Tafadhali Dkt. Dotto Biteko, tunaomba andiko lako la PhD

Tafadhali Dkt. Dotto Biteko, tunaomba andiko lako la PhD

Hii title hata wa master's udsm hawezi andika hivi, chakushangaza imekuwa kabisa published kwenye hiyo journal, walikosa editor kabisa?
PhD za kibongo, ( Permanent Head Damage)
"Mining SMEs" seems like grammatically correct English
 
Kwa ulimwengu huu wa teknolojia unashindwa kutumia hata Grammarly ikasahihisha makosa madogo madogo kama hayo kwenye title na abstract ? sasa kama kwenye mambo ya masomo wanaboronga hivyo huko kwenye mikataba ya madini itakuaje ?😆
Huku kwenye madini ndiyo game mnayocheza hapa hizo nyingine porojo tu lakini takwimu mchango wa madini ktk GDP sasa ni asilimia 7.9! Mikataba inaandaliwa na Waziri? Wanasheria wanafanya nini?...😀😀😀
 
Huku kwenye madini ndiyo game mnayocheza hapa hizo nyingine porojo tu lakini takwimu mchango wa madini ktk GDP sasa ni asilimia 7.9! Mikataba inaandaliwa na Waziri? Wanasheria wanafanya nini?...😀😀😀
Inamaana Waziri anasaini tu mkataba hatakiwi kuelewa chochote kilichoandikwa, na kukata utepe wakati wa kuzindua mradi ?😆
 
Wacha zako na wewe ndugu yangu; umbea hausaidii. Magufuli amwue mtu na "bastola yake" habari sizijulikane miaka yote hii. Alipoanza kuugua tu uvumi ukawa umasamaa sehemu zote, ingawa watu wake wa karibu walikuwa wanaficha iwe hili la mauji kusiwe na uvumi siku zote hizo hasa wakati wa kuelekea uchaguzi? Halafu ametupwa baharini bado mwili usipatikane? Walienda kumtupa Mauritius? mwili uliozama baharini ukanda wa maili 10 kutokea ufukweni ni lazima hutupwa na maji ufukweni. Sasa hiyo process ya kumwua na kumtupa baharini umbali huo itakuwa ilihusisha watu wangapi na taarifa hizo zisitoke nje kabisa?
Kichuguu siyo kwa sababu wewe huna taarifa ukadhani wote hatuna taarifa

Kama unapinga kuwa Ben Saanane hakuuliwa na Magufuli na mwili wake kutupwa baharini kwenye viroba, basi NIONYESHE aliko Ben Saanane au lilipo kaburi lake. Otherwise funga domo lako

Iko siku CCM haitakuwa madarakani, na Makonda akiwa hai atakuja kututhibitisha haya kama Sabaya alivyokiri kutumwa na Magufuli kufanya ule uovu.
 
Punguzeni maswali Maana hata hampati majibu zaidzaid mnatengeneza chaos tu
 
Inamaana Waziri anasaini tu mkataba hatakiwi kuelewa chochote kilichoandikwa, na kukata utepe wakati wa kuzindua mradi ?😆
Anajua kwa sababu anakuwa involved. Ila taratibu za kisheria, kuandaa docs za kisheria si yeye. Kwa hiyo ukisoma comment moja moja humu...utaona baadhi wanapigana vita ya madini. Mpeni Dk. Biteko breathing space...dah! 😀😀
 
Kuhusu Ph.D ya magufuli, ni kweli ilikuwa haitoshelezi lakini ilikuwa na ubora wa kukubalika. Alianza research kabla hata hajawa mwanasiasa, alianza mara ya kumaliza masters, akachelewa nayo kwa muda mrefu sana alipoanza siasa. Nadhani ilimchukua zaidi ya miaka kumi na tano kuikamilisha baada ya kuwa kwenye siasa zaidi ya kwenye academcis. UDSM hawakumpa burebure
Prospectus ya UDSM ya mwaka 2006 kifungu 2.7.7 kilisema mwanafunzi wa full time wa PhD minimum muda wa kumaliza ni miaka 3 na mwanafunzi wa kutoka kazini ni miaka 5.

Like chapisho alikopi kutoka kwa Dr J Y Philip ambaye alikuwa anafanya sandwich program limaitwa "The potential of anarcadic acid self assembled monopolymers from cashewnut shell liquid as corrosion protection coating"

Supervisor wake alikuwa Prof Bucheschwaija ambaye alimsimamia Dr J Y Phillip as well.

Mwaka 2016 alipopata uRais wa Tanzania akampa Prof Bucheschwaija uwenyekiti wa Bodi ya TIB kama kumpoza kwa kwa kazi aliyomlinda kwenye fake PhD.

Halafu Kichuguu upuuzi wa kusema Magufuli alianza research ya PhD baada ya kumliza masters kadanganye wanao mkiwa sebuleni
 
UDOM college iliyo serious ni College of Informatics peke yake. Pale kuna mwalimu kasoma miaka 8 ndo kapata PhD. Na mwaka huu zimetoka PhD 2 tu kwenye ile college, acha huku Social/Business wanatoa PhD takataka tu …
 
...
Like chapisho alikopi kutoka kwa Dr J Y Philip ambaye alikuwa anafanya sandwich program limaitwa [COLOR=REDP"The potential of anarcadic acid self assembled [U]monopolymers[/U] from cashewnut shell liquid as corrosion protection coating"[/COLOR] ...

Hoja yako ingekuwa na mashiko kama ungeweka machapisho ya hizo PhD thesises kuthibitisha kama kulikuwa na plagiarism.

Magufuli PhD 2009 doctoral thesis was titled “The Potential of Anacardic Acid Self – Assembled Monolayer from Cashew Nut Shell Liquid as Corrosion Protection Coating”

Dr Philip PhD thesis ilihusu monopolymers wakati ya Magufuli ni Monolayer. Kwa msingi huo naamini unajua kuwa katika utafiti wa kitaaluma, mtafiti anaweza kurudia utafiti wa awali kuthibitisha matokeo yake (generalisation) au kuendeleza kilichosahaulika (knowledge gap)
 
Prospectus ya UDSM ya mwaka 2006 kifungu 2.7.7 kilisema mwanafunzi wa full time wa PhD minimum muda wa kumaliza ni miaka 3 na mwanafunzi wa kutoka kazini ni miaka 5.

Like chapisho alikopi kutoka kwa Dr J Y Philip ambaye alikuwa anafanya sandwich program limaitwa "The potential of anarcadic acid self assembled monopolymers from cashewnut shell liquid as corrosion protection coating"

Supervisor wake alikuwa Prof Bucheschwaija ambaye alimsimamia Dr J Y Phillip as well.

Mwaka 2016 alipopata uRais wa Tanzania akampa Prof Bucheschwaija uwenyekiti wa Bodi ya TIB kama kumpoza kwa kwa kazi aliyomlinda kwenye fake PhD.

Halafu Kichuguu upuuzi wa kusema Magufuli alianza research ya PhD baada ya kumliza masters kadanganye wanao mkiwa sebuleni
Unaongea kwa hisia na kuunganisha conspiracy theories bila kuleta na facts za kutosha; nasikikita kusema kuwa niliyondika ni upuuzi lakini ni maoni yako.

Kwanza elewa kuwa Prosepectus hiyo ya UDSM huwa haizuii candidate kuomba extention, ambazo hazina limit mradi tu kuwe na sababu za kuridhisha; hakuna chuo chochote duniani kinazuia mwanafunzi kuomba extension. Mwanafunzi akiugua akaenda kutibiwa kwa miaka 15 prospectus hiyo haimzuii kumaliza masomo yake akishapona. Magufuli alipata sana extension hizo ambazo zilikubaliwa. Prospectus inazuia mtu kuendelea kufanya masomo kwa muda mrefu bila kuwa na sababu ya kuridhisha. Ninajua Magufuli hakutumia muda wa kutosha Lab kuanzia mwaka 2001 lakini kati ya 1995 hadi kipindi hicho alikuwa anakwenda Lab mara kwa mara japokuwa alikuwa kwenye siasa. Alipata Ph.D hiyo mwaka 2006 ikiwa ni takriban miaka kumi kabla ya kuwa rais.

Kuhusu topic kufanana na mwanafunzi mwingine ni jambo la kawaida sana hasa iwapo wote wemefanya chini ya uangalizi wa profesa yule yule, kinachomata ni ile contribution ya studies zao. Ungesaidia sana kama ungeleta kopi za machapisho yote tuyasome kuona kuwa moja ni kopi ya nyingine. Unaweza kukuta mmoja alionyesha kuwa mafuta ya korosho yanaweza kuzuia kutu, halafu mwingine akaonyesha kuwa ili yazuie kutu inabidi yachemshwe mpaka digrii 400 halafu yaongezewe na calcium. Topic zinaweza kuwa zifananana lakini matokeo yao ni tofauti. Ndiyo maana kupata context kamili ni muhimu sana kuliko kutoa general statements tu kama hizo zako

Halafu kumteua profesa wake sioni kama hilo ni jambo la kukushangaza na kushupalia iwapo profesa huyo alikuwa na vigezo vinavyotakiwa na aliteuliwa kwa kufuata sheria. Sema tu iwapo hakuwa na vigezo na uteuzi wake ulikuwa wa kulazimisha, basi leta ushahidi. Mwanzoni Nyerere alikuwa anateua watu waliokuwa schoolmate wake na baadaye akateua wanafunzi wake na hakukuwa na tatizo kabisa.
 
kuna hatari Watanzania wote tukawa na Phd na maprofesa kuliko nchi yeyote duniani..

