Japo sina uhakika na andiko lako na la kwao, lakini kuna logic itakuwaje Trump amsifu JPM kwa swala la kuto kung'ang'ania madarakani wakati ndio kwanza kaingia madarakani? Wanao stahili sifa hiyo ni wale waliomtangulia, sababu wao waliachia madaraka kwa hiari na hawa kulazimisha kubaki madarakani, au aisifie Tanzania kwa kwa ujumla japo tayari tuna doa kule Zanzibar mambo haya kwenda sawa na hilo wamarekani wamelisema pia, na lingine ni sheria ya mitandao na vyombo vya habari hilo pia wamelipigia kelele na limetokea chini ya uongozi wa JPM. JPM kupata sifa toka mataifa ya western ni bado kabisa. Labda ubalozi wa USA Tanzania utatoa tamko kuhusu hilo.