wa imani ya Kikristo watakuwa wanafanya makosa wakisema Yesu Kristo ndiye Issa SA. Sio Kweli kwa mujibu wa Biblia.

Yesu Kristo hakuacha kusema kwa uwazi kabisa ni amri/utaratibu gani wanadamu wanapaswa wafanye ili kumfuata yeye. Lazima kama Mkristo ujue kuwa Bwana Yesu alikuwa Mungu kweli na pia Binadamu Kweli. Hivyo alipokuwa anaelekeza ni taratibu gani zitumike ili kuwa mfuasi wake alikuwa akitimiza majukumu mawili kwa wakati mmoja, yaani lile la Kiungu na lile la kinabii mwanadamu.

Hawa manabii wengine wote tunao wajua walikuwa wanatimiza majukumu waliotumwa na Mungu/ Bwana Yesu kwa wanadamu ili hatimaye wanadamu waweze kufika kwa Mungu wao mbinguni na wasiishie jehanamu/motoni.

Kwa mkristo anaye ijua Biblia vizuri kumuambia Mtume Muhamad SA ni mtume/ nabii wa Mungu kamwe hawezi kukubali. Maana atakuuliza, je alibatizwa kwa maji na Roho? Jibu ni hapana. Na kama ni hapa wala huyo hamjui Bwana Yesu/Mungu si mmoja kati ya wale wa Yesu. Kusema unamjua Bwana Yesu wakati hufuati yale maagizo aliyokupa ili uwe mfuasi wake ni kujidanganya kwa ajili ya kujifariji kibinadamu. Kweli Mungu ni mmoja kwa maana wote tunao amini katika umbaji twa amini yeye ndio muumba wa vyote. Lakini katika ufuasi/kumfuata Mungu hakika hatumfuati Mungu mmoja. Wako waliopata neema ya kumfuta Mungu wa Kweli na wako ambao hawajaipata hiyo neema, Wamepotea/wamepotezwa lakini hawajui.


Kuhusu Taifa teule la Mungu ni kweli huu ndio utaratibu wa Mungu alio jiwekea ambao unajidhihirisha kwetu hata kwa kutumia logic ya akili za kibinadamu.

Umeeleza Vizuri kuhusu Abraham kuchaguliwa kuwa uzao wake ndio utaunda hilo taifa teule la Mungu . Nimesha sema mara kadhaa humu ni taifa teule kwa maana ya kuwa Mungu ageliwatumia wazawa/baadhi ya watu kutoka vizazi hivyo kwa ajili ya kuwa humbiria/kutoa ujumbe/ unabii uhusuo mambo ya Mungu na jinsi gani ya kumtii na kumtumikia.

Utaona alimchagua Abraham kwanza, katika watoto wa Abraham akachaguliwa Isihaka, katika watoto wa Isihaka akachaguliwa Yakobo nk ,nk, Mwishowe alichaguliwa Mfalme Daudi ambaye hatimaye kwa kupitia uzao wake Mungu mwenyewe alikuja hapa duniani kama Emanuel ambaye ni Bwana Yesu.

Baada ya Bwana Yesu Kuja hapa duniani wafuasi wake, yaani wale walio mpokea yeye kuwa Bwana na Mwokozi wao, nao kwa kupitia YESU wamekua/wamefanywa kuwa taifa teule la Mungu. Na ndio maana Mungu Mwana au nafsi ya Mungu ya uana/ubinadamu ilitia timu yenyewe hapa duniani kufanya kazi hiyo.

Kuhusu dini ya kiyahudi ni kweli kuwa asilimia kubwa ya Wayahudi, Mungu kawanyima hiyo neema ya kumkubali na kumtambua akiwa hapa duniani. Hata hivyo Tora yao imewawekea wazi kabisa kupitia manabii ambao ni ndugu kati yao wanadamu, kuwa atakuja Masihi/Bwana Yesu kuchukua pahala pa Mfalme Daudi. Wao wakaishia kufikiria mambo ya kimwili zaidi na wakasahau ya Kiroho. Wakadhania Masihi angewashindia vita hivi vya adui wa Kimwili,. Kumbe Masihi ni kweli kawashindia ile vita ya kiroho ambayo ni kupambana na dhambi na kushinda adhabu yake ya kifo cha kiroho na kimwili. Ukisha shinda vita vya kiroho ndio umemshinda shetani, wafuasi wake na kazi zao zote.

Utaona kuwa baada ya Bwana Yesu/Mungu kuja hapa duniani na kuwa fanya wafuasi wake walio mpokea kuwa taifa teule, aliwapa wale wafuasi baraka za kwenda kuuhubiri ulimwengu mzima habari njema za Wokovu wa Mungu kwa mwanadamu. Pia akawapa msaidizi Roho Mtakatifu ambayo ni nafsi ya Mungu ya tatu kuwa ongoza.

