Tahadhari na gari toyota rav 4 T129DEZ

Tahadhari na gari toyota rav 4 T129DEZ

Tuanzisheni thread hapa jamvini inayo husu polisi na kazi zao jinsi wanavyo tuhudumia. Tueleze mabaya yote tunayo yapata toka kwao na hata mazuri. Tuweke wazi ni kituo gani, na polisi gani, jina ikiwezekana. Hili linaweza kusaidia kufikisha ujumbe kwenye ngazi za juu. Na sisi wananchi tukaelimishana kujua haki zetu na pia kuelimishana pale tunapokua na makosa.
Wazo zuri sana hili...tuuweke uozo wao wote wa polisi na matukio yao ya rushwa na ukiukwaji maadili kwa nchi nzima..hii itasaidia sana..moderators wazo hilo hapo,.
 
Ndugu zetu polisi tunaomba ushirikiano kwa masuala ya usalaama wetu wote na mali zetu kama mlivyo tuomba sisi wananchi kuhusu ulinzi shirikishi.Leo kufanyiwa raia kesho mtafaniwa ninyi na hapo ndipo mtaomba raia kutoa taarifa za uhalifu.Naomba polisi tutokomeze huu uhalifu ili tuishi kwa amani.
 
Wazo zuri sana hili...tuuweke uozo wao wote wa polisi na matukio yao ya rushwa na ukiukwaji maadili kwa nchi nzima..hii itasaidia sana..moderators wazo hilo hapo,.

Na pia ikiwezekana hizi tread iwe kwa mikoa ili iwe rahisi zaidi kufuatilia. Kila mkoa ukiwa na thread yake labda wahusika wa juu wa mikoa wataweza kufuatilia kiurahisi na wananchi wa mikoa husika kujua kinacho endeleana.
Kwa kweli tumesha choka na hao polisi na huduma Yao mbovu.
 
Jamaa naona umeamua kwenda kuripoti tukio kwa wezi wenzake huwezi kupata msaada huko! We chukua hatua mkononi kwani silaa yako hujaenda kuihakiki?
 
Sijui hawa Polisi wamejifunzia wapi hiyo taaluma yao??
 
Police wa Tanzania nii wazembe na wapenda rushwa..!file linapoteaje?
 
Na pia ikiwezekana hizi tread iwe kwa mikoa ili iwe rahisi zaidi kufuatilia. Kila mkoa ukiwa na thread yake labda wahusika wa juu wa mikoa wataweza kufuatilia kiurahisi na wananchi wa mikoa husika kujua kinacho endeleana.
Kwa kweli tumesha choka na hao polisi na huduma Yao mbovu.
Iwe hivyo mkuu maana hamna namna tena tumewachoka polisi wetu. Na sio eti sababu ya malipo/mshahara kidogo-HAPANA- ni hulka tu ya polisi wetu kupenda vya kunyonga.. Nimeishi majuu polisi wa kule sio kwamba eti wana mishahara mikuubwa , ni sawa tu na ya wabeba mabox wengine lakini hukuti wakidai rushwa au kupindisha maadili.Jeshi la polisi bongo linahitaji mabadiliko makubwa sana..NI JIPU SUGU.
 
Tuanzisheni thread hapa jamvini inayo husu polisi na kazi zao jinsi wanavyo tuhudumia. Tueleze mabaya yote tunayo yapata toka kwao na hata mazuri. Tuweke wazi ni kituo gani, na polisi gani, jina ikiwezekana. Hili linaweza kusaidia kufikisha ujumbe kwenye ngazi za juu. Na sisi wananchi tukaelimishana kujua haki zetu na pia kuelimishana pale tunapokua na makosa.
Mkuu umetoa point ya muhimu sana, polisi ni tatizo kubwa sana hapa Bongo. Mwenyew yalishanifika kama ya mtoa mada. Kila njia ninayojaribu ninayoona kama itafaa kuwatia watuhumiwa wangu ndani ninakutana na vikwazo vya hao hao polisi. Kuna mda nilikua ninajiuliza mwenyewe kua, hawa watu wana matatizo gani?? sababu kuna mambo mengine ni ya kutumia akili kidogo tu., ila wao ni kama hawapo.
 
