Kwanza nitoe Pongezi zangu Nyingi kwa Viongozi wa Kitaifa akiwemo Mh Rais Samia Suluhu Hassan, rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania.
Pongezi zingine ziwaendee viongozi wakuu wa vyama vya siasa Mh Freeman Mbowe na Mh Zitto Zuberi Kabwe. Bila kuwasahau na wananchi wote wenye Mapenzi Mema.
Tatu sitaweza kuwasahau pia viongozi hawa kwa upekee kabisa Askofu Emaus Mwamakula na Lecturer Dr Lwaitama kwa Nasaha zao za kila siku kuhusu Amani, umoja na haki ktk Taifa letu la Tanzania.
Hivi Karibuni niliandika kuhusu Generali mmoja wa Jeshi la Israeli anaitwa Yoabu. Huyu alikuwa kiongozi wa juu majeshi yote ya falme hiyo wakati wa Utawala wa Mfalme Daudi Kusini mwa Israeli yaani Hebroni.
Ktk makala ile ilikuwa kwa mfumo wa Swali, Je Tanzania kuna Yoabu? Pengine kutokana na uwasilishaji wangu( mimi sio mwandishi) kuna baadhi ya wasomaji hatukuelewana. Sio kosa!
Sisi wengine wenye imani nyingi za hapa na pale kila jambo huwa tunalipima na kulitazama kwa mujibu wa imani zetu. Elimu ya dini tunaitumia kama reference kwenye mazingira yetu ya sasa.
Juzi Tarehe 8 Machi Mh Rais Suluhu alihutubia Taifa akiwa kwenye Jukwaa la wanachama wa Chadema, baraza kuu la wanawake lenye heshima afrika mashariki na kati.
Ktk hotuba yake aligusia uwepo w watu conservatives yaani wenye misimamo isiyobadilika hata kwenye jambo lenye Maslahi ya Kitaifa. Hawa watu sometimes ni watu hatari. Alisema wapo CCM na Wapo Chadema.
Abneli Mwana wa Neli alikuwa ni Mkuu w Jeshi la Mfalme Sauli Yerusalem. Yeye alikuwa coordinator wa shughuli zote za ulinzi na maslahi ya ufalme wa Saul kipindi ambacho Mfalme Sauli alikuwa na migogoro ya kiutawala dhidi ya Mfalme Daudi.
Hofu ya Sauli ni kuhusu Daudi anayetaka kuchukua ufalme wa Israel yote yaani Hebroni na Yudea( Yerusalem).
Kulipiganwa vita mbali mbali kati ya Daudi na Sauli na kati ya Daudi na Wafilisti( waparestina).
Kutokana na uhasama kuwa mkubwa upande wa Sauli ulianza kushindwa kuhimili mapambano. Watu wa Sauli walikufa wengi, na wengine kubaki walemavu.
Jemedali Abneli mwana wa Neli akatumwa Mission kwenda kwa Mfalme Daudi kukaa kwa amani na kuridhiana ili suluhu ipatikane bila kuumiza wananchi wao.
Ugeni kwa upande mmoja ukiongozwa na Abneli na upande wa pili akiongozwa Mfalme Daudi Mwenyewe katika Ikulu yake.
Kitendo kile cha kufanya mazungumzo ya amani hakikumfurahisha General Yoabu. Alianza kuona Abneli anaweza kuwa Royal kwa Daudi na hivyo kuna uwezekano Abneli anaweza kuchukua nafasi ya Yoabu.
Ikawa walipomaliza maridhiano Daudi alisindikia msafara wa Abneli baadae akarudi Ikulu.
Wakati huo huo Mwanajeshi Katiri aoiyekuwa na roho mbaya kuwahi kutajwa katk Biblia Yoabu alikuwa ametoka kuongoza Vita huko Gathi kwa wafilisti na wa Amaleki.
Alipofika Ikulu akadokezwa kuwa muda mfupi uliopita Abneli alikiwa Ikulu akifanya mazungumzo na Mfalme.
Basi akapiga mbio kuwafata akina Abneli.
Kwa kuwa Abneli aliamini ni wakati wa amani na yakale yamekwisha si ndweli alisimamishwa na Yoabu akimwambia anataka wasalimiane na kukumbatiana.
2samweli 3: 24-25
Raraabii!! Abneli akaamini akamkumbatia Yoabu. Kumbe Yoabu alikuwa anaongozwa na Hila. Alikuwa ameficha kisu Mfukoni kwa nyuma. Wakati wakisalimia kwa amani Yoabu akamchoma Kisu tumboni. Abneli mwana wa Neli akafariki palepale.
