TRA wako katika oparesheni kabambe ya kukamata yeyote anaeingiza mafuta ya kula nchini baada ya kuzuia shehena kubwa ya mafuta. Mimi ni mmoja ya wasambazaji wa mafuta mikoani na leo jioni nimepenyezewa taarifa kwamba TRA wanatengeneza crisis ya mafuta na kilichowaudhi ni kuwa pamoja na kuzuia bandarini bado mtikisiko haujatokea kama ilivyokuwa wakati wa sukari ambapo kulitokea upungufu mkubwa lakini tofauti na mafuta ukiachana na kupanda kwa bei lakini bado yanapatikana mtaani. Ninavyoandika usiku huu wamesambazwa maeneo yote ya pwani ili kuzuia wanaoingiza kwa magendo tokea zanzibar kwa majahazi.
Tunachoshindwa kuelewa ni kwa nini wanafanya hivi, tungeweza kusema wanatengeneza demand ili mmoja ya wafanyabiashara wakubwa apige hela kwa kuuza shehena yake lakini wengi tunafahamiana hakuna mwenye mzigo wa kutosha, tulichobaki tunahisi kuna uwezekano TRA wanacheza dili mafuta yakipotea sokoni watangaze kuruhusu shehena toka nje ya nchi kuingia kufidia halafu serikali ijikabidhi jukumu la kuagiza, au kumpa mmoja ya wafanyabiashara kazi hii ili wapate pa kupigia kodi ili kuchakachua mahesabu yao. Wanasahau anaeumia ni mtanzania wa chini ambaye atapandishiwa bei ya mkate, chapati, maandazi na hata chakula. Mungu atusaidie.
Tunachoshindwa kuelewa ni kwa nini wanafanya hivi, tungeweza kusema wanatengeneza demand ili mmoja ya wafanyabiashara wakubwa apige hela kwa kuuza shehena yake lakini wengi tunafahamiana hakuna mwenye mzigo wa kutosha, tulichobaki tunahisi kuna uwezekano TRA wanacheza dili mafuta yakipotea sokoni watangaze kuruhusu shehena toka nje ya nchi kuingia kufidia halafu serikali ijikabidhi jukumu la kuagiza, au kumpa mmoja ya wafanyabiashara kazi hii ili wapate pa kupigia kodi ili kuchakachua mahesabu yao. Wanasahau anaeumia ni mtanzania wa chini ambaye atapandishiwa bei ya mkate, chapati, maandazi na hata chakula. Mungu atusaidie.