polisi wa Tanzania hawana msaada na raia pale mtu anaporipoti tatizo lake na anahitaji msaada.
mimi nilikua na ishu ya kuibiwa nikapata hadi na namba za wezi na mpaka maeneo wanayoishi ila sikupata maaada wa kuwakamata mpaka niliamua kuingia front mwenyewe na kuwapeleka kituoni.ilikua ni polisi chang'ombe.
Polisi ni jipu..weka RB namba na kituo hapa.
alafu muda mwingine wanaomba ela ya mafuta wakamkamate mwizi
 
Ungaliwaambia polisi gari lako la ccm basi hao wahalifu wangalishakamatwa.
 
Sina hamu na Polisi ...siku ukipata tatizo utajuta labda uamue kuhonga ....kiukweli zisipochukuliwa hatua za haraka tutaelekea kwenye uhalifu ambao hatujapata kushuhudia ....kama kungekuwa na ukaguzi wa kueleweka jinsi askari wanavyoshughulikia issues pengine askari wangekuwa na adabu ...ukaguzi wa doria, upelelezi n.k askari wangefanya kazi huku wakijua kuna watu wa kukagua utendaji wao. Lakini tatizo wakubwa wengi hawasimamii utendaji wa askari....wakati mwingine hata ukaguzi wa nguvu wa doria na ufanisi wake....labda wapelekwe maafisa wa JWTZ waliozoea maisha ya kulala porini wasimamie operations za polisi hadi watakapopatikana askari wanaoweza kufanya kazi za kijeshi kweli ...
 
pole mkuu waliotaka kuiba ni vibaka ukaenda kutoa taharifa kwa majambazi huwezi pata msaada tunashukuru kwa taharifa.
 
Wandugu nimeona ni bora nika share hili jambo nanyi ili mchukue tahadhari.
Hilo gari linatumika kwenye uwizi wa vifaa vya magari.

Nilikuta likiwa limepaki karibu kabisa na gari langu mida ya saa 4 usiku, walipo niona wa kaingia kwenye gari na kuondoka. Kutizama gari tayari walisha vunja kioo kidogo na bonet walisha fungua.nikakimbizana nao nikafanikiwa kusoma hizo no za gari.

Nime report hili swala polisi wiki ya pili sasa mara mpelelezi hajapangwa na mara ya mwisho nimeambiwa file limepotea niende nika andike tena maelezo. Nime amua kutokwenda na kulireport hili jambo hapa.
Hivi polisi wanavyosumbua hivyo wanataka tuwaeleweje?
 
Mimi niliwahi kuibiwa nikaenda kuripoti polisi, jamaa wakanijibu nifanye upelelezi mwenyewe nikimjua mwizi nikawaambie.
 
Tuanzisheni thread hapa jamvini inayo husu polisi na kazi zao jinsi wanavyo tuhudumia. Tueleze mabaya yote tunayo yapata toka kwao na hata mazuri. Tuweke wazi ni kituo gani, na polisi gani, jina ikiwezekana. Hili linaweza kusaidia kufikisha ujumbe kwenye ngazi za juu. Na sisi wananchi tukaelimishana kujua haki zetu na pia kuelimishana pale tunapokua na makosa.
Tuanzisheni thread hapa jamvini inayo husu polisi na kazi zao jinsi wanavyo tuhudumia. Tueleze mabaya yote tunayo yapata toka kwao na hata mazuri. Tuweke wazi ni kituo gani, na polisi gani, jina ikiwezekana. Hili linaweza kusaidia kufikisha ujumbe kwenye ngazi za juu. Na sisi wananchi tukaelimishana kujua haki zetu na pia kuelimishana pale tunapokua na makosa.
kwel kabsa
 
Back
Top Bottom