Taarifa za Kifo cha Abneli zilisambaa kwa kasi sana. Nchi nzima ya Israel ikaingia kwenye majonzi makubwa. Hofu na vilio vikatawala. Nchi nzima wakafunga na kusali kwa siku Tatu wakiomboleza.
Mfalme Daudi alisikia habari zile zikamsikitisha sana. Akalia na kuomboleza mbele ya Raia wake. Hata ushindi waliopata kule Amaleki ukaingia doa.
Daudi analia mbele ya Kaburi la Abneli akisema imekuwaja Abneli umekufa kizembe hivyo? Kwani ulifungwa miguu na mikono?
Kosa la Daudi ni kusahau kukumbuka kuwa ndani ya Utawala wale kuna Wahafidhina wasiopenda utengamano. Wasiopenda amani kwa wengine. Yaani kwao bora vita na mateso kuliko umoja na mshikamano.
Yoabu alitumia vita na vurugu kujinufaisha na kupata umaarufu kwa kuwa alijua kupigana na siraha za kutosha aliweza kuzitumia vyema. Hivyo alibaki kuwa ni kipenzi cha Mfalme.
Kwa lugha nyingine nje ya vita na uhasama Yoabu alikuwa hana sifa nyingine. Hana cha kumuonesha Mfalme. Hana maana na hana kazi. Hivyo migogoro kwake ilikuwa na Advantage kubwa bila kujali Mfalme alikuwa akichukizwa na hali ile. Ilifikia hatua Yoabu akamuua Mtoto wa Daudi kwa kumchoma Mkuki moyoni na mfalme akabaki analia tu asimfanye kitu Yoabu kwa kuwa alijua bila Yoabu vita nyingi vya maaduni asingetoboa. Hivyo mfalme alibaki kufadhaika moyoni tu.
Kwa Upande wa Viongozi wetu wa Kitaifa wameligundua hilo. Ni muhimu sana kuongeza umakini dhidi ya wahafidhina wasije wakavuruga hii mipango mizuri.
Na Mwenyezi Mungu awasimamie na kuwabariki sana.
Nimesikia kuna vikao vinaendelea kwa maslahi ya Taifa. Mungu awajali mkafanikishe jambo hili mweze kuwatumikia Wana wa Mungu wa Tanzania kwa mafanikio makubwa.
Asalam Aleykum.
2Samwel3: 20-39.
Pongezi zingine ziwaendee viongozi wakuu wa vyama vya siasa Mh Freeman Mbowe na Mh Zitto Zuberi Kabwe. Bila kuwasahau na wananchi wote wenye Mapenzi Mema.
Tatu sitaweza kuwasahau pia viongozi hawa kwa upekee kabisa Askofu Emaus Mwamakula na Lecturer Dr Lwaitama kwa Nasaha zao za kila siku kuhusu Amani, umoja na haki ktk Taifa letu la Tanzania.
Hivi Karibuni niliandika kuhusu Generali mmoja wa Jeshi la Israeli anaitwa Yoabu. Huyu alikuwa kiongozi wa juu majeshi yote ya falme hiyo wakati wa Utawala wa Mfalme Daudi Kusini mwa Israeli yaani Hebroni.
Ktk makala ile ilikuwa kwa mfumo wa Swali, Je Tanzania kuna Yoabu? Pengine kutokana na uwasilishaji wangu( mimi sio mwandishi) kuna baadhi ya wasomaji hatukuelewana. Sio kosa!
Sisi wengine wenye imani nyingi za hapa na pale kila jambo huwa tunalipima na kulitazama kwa mujibu wa imani zetu. Elimu ya dini tunaitumia kama reference kwenye mazingira yetu ya sasa.
Juzi Tarehe 8 Machi Mh Rais Suluhu alihutubia Taifa akiwa kwenye Jukwaa la wanachama wa Chadema, baraza kuu la wanawake lenye heshima afrika mashariki na kati.
Ktk hotuba yake aligusia uwepo w watu conservatives yaani wenye misimamo isiyobadilika hata kwenye jambo lenye Maslahi ya Kitaifa. Hawa watu sometimes ni watu hatari. Alisema wapo CCM na Wapo Chadema.
Abneli Mwana wa Neli alikuwa ni Mkuu w Jeshi la Mfalme Sauli Yerusalem. Yeye alikuwa coordinator wa shughuli zote za ulinzi na maslahi ya ufalme wa Saul kipindi ambacho Mfalme Sauli alikuwa na migogoro ya kiutawala dhidi ya Mfalme Daudi.
Hofu ya Sauli ni kuhusu Daudi anayetaka kuchukua ufalme wa Israel yote yaani Hebroni na Yudea( Yerusalem).
Kulipiganwa vita mbali mbali kati ya Daudi na Sauli na kati ya Daudi na Wafilisti( waparestina).
Kutokana na uhasama kuwa mkubwa upande wa Sauli ulianza kushindwa kuhimili mapambano. Watu wa Sauli walikufa wengi, na wengine kubaki walemavu.
Jemedali Abneli mwana wa Neli akatumwa Mission kwenda kwa Mfalme Daudi kukaa kwa amani na kuridhiana ili suluhu ipatikane bila kuumiza wananchi wao.
Ugeni kwa upande mmoja ukiongozwa na Abneli na upande wa pili akiongozwa Mfalme Daudi Mwenyewe katika Ikulu yake.
Kitendo kile cha kufanya mazungumzo ya amani hakikumfurahisha General Yoabu. Alianza kuona Abneli anaweza kuwa Royal kwa Daudi na hivyo kuna uwezekano Abneli anaweza kuchukua nafasi ya Yoabu.
Ikawa walipomaliza maridhiano Daudi alisindikia msafara wa Abneli baadae akarudi Ikulu.
Wakati huo huo Mwanajeshi Katiri aoiyekuwa na roho mbaya kuwahi kutajwa katk Biblia Yoabu alikuwa ametoka kuongoza Vita huko Gathi kwa wafilisti na wa Amaleki.
Alipofika Ikulu akadokezwa kuwa muda mfupi uliopita Abneli alikiwa Ikulu akifanya mazungumzo na Mfalme.
Basi akapiga mbio kuwafata akina Abneli.
Kwa kuwa Abneli aliamini ni wakati wa amani na yakale yamekwisha si ndweli alisimamishwa na Yoabu akimwambia anataka wasalimiane na kukumbatiana.
2samweli 3: 24-25
Raraabii!! Abneli akaamini akamkumbatia Yoabu. Kumbe Yoabu alikuwa anaongozwa na Hila. Alikuwa ameficha kisu Mfukoni kwa nyuma. Wakati wakisalimia kwa amani Yoabu akamchoma Kisu tumboni. Abneli mwana wa Neli akafariki palepale.
Taarifa za Kifo cha Abneli zilisambaa kwa kasi sana. Nchi nzima ya Israel ikaingia kwenye majonzi makubwa. Hofu na vilio vikatawala. Nchi nzima wakafunga na kusali kwa siku Tatu wakiomboleza.
Mfalme Daudi alisikia habari zile zikamsikitisha sana. Akalia na kuomboleza mbele ya Raia wake. Hata ushindi waliopata kule Amaleki ukaingia doa.
Daudi analia mbele ya Kaburi la Abneli akisema imekuwaja Abneli umekufa kizembe hivyo? Kwani ulifungwa miguu na mikono?
Kosa la Daudi ni kusahau kukumbuka kuwa ndani ya Utawala wale kuna Wahafidhina wasiopenda utengamano. Wasiopenda amani kwa wengine. Yaani kwao bora vita na mateso kuliko umoja na mshikamano.
Yoabu alitumia vita na vurugu kujinufaisha na kupata umaarufu kwa kuwa alijua kupigana na siraha za kutosha aliweza kuzitumia vyema. Hivyo alibaki kuwa ni kipenzi cha Mfalme.
Kwa lugha nyingine nje ya vita na uhasama Yoabu alikuwa hana sifa nyingine. Hana cha kumuonesha Mfalme. Hana maana na hana kazi. Hivyo migogoro kwake ilikuwa na Advantage kubwa bila kujali Mfalme alikuwa akichukizwa na hali ile. Ilifikia hatua Yoabu akamuua Mtoto wa Daudi kwa kumchoma Mkuki moyoni na mfalme akabaki analia tu asimfanye kitu Yoabu kwa kuwa alijua bila Yoabu vita nyingi vya maaduni asingetoboa. Hivyo mfalme alibaki kufadhaika moyoni tu.
Kwa Upande wa Viongozi wetu wa Kitaifa wameligundua hilo. Ni muhimu sana kuongeza umakini dhidi ya wahafidhina wasije wakavuruga hii mipango mizuri.
Na Mwenyezi Mungu awasimamie na kuwabariki sana.
Nimesikia kuna vikao vinaendelea kwa maslahi ya Taifa. Mungu awajali mkafanikishe jambo hili mweze kuwatumikia Wana wa Mungu wa Tanzania kwa mafanikio makubwa.
Asalam Aleykum.
2Samwel3: 20-39.