Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Tabora: Dk Slaa ataja orodha mpya ya mafisadi!

Status
Not open for further replies.
Limeanza jembe mpendazoe anatoa sababu za kutoka ccm,Fyi Dk atatembelea wilaya zote kukijenga chama
 
Naqsubilia list nianze kuhamasisha ndugu zangu huko TZ wafanye maandamano,haki ya mungu natamani kupanda pipa nije kuwaunga makamanda mkono,Tanzania yetu tajiri wachache wanaifaidi.Hope 2020 nitakuwa president adhabu ya mafisdadi itakuwa ni kifo.
 
Mkuu KOO tupe hizo habari maana maTV yetu yamepigwa mkwara kuonyesha makeke ya wanaharakati
 
Najisikia vizuri sana kuona kiu yangu inafikia tamati,nilipenda sana saa ya ukombozi ifike Tbr watanzania hawa nao wakombolewa kutoka mikononi mwa wauaji wao CCM,..sauti ya wengi ni...

Ndugu yangu tujuze kwa kila tukio
 
tupeni update, coz tunasubiri kwa hamu kubwa hiyo list ya mafisadi wapya
 
Wakuu tupeni taarifa tuondoe hasira alizowasha makinda the bogus leo asub
 
Sitashangaa kusikia Bashe, Martina (jina la kike kwa mwanamme) Nape na Makamba pamoja na JK(kwa mara ya pili) nimefurahi kusikia CCM wakisema, watuhumiwa wa ufisadi, kwa kweli neno hilo au watuhumiwa hao wametuhumiwa na CDM so CCM wanatekeleza sera za CDM! nimeipenda sanaaaa! Big Up cdm

Naona umeamka toka usingizini.

Huu ni msamiati ulioanzishwa na wabunge wapambanaji wa CCM waliokuwa wakiwapinga wale waliotajwa na kamati ya Bunge kushiriki ufisadi wa Richmond na Dowans.
 
koo vipi tena wangu.........let update mkuu.......
 
Subira yavuta heri! @ Kaka elly

mtu mzima akilia ujue kuna jambo au watu wamemshika pabaya
avatar15016_3.gif
 
Mpendazoe ameanza kuongea sasa na anasema juu ya nchi kukosa uongozi kutokana na chama dhaifu cha CCM.

Anasema kuwa CCM haijajivua gamba kwani ameingia Zakia kwenye CC wakati yeye ndio alikuwa wazirio wa fedha wakati wa EPA na Kagoda, anasema kuwa Chiligati ndio aliwaambia wabunge wa CCM kuwa wale wanaopambana na ufisadi ndani ya chama watoke kwani hawana hoja kwenye kikao cha kamati ya wabunge.
anasema hapo hakuna gamba lililoptoka ila wameongeza kuimarisha magamba yao.

CCM haiwezi kujivua gamba kwani imepoteza dira ,

Uozo wa CCM umeanzia kwenye matawi kwani ukiona viongozi wa matawi wa CCM wakigombea wanauana wakati hakuna mshahara .

anasema kuwa
 
Mpenda zoe anawachana mafisad anasema hawajajivua magamba waongo,anasema pia anamtaka katibu mwenez awataje walio hucka na meremeta,richmond,kiwila etc then ndo awape cku 90
 
Inaonekana huko mtandao unasumbua au?
 
Uwanja unaojulikana kama uwanja wa vita umefurika watu wote wakiwa na shahuku ya kutaka kujua nani na nani watajiunga katika orodha mpya ya mafisadi na ufisadi waliofanya.
Vijana wazee akinamama na watoto wote wapo hapa wakimsubiri mh dr slaa ili awajuze tayari uwanja umeshajaa na kinacho enderea kwa sasa ni wasanii kuimba nyimbo za uhamisishaji na vijana wa chuo kikuu cha saut tawi la tabora ambao hivi karibuni wamefungua tawi la chadema chuoni hapo wamekusanyika wote wakiwa wamevaliia gwanda za kaki nakuonyesha mshikamano wa hari ya juu. Nashindwa kuweka picha kutokana na ufinyu wa taaluma ya it lakini nikifanikiwa nitawawekea.

thnx for info.
 
Amemtaka katibu mwenezi wa CCM awataje kwanza fisadi wa EPA ni nani na Dowans ni nani ndipo awaambie waondoke CCM ndani ya siku tisini .
 
CCM ni mfu atembeaye. List mpya ya mafisadi walafi hao ndio jibu sahihi la kuwa chama hiki kama kinajiita safi sasa ni mfa maji, na Nape ajue kama kapewa chama mfu ni ngumu mno kukijengea uhai tena. Kama anasahau kuwa kapewa ukuu wa wilaya kishkaji au kifisadi, watanzania wanalijua hilo. naye ni fisadi mtoto, ukimuunganisha na akina riz1, jan, beno, shigella, wote hao ni walinzi wa lile genge kuu la wezi na mafisadi wa taifa.
Nape mwenyewe kamshindwa kamanda Mnyika peke yake, ataiweza CDM? Mfupa anaoudodosa ulishawashinda Chiligati na Al-Sahaf Kinana. Mwenyewe atarajie anguko zaidi la CCM. Vijana sana wamejaa akili na utashi, wanajua CCM si chama, ni mfu, hivyo awepo Nape, Mkama au yeyote ajae, nchi na siasa zimewashinda na vijana hawadanganyiki tena kamwe.
go Dr Slaa, go CDM!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom