system hacker
JF-Expert Member
- Mar 13, 2022
- 426
- 706
Hii natoa tahadhari kwa kiongozi yeyote wa Umma kuanzia ngazi ya juu hadi ya chini. Msiwachukulie poa watanzania....watanzania sio kabisa. Ni wavumilivu kweli, lakini uvumilivu una mwisho. Tuishi.
Nasikia sikiaga watu wakisema watanzania ni waoga, tena sana. Kwamba, Kenya ndio watu sio waoga. Eeeehhhh?
Tema mate chini. Wape platform wakuonyeshe. Usiwanyime platform ndo utawajua vizuri zaidi watanzania ni watu gani. Kariakoo iwafumbue macho na muelewe.
Ule mkutano wa Kariakoo na Waziri Mkuu wananchi wa kawaida waliwachanachana vibaya sana viongozi wa Serikali bila kujali cheo wala umri.
Kuanzia waziri, polisi na yeyote yule alichanwachanwa vibaya sana live kwenye runinga Dunia nzima ikiona. Tena waliwasuta hasa na maneno ya shombo wakiwa live kwenye runinga. Wote wanaume kwa wanawake.
Kamuulize Mwigulu, Kijaji, TRA na polisi watakwambia. Kuna mwamba alichana hadi jukwaa la waziri mkuu mwenyewe mbele ya uso wake. Ilibidi PM aishie kucheka tu.
Wasiwasi wangu ni huu: Itakuja kutokea nyakati watanzania watapata platform huru kisiasa na katika kila eneo. My friend ogopa sana hao watu unaowadhania ni waoga. Ogopa sana.
Take care, watanzania ni watu tofauti sana na wengi wanavyowachukulia.
Nasikia sikiaga watu wakisema watanzania ni waoga, tena sana. Kwamba, Kenya ndio watu sio waoga. Eeeehhhh?
Tema mate chini. Wape platform wakuonyeshe. Usiwanyime platform ndo utawajua vizuri zaidi watanzania ni watu gani. Kariakoo iwafumbue macho na muelewe.
Ule mkutano wa Kariakoo na Waziri Mkuu wananchi wa kawaida waliwachanachana vibaya sana viongozi wa Serikali bila kujali cheo wala umri.
Kuanzia waziri, polisi na yeyote yule alichanwachanwa vibaya sana live kwenye runinga Dunia nzima ikiona. Tena waliwasuta hasa na maneno ya shombo wakiwa live kwenye runinga. Wote wanaume kwa wanawake.
Kamuulize Mwigulu, Kijaji, TRA na polisi watakwambia. Kuna mwamba alichana hadi jukwaa la waziri mkuu mwenyewe mbele ya uso wake. Ilibidi PM aishie kucheka tu.
Wasiwasi wangu ni huu: Itakuja kutokea nyakati watanzania watapata platform huru kisiasa na katika kila eneo. My friend ogopa sana hao watu unaowadhania ni waoga. Ogopa sana.
Take care, watanzania ni watu tofauti sana na wengi wanavyowachukulia.