Tahadhari kwa waumini wa Gwajima

Tahadhari kwa waumini wa Gwajima

Bahati nzuri Dr Slaa ni mtumishi wa Mungu kwa cheo cha upadri na ni mtu anayejua nini maana ya siri na nini maana ya kutunza siri.

Gwajima naye ni mtumishi wa Mungu mwenye cheo cha uasikofu kama ilivyo kwa Dr slaa naye ana jua siri ni nini na namna ya kutunza siri.

Kwa pamoja wote ni watumishi wa Mungu wanaopaswa kutunziana siri pamoja na siri za watu wengine.

Kama kuna mtumishi mmoja kaamuwa kumwaga ugali hadharani,mwenzake kajibu kwa kumwaga mboga hadharani,huyu mtumishi wa pili aliyejibu kwa kumwaga mboga hadharani ana laumiwa kwa kosa gani?.

huu unaitwa ukweli unaouma... hakuna anaependa kusikia ukweli huu
 
Gwajima aliwarekodi watu aliokuwa anaenda kuwapa ushauri wa kiroho.
Halafu anatangaza ushauri huo na matatizo yao hadharani.
Ole wako...ukimwambia siri zako utajuta.

Ukimwambia umuheshimu usitoke na kuwadanganya wana nchi.
 
Bahati nzuri Dr Slaa ni mtumishi wa Mungu kwa cheo cha upadri na ni mtu anayejua nini maana ya siri na nini maana ya kutunza siri.

Gwajima naye ni mtumishi wa Mungu mwenye cheo cha uasikofu kama ilivyo kwa Dr slaa naye ana jua siri ni nini na namna ya kutunza siri.

Kwa pamoja wote ni watumishi wa Mungu wanaopaswa kutunziana siri pamoja na siri za watu wengine.

Kama kuna mtumishi mmoja kaamuwa kumwaga ugali hadharani,mwenzake kajibu kwa kumwaga mboga hadharani,huyu mtumishi wa pili aliyejibu kwa kumwaga mboga hadharani ana laumiwa kwa kosa gani?.

Nakubaliana nawe kuwa Dr. Slaa alimwaga mboga na kajibiwa na Askofu Gwajima na kwa hili hakuna tatizo bali ni mafundisho tu madogo kwa Dr. Slaa kuwa si vema kusema uwongo kwa kudhani kuwa wewe ndiye mwenye uwezo wa kuongea pekee.

Watanzania wenye uwezo wa kuongea wapo wengi tena si wanansiasa pekee bali hata raia wa kawaida, tatizo ni kuwa fursa ya kuongea kwenye vyombo vya habari kama Redio na Tv ndiyo inayokosekana.
 
Siasa zinashangaza sana.
Ni amazingi Chadema wanavyompenda Lowassa kipindi hiki.
Anaitwa mwokozi, Mussa, Yesu etc...lakini juzi tu alikuwa anatukanwa kila aina ya tusi na Chadema.
Siasa bwana 😆

Hata CCM waliita Akina EL, Sumaye,Masha makapi baada ya kuhama CCM, ndo siasa
 
eti Josephine alizimia coz of majini,Dr alimpigia Gwajima ili apate msaada leo kaitumia hii against Josephine,kwamba ana mapepo mbaya sana hii

gwajima ni mwongo. anataka kutuaminisha kuwa yeye ana nguvu za uponyaji wakati yeye alilazwa icu! anaona vibaya maaskofu kutukanwa wakati yeye alitukana mpaka akafunguliwa kesi! ina maana hizo nguvu zake za ajabu ndizo zinazojaza watu kwenye kampeni bila wao kujitambua? huyu mtu ni weka mbali na watoto.
 
Samahani kidogo jamani!hivi kiongozi wa dini ukidhalilishwa huna haki ya kuusema ukweli ili kuiweka sawa jamii unayoitumikia?Ukipigwa shavu la kushoto unatakiwa ugeuze na la kulia utandikwe?
 
Bishop anajiamini,anajua na pia smart...mshenga daraja la moja.
 
Ni muda mrefu jamii yetu imekuwa ikiwaheshimu na kuwaamini viongozi wa dini katika masuala mbalimbali ya kiroho na ustawi wa familia.

Ni jambo la kawaida sana kwa waumini wa dini zote kupeleka matatizo yao mbalimbali ya kifamilia kwa viongozi wa dini.

Ni dhahiri kwamba wengi wetu hupeleka masuala mbalimbali hata yale ya unyumba na siri nzito nzito za chumbani na familia kwa ujumla kwa kuwa tuna imani viongozi wa dini wana hulka ya kutunza siri na kusaidia kutatua matatizo yetu ya kiroho au kifamilia.

Hii ni tofauti kwa Gwajima ambaye ni mtomvu wa heshima ya kiongozi wa dini kwa kueleza siri za familia aliyoipa huduma za kiroho kisa tu kachokozwa kisiasa na yeye kajibu kwa kutoa siri za familia ya Slaa.

Angekuwa daktari angeweza kufutiwa cheti na kudaiwa fidia.

Lakini tukumbuke ni Gwajima huyu huyu aliyeshutumiwa kuvuruga ndoa ya Mbasha badala ya kutatua mgogoro wa familia hiyo.