Ila maajabu pia, pamoja kuwa na maprofesa na madr kuliko nchi yeyote, utakuta pia hakuna tafiti wala ugunduzi wowote ambao umeshafanyika..
Ewaaaaa hapa kwa kweli na mimi napata taabu sanaa, hakuna ugunduzi mpya wowote, hakuna solution mpya from many problems facing Watanzania kutoka kwenye hivi vyuo vikuu but kila siku masters na PhD zinatolewa daaah. Si kwenye Kilimo, ufugaji, uvuvi, utabibu, biashara etc etc shida ziko pale pale...
 
Si kila masters ni lazima kufanya journal publication.

Kuna namna zaidi ya moja za kufanya PhD, mtu anaweza kuchagua kufanya utafiti moja kwa moja au kukaa darasani kisha kufanya utafiti.
[/QUOTE
Kutokana na TCU guidelines za Sasa mwanafunzi was masters ni lazima apublish paper ili agraduate.
Tena baadhi ya vyuo kama Nelson Mandela Arusha unatakiwa upublish kwenye journal kali sio predatory sababu wanasreen paper.
Sasa huyu waziri anapublish journal ya Chuo cha Ushirika kweli haoni aibu eti naye ni daktari.
Tatizo ukishakuwa mwanasiasa nchii Hii hakuna wa kukugusa...TCU wako kimya sijui hizo guidelines huwa wanatoa za nini kama hawazisimamii
 
Nimekupata, naomba niongezee kidogo...

1. kwa hiyo kama mtu anasoma Msc in GIS by coursework and desertation ina maana hii ni academic degree na ni lazima achapishe andiko? Kama ndio je anahitaji pepa ngapi ziwe published ili atunukiwe masters yake?

2. Je ikiwa Msc in GIS by thesis nayo ni lazima achapishe chapisho?

3. Je kama mtu akisoma "Msc by thesis" katika ufundishaji wa chuo inakuaje? Maana nnavyo jua msc by thesis haina GPA na kwenye matangazo wanataka uwe na Msc yenye GPA. Hapo imekaaje?

Thanks in advance.
Kutokana na TCU guidelines ya Sasa Msc by coursework and dissertation unapaswa kupublish paper moja na Msc by thesis paper mbili ndio ugraduate.
 
Mnaishambulia UDOM bure tu, kuna watu wamepata PhD za michongo kule open university na baadhi ya vyuo vya private mpaka unabaki unasikitika tu.

Pia kwa wanasiasa bongo hii vyuo vyote kwao ni mtelezo tu. Ilishawahi kuhojiwa PhD ya mwendazake humu na ya mh wa fedha na uchumi. Zote hizo zilionekana kuwa na chuplichupli kibao. Je! Hao pia walisomea UDOM?
Wanaoshambulia udom ni hao waliosoma udsm wakijiona ni wasomi wakati ni takataka tupu. Mwendazake kajipatia PhD yake ud, huyo wa fedha na hata akina ndalichako masters yake aliipatia pale pale ud wanajifanya kutoona. Kiufupi vyuo vya bongo vyote mchongo mtupu
 
Mimi navyojua Kazi ya Kusoma ni Ngumu sana And More so Kuandika Thesis inataka muda sana...inataka ujitoe kweli PHD sio mchezo jameni Ukisikia mtu anaitwa Dr Mheshimu.Nawambia Ukweli.

Ila Hao wanaokua Na Uwaziri na Kusoma na kumaliza PHD!!! Kweli sielewi wanafanyaje...Ni ngumu sana....
 
Mwana UDOM umehamua kutoa yaliyo moyoni
Mimi sijasoma chuo chochote Cha ndani ya nchi. Nimeona tu hasira nyingi kwa udom wakati vyuo vyote hapa bongo viko kimchongo sana. Open university inaongoza. Kuanzia degree ya kwanza mpaka PhD kote shida tupu. Na wanasiasa baada ya kuona kigezo mojawapo Cha teuzi ni PhD wamechangamkia fursa
 
Back
Top Bottom