UDOM imejishusha sana kwa kugeuka kuwa degree mill inayomilikiwa na Serikali. Mtu amejiunga part-time mwaka 2018, leo baada ya miaka minne (ambyo ni equivalent ya miaka miwili au chini yake kwa full time) tayari Ph.D inatunukiwa. Huwa wana publish wapi hizo Ph.D zao? Ninawanafunzi wawili wa masters ambao wamechelewa kupata degree kwa vile journal publications zao zimechelewa kwenye review process ingawa wana peer reviewed conference papers bado inatakiwa journal publication; mtu hapati degree bila kuwa na journal publication. Naona kwa UDOM Ph.D. zinagawiwa kama free sample tu. Ni afadhali wangekuwa wanatoa subject degrees kama Doctor of Political Science (D.Phil-Politcs), Doctor of Education (D.Ed), Doctor of Public Administration (D.P.A) au Doctor of Business Administration (D.B.A) kuliko kutoa Ph.D.; ni kama hawajui tofauti kati ya Ph.D na doctorate degrees nyingine.