Tahadhari ya utapeli mpya Dar kwa sasa

Niliozwa mke kumbe alikuwa mke wa mtu, siku tumelala saa sita usiku eti mjumbe na mume mwenzangu wamekuja kunifumania! Eti akanisamehe ila mke kamchukua, dili la pande mbili, nilikooa eti yule ni yatima hapa si kwao walipanga tu kwa muda.
 
Kuna kijana mtaani kwangu,Ni wakala wa m-pesa na kusajili line,

Kamsajilia mtu kwa kitambulisho chake,kaenda kufanya uhalifu,

Hapa ameuza nyumba yake kwa Bei ya kutupa amalize kesi,

Kaiuza juzi tu aisee
Duuuuh
 
kuna siku kiduchu wale washenzi wauza tyre used wakidai mpya kwa bei cheee waniunguze....yaani walinilenga vema na ilikuwa time za Christmas unajianda service gari tukale mbege....wakanitokea ghafla, full package brand new tyre...nne...bei ilikuwa nafuu ajabu...na zangu zilikuwa choka hatarii...kuwauliza mmepiga wapi...wakanambia wanafanya kwa godown ya mhindi....nikajiuliza hizi toka vingunguti mpaka sinza wamekosa mteja kweli hapo kati???... walikuwa wako na bodaboda mbili....nikazichukua tyre...nikawambie twendeni pale kwenye mpesa nkawalipe....kwa pembeni ya mpesa wanaziba pancha.....nkawaambia jamaa wa pancha naomba mniwekee tyre zangu mpya......kwani najua wale jamaa waliondoka saa ngapi....kuzifunua ni chakavu hatari......wamezipack vizuri ajabu....na wengi weshapigwa kihivyo...
 
Mnatakiwa mkauziane kwa makubaliano Polisi na au kwa mwanasheria au ofisi za serikali ya mtaa anapotoka.
Bado mtu hata kama una box anaweza kudai aliibiwa navyo pia mwisho wa siku ukang'ang'aniwa.
Kuibiwa cm na box uongo mkuu, swali la kwanza Ni je, yeye anaeshitaki ana ushaidi gani kuwa simu Ni yake? Me tayari ushaidi Ni box nasema nilinunua dukani yeye je?
 
Yupo dada ana page insta anajiita Veethriftstore anauza vitu used. Jina lake halisi ni Victoria. Nilitaka kununua washing machine used mwezi wa 6 akadai hela kabla nikarusha, delivery akasema baada ya siku 2. Mpaka leo siku 2 hazijafika na kufatilia refund ofisini kwake nikakuta mtu mwingine naye anadai refund amekata mpaka RB.Mimi nikaambiwa mzigo wangu haujafika. Baada ya kufatilia sana kwa simu, maana ofisini hawafungui tena hata geti, nikajibiwa nisimtishe. Bado namwona yupo insta analiza watu kule...ila dawa yake inachemka
Lete mrejesho
 
kna mdada aliliwa lak 5 nch 45, alilia huyo nusu awe chizi

Hahah!!

Wale washiraz koko hawana cha mswalie mtume...wameshaliza watu wengi mno!!!

Wamesharipotiwa sana kwenye vyombo vya dola lakini hakuna hata aliyweza kamatwa...
 
Mie niliuziwa iPhone feki

Kuna jamaa ashauziwa kipande cha sabuni akijua ni simu...dukani katest fresh kabisa, kafungiwa kwenye boksi lake fresh...

Lakini alipofika nyumbani, akakutana na kipande cha sabuni za rangi rangi zile kama batiki...
 
Yupo dada ana page insta anajiita Veethriftstore anauza vitu used. Jina lake halisi ni Victoria. Nilitaka kununua washing machine used mwezi wa 6 akadai hela kabla nikarusha, delivery akasema baada ya siku 2. Mpaka leo siku 2 hazijafika na kufatilia refund ofisini kwake nikakuta mtu mwingine naye anadai refund amekata mpaka RB.Mimi nikaambiwa mzigo wangu haujafika. Baada ya kufatilia sana kwa simu, maana ofisini hawafungui tena hata geti, nikajibiwa nisimtishe. Bado namwona yupo insta analiza watu kule...ila dawa yake inachemka

Huyo mbona anajulikana ni tapeli na wajanja walishamuanika..tumia muda mwingi kuchunguza hao wafanyabiashara wa insta...

Kukusaidia tu usinunue kitu insta kama vitu hivi havipo sawa...

1. Jitahidi ununue kwa watu wenye physical address/goli la biashara na sio wale wasioweka hata anuani ya mahali wamepanga au makazi...

2. Lipa hela pale unapokiona unachokihitaji na kukihakiki...

3. Fanya mawasiliano ya SMS/Whatsapp ili mbeleni uje kutumia kama ushahidi, usitegemee sana simu/audio...

4. Tumia muda mrefu kupitia comments/reviews kwenye page ya muuzaji, matapeli wengi huwa wana disable comments...
 
Hahah!!

Wale washiraz koko hawana cha mswalie mtume...wameshaliza watu wengi mno!!!

Wamesharipotiwa sana kwenye vyombo vya dola lakini hakuna hata aliyweza kamatwa...
Yaan kabla hajatuma pesa, alivyokua analainishwa maneno, mara atumiwe picha ya TV screen enyewe, mara abembelezwe, alivyotuma tyuuh,

Mbna aliambulia vumbi tyuuj text hazijibiwi cm haipokelew, mara inakatwa yaan full vituko, mdada acha aanze kulia
 
Kuna jamaa ashauziwa kipande cha sabuni akijua ni simu...dukani katest fresh kabisa, kafungiwa kwenye boksi lake fresh...

Lakini alipofika nyumbani, akakitana na kipande cha sabuni za rangi rangi zile kama batiki...
Za magadi?
 
Kwenye issue ya cm used au za kununua mikononi nahisi box Ni la muhimu sana, ukinunua simu ya mtu mkononi muambie akupe na box lake.
Mimi pia nimenunua simu mikononi kwa mtu mbaya zaidi hata aliyeiuza simjui zaidi tu imepita mikononi kwa rafiki yangu ndie anayemjua huyo muuzaji mana alinambia ni best yake.
Niliinunua lakini nikawa naogopa mwezi unaisha sasa nilishasahau sasa mkizungumzia hizi mada napata kihoro.
Sijawahi kununua simu mikononi mwa mtu hii ndio mara yangu ya kwanza na mwisho sirudii tena.
Hela yako inakukosesha amani mana hujui mazingira ilipotoka kama imetoka kwa usalama.
 
Mbona umuongoo kama pole pole kwahiyo cm ulinunua ukalizwa gari umelizwa tv umelizwa hee au Huna cha kuandika
 
Back
Top Bottom