Yeyote aliye kuja na Imani ya Kiislam alikuwa makini kwa kujinasibisha kwa Mungu pale aliposema tunamkubali Nabii Issa SA (kwa mujibu wao Bwana Yesu/Issa bin Mariam) na mafundisho yake na akaenda mbali kwa kutengeneza mazingira ya kuwa aminisha wanadamu kuwa Mungu/Bwana Yesu ndio Nabiii Issa bin Mariamu ndiye Yesu. Wakati kama wewe ni mkristo uliye pataa neema ya Mungu ya kulijua neno la uzima la Mungu/Biblia kinachotajwa na wenzetu wa Uislam kusuhu Bwana Yesu eti ndiye Nabii Issa SA sio kweli. Na Mkristo kusema Nabii Issa wa Quran Tukufu ndiye Bwana Yesu wa Biblia anatenda dhambi ya uongo na anapaswa kutubu.




Sawa Mkuu,sote tuko sawa kwa Mungu,isipokuwa Bani Israel wao walichaguliwa kama binaadamu wa kusambaza yale aliyoyataka Mungu,yaani kuabudu Mungu mmoja na kufuata sharia zake..

Mapenzi ya Mungu kwa Bani Israel,na ule uteule aliowapa wa kusambaza aliyoyaamuru kayaondoa kwasababu hawa jamaa wameshindwa kuyafanya yale anayoyataka Mungu,Hawa jamaa wamelaaniwa,hakuna hata Mtume mmoja walioletewa wakamkubali…

Baada ya kumkana Musa,Bani Israel(Wayahudi) walikuwa wanasubii Masaya(Kristo kwa lugha ya kigiriki),Mungu akawaletea Masaya(Yesu aka Isa aka Iso aka Yoshua aka Jesus) lakini hata hivyo wakamkejeli na kumsulubu Msalabani..

Kuna watanzania humu JF wanafikiri dini ya kiyahudi(Hebrew) inamkubali Yesu(Isa) lakini hawajui kuwa Wayahudi wa kale na hawa wa sasa hawana habari kabisa na Yesu kwao wao wanamuona Yesu tapeli,mzushi tu..

Kutokana na Kukataa na kuwakejeli Mitume,Mungu kaahidi kwenye Quran kuwa,wale wataowakejeli na kuwakataa Mitume atawaondoa na kuwachagua Wengine,Mungu kamleta Muhamad ambae ni mtume pekee ambae sio Myahudi,Muhamad kafundisha yale yale aliyoyaleta Musa sema akasawazisha mengine na kuzidisha yale yaliokuwa hayajamaliza kuyafundisha Isa(Yesu)...
 
Israel walilaaniwa the moment walipokengeuka na kukufuru neema walizopewa kupitia kwa Nabii Musa...laana ile iliendelea mpaka kufikia kipindi cha Nabii Issa na bado waliendelea kukufuru na kumtishia kumuua Nabii Issa. Laana hiyo iliendelea na mpaka sasa inaendelea. ISRAEL ni Taifa lililolaaniwa.
Mkuu nakuunga mkono but Issa siyo yesu jaribu kuelewa.
 
Mkuu nakuunga mkono but Issa siyo yesu jaribu kuelewa.
Nabii Issa ni Mtume wa Mungu alyezaliwa na Maryam Bint Imran ..Nabii Issa hakuzaliwa hana Baba na huu ndo Muujiza mkubwa juu ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu..Nabii Issa alikuja na ujumbe wa kumuabudu Mungu aliye mmoja , kusali na kutoa zaka pamoja na kufanya yaliyo mema hakuuliwa wala hakusulubiwa kwa mujibu wa imani yangu ya Uislam.


Naomba nieleweshe juu ya Yesu.
 
Mkuu Mshana Jr kwa maoni yangu kwa reference ya bible/apocrypha na vitabu vya kiyahudi... Ni kwamba baada ya gharika tunaona dunia nzima yaani familia ya Nuhu ilikuwa inamuabudu Mungu mmoja ila baadae alipokuja wasumeria wakaanza ibada za masanamu huko shinar chini ya mfalme Nimrod ambaye aliweza kushawishi koo za Ham na Japhet kumfuata ila ukoo wa shem pekee ndio baadhi walibaku kumuabudu Mungu

