Tafadhali Dkt. Dotto Biteko, tunaomba andiko lako la PhD

Tafadhali Dkt. Dotto Biteko, tunaomba andiko lako la PhD

Kutegemea na miongozo ya chuo, kuna aina tatu ambazo wanawapa phd. Wanaweza kupata kwa kuandika monograph, publishable manuscript, na published manuscript thesis. Sasa kama ametumia monograph anaweza kuwa amefanikiwa. Pia kama ni published manuscript thesis anaweza kufanikiwa pia ka paper zake amepeleka kwa open access journals zinazolipiwa kuanzia dol elfu mbili. Hawa wanafanya kazi kwa haraka na wanatools nyingi za kumsaidia mwandishi/mtafiti.

Najaribu kutafuta wema katika utaratibu huu wasasa.
1. Hiyo ya Miongozo ya Chuo hatupingi, ndiyo maana kuna vyuo vyenye ubora ambavyo mingozo yao ni thabidi na viongozi kama UDOM ambao miongozo yao ni kama hivyo.

2. Elewa kua thesis nyingi huishia kuwa Monograph pia. Academic monographs zote hupitia peer review process kabla ya kuwa published. In fact hata Ph.D zinazotolewa kwa watunzi wa muziki pia hupitia peer review process. Ninajua kuwa Marehemu Dr Mgandu alichelewa sana kupata Ph.D yake kwa sababu ya peer-review ya tungo zake ilichukua muda mrefu, na tungo kadhaa zilikataliwa hata kama zilikuwa nzuri masikioni mwa wasikilizaji, ikabidi aongeze tungo nyingine zinazokidhi vigezo.

3. Kama amepeleka kwenye open access journals ambazo unalipia na kuwa published kesho yake, halafu chuo kikakubali, inabidi turudi kwenye item ya kwanza hapo juu kwa sababu credibility ya publisher huangaliwa sana (impact factor, peer review process, editorial board na vitu kama hivyo). Hiyo ya UDOM kupublish kwenye journals za vitivyo vyao ambapo wao wenyewe ndio ma-reviewer ndio upuuzi wenyewe huo.
 
Kwani yule gaidi ile div 0 yake abasemaje ?
kuna hatari Watanzania wote tukawa na Phd na maprofesa kuliko nchi yeyote duniani..

Ila maajabu pia, pamoja kuwa na maprofesa na madr kuliko nchi yeyote, utakuta pia hakuna tafiti wala ugunduzi wowote ambao umeshafanyika..
 
Kwani ile Div 0 ya gaidi iko vipi ?
kuna hatari Watanzania wote tukawa na Phd na maprofesa kuliko nchi yeyote duniani..

Ila maajabu pia, pamoja kuwa na maprofesa na madr kuliko nchi yeyote, utakuta pia hakuna tafiti wala ugunduzi wowote ambao umeshafanyika..
 
PhD ya part time kuanzia 2018 leo Gamba ameshapata.Awamu ya tano teuzi nyingi kigezo kilikuwa PhD hata Kama uwezo ni mdogo na PhD holder,hajui utafiti wake ulihusu nini na umeongeza nini kwenye tasnia husika.Aidha hizo tafiti zao huwezi kuzipata maktaba au mitandao kwa rejea.

Ushauri
Tafiti zote ziwe zinapatikana maktaba kwa ajili ya watu kuzisoma isije ikawa wamenakiri mawazo ya wengine.
Mkuu ni utaratibu wa kitaaluma kwamba tasnifu zote zinapatikana kwenye maktaba za vyuo vikuu husika. Ikitokea haipo ujue kuna walakini.
 
Anawakaribisha madokta wenzake kwenye vikao vya kisomi.
Ha ha ha; kwa kuanzia tunategemea kumwona (Dr. Kasheku) kwenye Kigoda cha Mwalimu mwakani akitema nondo.

Prof. Shivji ahakikishe anamwalika mwanamajumuni huyu aliyeonesha maajabu ya kisomi ndani ya muda mfupi mno. Ni hazina kubwa kwa taifa.
 
Back
Top Bottom