Hii ni trend ya Gwajima anayejiita Bishop ambayo inatakiwa kuangaliwa kwa jicho la Tahadhari hasa hasa na waumini wake wanaompelekea siri za ndani.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANI!!

inavyooneka hukumckiliza vizur hoja zake.ila ulickiliza kishabik ukiwa na chuki binafc nae na kumuunga mkono dr kwa sabb zako binafc.



think big
 
sisi kinachotuuma ni ndugu zetu waumini,aina ya wachungaji kama ngwajima,hachelewi kukuita ufyonze maziwa ya baraka toka kwenye naniliu yake,eti ili utokwe na mapepo...

Ha ha ha ha ha we jamaa bhana....
 
Mkuki kwa nguruwe. ....aliyeanza kumchafua mwenzake nani?

Hapo mkuu hawataona kuwa alitakiwa aeleze jinsi anavyomfahamu Slaa aliemsingizia kumwambia mapadre thelathini kati ya thelathini na wanne wamehongwa na Lowassa. Yeye Gwajima hana uthubutu wa kusema mwenyewe hadi amtume Slaa? Gwajima alileta ushahidi mpaka wa walinzi na sms kwa nini hawaendi tcra kuthibitisha kama ni ya Slaa na ilitumwa saa ngapi na tarehe ngapi ili kuamini? Slaa alisema mengine ameyaweka akiba kwa atakaemjibu nae Gwajima kaweka nae akiba endapo mhusika atayakataa. Kosa lake ni lipi la kulaumiwa eti katoa siri za mtu aliempatia huduma?Sasa kama Slaa aliyaeleza hayo kupitia waandishi wa habari na vyombo vingine kama tvs na radio sasa Gwajima angemjibia wapi? Kwa m/kiti tume ya uchaguzi au kwa kumwandikia Slaa barua? Hapa hadanganyiki mtu.
 
bila kumungunya maneno wala kumeza mate. huu ni ukweli na kama unabusara si za ndani hata za nje tena mbali utaona ukweli.
 
Hivi hapa tunajipa taabu ya nn.Watu ewawili tena wenye sifa zinazofanana wamerushiana maneno ss tunakuja juu na kilanga.. chetu kushindana humu kama si ushabiki wa kisiasa ni nn?wao wapo kimya ss tunatoana macho.Hao wanajusna shetani kapita tu katikati yao.Wataelewana muda si.mrefu.Mungu Lowasa yupo pamoja nawe.Nina uhakika kupitia kwako Mungu analitoa taifa hili gizani.Ahsante Mungu.
 
Uccm unakuwehusha!
Watumishi wa Mungu Huwajibishwa Na Mungu Mwenyewe,Kufanya Hivyo Unajipandia laana wewe na kizazi chako baada Yako.
Ungepaswa Kujiuliza "ALIYEANZISHA zari Ni Mtakatifu Josephati Gwajima,Au Dkt Mihogo Maharagwe.
Biblia Inasema"MJIBU MPUMBAVU SAWASAWA na Umbumbavu Wake,Asije Akajiona Mwenye Hekima Machoni Pake"
Hivyo Ndivyo Kefanya Mtakatifu Josephati Gwajima.
NA ALAANIWE NA MUNGU KILA MTU ANAYEHOJI MANENO YA VINYWA VYA WATUMISHI WA MUNGU YEYE NA KIZAZI CHAKE BAADA YAKE.NA KILA MTU ANAYEIPENDA TZ ASEME.AMEN.AMEN.AMEN.AMEN.

Wewe! hicho kitabu(bible) usikitumie vibaya.. mimi nimekisoma sana nilipokuwa mdogo,nilibaini kuwa watu wengi hadi wachungaji hukitumia kwa manufaa yao tofauti na ya YEHOVA.
 
Umeandika kishabiki ila huu ni ukweli mchungu anaweza kuku expose huyu mtu
 
Hivi hapa tunajipa taabu ya nn.Watu ewawili tena wenye sifa zinazofanana wamerushiana maneno ss tunakuja juu na kilanga.. chetu kushindana humu kama si ushabiki wa kisiasa ni nn?wao wapo kimya ss tunatoana macho.Hao wanajusna shetani kapita tu katikati yao.Wataelewana muda si.mrefu.Mungu Lowasa yupo pamoja nawe.Nina uhakika kupitia kwako Mungu analitoa taifa hili gizani.Ahsante Mungu.

Tatizo sio..kumbuka kuwa slaa ni icon ya taifa..na gwajima pia ni icon ya taifa..
Nyuma ya hoa watu wawili kuna kundi kubwa la watu.

Kama viongozi wetu wanafanya ndivo sivyo lazima tujadili.


Ila huyo asikofu kwa kweli amekurupuka kama kawaida yake.
Ila mimi simshangai ,,maana kuna kipindi alikurupuka akamtukanapengo.
Kwa kweli huyu mtumish kuna kipindi busara ya utumish inapita kushoto
 
Gwajima anaongelea credibility ya maaskofu wa kanisa Katoliki wakati siku si nyingi alimtukana kadinali Pengo.
 
Back
Top Bottom