Sasa Mungu akajinasibisha kupitia shem baada ya mnara wa babeli maana dunia nzima ilishaanza kuabudu masanamu..... Kupitia shem ndipo Abraham anazaliwa na anaishi kwenye pango kwa shem na kufundishwa habari za MUNGU wa kweli na alipotoka hapo aliweza kusimama katika imani na hilo likapelekea Mungu kuendelea kujitambulisha dunia kupitia ukoo wa SHEM na hilo likaendelea hadi Abraham then Yakobo mpaka Israel iliyofuata

HOWEVER baada ya wayahudi kumkana Mungu na kuanza kufanya waliyokatazwa Mungu akawalaani na kuwapa hukumu ikiwemo kuwatawanya duniani.... Kwenda utumwani na kushambuliwa na magonjwa kibao hivyo baada ya Israel kufanya uasi Mungu akaendeleza agano na abraham ila kulingana na maandiko wote wenye imani kwa Mungu wanakuwa uzao wa abraham by default na Yesu alipigilia msumari wa mwisho maana alileta wokovu kwa mataifa yote hivyo wanadamu wote tumekuwa taifa teule sio israel tena maana leo hii Mungu anaabudiwa dunia nzima tofauti na enzi hizo kila nchi ilikuwa na ibada zake na miungu yake

So kwa maoni yangu wanadamu wote tumekuwa taifa teule ila Israel ni mambo ya agano la kale tu na unabii wa siku za mwisho ila wote tupo sawa sasa na waisrael wanaofanya maasi na kutesa watu huko palestina wataonja moto wa jehanum kama kawaida unless na wenyewe wamrudie MUNGU wa kweli

Ni hayo tu

Labda niite wataalam wa historia na maandiko waje wanirekebishe ili tujifunze zaidi

Cc Malcom Lumumba tikakami wa lopelope chabuso blackstarline popbwinyo hearly

Mkuu Zitto Junior, naomba nikurekebishe mahali

Ahadi za Mungu kwa wana wa Israeli hazifutiki kamwe mpaka mwisho wa dahari, hilo ni agano la MUNGU na Ibrahimu hili ni agano la milele na milele

YEREMIA - SURA YA 31
1 Wakati huo, asema Bwana, nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Israeli, nao watakuwa watu wangu.
2 Bwana asema hivi, Watu wale walioachwa na upanga walipata neema jangwani; yaani, Israeli, hapo nilipokwenda kumstarehesha.
3 Bwana alinitokea zamani, akisema, Naam nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.


Kuhusu Waisraeli kuwakataa mitume na Manabii mtume Paulo alishasema sababu na chanzo chao

25 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.
26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.
27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao. (isaya 27:9) kuijua hiyo ahadi
28 Basi kwa habari ya Injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu.
soma warumi 11 sura nzima

Kwa maelezo zaidi juu ya hawa watu

soma Isaya na Yeremia
 
Nabii Issa ni Mtume wa Mungu alyezaliwa na Maryam Bint Imran ..Nabii Issa hakuzaliwa hana Baba na huu ndo Muujiza mkubwa juu ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu..Nabii Issa alikuja na ujumbe wa kumuabudu Mungu aliye mmoja , kusali na kutoa zaka pamoja na kufanya yaliyo mema hakuuliwa wala hakusulubiwa kwa mujibu wa imani yangu ya Uislam.


Naomba nieleweshe juu ya Yesu.

Alikufa au hakufa? Na kama alikufa alifufuka au hakufufuka. Kama hakufufuka yuko wapi? Maana wafu wako kaburini wakisubiria ile siku ya mwisho wa dunia yaani siku ya hukumu. Kiranja wa hiyo siku ni Bwana Yesu mwenyewe.

Bwana Yesu aliteswa, alisulubiwa, akafa, akazikwa na siku ya tatu akafufuka. Ameshinda kifo na dhambi, hatimaye akapaa akishudiwa na watu kwenda mbinguni.
 
Nabii Issa ni Mtume wa Mungu alyezaliwa na Maryam Bint Imran ..Nabii Issa hakuzaliwa hana Baba na huu ndo Muujiza mkubwa juu ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu..Nabii Issa alikuja na ujumbe wa kumuabudu Mungu aliye mmoja , kusali na kutoa zaka pamoja na kufanya yaliyo mema hakuuliwa wala hakusulubiwa kwa mujibu wa imani yangu ya Uislam.


Naomba nieleweshe juu ya Yesu.

Yesu ni kwetu wakristo, nyie ndio mnamwita nabii Issa
 
inawezekana waisrael wangemkubali Kristo dunia au watu wa mataifa wasingemjua kwa nafasi aliyo nayo.

28 Basi kwa habari ya Injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu.

Bibilia haijasaza kitu
 
Back
Top Bottom